Kila aliye tayari aeleze jinsi Corona ilivyomuathiri Kiuchumi na Kijamii

[emoji58][emoji58][emoji58]Baada ya izi mambo za corona kuisha,,tutakumbuka wosia wa baba mmoja kutoka safari ya mbali
''Kama mnataka Mali mtaipata shambani''

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa upande wangu nafanya kwenye NGO ya wamarekani, Sasa since tarehe 16 mwezi wa tatu tuliambiwa we have to work from home mpaka June, kwa hiyo HQ office imefungwa ambayo ipo DC and all country offices globally zimefungwa, pamoja na kwamba they provide all facilities za kutuwezesha kufanya kazi tukiwa majumbani Kama vile internet, muda wa maongezi, laptops , and other stuffs na mishahara wanaingiza on time, changamoto ni kufanyia kazi nyumbani huku watoto wote wapo likizo, to be honest imenifanya nashindwa kugawa muda wangu maana nikiona mtoto analia nanyanyuka nataka nikae nae, nikiona Hawa wengine wanacheza natamani nicheze nao,ikifika muda wa kupika, naingia jikoni Kama kawa, yaani kaa vile Sasa rtiba ya nyumbani naip akipaumbele kuliko ya ofisini. na pia kukaa nyumbani tu Yani morning to evening 24/7 sio kitu kirahisi hasa kwa sisi tuliozoea kutoka asubuhi na kurudi jioni.

Pili, Kuna zile transport allowance za kila mwezi kwa Sasa zimesimamishwa maana Kila mtu anafanyia kazi nyumbani, kibongo bongo transport allowance huwa hatuitumii yote tuunasave ingine tunaingiza kwenye Mambo mengine na hapa hatujui Kama hiyo June watasema tuanze kwenda ofisini au wataongeza muda, hii inategemea Hali itakavuokua kule Marekani

Mbaya zaidi Hawa wenzetu wanaamini kwamba serikali yetu haotoi data sahihi kuhusu wagonjwa wa Corona nchini kwa hiyo kila kukicha wanatuasa kuchukua tahadhari na kukaa ndani Kama huna Sababu ya msingi ya kutoka maana wanaamini wagonjwa ni wengi tofauti na idadi inayotangazwa

Kiukweli mi nshachoka kukaa ndani Kama Mwali[emoji3][emoji3]
Sent using Jamii Forums mobile app
 
week iliyopita tumeitwa makao makuu ya kampuni ninayofanyia kazi na kuwekwa wazi kuwa kuanzia sasa shuguli zoote zinafungwa rasmi kwahiyo hali halisi tunaiona so hakuna wakumdai mwenzake.
kila mtu apambane na hali yake, tutakuwa tunapigiana simu tu kujuliana hali, ukimpia mtu simu ukiona hapokei then hapatikani BASI UJUE KISHAKUFA.
 
Pole mate,
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…