Kijana wangu anakesha kwenye games analala alfajiri

Malezi yako yalikuwa mabovu tangu awali pole, games ni ugonjwa mbaya ukiunza hata masomo utakuwa hufaulu vizuri
Sio swala la malezi. Nina house girl ambaye hajawahi kuwa na simu. Nimempa simu ninahakika mshahara wake wote anamalizia kwenye vocha.
 
Sasa bora uyo anayeliwa nyuma je, ayajakukuta ww muongezee game zingine mpya ili ata asiwaze bange na pombe akakuuza adi ww akichoka kucheza ataacha mwenyewe
 
Kuna family moja INA watoto wakiume watatu..

wanajiita ant social, yaani hata ukifika kwao hawana time ya kusalimia wapo busy na Simu,games n.k

issue imekuja baada ya huyu mkubwa kujiajiri,Customer care imemshinda kabisa,hana kauli hajui kuinteract na wateja.

Hiyo hali siyo njema sana.
 

Wewe si unalea kizungu aya sawa endelea kwamba kila anachotaka unampa.

Kuna kipindi kwenye Maisha inabidi ubadilike na kuwa mkali kuna vitu inabidi umfunze kua ni hapana ata kama ni ndio sasa.

Games sio mbaya ila utumiaji wa kupindukia ndio mbaya nakumbuka kipindi niko primary nlikua nkitoka shule nakuta wameishakula wameniachia vyombo vya kuosha nyumba nzima nakula chakula changu naosha vyombo vyote ndipo naenda kucheza nlikua naumia naona nateswa but nimekuja jua Shangazi alikua ananipenda sana yani nlikua nkiomba kitu napewa ila kama hana uwezo anasema hiki sina na hiki sitaki mfano ntacheza nje ila saa moja jioni shart niwe ndani kinyume na apo ni fimbo displine hii ilinijenga mpk najitegemea nikitoka kazini kipindi nipo mkoa ni straight nyumbani sina kona sijui bar, sijui kwenye mpira nkitaka kunywa nanunua naenda kunywa nyumbani.

Mtoto anafundishwa kwa njia tofauti tofauti ata mbaya ili kitu kimwingie sasa kama kijana amekua mtu mzima ivyo jua kuna vitu apo

1. Kashajua yeye ni mkubwa so kuna kibri ( kashabarehe)

2. Mentality yake inamwambia ata wafanyeje hawawezi nipiga mimi si mtu mzima watasema wee Wataacha

3.Ninapendwa na Mama na Baba so mimi ni Tunda lao zuri sasa hapa ndio inawafanya wafanye chochote

Mwisho nakwambia umeongea wee umeona haifai sasa njia ni mbili tu kibongo bongo sisi tulikua tukizingua tu si atuskii tunapelekwa polisi ata masaa 3 tu unakaa pale kituoni unaona machungu yake ukitoka umenyooka

Option ya pili ni kusubiri ametoka chumbani au ameenda matbezi wewe ingia chumbani kwake toa takataka zote za games fungia stoo kaa na funguo akirudi akute azipo atajiongeza na badala ya kutoa games jitahid umtafutie ata books nzuri za stories atleast awe anasoma na wewe unakaa nae mna discuss aya ndio malezi.

una muuliza challenges zake anazopata mfano mimi mpk namaliza chuo Aunt yangu hakuwai niskia na ukaribu na mwanamke mpka akaniuliza tukakaa alikua na lengo la kunisaidia kwa kua alihisi ninatatizo but alipokuja jua kua mimi si mtu wa high profile akajua niko njema na ninamshukuru kwa ilo.

Maisha ni kupanga Dada angu sometimes ulezi wa kizungu ni mzuri ila unamadhara yake na wa kibongo au kiafrica unamadhara yake so jaribu kubalance.

Sisi ambao tulilelewa na Ndugu Mashangazi tukiwa na miaka 2 mpk leo hii watu na ndevu tunajua kabisa hapa tulipitishwa kwenye moto na tunawashukuru sana waliotulie.
 
Mbona kawaida hiyo. Ndio kitu anapenda, uzuri gamers wanajua namna ya kujitune inapofika wakati Fulani. Saa hii anajua yupo free muda mwingi ndio maana anatumia muda wake effectively kumaliza mission zote.
Tembelea ule Uzi wa Kcamp wa Mods za ETS unaweza sama wajuba Ni truck drivers ( Masafa marefu) jinsi tunavyozungumzia mitaa ya Russia, Europe, Brazil, Scandinavia kumbe wapi. Sasa mfano vile kukesha Ni inevitable

Hivyo usiumize kichwa kijana yupo safe, nasema hivi from experience
 
Toa ps zote humo chumbani.. Alafu kwa kumkomoa mtafutie kwio wake Wafungie humo chumbani
 
Kawaida sana wala usiwaze

Mimi mpaka leo na utu uzima wangu huu huwa nakesha nakipiga FIFA yani unanikuta niko siriaz kabisa
 
Mama hana muda na mtoto kutwa kucha kusambaza propaganda za CHADEMA na TUNDU LISSU majukumu yako hufanyi unategemea nini
 
na huyo ni mwanafunzi wa chuo tena second year? wazazi wengine mnajitia stress zisizo na msingi
 
Punguza makasiriko mama si ni life tu??
Motto anaweza asiwe gamer.
Akawa mvuta bange,mlevi.shoga,mwizi,jambazi,tapeli.
Kama anasoma chuo fresh hiyo game ni sehemu ya hobby tu soon ataacha
 


Aisee mkanye kwa nguvu kubwa sana kwa sababu very soon ata advance na kuingia kwenye kamali kabisaaa
 

Mtafutie demu[emoji2] awe anampotezea muda
 
Mimi naona ni kawaida na tusiwalaumu sana watoto. Sisi wenyewe tunashinda mitandaoni, jf, fb, twitter, Instagram muda wote unadhani watoto wanajifunza nini.

Ukitaka umuumize mtu, chukua smartphone yake kwa nusu siku tu.
 



Acha kulalamika c bora unakua na uhakika na mwanao yupo ndani tuu je angakua cha pombe ungesemaje cha muhimu muache tuu au asbh toka nae kma offc yako inaruhusu uwe unamkeep busy thn jion anarud amechoka japo htacheza lkn sio sana
 
Ulimlea hvyo na amekuwa hvyo. Usitegemee kuvuna karanga wakati ulipanda maragwe.

Cha muhim tumia hiyo kama fursa kwa sasa, ulaya na nchi za far East wao wana challenges kabisa za video games na mshindi anaondoka na dollar zake sasa mtaftie connection aanze kucheza online games za kulipwa anaposhinda wenda ikawa na faida kwake na familia kiujumla.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…