Kikwete (Rais Mstaafu) ni Muungwana kuliko, mwenye huruma na utu uliopitiliza

Kikwete (Rais Mstaafu) ni Muungwana kuliko, mwenye huruma na utu uliopitiliza

Mkuu inaonekana ulikuwepo kwenye kuchuja mafaili wewe [emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Kuna kaka yangu mmoja aliongoza kitengo Mwanza. Yule jamaa alipotea hata Social Media huwezi kumuona.
Why alipotea? Kwa kufa au ni wale hawatak kuonekana wala kujulikana walipo
 
Daah, literally Rugemalira bought an entire government. Wewe ushawahi kuona wapi mahamakama inaendeshwa saa nane usiku ? Basi ndivyo ilivyofanyika High Court Commercial Division ambapo bwana Rugemalira alifanya Voluntary Winding Up ya kampuni lake bila hata Creditors kutoka nje kushirikishwa. Marehemu Jaji Utamwa akamaliza kazi, asubuhi watu wanaamka vitabu vya kampuni vimefungwa na akaunti ya ESCROW imeshatangazwa kuwa ni mali ya mtu siyo serikali. Wahuni wakagawana pesa kama mikate na samaki za Yesu, it was a frenzy.

Bwana Yohana alivyoingia madarakani and His gospel of envy, aah walizitapika. Ulikuwa unaitwa kule juu BoT unamkuta anakusubiri. Sasa akikwambia toa pesa ukakataaa inakula kwako. Kiufupi Rugemalira ameua career za watu wengi mno na mapesa yake. Kuna majaji walilazimishwa kujiuzulu kisa Ruge aliwapa milionI 400, eti mchango wa harusi. Mzee wako aliona mbali, angelambishwa tu mlungula ingekula kwake hadi kwenu.​
Ndio maana mwamba aliitwa Jiwe, Chuma,
Sipati picha unamkuta kakaa kile kiti cha boss wa BoT na lafudhi yake ya kisukuma, We rugee hela utatoa hutoi?
 
Huyu mzee alikuwa anakuja nyumbani kuongea na mshua wangu. Zamani sana kabla ya haya mambo ya Escrow. Miaka ya mwanzo ya 1990s.

Sasa, ikafika wakati nikawa simuoni.

Nikamuuliza mshua. Mbona yule rafiki yako Mzee Rugemalira simuoni kuja nyumbani siku hizi?

Mshua akaniambia, mwanangu, unajua dunia hii kuna marafiki wengine wanakuwa marafiki kwa kutaka kitu fulani kwako, wakikikosa, na urafiki wao unaisha.

Basi kwa miaka mingi jibu lile lilikuwa kitendawili kwangu, nilikuwa sijalielewa vizuri.

Baadaye sasa kwenye hii issue ya Rugemalira kugawa pesa kama hana akili nzuri, ndiyo nikajumlisha moja na moja kupata mbili, kwamba huyu mzee alitaka kumhonga mshua wangu apate favors fulani, mshua akamkatalia.
Na alivyo kataliwa akakata naye miguu 😄
Ila ule mgao nadhani ulipita kwa wale wote walio fanikisha kwa namna moja au nyingine kutoka
 
Hiyo ya mshua ilikuwa kabla kabisa ya ule mgao, hiyo ilikuwa kipindi cha Mwinyi early 1990s.
Nasema huu mzigo wa escrow ulivyotoka
Wale wote waliopewa pesa walichangia kwa namna moja au nyingine mzigo kutoka
 
FB_IMG_1595423587344.jpg
Mzee Kikwete akipata mlo pamoja na waombolezaji wenzake kwenye moja misiba aliyohudhuria
 
Jamani habari wanajf, ukweli Rais Mstaafu Dkt. Kikwete ni kiongozi wa kipekee Sana tangu nianze kuwafahamu viongozi wengine. Ni kiongozi anayeguswa na matatizo ya watu moja kwa moja hasa misiba, na matukio ya kijamii. Mhe. Kikwete hajawahi kusikia Msiba kwa watu ambao unafikika akashindwa kufika. Ni Kiongozi aliyejishusha kuliko. Nani kiongozi Kama Dkt. Kikwete. Ubarikiwe Sana Mhe. Tumuombe Sana huyu kiongozi wetu Mstaafu. Leo nimemuona kwenye Msiba wa mke wa mtangazaji Gerald Hando. Viva Dkt. Kikwete.
Na ni kiongozi pekee aliyefanikiwa kuigeuza Kigoma kuwa Dubai ya Afrika ndani ya miaka mitano(5), hongera zimfikie kijana wa Msoga.
 
Jakaya Mrisho Kikwete,Namkubali sana huyu mzee,Mzee yuko smart sana kichwani aisee,Strategies anazotumia ili kuendelea kusurvive zinanifanya nimkubali mpaka kesho.

Ndani ya C.C.M kwa sasa sioni mtu yeyote anayeweza kupambana na huyu mzee strategically,labda wasubiri aishiwe nguvu kabisa kama MUGABE😁
A MAN WILL DIE NATURALLY.
Hakika mkuu
 
Daah, literally Rugemalira bought an entire government. Wewe ushawahi kuona wapi mahamakama inaendeshwa saa nane usiku ? Basi ndivyo ilivyofanyika High Court Commercial Division ambapo bwana Rugemalira alifanya Voluntary Winding Up ya kampuni lake bila hata Creditors kutoka nje kushirikishwa. Marehemu Jaji Utamwa akamaliza kazi, asubuhi watu wanaamka vitabu vya kampuni vimefungwa na akaunti ya ESCROW imeshatangazwa kuwa ni mali ya mtu siyo serikali. Wahuni wakagawana pesa kama mikate na samaki za Yesu, it was a frenzy.

Bwana Yohana alivyoingia madarakani and His gospel of envy, aah walizitapika. Ulikuwa unaitwa kule juu BoT unamkuta anakusubiri. Sasa akikwambia toa pesa ukakataaa inakula kwako. Kiufupi Rugemalira ameua career za watu wengi mno na mapesa yake. Kuna majaji walilazimishwa kujiuzulu kisa Ruge aliwapa milionI 400, eti mchango wa harusi. Mzee wako aliona mbali, angelambishwa tu mlungula ingekula kwake hadi kwenu.​
Mkuu hii simulizi inatufunza kitu. Ipo siku ataingia Yohana mwingine pale ofisi kuu atawatapisha watu pesa ya DP World.
 
Back
Top Bottom