Kikwete azindua mradi wa Umeme uliojengwa na Kanisa Katoliki

Kikwete azindua mradi wa Umeme uliojengwa na Kanisa Katoliki

Hongera zao wakatoliki kwa hilo suala la maendeleo, lakini chondechonde Kikwete, hizo ahadi unazoahidi kila uchao, watu wanaandika umesema ajira 8,000 ingawa hujafafanua, zisije kukutokea puan i siku moja. Lakini mbunge wa huko jasiri kumwambia leo huko ndiyo wanapata uhuru, kwahiyo miaka 50 ya uhuru huko haipo, safi sana kuwa mwazi.
 
Are you familiar with research hypothesis. Jibu la swali la mhusika liko katika swali linalouliza Je serikali ya Tanzania haina dini? Sasa chunguzeni matendo yenu mjijibu ila waislamu washawatambua kitambo humdanganyi mtu. Ndio maana wazanzibar hao wanawakimbia tutabakia na Tanganyika yetu tukabane mashati.
Kimsingi waislamu hawana cha kumfanya raisi aje akifungue.......... wao kila kukicha kodi zinaibwa na wakristu lakini hakuna anayekwenda mahakamani kuwashitaki hao wakristu kwa wizi wanaousema........ WAMECHUKULIWA KIWANJA PALE KIBASILA (MCHICHA) WAPO KIMYAAA MPAKA SASA.......... Na kwa jinsi wanavyopeleka mambo yao hovyo USISHANGAE UPANUZI WA BARABARA NYINGI UNAHUSISHA UBOMOAJI WA MISIKITI.... They dont plan ujenzi .... they dont see next 20 years kama hapo wanapojenga patapita barabara e.g msikiti wa mtoni mtongani........
 
Hongera Kanisa Katoliki lakini tusifanye hii issue ni ya kidini ndugu zangu...

Ni Tanzania kila mtu ana haki, yeah wanataka Kadhi lakini rais kasema hapana;

Tufurahie huu Umeme utanufaisha wote hautajali Dini, Rangi, Kabila...

Asante nngu kwa kuliona hilo. Masuala ya dini yawekwe pembeni. Mradi huu unanufaisha wote bila kujali wanaabudu wapi.
 
Huyo Bwn Mkandara kafanikiw kuyumbisha mada, badala ya ku concentrate kwenye swala lamsingi la uzinduzi wa mradi wa umeme ameelekeza kwenye negative attitude ya CCM na wana maghamba's!!!!!!!!!! Wacha wivu watu wakijituma kusaidia Watanzania wapewe pongezi sio hujuma na kupotosha watu!!!!!!!!!!!
Anaweza kuwa kafanikiwa in one way or the other, lakini kila alichouliza kajibiwa ila NAMSIFU KWA UBISHI...............
 
@Mkandara, labda tukuabaliane kwanza kwamba ni kitu gani hasa kinaifanya serikali/nchi iwe ina dini, au secular? Kwa uelewa wangu ni sheria mama yaani Katiba. Katiba ndiyo inayotoa mwongozo kwamba nchi itaendeshwaje na haki za watu ni zipi etc etc.

Na ili mtu awe ametenda kosa ni lazima kwenye sheria mama kuwepo na kifungu kinachosema hivyo. Kwa mfano nchi zinazongozwa na SHARIA kama IRAN na Saudia, ndani ya sheria zao wanaruhusu watu wa dini nyingine kuabudu kivyao (with specific instructions). Pombe ni haramu na ukikamatwa unakunywa pombe hadharani hata kama wewe ni mkristo utachukuliwa hatua kwa sababu sheria za nchi hazirusuhu. Kama watakufumbia haimanishi hujavunja sheria maana sheria ipo inayokataza kufanya hivyo.

Hivyo basi, ili kuwepo na kosa, lazima katiba iwe imetamka kwamba kufanya jambo fulani ni kinyume na sheria za nchi. Sasa ni kifungu gani cha sheria kinachokataza serikali kushirikiana na taasisi za dini katika kutoa huduma za jamii?
Mkuu sijui unaandika kutokana na jinsi unavyofikiria wewe au kweli umezisoma katiba za Iran na Saudia. Katiba yao haisemi kunywa Pombe ni haramu isipokuwa inafuata Sharia Law na katika kutafsiri Sheria hizo, wanasheria na mahakama hutumia vifungu vya sheria (act) ambavyo sii lazima vimeandikwa ndani ya katiba mama with specific instructions kama madai yako. Narudia kusema hakuna katiba mama inayosema Pombe ni haramu (Iran na Saudia) wala hapa kwetu Tanzania hakuna mahala ktk katiba mama imeandika Ushoga ni haramu na kutoa specific instructions...Hilo kwanza.

Katiba imetamka kwamba serikali yetu haina dini na nimewauliza ina maana gani ktk usemi huu - hadi sasa hivi mnazungusha huku na kule kujibu hamtaki na kama kweli wewe mpenzi wa haki tuirudie katiba na kuitafsiri ipaswavyo na sii kulazimisha kudai katiba mama lazima iseme kwamba ni haramu kushirikiana na vyombo vya dini. halafu mnaipotosha maana swala sio kushirkiana serikali inaweza kushirikiana na chombo chochote kile isipokuwa kuunda Partnership na chombo kimoja cha dini kwa kutumia kodi zetu hii ndio hoja yetu ambayo nina hakika inatokana ana muafaka wa MoU.. na tunasema muafaka ule ulikuwa makosa makubwa ya kiutawala..

Mnachobisha nyie ni sawa kabisa na sisi enzi zile za Nyerere, kutaifisha mali za watu, means of production kuhodhiwa na serikali kisha mnakataa kwamba sisi sio Ma- Communist kwa kutafuta tofauti zetu na Ukomunist wakati mnaupiga vita Ubepari kwa hali zote!. Kifupi nitakwambia hivi Usocialist upo karibu sana na Ucomunit kuliko Ubepari hivyo Bepari akisema wewe Mcommunist bora kwanza kubali kisha elezea tofauti zako na Mkominist lakini kwangu mimi hawa ni walewale - Nyani na Ngedele...Yanayofanyika sasa hivi serikali ipo karibu sana na kanisa kiasi kwamba inafungamana na kanisa na kuunda Partnership which is very wrong!

Mfumo wa kiutawala unavyofanywa sasa hivi na CCM ambayo maajabu wanaChadema mnaichukia mnakubaliana na sera hizi za CCM jambo ambalo kisiasa linanifanya nijiulize kwa nini nyie sio CCM ikiwa sera za Udini zinazopendelea kundi moja mnazikubali?.. Halafu kesho mtaanza tena kumtukana JK wakati anatimiza wajibu wenu kama mnavyotaka. Wakati huo huo Waislaam nao wanampa support JK ambaye anazidi kuwagawa na kuwakandamiza. Hizi siasa zenu kama sio Unafiki tena ktk imani za dini kitu gani?...
 
Muzee uzee unakuingia vibaya au? weekend ilikuwa ndefu kidogo, hapo ni kwamba serikali kutokana na ukwasi walishindwa kufanya huo mradi ndio kanisa likaona kwamba linaweza kuinvest sasa kama wamekosea basi tuwasome fatwaa

Acha ujinga ndugu soma mradi umefadhiliwa na nani,
kanisa Katoliki jimbo la Njombe linatekeleza mradi huo kwa ufadhili wa shirika lisilo la kiserikali la ACRA.

Aliwataja wahisani wengine kuwa ni wizara ya mambo ya nje ya Italia,mkoa wa Lombaridia-Ilaty,Itervita,Foranzione Cariplo na umoja wa nchi za Ulaya
 
...Katiba imetamka kwamba serikali yetu haina dini na nimewauliza ina maana gani ktk usemi huu - hadi sasa hivi mnazungusha huku na kule kujibu hamtaki na kama kweli wewe mpenzi wa haki tuirudie katiba na kuitafsiri ipaswavyo na sii kulazimisha kudai katiba mama lazima iseme kwamba ni haramu kushirikiana na vyombo vya dini. halafu mnaipotosha maana swala sio kushirkiana serikali inaweza kushirikiana na chombo chochote kile isipokuwa kuunda Partnership na chombo kimoja cha dini ni sawa kabisa na sisi enzi zile kutaifisha mali zote, means of production kuhodhiwa na serikali kisha mnakataa kwamba sisi sio Ma- Communist kwa kutafuta tofauti zenu na Ukomunist wakati mnaupiga vita Ubepari kwa hali zote....
Mkandara hilo la maana ya serikali kutokuwa na dini limeshajibiwa mara kadhaa kwenye thread hii. Labda useme majibu hayo hayaendani na vile unavyotaka wewe, in which case inabidi wewe ndio utumabie hiyo maana unayotaka au unayoona ni sahihi.

Labda tujaribu kurudi kwenye hoja/habari ya msingi...JK amefungua mradi wa umeme huko Njombe ambao umeasisiwa na kanisa katoliki likishirikisha wadau mbalimbali (wakatoliki na wasio wakatoliki). Labda sasa ufafanue hoja yako ya kikatiba ya serikali kutokuwa na dini (au serikali kuwa na dini, for that matter!), katika muktadha wa mradi huu wa umeme. Hii itasadie tuwe na mjadala unaoeleweka badala ya ku 'flip flop' kwenye manung'uniko kadhaa ya waislamu wa Tanzania.
 
Acha ujinga ndugu soma mradi umefadhiliwa na nani,
kanisa Katoliki jimbo la Njombe linatekeleza mradi huo kwa ufadhili wa shirika lisilo la kiserikali la ACRA.

Aliwataja wahisani wengine kuwa ni wizara ya mambo ya nje ya Italia,mkoa wa Lombaridia-Ilaty,Itervita,Foranzione Cariplo na umoja wa nchi za Ulaya
Unajua watu wengine hata kufikiri kwao kuna kikomo..inasikitisha sana. Hivi tuliwakataa Richmond kwa sababu gani? nipeni sababu zote ambazo tuliwakataa Richmond hata kiutaalam kisha tutazame je kanisa lina sifa hizo za uzalishaji umeme? Jamani why kanisa lizalishe umeme na kuuza kwa wananchi - I guess ndio Taasisi ya kwanza nchini kupewa nafasi hiyo..
Hivi kweli kuna tofauti na Utawala, tukitumia sababu ya kutoa huduma kwa wananchi wote!
Basi bora wapewe nchi kabisa, watawale lijulikane moja..
 
Mkandara hilo la maana ya serikali kutokuwa na dini limeshajibiwa mara kadhaa kwenye thread hii. Labda useme majibu hayo hayaendani na vile unavyotaka wewe, in which case inabidi wewe ndio utumabie hiyo maana unayotaka au unayoona ni sahihi.

Labda tujaribu kurudi kwenye hoja/habari ya msingi...JK amefungua mradi wa umeme huko Njombe ambao umeasisiwa na kanisa katoliki likishirikisha wadau mbalimbali (wakatoliki na wasio wakatoliki). Labda sasa ufafanue hoja yako ya kikatiba ya serikali kutokuwa na dini (au serikali kuwa na dini, for that matter!), katika muktadha wa mradi huu wa umeme. Hii itasadie tuwe na mjadala unaoeleweka badala ya ku 'flip flop' kwenye manung'uniko kadhaa ya waislamu wa Tanzania.
Alojibu tulimalizana na hakurudi tena nataka wewe jibu lako kisha tujadili tu kuhusu katiba na sio vinginevyo..maanake toka nimemjibu hamkurudi tena mkabadilisha hoja ikawa Mkandara mkimbizi..Makosa sio kufungua mradi huu kwa sababu muafaka wa MoU unawapa sheria kama ulivyotokea Muafaka wa CCM na CUF walipomaliza kupitisha na wakaunda chama chao nje kabisa ya kuvishirikisha vyama vingine. Na ndio maana leo mnawaita CUF ni CCM - B... Mtazamo ni ule ule haubadiliki ktk swala hili la kanisa na CCM.
 
Unajua watu wengine hata kufikiri kwao kuna kikomo..inasikitisha sana. Hivi tuliwakataa Richmond kwa sababu gani? nipeni sababu zote ambazo tuliwakataa Richmond hata kiutaalam kisha tutazame je kanisa lina sifa hizo za uzalishaji umeme? Jamani why kanisa lizalishe umeme na kuuza kwa wananchi - I guess ndio Taasisi ya kwanza nchini kupewa nafasi hiyo..
Hivi kweli kuna tofauti na Utawala, tukitumia sababu ya kutoa huduma kwa wananchi wote!
Basi bora wapewe nchi kabisa, watawale lijulikane moja..

Huu sasa ni wivu, kwani wengine walianzisha project kama hii wakazuiwa?
 
Humu kuna watu wanaugua udiniasis! Poleni sana maana virusi vya huo ugonjwa havina dawa zaidi ya kufikiri nje ya ugonjwa wenyewe!
 
Kimsingi waislamu hawana cha kumfanya raisi aje akifungue.......... wao kila kukicha kodi zinaibwa na wakristu lakini hakuna anayekwenda mahakamani kuwashitaki hao wakristu kwa wizi wanaousema........ WAMECHUKULIWA KIWANJA PALE KIBASILA (MCHICHA) WAPO KIMYAAA MPAKA SASA.......... Na kwa jinsi wanavyopeleka mambo yao hovyo USISHANGAE UPANUZI WA BARABARA NYINGI UNAHUSISHA UBOMOAJI WA MISIKITI.... They dont plan ujenzi .... they dont see next 20 years kama hapo wanapojenga patapita barabara e.g msikiti wa mtoni mtongani........

Wana JF wenzangu naamini MUNGU alitupatia dini kusaidia kufanya mahusiano yetu na maisha kwa ujumla yawe na maadili ambayo msingi mkubwa ni kuvumiliana (katika tofauti zetu kiimani na kimawazo) na kusihi kama ndugu kuifanya dunia mahala pema na pazuro zaidi kuishika.

Makelele yenu ya dini X ina hiki, diniY wanafanya hiki ambacho ni haramu n.k. Yanaharibu maana yetu nzima ya kuwa waumini wa dini tunazojifanya twaziamini na kuenzoi kuliko hata founders wake!
 
Alojibu tulimalizana na hakurudi tena nataka wewe jibu lako kisha tujadili tu kuhusu katiba na sio vinginevyo..maanake toka nimemjibu hamkurudi tena mkabadilisha hoja ikawa Mkandara mkimbizi......
Nilishajibu post #46! Tujadili kuhusu katiba katika muktadha wa mradi huu wa umeme...vinginevyo tutakuwa tunaendelea kuiharibu hii thread.

Hilo la ukimbizi hata kama lipo, sikulitoa mimi na kwa maoni yangu halina mchango katika hoja hii. Pengine aliyeliibua ilikuwa ni reaction ya kuona ati mtanzania wewe unajivunia kukaa nje ya Tanzania (nchi za kikristo!) kwa muda mrefu! Anyway tuweke hili kando ni siasa za majitaka tu.

...Makosa sio kufungua mradi huu ....
Kumbe tatizo la kikatiba ni nini hasa juu ya mradi huu?
 
Mfumo kristo yaani sisi hata hospital ya wilaya hatuna wenzetu wanazalisha umeme ?.


GO9G8317.JPG




Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe (kushoto) na aliye kulia kwa Mbunge Deo ni ambaye amevaa shati jeupe lenye roman collar ni Askofu wa jimbo katoliki la Njombe, Mhashamu Alfred Maluma, mara baada ya kutua mkao makuu ya tarafa ya Mawengi Ludewa kufungua mradi wa umeme ulioasisiwa na kuendeshwa na Kanisa Katoliki kupitia Parokia ya Madunda.



nj+(32).JPG





Aliye katikati ya Rais Kikwete na First lady Mama salma, ambaye ana shati jeupe lenye roman collar ni Askofu wa Jimbo Katoliki la Njombe Mhashamu Alfred Maluma. Ni mchezaji mzuri sana wa mpira wa miguu, na siku za nyuma kabla hajateuliwa Na Pope kuwa Askofu akiwa jimboni Njombe kwa kushirikiana na Padre Chaula mkurugenzi wa vijana, alianzisha timu ya mpira wa miguu kutokana na umoja wa vijana katoliki Njombe (UVIKANJO) timu ambayo ilipanda daraja hadi kucheza Ligi kuu na ilizoeleka kuitwa timu ya Baba Askofu, wakati huo askofu wa jimbo la Njombe alikuwa Askofu mstaafu Raymond Mwanyika. Timu hiyo ilisuasua wakati Mhashamu Alfred Maluma alipohamishiwa Peramiho Songea kuwa Rector (gombera) wa Serminari Kuu Peramiho ambako uteuzi wa kuwa askofu ulimkuta akiwa instructor wa Seminari hiyo baada ya kuhitimu chuo kikuu cha Rome, Italy, alikosoma Dr. Slaa.








RAIS KIKWETE APONGEZA KANISA KWA MRADI WA UMEME ,ATAKA WANANCHI KULIPA BILI KWA WAKATI


RAIS Jakaya Kikwete amelipongeza kanisa la Romani Katoliki jimbo la Njombekwa kusaidia serikali kutatua tatizo la umeme kwa wakazi wa kijiji cha Mawengiwilaya ya Ludewa huku akiwataka wananchi kuendelea kutunza nyanzo vya maji ilikuwezesha maradi huo wa umeme wa gharana nafuu kwa wananchi kuendeleakusambazwa zaidi katika vijiji vingine vya wilaya ya Ludewa kwa msaada wa kankisa hilo.Akiwahutibia wananchi wa kata ya Mawengi mara baada ya kuzindua mradi wa umeme wa Lumama Electrical Asosoation jana ,Rais Kikwete alisema kuwa hatari ya maradi huu kufa itasababishwa na wananchi wenyewe wa kata hiyo iwapohawatatunza vyanzo vya maji na kusababisha mradi huo ambao unategemea zaidi maji ili kuendeshwa kushindwa kufanya kazi kwa uhakika .


“Waswahili wanasema hivi kitunze kidumu ,kitunze kikutunze ….sasa nawapongeza mmeanzisha chombo chenu cha kusimamia mradi Lumama …..sasa nawaombeni Lumama iendelee kusitawi ili kuhakikisha mazingirahayaharibiwi na maji yanaendelea kuwepo kwani kama vyanzo vya maji vitaharibiwabasi mradi utakufa….pamoja na kuwa maji haya ni neema ya Mungu ila Mungu ametua maarifa ya kuvitawala vyanzo hivyo ili vidumu zaidi kwa kutumia kanunizinazotawala mazingira ili yaendelee kuwepo” Hivyo aliwataka wananchi kupitia umoja wao wa Lumama kuhakikisha wanatunzavyanzo vya maji kwa kutoharibu ovyo mazingira , kuchangamkia fursa hiyo kwakuingiza umeme katika nyumba zao huku akiwakumbusha kulipa bili kwa wakati . Aidha alisema kuwa serikali kupitia shirika lake la huduma ya umeme vijijiniitaendelea kusaidia mradi huo ili uweze kusonga mbele zaidi na kuwanufaishawananchi wengi .


Rais Kikwete pia aliwahakikishia wananchi na wahisani hao kuwa serikaliimeendelea kutoa mchango wake katika mradi huo na itaendelea kuaunga mkonojitihada za kanisa hilo na wahisani wake kwa kusaidia fedha zaidi kwa awamu ya pili ili kuwezesha mradi huo kujitanua zaidi. Alisema kuwa hadi sasa makao makuu ya wilaya ya Ludewa kuna umeme wa Genereta ila bado mkakati wa serikali ni kuiunganisha wilaya hiyo ya Ludewa na umeme wa uhakika wa Gridi ya Taifa ambapo kazi hiyo kubwa mchakato wakeunaandaliwa. Pia alisema kuwa mkakati mwingine wa serikali ni kupeleka umeme wa gridi yaTaifa wenye uwezo wa KW 232 kutoka Makambako wilaya ya Njombe kuelekeaSongea mkoni Ruvuma na kuwa umeme huo utapoonza madaba ili kufikia KW 11na baada ya hapo wananchi wa vijiji vya Ndolela ,Mkongobaki, Shauri moyo ,Mavanga , Mndindi ,Lugarawa ,Mbwila,Mkiu ,Mlangali na Luana . Alisema kuwa wananchi wa kata hiyo ya Mawengi mbali ya kuwa na mradi huo wa umeme wa Lumama bado serikali ipo katika mchakato wa kupitisha umeme wa gridi ya Taifa utakaotokea katika kituo cha Madaba na kupitishwa katika maeneo yao kwenda makao makuu ya wilaya.


Rais Kikwete kabla ya kufika katika kijiji hicho alizuiwa na wananchi wa kijiji cha Mlangali kata ya Mlangali ambao waliziba barabara na kulazimika kusimama kuwasikiliza na kujibu madai yao mbali mbali likiwemo na kuchelewa kufika kwa gari la wagonjwa ambao alipata kuwaahidi wakati wa kampeni ,tatizo la soko la Mahindi kusimama na kero ya maji ambapo aliwahakikishia kuwa malalamiko hayo yatafanyiwa kazi na majibu ya madai yao atampa mbunge wao Deo Filikunjombe iliawafikishie. “kwanza niwashukuru sana wananchi wa Ludewa kwa kukichagua chama cha mapinduzi (CCM) na kumpitisha mbunge wenu Deo Filikunjombe bila kupingwa ….sasa nawahakikishieni madai yenu yatafanyiwa kazi na kuhusu soko la mahindi wiki ijaya fedha za kununua mahindi zitakuja hapa”


Kuhusu liganga na Mchuchuma Ludewa ,Rais Kikwete alisema kuwa sasa umefikawakati wa kuanza kutekeleza mradi huo kwa kampuni kutoka nchi ya China ambaokuanzia wiki ijayo wawekezaji hao watafika na kuanza kutekeleza mradi huo na ajira 8000 hivyo kuwataka vijana kuacha kuhoji juu ya maisha bora na badala yake kwenda kuomba kazi . Hata hivyo alisema barabara ya lami ya uhakika na Reli kwa ajili ya kupitisha makaa ya mawe na chuma kutoka wilaya ya Ludewa na kwenda kuyauza nchi za nje mkakati wake kuanza kuandaliwa . Alisema kuwa kila jambo lina wakati wake na kuwa sasa ni zamu ya wilaya ya Ludewa kubadilika kimaendeleo .



Awali mbunge wa jimbo hilo la Ludewa alimweleza Rais Kikwete kuwa pamoja naTaifa linasherekea miaka 50 ya Uhuru ila wakazi wa wilaya ya Ludewa wao baada ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika mwaka huu chini ya utawala wa RaisKikweye ndio wanapata uhuru wao baada ya kuwa na uhakika wa barabara ya lami na kuanza kuchimbwa kwa mradi wa Lingana na mchuchuma.

Kwa upande wake meneja wa mradi wa umeme wa Lumama Alice Michelazziakisoma taarifa ya mradi huo mbele ya Rais Kikwete alisema kuwa mradi huo ulianza toka mwaka 1998 kwa kufanyiwa utafiti uliogharimu kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 8.900. Hata hivyo alisema kuwa shughuli za mradi kwa sasa ni kujenga mtambo wa kuzalisha umeme wa kiasi cha KW 150 ambao tayari umekamilika mwaka 2010 nakuwa kanisa Katoliki jimbo la Njombe linatekeleza mradi huo kwa ufadhili wa shirika lisilo la kiserikali la ACRA.

Aliwataja wahisani wengine kuwa ni wizara ya mambo ya nje ya Italia,mkoa wa Lombaridia-Ilaty,Itervita,Foranzione Cariplo na umoja wa nchi za Ulaya
 
Mkandara swali kama hili sikutarajia litoke kwako ?.

Ndio makosa yanayofanywa kiutawala sasa iwe mfumokristu ama nini lakini swala la UMEME kuendeshwa na jumuiya za kiimani huoni kama serikali ina dini?.. mimi naomba mtu aje hapa anambie hasa maana ya kusema serikali haina dini ikiwa leo Umeme ambao serikali ina wizara yake wanashirikiana na kanisa kufungua nguvu hizo, tena akiwaagiza wananchi walipe bill za umeme huo mapema.
Nipeni maana ya neno hili -Serikali haina dini - MAANA TU, halafu tuendelee..
 
Alojibu tulimalizana na hakurudi tena nataka wewe jibu lako kisha tujadili tu kuhusu katiba na sio vinginevyo..maanake toka nimemjibu hamkurudi tena mkabadilisha hoja ikawa Mkandara mkimbizi..Makosa sio kufungua mradi huu kwa sababu muafaka wa MoU unawapa sheria kama ulivyotokea Muafaka wa CCM na CUF walipomaliza kupitisha na wakaunda chama chao nje kabisa ya kuvishirikisha vyama vingine. Na ndio maana leo mnawaita CUF ni CCM - B... Mtazamo ni ule ule haubadiliki ktk swala hili la kanisa na CCM.

Hivi kama ni kweli kanisa na ccm wana mou yenye uelekeo unazungumzia wewe kwa nini bakwata ni pro ccm? Si wangeisusa hiyo ccm?
 
Wana JF wenzangu naamini MUNGU alitupatia dini kusaidia kufanya mahusiano yetu na maisha kwa ujumla yawe na maadili ambayo msingi mkubwa ni kuvumiliana (katika tofauti zetu kiimani na kimawazo) na kusihi kama ndugu kuifanya dunia mahala pema na pazuro zaidi kuishika.

Makelele yenu ya dini X ina hiki, diniY wanafanya hiki ambacho ni haramu n.k. Yanaharibu maana yetu nzima ya kuwa waumini wa dini tunazojifanya twaziamini na kuenzoi kuliko hata founders wake!

Nakubaliana na wewe 100%
 
Narudia kuuliza hili swali
Tatizo la Tanzania nini?
  • Ni "kanisa"?
  • Ni kanisa Katoliki?
  • Ni wakristu ?
  • Ni baadhi tu ya wakirstu?
  • Ni baadhi ya waislam?
  • Ni baadhi ya wakristu na baadhi waislam
  • Ni baahi ya watanzania?
BTN
Inakuwaje kuna watu hawana aibu wanatumia jina la nyerere negatively kwenye thread hii na wakati huo huo huo wanashindwa kupata ujasiri wa kumtaja Jakaya Mrisho (Positvey au Negatively) amabaye kwenye Movie hii ni kati ya masterling wakuu
. Alafu mtu kma huyo ndiyo analijua tatizo.
 
Hivi kwani Waislam wamezuiwa kuomba misaada SAUDIA ili wafanye mambo ya maendeleo? Siamini kama Mashirika na watu binafsi UAE watakataa kufadhili miradi ya waislamu wenzao, naamini misikiti ikaweka masheikh wasomi wakaandaa proporsal zenye akili-hasa katika miradi ya viwanda vya siraha kama mabomu na bunduki watapata tu wadhamini!!!! Taratibu vidole na macho jamani, hii miradi inatunufaisha wote bila kujali mimi m-protestanti, shangazi yangu muislam au mjomba yangu mkatoliki; sote tunatibiwa kwenye Hosptitali za hawa jamaa, na watoto wetu wanasoma Vyuo vyao biila ubaguzi..hata huu umeme wao ukiunganishwa kwenye gridi ya taifa wallah Ustaadh Jumaa atafurahia kuwasha kijilaptop chake na watoto kuangalia TV bila kujali umeme wa warumi!!!
 
Kama Mrisho Kikwete, Nazir karamagi , nk na wenyewe ni shemu ya so called mfumo kristo au kanisa au Kanisa katlolkii then that name is used to mislead People.
Je kwa nini wanawa mislead watu?
 
Back
Top Bottom