Tetesi: Kikao cha dharura cha wakuu wa vyuo vyote vikuu nchini kinaendela mjini Dodoma , kuna tatizo kubwa

Tetesi: Kikao cha dharura cha wakuu wa vyuo vyote vikuu nchini kinaendela mjini Dodoma , kuna tatizo kubwa

Ukimchukua manafunzi wa IT au Engineer ambao wapo mwaka wa mwisho,waulize swali hili "Hivi wewe mpaka sasa unajua nini au umespecilize ktk eneo gani",huwezi amini hili swali 90% watashindwa kukujibu watakwambia "mimi najuajua",wamesahau ktk dunia hii ya sasa ambayo teknolojia inakuwa kwa kasi unatakiwa UJUE HASWA.

Kuna madogo walisoma Electronics and Commubication,Telecommunication Engineering walikuja field nikawaulizwa swali kama hili,wote walishindwa kunijibu na wengi wao wana amini kazi watajulia kazini,chuoni wameenda kutafuta GPA za kukariri.

Basi huwaga unawashauri vitu vya kusoma,unawapa softwares kwa ajili ya kufanya practical,unawapa tutorial za online,vitabu, unawa ambia ukishindwa ni ulize nikuelekeze,lkn hawakufuati wanakuja field hawabebi hata PC.Wapo wapo story zao series,madem na mabash unawatizama unawaonea huruma,sababu mtaani kugumu sana.
Kuna kasumba moja vijana wa vyuo wanayo wanapokuja field! Namna wanavyo behave ni kama wengine wote hawajawahi kufika chuo ila wao tu! Ndiomaana ni wachache sana wanakuwa na utayari wa kuuliza au kuomba waelekezwe jambo fulani. Na hii ni kwa karibu fani zote

Ki ukweli system yetu ya elimu inahitaji maboresho makubwa sana! Huwa nawatania wenzangu wanitajie vitu walivyosoma chuo ambavyo hadi sasa bado wanavi-apply kwenye kazi zao ofisini

Chuoni unasoma ma vitu mengi lakini huyatumii yote! Na mwisho wa siku unaweza kuwa uko vizuri kwenye unit mojawapo GPA ikakukosesha kazi


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna tetesi kuwa kikao cha dharura kimeitishwa mjini Dodoma kinachowakutanisha wakuu wote wa vyuo vikuu nchini.

Hatua ya kuitia kikao hicho imetokana na hali mbaya ya wahitimu wa vyuo vikuu nchini ambapo mara wanapoajiriwa katika sehemu mbalimbali wanashindwa kufanya kazi ambazo zingine ni rahisi kabisa.

Wahitimu wengine wanashindwa kuandika barua za maombi ya kazi, kushindwa kufanya majaribio mbalimbali na hata pia kushindwa kuandika taarifa kwa kwa lugha ya Kiswahili na pia kwa lugha ya kiingereza.

Waziri wa elimu profesa Ndalichako ameamua kuitisha kikao hicho kujadili kuona wapi kuna tatizo.

Pia kikao hicho kinatarajiwa kujadili hali ya utoaji wa rishwa ya ngono kwa wanafunzi wa kike vyuoni ambapo huahidiwa alama za juu ili kufaulu mitihani yao ya mwaka wa mwisho kwa masharti ya kushiriki vitendo vya ngono na wahadhiri wao.

Ni muhimu taarifa kama hizi zikawekwa kwenye umma ili kuuelimisha kuhusiana na hali halisi ya kudorora kwa kasi ya juu kwa utaji wa elimu ya juu nchini na kuachia wanafunzi khasa wa kike kutegemea kutoa miili yao ili kupata alama nzuri.
Tuna matatizo ya zaidi ya vyuo vikuu.

Tuna matatizo ya utamaduni.

Tuna matatizo ya maadili.

Ndiyo maana mhadhiri anaweza kuomba rushwa ya ngono kwa mwanafunzi, ili ampe alama za juu.

Na mwenye alama za juu anaweza kufelishwa.

Sasa, mwanafunzi akishajua hilo, atasoma ili apate alama za juu kwa sababu gani?

Hatuna utamaduni wa kuthamini usomi. Ndiyo maana hata wanaoitwa wasomi katika uongozi wanaweka mbele kujipendekeza kwa unafiki kuliko kushauri kisomi.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siku za nyuma kulikuwa na mashindano ya Coka cola ngazi ya vyuo vikuu Afrika mashariki, kujieleza kwa watanzania ni issue!!! Interview ni shida! Kulikoni?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilifikiri wanajadili boom[emoji124][emoji124][emoji124][emoji124]

Hasara Umfika Mwenye Mabezo
 
Tatizo liko huku kwenye mizizi. Lakini na maprofesa wa PhD wanataka kulitatua kule juu kileleni kwenye matawi.
Mimi ningeona wangeanza kujichungiza wenyewe kama hizo PhD zao ni za kweli.
You can't solve a problem by curing the symptoms.
Kuna shule wanafunzi wa FOM TUU (kidato cha 2) hawajui kusoma na kuandika. Tungeruhusiwa kufanya independent research sio ajabu tukakuta kuna form six hajui kusoma na kuhesabu.
Hao wa form 2 ndo wale wakifika form 4 utasikia matokeo ufaulu umeongezeka hadi 90 +%
 
Hao ni waliopika vyeti ndo hawajui kuandika barua . Kwa wachuo siamini. Mana utandawazi uko nje nje .

Ulie leta uzi ni muongo, mnafki na mzushi leta ushaidi kama unauhakika na icho kikao tuone nami nisikie kinaongelea Nini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakubaliana na wewe 100%. Wakuu wa vyuo hawawezi na sio suruhu na sio tatizo katika hili. Serikali inajikuna yenyewe katika hili. Kuna wanafunzi vyuo vikuu hawawezi kuandika sentensi ya kiingereza. Na shule za kata zimekuja kuwa hovyo kabisa na ndio matunda haya tuyaonayo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kama wanafunzi hawawezi kuandika hata sentensi moja ya kiingereza, wanafunzi hao wanawezaje kuhitimu?
Nadhani hao wange-disco muhula wa kwanza wa mwaka wa kwanza.
Au unaonaje mkuu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hao ni waliopika vyeti ndo hawajui kuandika barua . Kwa wachuo siamini. Mana utandawazi uko nje nje .

Ulie leta uzi ni muongo, mnafki na mzushi leta ushaidi kama unauhakika na icho kikao tuone nami nisikie kinaongelea Nini.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ubinashi ni asili yako? Unaishi dunia gani? Suala uwezo wa wahitimu wa miaka hii ni afadhali ukutane na mwanafunzi wa kidato cha tatu wa miaka ya tisini.

Yaani ni shida. Elimu imeporomoka sana

-
 
Ubinashi ni asili yako? Unaishi dunia gani? Suala uwezo wa wahitimu wa miaka hii ni afadhali ukutane na mwanafunzi wa kidato cha tatu wa miaka ya tisini.

Yaani ni shida. Elimu imeporomoka sana

-
Hata kama imepolomoka si kwa kiwango unachokisema . Uwe muelewa basi. Kwamba unataka nikubali wanafunzi wanakuwa vilaza kana kwamba Wana baki na Zero intelligence.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom