Na hamna maisha mabaya kama ya kutegemea mshahara hasa mshahara wa serikali.Nina kumbi mbili za kuonesha mpira (vibanda umiza), nilikua sitegemei mshahara kabisa, lakini kwa sasa naonja uchungu wa corona kila leo naingia mtandaoni kuona kama kuna chanjo imepatikana lakini wapi. Aseeeee Mungu tunakuomba utufanyie wepesi
Sent using Jamii Forums mobile app
Inabidi wafungue mapema. Haya mambo ya "lockdown" tuwaachie wazungu.Mimi mwenyewe hili la kufanga vyuo limeniathiri vibaya mno.
Nitakusaidia kumtunza mmoja wakati wa lockdown [emoji14][emoji14]Mimi kwa sasa hivi mambo yangu sio mabaya sana ila ninahofu kubwa na siku zijazo
Nina wake wawili sijui itakuwaje siku zijazo
Kama anavyowaingiza wake zako wawili!Tuongelee maisha ndani ya dimbwi la corona kama wewe unauhakika na buku saba sisi tunapambana kivyetu
Iko siku Polepole atakuomba aingize kichwa
sie wengine hali zilikuwa mbaya teyar hii corona imekuwa kisingizio tu ila mambo yalishabumaaa muda tu.Mbali na kujadili mambo mbalimbali yanayohusiana na corona, nadhani ni wakati muafaka na sisi watumiaji wa mtandao huu wa JamiiForums tukaeleze ni jinsi gani janga hili limetuathiri kiuchumi na kijamii kwani ni wazi karibu kila mtu atakuwa ameguswa kwa namna moja au nyingine.
Maelezo yetu/ yako yatasaidia kutoa mwanga wa nini kinaweza kutokea au kuwapata watu wengine iwapo gonjwa hili litakuwa king'ang'anizi na pia iwapo tutalazimika kuchukua hatua kali kukabiliana na ugonjwa huu kama ilivyo kwa mataifa mengine.
Tupe athari zilizukukumbuka na hata kama umefaidika na uwepo wa gonjwa hili, tueleze ni kwa namna gani kwani kila kitu kina faida na hasara zake.
Tupeana uzoefu, maana uzoefu wako mbali na mambo mengine,pia unaweza kusaidia wengine kujipanga/kuchukua tahadhari kibiashara, kijamii, kiafya n.k endapo tatizo hili litaendelea.
Kwa upande wangu corona imeongeza market volatility kwenye forex hivyo pesa zinamwagika tu sasa hivi. Price zinakimbia hatati. Hakuna pair isiyomwaga pesa.Mbali na kujadili mambo mbalimbali yanayohusiana na corona, nadhani ni wakati muafaka na sisi watumiaji wa mtandao huu wa JamiiForums tukaeleze ni jinsi gani janga hili limetuathiri kiuchumi na kijamii kwani ni wazi karibu kila mtu atakuwa ameguswa kwa namna moja au nyingine.
Maelezo yetu/ yako yatasaidia kutoa mwanga wa nini kinaweza kutokea au kuwapata watu wengine iwapo gonjwa hili litakuwa king'ang'anizi na pia iwapo tutalazimika kuchukua hatua kali kukabiliana na ugonjwa huu kama ilivyo kwa mataifa mengine.
Tupe athari zilizukukumbuka na hata kama umefaidika na uwepo wa gonjwa hili, tueleze ni kwa namna gani kwani kila kitu kina faida na hasara zake.
Tupeana uzoefu, maana uzoefu wako mbali na mambo mengine,pia unaweza kusaidia wengine kujipanga/kuchukua tahadhari kibiashara, kijamii, kiafya n.k endapo tatizo hili litaendelea.
The same same.Binafsi kuna hela niliitarajia kuipata mwezi huu sasa nimeikosa mpaka hali itakaporejea kuwa ya kawaida na kibaya nilichukue fedha mahali nikitarajia kulipa kwa kutumia hela ambayo ningeipata huu mwezi na matokeo yake imebidi nifanye kazi ya ziada kurudisha hela ya watu.
Nashukuru sikuchukua hela nyingi zaidi kama nilivyotaka kwani kazi ya kulipa ingekuwa mara mbili.