Kikao cha kuunda TANU nyumbani kwa Hamza Kibwana Mwapachu - Nansio, Ukerewe 1953

Swali najiuliza Nyerere alikuwa na karama zipi za ziada ambazo zilisababisha wazee wa kiislam wang'ang'ane kumpa uongozi ilhali alikuwa mgeni na asiyejulikana dsm kama unavodai, kwanini iwe Nyerere tu na wasiwe watu wengine hasa wale waanzilishi?...kuna upotoshaji wa makusudi toka kwako
 
Naona mzee Saidi anajitahidi sana kutaka kuiandika upya history kwa kupotosha. Anataka kuonesha kwamba Nyerere hakupata uongozi kwa uwezo wake bali kwa kupewa kama hisani na wazee wa kiislam.
Kweli, anachotaka ni kumdogosha Nyerere , na kuwapa sifa akina Abdul Sykes kwamba walifanya kazi kubwa kudai uhuru zaidi ya Nyerere....Ukweli ni kwamba waislamu akiwepo Abdul Sykes walianzisha chama chao cha kiislamu (AMNUT) tena ofisi zikiwa nyumbani kwa Abdul Sykes,....Ulitegemea Nyerere angefanyaje zaidi ya kuwaondoa kwenye TANU?
 
Vito,
Shida yote hiyo inipate kwa kutaka kitu gani au nithibitishe nini?
Nataka tudhibitishe kwamba TAA hakikuwa chama cha siasa, bali TANU ndio ilikuwa chama cha siasa...kwanza TAA haikuwa na katiba, ndio maana TANU walienda kukopy katiba ya chama chao kutoka chama cha GHANA.
 
Vito...
Nimekueleza sheria za uandishi ni nukta tatu...

Huijui historia ya TANU wala huijui historia ya AMNUT.

Ushauri wangu kwako ni jifunze kwanza historia ya vyama hivi.

Haipendezi wewe kuandika mambo ya uongo.

Haipendezi pia mimi kujadili historia ya Tanganyika na mtu asiye na elimu ya somo tunalojadili.

Waasisi wa AMNUT ni Ramadhani Mashado Plantan na Abdallah Mohamed.

Abdul Sykes maisha yake yote alikuwa mwanachama wa TANU mwenye kadi no. 3.

Ofisi ya AMNUT ilikuwa Libya Street na iliposhindwa kulipa kodi ikahamia Mtaa wa Narung'ombe.

Endapo ningeandika kitabu kwa madhumuni ya kumdogosha Nyerere kitabu cha Abdul Sykes kingekufa zamani sana.

Kitabu hiki sasa kipo sokoni miaka 24 na kinakwenda chapa ya tano kuwa ni kitabu kilichoeleza ukweli kadri ilivyostahili kuelezwa.
 
Abbass alikuja kuwa Mh. Balozi nazani...
 
Nataka tudhibitishe kwamba TAA hakikuwa chama cha siasa, bali TANU ndio ilikuwa chama cha siasa...kwanza TAA haikuwa na katiba, ndio maana TANU walienda kukopy katiba ya chama chao kutoka chama cha GHANA.
Vito...
Umepata wapi kuwa TANU ilinakili katiba ya CPP ya Kwame Nkrumah?
 
Vesuvius...
Hapakuwa na mzee yeyote katika kamati ya ndani iliyoasisi TANU ukimtoa John Rupia.

Wakati Abdul anajuana na Nyerere 1952 Abdul alikuwa na umri wa miaka 28 na Nyerere miaka 30.

Lakini Abdul alianza mazungumzo ya kuunda TANU mwaka wa 1950 akitaka Chief David Kidaha Makwaia aongoze harakati za kudai uhuru.

Kama kuna mtu alinga'anga'niwa mtu huyo ni Chief Kidaha si Nyerere.

Mimi sipotoshi kitu.

Nakueleza haya kutoka Nyaraka za Sykes sasa zina miaka inakaribia 100.

Wewe hujui.

Mimi najua yote na nimeandika kitabu na nimeshiriki katika uandishi wa Dictionary of African Biography (2011) na nimewaandika akina Sykes humo.

Ukitaka kujua mimi niko tayari kukufunza yote kuhusu historia ya TANU.

Anza kujifunza na vitabu hivyo uone tofauti kati ya waandishi hao na mimi.

 
Sijui Maalim, Naomba unifundishe.
Vito...
Historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika ni historia ya wazee wangu na inaanza mwaka wa 1929.

Mimi nimeandika historia ya wazee wangu na Mwalimu Julius Nyerere ameingia kwa kuwa alikuja Dar es Salaam ambako ndiko mimi nimezaliwa na kufahamiana na wazee wangu ambao ndiyo walianzisha harakati za siasa kupitia African Association.

Sikuwa mimi nililenga kuandika historia ya Mwalimu Nyerere.
Nyerere kaingia kama mmoja katika timu ya wachezaji waliopigania uhuru wa Tanganyika.

Kuandika historia hii ilikuwa kazi ngumu na ya kutisha kwani miaka ile kuandika chochote kinyume na kilivoelezwa na mamlaka ilionekana ni uasi na uhaini sikuambii kuandika historia ya Waislam katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Historia rasmi ya TANU ilikuwa tayari imeshaandikwa na haikutegemewa kuwa atatokea mtu kuandika historia kinyume na historia ya Chuo Cha CCM Kivukoni.

Laiti kama Sykes wasingenifungulia nyaraka zao kuzisoma historia ya kweli ya TANU iikuwa ishafutwa.

Earle Seaton alikuwa mshauri wa Abdul Sykes katika mambo ya Mandate Territories.
 
Nimeita wazee kwa muktadha maalum wa sasa bila kujalisha umri gani walikuwa nao wakati huo.

Pili, Hujajibu hoja ni turufu gani Nyerere alikuwa nayo hadi ikawa yeye kupendelewa kuwa mwenyekiti na sio hao wengine? Unajaribu kwa nguvu kukwepa hoja/ukweli kuwa Nyerere alikuwa ni mtu mwenye karama na kariba ya kipekee ilovuta uongozi kwake
 
Vesuvius...
Nimekueleza kuwa Abdul Sykes alianza mazungumzo na Chief David Kidaha Makwaia kuchukua nafasi ya TAA President waunde TANU.

Nadhani hili halikukupendeza na pengine hukupata kulijua.

Wengi wenu hampendezewi na ukweli kuwa harakati za kuunda TANU zilianza hata Nyerere hajafahamika Dar es Salaam.

Ndiyo mnakuja na "wazee" wa Nyerere na ambao hata majina yao hamyajui kueleza "karama" zake.

Kama kulikuwa na wazee katika kumuunga mkono Nyerere mbona mchango wa Sheikh Hassan bin Ameir Mufti wa Tanganyika hauelezwi au wa Mshume Kiyate?

Kama kweli ziko karama TANU isingesubiri iundwe nyumbani kwa Hamza Mwapachu katika kikao cha watu watatu - Hamza Mwapachu, Abdul Sykes na Ali Mwinyi Tambwe.

Hii mipango ikaendelea katika mikutano ya siri nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukuu nyumba ambayo Nyerere alikwenda kuishi baada ya kuacha kazi ya ualimu?

Nyerere inaelekea hakuipenda historia hii na ndiyo maana ikafutwa.

Wengi historia ya kweli ya TANU inakutaabisheni.

Aliyekwepa ukweli wa historia ya TANU kwa nguvu si mimi.

Mimi nimekuja hapa na historia ambayo wewe kwa mara yako ya kwanza umeisikia kwangu.

Historia hii ni historia ya wazee wangu na nina haki ya kuieleza na kuilinda isivurugwe.
 
Hii historia ni nzuri lakini swali langu ni je kuna maslahi yoyote labda watu hawa walistahili hawakupata au ushindani ni wa nini labda?

Au Nyerere hakustahili sifa zote anazopewa kama Baba wa Taifa?
 
TANU wasingeweza kuandika kuhusu Mufti Hassan Ameir, aliefukuzwa Tanganyika kwa sababu za kueneza chuki za kidini na kuwagawa wananchi.....Utaandikaje historia ya mtu kama huyo? Hata historia ya Oscar Kambona imefutwa kwa makosa yake ya UHAINI....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…