Elections 2010 Kikwete on ITV, maswali na majibu toka kwake

Elections 2010 Kikwete on ITV, maswali na majibu toka kwake

Dola mil 7 kutibu waheshimiwa nje!mwananyamala hosp wazazi wanalala wa 3 kitanda kimoja
 
Yale Maswali tuliyotengeneza mchana hamkuyapeleka tena? Limeulizwa moja tu la kuwakampenia wale waliotuhumiwa kwa ufisadi.
 
Kinana haamini macho yake... he is dumbstruck...anatamani ardhi ipasuke.. anatamani hata amnyang'anye mic....
 
Ni AIBU RAIS HAJUI HATA PATO LA SERIKALI LINAITWA JINA GANI. MRAHABA, MHABARA..POOR KIKWETE.

akili hizi ndio anguko la upinzani nchini, hizi ndio issue mnazoweza ku discuss kwenye draft
 
Maswali yalishaandaliwa kama ya wbunge na akafanya riheso namna ya kujibu.anaboa sana mtu huyu.
Mbona hakuna swali la nyongeza?
Gharama zinazotumika kurusha huo uchemfu TV zote zinaweza kusomesha watoto wangapi?

Hapa Mungu mwenyewe anaboreka
 
Duh! Hata maofisa wake wa polisi na jeshi waliopo ukumbini wanaonekana kutoridhishwa na majibu anayotoa.
 
Nimecheka ile ya E medicine jamani hospitali zinashindwa hata gloves syringe hata pamba na gauze hazipo anasema mtu yuko north caroline harafu anadirect operation huku mi nadhani awaomde samahani madaktari wetu anataka kusema hawana uwezo awape vifaa aone watakavyofanya
Na ya e-governance wakati mpaka sasa kuna government officials hawajui hata computer inawashiwa wapi pamoja na kuwa imekuwepo mezani kwake for years.........kazi zote anafanya secretary:hippie:
 
Hivi bandugu bangu, kwenye kile kisa chake cha fisi na sungura alivyokutana na mwanamke wa kimarekani akamkaribisha nyumbani kwake kulikua na relevance yoyote na kuchaguliwa kwake tena kuwa rais? naona kama vile haya maswali yamelengwa kumpotosha mshkaji aache kuongelea kampeni aongelee mambo mengine!!!
 
AHADIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII

Dodoma, atapeleka MELI KUBWAAAAAAAAAAAAAAAAAA
 
Kuanzia sasa mtu asimsumbue tena raisi wetu. Tumwache akapumzike kwa amani. Sio mumtese kwa maswali huku urahisi hamtaki kumpa.
 
akili hizi ndio anguko la upinzani nchini, hizi ndio issue mnazoweza ku discuss kwenye draft

Naona una bidii kweli...Hata ufanyeje huyu mkwere wako habebeki!!!
 
Back
Top Bottom