Kijeshi, Urusi imefeli vibaya sana huko Ukraine

Kijeshi, Urusi imefeli vibaya sana huko Ukraine

Haa ha ha; we jamaa yaani kati ya mafunzo ya SUMA JKT na mgambo yepi makali? SUMA JKT wale ni wana jeshi kabisa wale kaka, sheria tu ndio haiwaruhusu kufanya zaidi ya kile wanacho kifanya, alipo SUMA JKT police anapaogopa. Sorry kua nje ya topic ila umenifurahisha kwa mchango wako

Mgambo anafundishwa na nani na huyo Suma JKT anafundishwa na nani? Kwa muda gani na course content ikoje?

Suma JKT wako makundi mawili;
1. Wale waliopitia JKT kwa program ya kujitolea miezi sita ya kozi lakini mwisho wa siku wakakosa ajira kwenye vikosi vya Ulinzi na Usalama (serikalini),
2. Wale wanaookotwa kitaani kwenda crush program kupiga kozi fupi kisha kuvishwa uniform kuingia lindoni

Unatakiwa kujua kingine, kuna mgambo wameajiriwa Suma JKT pia kwa sababu Suma JKT ni shirika linaajiri kikubwa uwe na ujuzi wa mbinu za medani (Basic military training) hata wewe kama ulipita JKT zama hizo na cheti unacho hauna kazi nenda Suma JKT upate kibarua mwisho wa mwezi upokee laki 2 zako ukalale.

Kwanini Suma JKT wanakuwa watata na kupelekea watu wengi wawaogope? Hawa watu wengi wao wamekosa fursa za ajira ya moja kwa moja wengi wao wana hasira sana na wanafanya kazi kwa kujikakamua ili wasichukuliwe poa[emoji23][emoji23]

Ila kiuhalisia ni weupe tu zaidi ya mob psychology wanayoweza kuungana na kukufanyia vurugu, ukimbana mmoja mmoja hakuna jipya hata jioni ya leo kuna Suma JKT anawaza akitoka Lindoni pale atm ya crdb ataenda kula nini[emoji23][emoji23]
 
Unashangaa hili, Waziri wa Ulinzi wa Urusi yule Sergei Shoigu ni Civil Engineer na hakuwahi kuwa jeshini hapo kabla. Ni kama umbebe mtu Tanroads uko, sasa hajabu kwa mleta mada ni nini

Hakuna hajabu mkuu[emoji23][emoji23]
 
Kwa jicho la kijeshi!

Wengi humu kupitia michango yetu tunafahamu kuwa lengo mojawapo la Urusi kuivamia Ukraine lilikuwa ni demilitarization. Ila ni wachache sana tutafahamu kuwa, lengo hili mara nyingi hufanikiwa ipasavyo linapo ambatana na kuuondoa madarakani utawala wa adui.

Majeshi yote ya nchi huwa yako chini ya utawala wa nchi husika huku kiongozi wa nchi akiwa ndiye amiri jeshi mkuu. Hivyo, mara nyingi majeshi hutii amri na maagizo ya utawala uliopo madarakani. Hata katika masuala ya mobilization na recruitment ya majeshi pia viko chini ya supervision ya utawala uliopo.

Njia pekee zenye uhakika wa kuhakikisha kuwa zoezi la demilitarization dhidi ya adui linafanikiwa kwa ufanisi ni mbili:

1) Regime change. Kama nilivyosema, utawala uliopo madarakani ndiyo chachu kubwa ya kuyaongoza majeshi kuendelea kuilinda mipaka ya nchi. As long as utawala unaendelea kuwepo madarakani, basi majeshi yataendelea kufanya kazi zake.

Ushahidi wa hili ni katika vita kubwa zilizowahi kutokea duniani mfano, WW2. Iliyokuwa USSR ilipoteza wanajeshi wengi sana hasa dhidi ya Hitler wakati wa Vita ya Pili ya Dunia, lakini, uwepo wa serikali inayofanya kazi (functioning government) uliwezesha majukumu mengine kuendelea kama kawaida ikiwemo recruitment ya majeshi usiku na mchana kufidia upotevu.

2. Makubaliano. Hii ni njia ya pili ambapo pande zote mbili hufikia katika meza ya majadiliano na kisha kukubaliana kupunguza majeshi ya upande mmoja ama pande zote kwa maana ya demilitarization, kwa maslahi ya pande zote.

Uvamizi wa kijeshi wa Urusi nchini Ukraine kwa kiasi kikubwa ulikuwa na lengo la kuiondoa madarakani serikali iliyopo kama njia mojawapo ya demilitarization ambayo nimetoka kuisema. Lengo hili lilipo shindikana, ndipo tulipoanza kuona njia ya pili hapo ikijaribu kuchukua nafasi yake.

Kwa wale wanaosema kuwa Urusi haikuwa na lengo la kuingia Kyiv na kuuondoa madarakani utawala wa Zelenskyy nina swali moja kwenu ambalo ni rahisi tu.

Hivi, kwani hatukumsikia Putin mwenyewe mapema kabisa kwenye vyombo vya habari akiwaomba wanajeshi wa Ukraine wampindue ama wamuondoe madarakani Zelenskyy?

Je, majeshi ya Urusi yenyewe yalishindwa kutekeleza jukumu hilo, suala lililo pelekea mpaka kiongozi wa Urusi kutoka hadharani na kuliomba jeshi la adui yake kuwasaidia hilo jukumu?

Je, tuendelee kuziamini hizi hoja kwamba Urusi haikuwa na malengo ya kuiondoa madarakani serikali ya Zelenskyy? Wakati hata kauli za viongozi wa juu wa utawala wa Urusi zinaonesha dhahiri malengo hayo!
 
Ukiitazama hii vita katika jicho la kijeshi ni dhahiri urusi imefeli!
Imefeli kwa sababu imeshindwa kufikia malengo yake ya uanzishaji hii vita!

Lengo la Kijeshi la Urusi ilikuwa ni kuingia Kiev haraka, kukamata mji mkuu na kuuangusha utawala wa Zelensky. Lakini hadi leo hii takriban siku ya 60 ya kivita, Urusi imeshindwa kukamata Kiev, na majeshi yake baada ya kukutana na upinzani mkali yakakimbia(retreat) kutoka miji ya ndani na kurudi huko Mashariki ambako walikuwa wanapakalia toka mwaka 2014.

Urusi imepata hasara kubwa sana ya vifaa na askari. Vifaru vyake vilikuwa vikikaangwa kwelikweli na Javelin missiles, pamoja na drones za Bayraktaar.

Logistics za kupeleka chakula na silaha ndanindani kwa askari wake ilikuwa shida

Wakati huo vikwazo vikiendelea kuichakaza urusi kwelikweli.

Hadi hivi sasa Zelensky amefanikiwa kuilinda serikali yake, na kinachofuata sasa ni kuandaa operesheni kabambe ya kumtoa nyoka pangoni huko Mashariki, Hii itakuwa operesheni kali sana na ngumu sana lakini itawezekana.

Urusi ni Taifa kubwa lakini uchumi wake ni mdogo kuliko jimbo moja tu la Texas Marekani, haina fedha za kupigana hii vita kwa muda mrefu, itakachokifanya ni kutafuta kideal cha kizushi na Ukraine ili kuficha aibu ya uso wake!

Kikubwa nilichojifunza katika hizi vita, Moyo wa askari una nguvu kuliko silaha kali ktk mikono ya askari asiye na moyo wa mapambano!

Mafanikio ya kijeshi ya Urusi huko mashariki mwa Ukraine katika vita hii ya Sasa wala si jambo la ajabu maana warusi walishakuwepo huko toka mwaka 2014, hakuna kitu kipya!. Ni sawasawa na kupiga bomu mochwari na kisha kushangilia kuwa umeua!

Chukulia wamefeli ndio!!! Wewe unatakaje sasa
 
Kwa jicho la kijeshi!

Wengi humu kupitia michango yetu tunafahamu kuwa lengo mojawapo la Urusi kuivamia Ukraine lilikuwa ni demilitarization. Ila ni wachache sana tutafahamu kuwa, lengo hili mara nyingi hufanikiwa ipasavyo linapo ambatana na kuuondoa madarakani utawala wa adui.

Majeshi yote ya nchi huwa yako chini ya utawala wa nchi husika huku kiongozi wa nchi akiwa ndiye amiri jeshi mkuu. Hivyo, mara nyingi majeshi hutii amri na maagizo ya utawala uliopo madarakani. Hata katika masuala ya mobilization na recruitment ya majeshi pia viko chini ya supervision ya utawala uliopo.

Njia pekee zenye uhakika wa kuhakikisha kuwa zoezi la demilitarization dhidi ya adui linafanikiwa kwa ufanisi ni mbili:

1) Regime change. Kama nilivyosema, utawala uliopo madarakani ndiyo chachu kubwa ya kuyaongoza majeshi kuendelea kuilinda mipaka ya nchi. As long as utawala unaendelea kuwepo madarakani, basi majeshi yataendelea kufanya kazi zake.

Ushahidi wa hili ni katika vita kubwa zilizowahi kutokea duniani mfano, WW2. Iliyokuwa USSR ilipoteza wanajeshi wengi sana hasa dhidi ya Hitler wakati wa Vita ya Pili ya Dunia, lakini, uwepo wa serikali inayofanya kazi (functioning government) uliwezesha majukumu mengine kuendelea kama kawaida ikiwemo recruitment ya majeshi usiku na mchana kufidia upotevu.

2. Makubaliano. Hii ni njia ya pili ambapo pande zote mbili hufikia katika meza ya majadiliano na kisha kukubaliana kupunguza majeshi ya upande mmoja ama pande zote kwa maana ya demilitarization, kwa maslahi ya pande zote.

Uvamizi wa kijeshi wa Urusi nchini Ukraine kwa kiasi kikubwa ulikuwa na lengo la kuiondoa madarakani serikali iliyopo kama njia mojawapo ya demilitarization ambayo nimetoka kuisema. Lengo hili lilipo shindikana, ndipo tulipoanza kuona njia ya pili hapo ikijaribu kuchukua nafasi yake.

Kwa wale wanaosema kuwa Urusi haikuwa na lengo la kuingia Kyiv na kuuondoa madarakani utawala wa Zelenskyy nina swali moja kwenu ambalo ni rahisi tu.

Hivi, kwani hatukumsikia Putin mwenyewe mapema kabisa kwenye vyombo vya habari akiwaomba wanajeshi wa Ukraine wampindue ama wamuondoe madarakani Zelenskyy?

Je, majeshi ya Urusi yenyewe yalishindwa kutekeleza jukumu hilo, suala lililo pelekea mpaka kiongozi wa Urusi kutoka hadharani na kuliomba jeshi la adui yake kuwasaidia hilo jukumu?

Je, tuendelee kuziamini hizi hoja kwamba Urusi haikuwa na malengo ya kuiondoa madarakani serikali ya Zelenskyy? Wakati hata kauli za viongozi wa juu wa utawala wa Urusi zinaonesha dhahiri malengo hayo!
Umechambua vizuri sana mkuu

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Ukiitazama hii vita katika jicho la kijeshi ni dhahiri urusi imefeli!
Imefeli kwa sababu imeshindwa kufikia malengo yake ya uanzishaji hii vita!

Lengo la Kijeshi la Urusi ilikuwa ni kuingia Kiev haraka, kukamata mji mkuu na kuuangusha utawala wa Zelensky. Lakini hadi leo hii takriban siku ya 60 ya kivita, Urusi imeshindwa kukamata Kiev,
Sikuwa na nia ya kujibu Uzi huu na Uzi mwengine kwa sababu ya azma niliyojiwekea mwenyewe binafsi kwa kanuni na nidhamu ama misingi iliyoniwajibikia juu yangu. Isipokuwa ulichokiandika kimenifanya nami niandike.

Ningependa niende kwa vitendo kwa anuwani yako ya juu uliyoiwasilisha na vitendo vinazungumzo zaidi kwa sababu vinaepusha na kupunguza mlolongo wa maneno/maandishi zaidi.

Malengo ya Urusi kuanzisha hii vita ni haya:
Screenshot_20220420-183613.png

Mtafute huyu You Tube, kuna speech yote ya Putin na malengo ya kuanzisha hii vita ambayo wao wanaiita military operation Putin ameyataja humo. A-Z yapo tofauti na uliyoyataja wewe.

Wengi wetu katika sisi ukiwemo na wewe na ndivyo ilivyozoeleka na ndivyo ambavyo inavyofanyika kwenye vita, jambo muhimu baina ya nchi mbili zinaposigana kijeshi basi nikuteka mji mkuu wa nchi ya mwenzako. Hiki ndicho wengi tunachokifikiria.

Ikiwa hii nukta uliyoileta ndilo lengo la Urusi inatubidi tuwaze mbali zaidi. Ikiwa Urusi kujihakikishia usalama wa nchi yake ni kumuondoa Zelensky nchini Ukraine na kuikalia hiyo nchi hii mbinu itadumu kwa muda gani?

Ukoloni ni jawabu tosha! Hata uwe na nguvu namna gani huwezi kumtawala mtu milele. Hususani suala kubwa kama nchi huwezi kuitawala milele. Ikiwa lengo lako ni kulinda usalama wa nchi yako utatumia mbinu gani? Mabepari walitumia mifumo yao ya kuhakikisha sisi kuendelea kuwa tegemezi kwao ili wao wapate mwanya ama fursa ya kulinda maslahi yao. Hivyo unabakiwa na uhuru wa bendera.

Fursa ya namna hii kwa Urusi ipo nayo ni majimbo yaliyo mashariki mwa Ukraine ambayo ina wakazi wenye asili ya Kirusi. Usalama wa Urusi upo kwenye haya majimbo. Piga ua hakuna namna, haya majimbo Mrusi atahakikisha yawe huru kwa kujitegemea yenyewe ili kabla ya kumgusa Mrusi kwanza uwaguse wale.

Hili suala ukiliangalia lina njia nyingi sana ambazo ni faida maradufu kwa Mrusi. Tusifikirie kwa kimazoea! Ukiangalia anachokifanya Mrusi anapita kwenye njia zilizojengeka kimazoea kimbinu za kivita na kwenye uwezo wa watu kufikiri kukamilisha malengo yake.Ukitaka kuamini hili tusubiri vitendo vilevile vitaongea (mwisho wa hii vita).
 
Toka mwanzo wa vita wenzako walikua na maneno kama hayo mara uchumi wake sio imara hawezi kupigana vita mda mrefu mara kaishiwa chakula hawezi kulisha wanajeshi wake (muda huo huo anatoa tani za vyakula kusaidia wananchi walioko ukraine) mara kaishiwa silaha zimebaki za kupambana siku 3 tu, leo ni miezi bado silaha zipo na mashambulizi yanazidi kuendelea

Sisi wachambuzi ambao hatujui masuala ya kivita tunafanya analysis kwa kufuata hisia zetu tuendelee kuwa watazamaji tu hatujui malengo ya Putin yalikuwaje na hatujui kafanikiwa au vp kwa sasa kila mtu anachukua cheo cha kuwa military analyst anachambua anavyojua yeye.

Labda unaweza kuelezea Zelensky amefanikiwaje kuilinda serikali yake? Ukiangalia kwa jicho lako la kijeshi nani kapata losses nyingi kwenye vita hii?

K**"ma mamaako...usilete ushabiki watu wakifariki kwa vita....Urusi amevamia Ukraine kibabe...ameua wananchi wengi
 
Toka mwanzo wa vita wenzako walikua na maneno kama hayo mara uchumi wake sio imara hawezi kupigana vita mda mrefu mara kaishiwa chakula hawezi kulisha wanajeshi wake (muda huo huo anatoa tani za vyakula kusaidia wananchi walioko ukraine) mara kaishiwa silaha zimebaki za kupambana siku 3 tu, leo ni miezi bado silaha zipo na mashambulizi yanazidi kuendelea

Sisi wachambuzi ambao hatujui masuala ya kivita tunafanya analysis kwa kufuata hisia zetu tuendelee kuwa watazamaji tu hatujui malengo ya Putin yalikuwaje na hatujui kafanikiwa au vp kwa sasa kila mtu anachukua cheo cha kuwa military analyst anachambua anavyojua yeye.

Labda unaweza kuelezea Zelensky amefanikiwaje kuilinda serikali yake? Ukiangalia kwa jicho lako la kijeshi nani kapata losses nyingi kwenye vita hii?
Urusi kafeli saaana..
 
Hilo Lengo la kijeshi wee umelitoa wapi?
Au umeoteshwa?

Special operation ndani ya Ukraine malengo 3
1. Ku-denazify ukraine
2. Kuyakomboa majimbo ya donbass,luhansk
3. Kukifuta kikundi Cha kinazi Cha AZOV kilichojichimbia uko mariupol na Khakiv

Sasa wewe umeng'ang'ana na Kiev,

Unasahau miji kibao ndani ya Ukraine inatekeketea MDA huu.
KIUJUMLA Urusi wameshapata mafanikio makubwa sana katika hii vita. Ukraine na western allies wameshapotezwa, walihadaika na mipango ya urusi wakadhani urusi wana lengo la kuiteka Kiev, Siyo Kiev wala Kharikiv lilikuwa lengo la urusi. issue ilikuwa ni majimbo ya DONBASS NA LUHANSIK. na sasa harakati za kijeshi zinaendelea vizuri huko. western walitumia nguvu kubwa sana kuyazuia majeshi yenye malengo bandia yaliyokuwa yanatishia kuiteka kiev!
 
Ha ha ha ha ha ha
mpaka muda huu ukraine imegawanya kati kati miji ya ya lungnsk donenk mariupol kharkiv khersan oddess imeshakuwa chini ya Mrusi.

Mpaka muda huu ukraine haina tena bahari mijai tajawa hapo juu ni miji ya kichumi kwa ukraine. Kitenda cha urusi kuiteka miji hiyo kuna uwezekano uchumi wa ukraine usiufikie hata uchumi wa hapa morogoro

Alafu hii vita ni ya urusi na nato na nato wemepigika mno mpaka makamanda wao kukamatwa

Urusi sio marekani iliyoshindwa kuiteka kamji kadogo ka mogadishu pale Somalia.

ha ha ha ha ha ha ha
🤣🤣🤣
 
Wanakunywa konyagi na double kick kisha wanajizima data. Eti lengo "likikua kuikamata kiev na kuangusha serikali" then? Lengo la ukraine ni nini? Askari wake ku surrender? Kuangamizwa miji? Silaha na miundombinu? Ukraine ame archive nini mpaka sasa.?

Acheni uoga, matokeo yatakuja kwa uwazi, saizi mnafichwa na BBC na CNN. Mpaka sasa serikali ya Ukraine haina control na majimbo yote ya mashariki, kuanzia cremea, mariupol donbase nk. Hili hutoambiwa na BBC, watu wamepiga kura kujitoa ukraiane, pale zinaenda kutokea nchi 3. Stay tuned... uongo na ukweli hutengana kama mafuta na maji.
📌📌📌🤣
 
Kwa jicho la kijeshi!

Wengi humu kupitia michango yetu tunafahamu kuwa lengo mojawapo la Urusi kuivamia Ukraine lilikuwa ni demilitarization. Ila ni wachache sana tutafahamu kuwa, lengo hili mara nyingi hufanikiwa ipasavyo linapo ambatana na kuuondoa madarakani utawala wa adui.

Majeshi yote ya nchi huwa yako chini ya utawala wa nchi husika huku kiongozi wa nchi akiwa ndiye amiri jeshi mkuu. Hivyo, mara nyingi majeshi hutii amri na maagizo ya utawala uliopo madarakani. Hata katika masuala ya mobilization na recruitment ya majeshi pia viko chini ya supervision ya utawala uliopo.

Njia pekee zenye uhakika wa kuhakikisha kuwa zoezi la demilitarization dhidi ya adui linafanikiwa kwa ufanisi ni mbili:

1) Regime change. Kama nilivyosema, utawala uliopo madarakani ndiyo chachu kubwa ya kuyaongoza majeshi kuendelea kuilinda mipaka ya nchi. As long as utawala unaendelea kuwepo madarakani, basi majeshi yataendelea kufanya kazi zake.

Ushahidi wa hili ni katika vita kubwa zilizowahi kutokea duniani mfano, WW2. Iliyokuwa USSR ilipoteza wanajeshi wengi sana hasa dhidi ya Hitler wakati wa Vita ya Pili ya Dunia, lakini, uwepo wa serikali inayofanya kazi (functioning government) uliwezesha majukumu mengine kuendelea kama kawaida ikiwemo recruitment ya majeshi usiku na mchana kufidia upotevu.

2. Makubaliano. Hii ni njia ya pili ambapo pande zote mbili hufikia katika meza ya majadiliano na kisha kukubaliana kupunguza majeshi ya upande mmoja ama pande zote kwa maana ya demilitarization, kwa maslahi ya pande zote.

Uvamizi wa kijeshi wa Urusi nchini Ukraine kwa kiasi kikubwa ulikuwa na lengo la kuiondoa madarakani serikali iliyopo kama njia mojawapo ya demilitarization ambayo nimetoka kuisema. Lengo hili lilipo shindikana, ndipo tulipoanza kuona njia ya pili hapo ikijaribu kuchukua nafasi yake.

Kwa wale wanaosema kuwa Urusi haikuwa na lengo la kuingia Kyiv na kuuondoa madarakani utawala wa Zelenskyy nina swali moja kwenu ambalo ni rahisi tu.

Hivi, kwani hatukumsikia Putin mwenyewe mapema kabisa kwenye vyombo vya habari akiwaomba wanajeshi wa Ukraine wampindue ama wamuondoe madarakani Zelenskyy?

Je, majeshi ya Urusi yenyewe yalishindwa kutekeleza jukumu hilo, suala lililo pelekea mpaka kiongozi wa Urusi kutoka hadharani na kuliomba jeshi la adui yake kuwasaidia hilo jukumu?

Je, tuendelee kuziamini hizi hoja kwamba Urusi haikuwa na malengo ya kuiondoa madarakani serikali ya Zelenskyy? Wakati hata kauli za viongozi wa juu wa utawala wa Urusi zinaonesha dhahiri malengo hayo!
Very objective comment
 
K**"ma mamaako...usilete ushabiki watu wakifariki kwa vita....Urusi amevamia Ukraine kibabe...ameua wananchi wengi
Kutukana hakukufanyi uonekane una uchungu sana na raia wa Ukraine kufa, neither haifanyi vita iishe wala Ukraine ashinde zaidi sana inaonyesha uwezo hafifu wa kufikiri kwako.

Urusi kavamia ukraine kaua watu then what? Nini utafanya wewe kama wewe ili kuzuia watu wasife Ukraine? Kwa kutukana?
 
Ukiitazama hii vita katika jicho la kijeshi ni dhahiri urusi imefeli!
Imefeli kwa sababu imeshindwa kufikia malengo yake ya uanzishaji hii vita!

Lengo la Kijeshi la Urusi ilikuwa ni kuingia Kiev haraka, kukamata mji mkuu na kuuangusha utawala wa Zelensky. Lakini hadi leo hii takriban siku ya 60 ya kivita, Urusi imeshindwa kukamata Kiev, na majeshi yake baada ya kukutana na upinzani mkali yakakimbia(retreat) kutoka miji ya ndani na kurudi huko Mashariki ambako walikuwa wanapakalia toka mwaka 2014.

Urusi imepata hasara kubwa sana ya vifaa na askari. Vifaru vyake vilikuwa vikikaangwa kwelikweli na Javelin missiles, pamoja na drones za Bayraktaar.

Logistics za kupeleka chakula na silaha ndanindani kwa askari wake ilikuwa shida

Wakati huo vikwazo vikiendelea kuichakaza urusi kwelikweli.

Hadi hivi sasa Zelensky amefanikiwa kuilinda serikali yake, na kinachofuata sasa ni kuandaa operesheni kabambe ya kumtoa nyoka pangoni huko Mashariki, Hii itakuwa operesheni kali sana na ngumu sana lakini itawezekana.

Urusi ni Taifa kubwa lakini uchumi wake ni mdogo kuliko jimbo moja tu la Texas Marekani, haina fedha za kupigana hii vita kwa muda mrefu, itakachokifanya ni kutafuta kideal cha kizushi na Ukraine ili kuficha aibu ya uso wake!

Kikubwa nilichojifunza katika hizi vita, Moyo wa askari una nguvu kuliko silaha kali ktk mikono ya askari asiye na moyo wa mapambano!

Mafanikio ya kijeshi ya Urusi huko mashariki mwa Ukraine katika vita hii ya Sasa wala si jambo la ajabu maana warusi walishakuwepo huko toka mwaka 2014, hakuna kitu kipya!. Ni sawasawa na kupiga bomu mochwari na kisha kushangilia kuwa umeua!
Kwa maoni yangu ni mapema sna kutuaminisha kua urusi imeshindwa hii operation yake nchini Ukraine [emoji1255], siku katibu wa UN alipokua Kiev, urusi alishusha makombora kama yote
 
Kwa maoni yangu ni mapema sna kutuaminisha kua urusi imeshindwa hii operation yake nchini Ukraine [emoji1255], siku katibu wa UN alipokua Kiev, urusi alishusha makombora kama yote
Mbona wakienda viongozi wa Magharibi hashushi hayo makombora,anawaogopa?
 
Back
Top Bottom