Kikwete siyo safi! - yes I said it!

Natamani ninge ikopi hii thread nimpatie kila mtanzania aisome na aielewe na hakika hakuna atakaye mpa kura jk,
 
CCM walikosea sana walipomtosa Salim Ahmed Salim kwa sababu zisizo na maana...Ubaguzi. Mbona mjaluo anaiongoza Marekani
 
Kisikichampingo kama una mawasiliano nao waambie Wamrudishe Salim Ahmed Salim!
 
Natamani ninge ikopi hii thread nimpatie kila mtanzania aisome na aielewe na hakika hakuna atakaye mpa kura jk,


Kweli ingefaa sana, hata hivyo ni wakati muafaka kwa Mkjj ku update thread hii iende na wakati kwani toka 2007 tayari madudu mengi yamejitokeza
 
salim eti hakutokana na aspkule zenji, asp na ccm waliingia mkataba mzanzibari yoyote ambaye hajawai tokea asp hawezi kua rais
 
Kikwete hawezi kujisahihisha hata akipewa miaka 20 zaidi ya kutawala kama naye alivyowaambia TUCTA kwamba hata wafanyakazi wagome miaka minane ijayo kima cha chini cha 315,000 hakilipiki.TATIZO NI KUBWA ZAIDI YA KIKWETE. Hadi hapo Watanzania tutakapoamua kuwatazama wanasiasa na vyama vya siasa kama vyombo vya kututumikia badala ya kuviona kama vilabu vya mpira NA KUONDOA USHABIKI; pale tutakapoamua kutowahakikishia wanasiasa na vyama vyao nafasi za uongozi wa kudumu; kwamba wakifanya madudu basi ni nje tu, hapo ndipo tutakapotatua tatizo la jeuri za akina Kikwete & co.

Mtu anathubutu kukejeli madai halali ya wafanyakazi kwa taarifa za ubabaishaji na kuzipuuza kura zao. Jeuri hii inatoka wapi? Kama sio kwa kuhakikishiwa ushindi wa kishindo kupitia CCM. Na hili si tatizo la CCM au Tanzania tu. Chama chochote cha siasa katika nchi yeyote duniani kikipewa gerentii ya kuwa madarakani milele hata kifanye uozo gani, uozo utaendelea! Hulka ya binadamu wa kawaida ni kujitafutia ulaji mkubwa iwezekanavyo na kukwepa wajibu kwani wajibu una gharama na usumbufu mwingi. Tuliopitia JKT enzi zile, mtindo ulikuwa ni kusaka msosi kwa wingi na kutega kazi (kujongo) iwezekanavyo. Shuhudia Obama anavyosota na kashkash la BP huko Ghuba ya Mexico. Wapiga kura wa Marekani si mchezo. Tena wakati mwingine hupitiliza mantiki inapokuja suala la kuwawajibisha viongozi wao.
 
kwenye toleo la jumatano nitapanua kidogo hoja hii kuwa "kikwete naye si safi - yes i said it!"

natamani watanzania wote tuwe walinzi wa haya majambazi yanayoongozwa na jk. Ianike. Ili huyu jambazi aache kununua uokta kutoka kwa maprofesa uchwara and wanafiki
 
mzee mwanakijiji, asante sana kwa kui update makala hii,sikupata nafasi ya kuisoma kabla ila nimefanikiwa ku i printi na kuiweka kwenye file na nitawapa wengi waisome. Asante sana mungu akubariki, wewe ni mzalendo wa kweli.
 
Asante sana mzee mwanakijiji, Kuna TETESI kuwa Jim Sinclair na makampuni ya madini yalichangia fedha za kutosha katika kufadhili mtandao uliomwingiza kikwete ikulu 2005 na kwamba mwaka 2010 pia walitoa fedha za kutosha kuhakikisha kuwa JK anarudi madarakani, tafadhali kama kuna mtu anadata atumwagie hapa ili tumjue vzuri Rais wetu.
 
Tabia ni kama ngozi mkuu.,haibadiriki! hata ukijaribu kuibadili bado madhara yake hayaishi daima
 
Natamani ninge ikopi hii thread nimpatie kila mtanzania aisome na aielewe na hakika hakuna atakaye mpa kura jk,

Mkuu fanya hivyo hata kwa watanzania wachache ambao ni wasomi,nakuhakikishia sumu itaenea tanzania nzima!!
 
We need a President like Levy Mwanawasa hapa. Aliweza kumwondolea kinga short chasis Chiluba ili ashtakiwe. Alifanya hivyo kwa sababu kuu mbili. Kwanza alikuwa jasiri na pili yeye binafsi alikuwa msafi. Kiongozi yoyote anayekosa moja au sifa zote hizo hawezi kuchukua hatua. Ni dhahiri kwa taarifa za wilileaks Kikwete hawezi kumchukulia hatua Mkapa. Mkapa naye hakufanya hivyo kwa Mwinyi licha ya ripoti ya Warioba kuonyesha dhahiri madudu yake. Ni utamaduni unajengwa kidogo kidogo. Rais anakuja, anaiba na anayefuata anasita kuchukua hatua.
Tunajua hawafanyi hivyo kwa kuwa wao wenyewe si waadilifu. Utapigaje kelele ya mwizi wakati wewe mwenyewe ni mwizi? Lakini pia tunajua atatokea rais ama wa CCM au upinzani atakuwa msafi na ujasiri wa kutosha kuchukua hatua. ndio wakati Tanzania itaweza kuanza kupiga hatua tena kwenda mbele maana kwa sasa tunarudi nyuma. GOD BLESS Tanzania!
 

ndugu yangu ili tupige hatua nchi inatakiwa rais makini sana na mwenye uchungu na kujua kizazi cha kesho kitarithi nini
 
Kwa UKweli huu kama makamba na Tambwe wakiusoma watasema Wadini hawa hawana lolote, je kama kuna mdini mbona hata Mr. Safi BWM anahusika na ishu zote hizi maana ndiye wa kwanza kuaribu Afadhali ya Mazee wetu AHM yeye aliuza Twiga na Loliondo tu sio Nchi bali wanyama tehe tehe!! Tungempata balali akiwa hai tukamshauri aokoke angewaumbua wengi maana malipo yote yeye alihusika, hat hivyo nasikia kiwira haijarejeshwa serikarini. na Kesi za Ngonja na Mshindwa Ubunge Mramba sikuhizi zimedoda lakini ya Twin Tower (Mzee wa Vitoto) Liyumba ilienda fasta, au ni kwa sababu Mramba alimhusisha BWM?
 
Nchi zote duniani hupata viongozi wanaozistahili. Mkiwa na kiongozi mzuri ni kwa kuwa ndiyo stahili yenu. Vivyo hivyo mkiwa na viongozi wezi wanaojali matumbo yao ndiyo stahili yenu! Na sababu ni ndogo tu. Kwa kuwa mnakubali hali hiyo! kama Arusha yameanza kuonyesha njia.
 
Naona sasa wakati umefikia wa mimi kubadili jina....maana hii misamiati yenu mnayotumia neno/jina "nyani" saa ingine hunipa shinikizo...
we bado nyani tu pambaf saaako.......................JK sio safi kabisaaaaaaa
 
Asante sana JF, hizi kumbukumbu zidumu ili vizazi vijavyo angalau vielewe kuwa pamoja na utawala wa kidhalimu wa viongozi kama Jakaya Mrisho Kikwete, kuna wazalendo wachache ambao hawakusita kuita koleo kwa jina lake, hawakutetereka katika kutetea maslahi ya taifa, hawakurudi nyuma hata walipokabiliana na nguvu za dola zikisimamiwa na mafisadi na wala hawakumung'unya maneno katika kuwaanika maadui wa taifa bila kujali nguvu na nyadhifa zao.

Wataelewa kuwa ingawaje nchi iliendeshwa na genge la wahuni, wezi na wauaji kwa kivuli cha chama tawala, CCM, wapo wananchi waliosimama kidete kupambana nao hata ikibidi kupoteza maisha. Kwa kifupi watafahamu umasikini uliowatafuna babu zao kwa miaka hamsini ulisababishwa na nani kwa uroho wa kubaki madarakani. Kwamba kulikuwa na wachache waliojitolea kukabiliana na hawa mafisi na manyang'au, bila shaka kutawapa faraja na kuwapunguzia machungu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…