Kikwete, huu mtandao ni hatari! Be careful, otherwise waweza kuwa historia (Part 1)

Kikwete, huu mtandao ni hatari! Be careful, otherwise waweza kuwa historia (Part 1)

Kwa mtandao huu unaotajwa, maombi yangu kila siku ni kuomba wafanikiwe ku'lobby hadi hatimaye EL apendekezwe kuwa mgombea pekee!

Hapo hakika mbingu zitakuwa zimefunguka, na Mungu kusikia sala za wanyonge!

Huyu mtu hata kama ana fedha kiasi gani, hata kama ana uwezo wa kumhonga kila Mtanzania milioni 50, bado hawezi kununua fikara za Watanzania, japo si wote!

Mungu atujalie uhai, somewhere in 2014 ataamua kukatiza safari yake hiyo na kujikita kumsaidia mtu fulani, ambapo pia itakuwa ni aibu tupu, mbinu zake zitadhihirika!
 
Huna Address ya Magogoni? Kikwete huwa hachungulii huku akipita anaweza kufa kwa presha za humu JF.
MKUU, Si yeye tu, hata mimi nimeanza kusikia roho ikiuma. Mtoa hoja amalizie yale mengine anayoyajua ili tuone jinsi ya kuokoa jahazi mapema. Kama ukitoboa jahazi au ukimwona abiria mwenzako anatoba jahazi ulilomo na wewe ukanyamaza basi bila shaka umeridhia kuzama nalo.
 
CHADEMA wanajidanganya. Nakubali ndio watashinda kula za urais, hilo halina ubishi, ila EL ndiye atakayeapishwa kuwa rais.
Wasichojua ni kwamba, unaweza kulinda kura za udiwani na ubunge, lakini za Uraisi ni ngumu sana.

kama haya kweli yanaweza kufanyika, then kwa nini tuingie gharama za kufanya uchaguzi every five years? all in all, it is high time wasanii wetu wajitokeze kuandaa tamthiliya kali spanning over a number of generations (kama Godfather vile) based on these machiavellian gimmics
 
Lakin nawe upo kwenye mtandao
Wakuu naona nimeulizwa maswali mengi Sana ila nitajibu kwa ujumla.
Suala la Shein liliamuliwa na CC ya CCM na sio kingmakers. Kwahiyo story hapo juu ni uongo mtupu!

cha pili kuuana sio kweli ni mandikaji kutumia Mwakyembe na Mwandosya kuugua na kuunganisha story.

mchunguzi names calling will not help you. Thanks to people who know me, mie sio wa kununuliwa labda nimnunue mie Lowassa. Soma soma humu utaona watt wanaonifahamu wananikubali sio wa kununuliwa mie kaka.

Mchunguzi nenda kwenye PM nikueleze kwanini namkubali Lowassa, tujadiliane huKo mpaka mwisho. achana na magazeti kaka na mtandao.
 
Siamini kama huu ni udaku, ila hata udaku huwa na kweli.

Naamini Mengi ni kweli, Maana UWT huwa wanapenda kuongeza chumvi ili story isomeke mpaka mwisho...
 
CHADEMA wanajidanganya. Nakubali ndio watashinda kula za urais, hilo halina ubishi, ila EL ndiye atakayeapishwa kuwa rais.
Wasichojua ni kwamba, unaweza kulinda kura za udiwani na ubunge, lakini za Uraisi ni ngumu sana.
Na ndio juhudi zinafanyika ili wanajeshi, askari, usalama wa taifa na wengine wote walio sehemu nyeti wapate elimu ya kutosha na kuacha kupokea amri ovu hata kama akili zao zinaona hivyo.

Hilo somo ndio kwanza limeanza na litakuwa more structured as time unfolds. Ikifika 2015 hamtawadanganya tena na hapo ndipo akina Pasco na kundi lake la mafisadi hawataamini. Ni kama mvua zilizoleta maafa Dar, mabadiliko hayazuiliwi!!
 
Mkuu BAK, FP is right kutumia PM kwa mambo mengine, safari ya kuelekea 2015 ni safari ya kweli na timu za ukweli zipo, na mbinu safi na chafu za ukweli zipo!.

Sasa kama mimi nimetokea kunusa mahali, watu wanakuotea vibaya wewe BAK, kama mtu makini, sitakuibukia open, nita ku PM.

Kwenye hili la Lowassa, kuna mahali FP anaposimamia, hata Mzee Mwanakijiji avyopafahamu, nae sasa anasimama na Lowassa!.

Msome Mkuu Mkandara post no 132 hapo juu, amesema nanukuu Lowassa "It's a blessing! - bring it on!". Sasa kwa wale wazito kabisa kuelewa, ni wa kueleweshwa kwa pm, adui akijua route yako, anaweza kukuzungukia na kukumaliza kwa ambush!

Pasco ana tactics za kitoto sana, eti anatutajia majina anayodhani ni makubwa JF kuwa wapo na Lowasa, anafikiri JF ni ya kufuata mkumbo kama alivyo yeye.

Personally naitaka Tanzania yenye neema and i do not see kwamba neema italetwa na wezi akina Lowasa et al. Ntabaki peke yangu na Mungu wangu napingana na uovu wao, na mimi na Mungu wangu tutashinda. Mark these words.
 
UPUPU wa kutaka kumchafua Lowassa na Rostam.

Hata mkifanyaje tunawajua wala hatushikiki. Good story telling though.
Hao walishajichafua wenyewe. Hakuna mtanzania anayeweza kupoteza muda kuwachafua zaid mana uchafu walionao unatosha kbs, sana sana ukitaka kuwachafua kwa uchafu walionao unaweza kuta na wewe unajipaka uchafu wao.
 
Mkuu The Boss,

Ni kweli Shein alipendekezwa na Mkapa kuwa Makamu wa Rais wa Mkapa mara baada ya kifo cha Dr. Omar Ali Juma. Ilipokuja zama za JK, JK tayari alikuwa na chaguo lake ambalo watu wa mtaani wanasema alikuwa ni Mama Zakhia Meghji. So, according to Hutaki Unaacha na redio mbao nyingine za mtaa wa pili, Dr. Shein hakuwa chaguo la JK bali alikuwa ni chaguo la Mkapa. Hoja ya Mkapa kwenye kumtaka JK amrithi Dr. Shein kama Mgombea Mwenza ilikuwa ni kwamba ingeleta picha mbaya kwamba the guy amefanya kazi muda mfupi halafu anakuja kurukwa na kupewa mtu mwingine.

Kwa nyongeza tu, hata uteuzi wa EL kuwa PM, Mkapa hakukubaliana nao. Chaguo la Mkapa ilikuwa ni John Pombe Magufuli.

It is very true kwamba Dr. Bilal haivi na Karume kwa kuwa zama za Komandoo Dr. Salmin Amour, Karume alipigwa panga na Komandoo ili Dr. Bilal aweze kuingia Ikulu ya Unguja. Uteuzi wa Dr. Bilal kuwa mgombea mwenza ilikuwa ni kunusuru mpasuko ambao ungetokea Unguja haswa baada ya Dr. Bilal kupigwa chini. Lakini linapokuja swala la politics, huwa hakuna permanent enemies wala permanent friends. Binafsi sioni connection yoyote kati ya Dr. Bilal na Karume.

Lakini ukisoma maelezo ya mtoa mada, mengine yana ukweli na mengine yana walakini. Muhimu kila mmoja anatakiwa kuchanganya na zake then anafanya conclusion kivyake.

Wewe kweli ni Great Thinker !
 
Mr President,

Ningekuwa na muda ningekueleza mengi sana. Muda wangu ni kidogo sana ndiyo maana nashindwa hata kupost mambo mengi kuhusu taifa hili hapa JF. Ninatuma post hii si kwa lengo la kukutisha. Lengo ni kukukumbusha uwe makini ili usijefanya uamuzi wa hovyo na kuliingiza taifa katika machafuko na kuharibu timetable za watanzania. Machafuko ndiyo tunayoyakwepa lakini si wewe (I have to tell you the truth because you are not my breadwinner at all).
We ndio ulipost kitu kama hiki kuhusu MEMBE!!!!!!!!!!!!!!!
 
Watanzania,

Hivi kweli mnapenda story za udaku namna hii?.

Kila siku huwa nasema na kusisitiza anzeni kufikiri kwa kutumia ubongo wenu acheni magazeti na mitandao kuwafikiria.

Ndio maana mnalialia kila kukicha maisha magumu, hayawezi kuwa raisi kama mnaamini story ya kutunga kama hiyo hapo juu.

Mdau inaonyesha wewe humu JF ujui lolote!!!!!!!!!!!!!!! .Kwa kuwa mtoa mada kalenga kutuongezea ufahamu wetu yale tunayojua wenyewe halisia tukachanganya na mbayuwayu wa JK jibu tunalo tunasubilia part tu tunendeleze kupigia mstari na kusubilia bomu liwapasukie wahusika watanzania yetu macho.

Hivyo wewe kaa kushoto otherwise wewe u mmoja wa wahusika,zako ziko jikoni wanakukaangia zikichemka utapewa,.
 
Hutaki Unaacha,

Kwanza asante kwa hii. Wanabodi hii mada si ya kupuuzwa hata kidogo bali ni uthibitisho tuu 2015 ni CCM ni Edward Lowassa na mgombea Mwenza Amani Karume, Rais wa Zanzibar ni Maalim Seif, Makamo wa kwanza ni Ismail Jussa!. Waziri Mkuu wa rais Lowassa bado sijamjua ila King Maker!, nimemvulia kofia!.

Waraka huu ni uthibitisho wa sisi tunaompigia debe Lowassa tuko right.

It's very very unfortunate rais Jakaya Kikwete kwa Mtandao wa Lowassa, yeye si lolote sii chochote!. Yaani hawezi kufanya lolote it's too late now!.

Waraka huu umenipa mwanga ambao sikuufahamu kabla, ni ile siri ya muafaka walikuwepo Jussa na Maalim Seif tuu na Karume!. Taarifa za Shein kutoshinda uchaguzi wa Zanzibar nilizisikia na siku ya kutangazwa matokeo nilikuwepo Zanzibar, kwa Seif ninayemjua mimi, sikupata picha alikubalije!. Sasa nimeelewa, anaerum CUF ni Jussa sio Seif na ndio maana Hamad Rashid kuonyesha interest ya Ukatibu Mkuu ataharibu na ikibidi watammaliza!.

Wapenzi wa JK samahanini sana kuwaeleza yeye si chochote si lolote mbele ya EL kuelekea 2015 kwa sababu kama ni King Maker alimweka pale Sitta na akamng'oa na kumweka Anne!. Then JK hana option zaidi ya kumuahidi EL ikulu 2015 vinginevyo mwakani baada ya uchaguzi wa CCM, EL atamtaja yule mwenye zigo la Richmond alilombebea na kupitia Bunge, impechment process will be initiated na ikisail through that is the end of the road kwa CCM!. Ila RA ataiback up CUF na sio Chadema ndio maana Jussa ni strategic link!.

Suluhu pekee kwa JK na CCM kubaki salama ni kumteua Lowassa ili asimwage mboga!.

Kwa kweli baada ya kuzisoma powers za King Maker, nami Pasco wa JF najiandaa kukaa karibu na wafalme ili japo ninukie manukato!.

Kwa waraka huu, Lowassa ndio tayari Mgombea, Dr. Bilal ni spent force atapumzishwa!.

Kwa wasiojua politics is a dirty game, wait and see for yourself as 2015 draws near!. Kitu ambacho sijafahamu ni jee watu safi kama Dr. Shein, Nahodha na Dr. Mwinyi zamu zao zitakuwa lini kuuonja urais wa Muungano au urais wa Tanzania kwa Mzanzibari ni nehi kimoja?.

Pasco wa jf.
Pasco Unataka kusema bomu la kumlazimisha JK asujudie kumsimamisha EL kuwa Rais ni lipi ilo ambalo Watanzania wa Chini wasilojua mchezo wa Richmond ilikuwa ni BLACKMAIL.
Tafuta hoja nyingine kuwahalalishia wanajamii forum nguvu za EL, wabongo mpaka wa mitaani kwenye vijiwe wanajua mmoja ALiBRACKMAIL mwenzie.Ndio maana limekuwa ni kaa linalochoma kila siku.sema jingine tusilojua.
 
Kwa mtandao huu unaotajwa, maombi yangu kila siku ni kuomba wafanikiwe ku'lobby hadi hatimaye EL apendekezwe kuwa mgombea pekee!

Hapo hakika mbingu zitakuwa zimefunguka, na Mungu kusikia sala za wanyonge!

Huyu mtu hata kama ana fedha kiasi gani, hata kama ana uwezo wa kumhonga kila Mtanzania milioni 50, bado hawezi kununua fikara za Watanzania, japo si wote!

Mungu atujalie uhai, somewhere in 2014 ataamua kukatiza
safari yake hiyo na kujikita kumsaidia mtu fulani, ambapo pia itakuwa ni aibu tupu, mbinu zake zitadhihirika!
God, grant me the serenity to accept the things I cannot change

Courage to change the things I can...

And wisdom to know the difference...
 
Hilo somo ndio kwanza limeanza na litakuwa more structured as time unfolds. Ikifika 2015 hamtawadanganya tena na hapo ndipo akina Pasco na kundi lake la mafisadi hawataamini. Ni kama mvua zilizoleta maafa Dar, mabadiliko hayazuiliwi!!
Chesty, mimi nakiri wazi, kuwatetea mafisadi kwa nguvu zangu zote, wengi wasionielewa vizuri, wanaamini utetezi wangu kwa Lowassa ni utekelezaji wa kazi niliyotumwa na mtandao wake, tena naifanya kwa ujira, hivyo hao mafisadi wakishatinga ikulu, angalau na mimi nikumbukwe kama alivyofanya Salva na ile kazi yake nzuri pale Mtanzania mwaka, 2005!. Kama hivi ndivyo nawe unavyoamini, sawa mimi na mafisadi dam dam!
 
Back
Top Bottom