Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,722
- 20,610
Ndugu zangu Kama ukiacha akili yako iwe huru, ukaondoa mawazo ya uchama kichwani, ukatazama uongozi wa Rais Samia kwa mawazo huru yasiyofungwa na chochote Wala kupofushwa na chuki binafsi kwa Rais Samia, utakubaliana nami kuwa Rais mama Samia kafanikiwa kufanya kazi njema na ya kutukuka katika kila secta na kila eneo linalogusa maisha ya watanzania wanyonge.
Utagundua kuwa Rais Samia kafanikiwa kugusa maisha ya watanzania moja kwa moja, kajenga uchumi unaomgusa mtanzania,utagundua kuwa Mama Samia anaelekeza mamilioni kwa mabillioni ya pesa za kitanzania katika miradi inayogusa na kumnufaisha mtanzania mnyonge katika maisha yake ya kila siku
Mfano ukienda katika kilimo secta iliyobeba kundi kubwa la watanzania unakuta Rais Samia kaelekeza mabillioni ya pesa takribani billioni Mia moja hamsini kama Ruzuku , Hatua hii ya makusudi , kimkakati , kishujaa na kijasiri imepelekea kushuka kwa Bei ya mbolea sokoni,. Mfano mbolea ya DAP msimu uliopita ilikuwa inauzwa shillingi laki moja na 40 lakini msimu huu inapatikana kwa elfu 70 tu, hii imewasha Taa ya Matumaini katika mioyo ya mamilioni ya watanzania wanyonge ambao wanategemea kilimo kuendeshea maisha yao,kwani hatua hii itafanya wakulima kuongeza uzalishaji na hivyo kuinuka kiuchumi na kupunguza umaskini wa Kaya.
Ukija katika Elimu unakuta mh Rais Samia kachukua uamuzi wa kufuta Ada na kufanya Elimu kuwa bure Hadi kidato Cha sita, hatua hii imewafuta machozi na jasho na kuwatua mzigo wazazi wengi waliokuwa wanahangaika kutafuta Ada kwa ajili ya kusomesha watoto wao,lakini pia hatua hii ya mama yetu mpendwa mama Samia imewasha na kuamsha Matumaini kwa wanafunzi wanaotoka katika familia duni nafasi ya Kuendelea na masomo yao bila kikwazo chochote kile,
Lakini pia mama yetu shupavu na Mama wa shoka amehakikisha ujenzi wa shule mpya nchini kwote na ujenzi wa vyumba vya madarasa zaidi ya elfu nane nchini,Hali iliyopelekea na kutoa nafasi kwa wanafunzi wote wanaofaulu kupata Nafasi ya kwenda shule kwa wakati bila kukaa nyumbani Kama ilivyokuwa zamani ambapo wanafunzi wengine walikuwa wanakwenda muhula wa pili na hivyo kuwa nyuma kimasomo ukilinganisha na wenzao waliotangulia tangia mwezi January.
Ukija katika Afya,Unakuta mama wa shoka kipenzi Cha watanzania Tumaini la wanyonge na chaguo la watanzania Mama Samia ameimarisha Sana secta ya Afya kwa kuhakikisha ujenzi wa zahanati na vituo vya Afya mbalimbali nchini,mfano majuzi hapa takribani vituo vya Afya 234 vimejengwa nchini kwote,lakini pia ameimarisha upatikanaji wa vifaa Tiba , madawa na hata wataalamu wa Afya nchini kwote Kama ambavyo tumeshuhudia utoaji wa ajira za Afya miezi michache iliyopita ambapo zilitoka pamoja na zile za ualimu,
Hatua hii imesaidia na kusogeza huduma Karibu kabisa ya mtanzania na kupunguza adha ya kusafiri umbali mrefu kutafuta huduma. Lakini pia huduma za kibingwa zinapatikana na hivyo kupunguza zile safari za kupeleka wagonjwa nje ya nchi ambapo watanzania masikini wasio na uwezo wa kupeleka wagonjwa wao nje ya nchi waliishia kuwapoteza na kubaki na majonzi na uchungu mioyoni mwao ya kupoteza wapendwa wao kwa kukosa tu fedha, Sasa Hali Ni ya Matumaini Sana kwetu watanzania kutokana na juhudi za Rais Samia kuimarisha secta ya Afya
Ndugu zangu kila eneo utakalo kwenda iwe Ni suala la demokrasia au usambazaji wa maji, au umeme unakuta Rais Samia kafanya kazi kubwa Sana ya kugusa maisha ya watanzania, Ni ngumu kumaliza yote aliyoyafanya Rais Samia maana hapa patajaa kabisaa
Watanzania tukubali kuwa taifa Letu halitaongozwa na Malaika kwa kuwa hatuna Malaika miongoni Mwetu, Na katika Ubinadamu wake Rais Samia Anastahili pongezi kubwa Sana kutoka kwetu watanzania, Anastahili kuungwa mkono na kila mtanzania mwenye mapenzi mema na nchi hii, Anastahili kuombewa na kila mtanzania ili mwenyezi Mungu amjalie Afya njema na nguvu za kututumikia watanzania.
Watanzania tunataka Nini Tena ambacho Rais Samia hajafanya? Nini ambacho Hakipo katika mipango ya Rais Samia ambacho tunaona kina umuhimu kwetu? Nini na wapi ambako hajagusa kiutendaji? Mimi naona kagusa na kufanyia kazi kila eneo linalo gusa maisha ya mtanzania mnyonge, kila eneo kaweka mkono wake wa upendo na huruma kwa mtanzania mnyonge na kila eneo kalitazama kwa macho ya utayari
Kazi iendeleee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu
Utagundua kuwa Rais Samia kafanikiwa kugusa maisha ya watanzania moja kwa moja, kajenga uchumi unaomgusa mtanzania,utagundua kuwa Mama Samia anaelekeza mamilioni kwa mabillioni ya pesa za kitanzania katika miradi inayogusa na kumnufaisha mtanzania mnyonge katika maisha yake ya kila siku
Mfano ukienda katika kilimo secta iliyobeba kundi kubwa la watanzania unakuta Rais Samia kaelekeza mabillioni ya pesa takribani billioni Mia moja hamsini kama Ruzuku , Hatua hii ya makusudi , kimkakati , kishujaa na kijasiri imepelekea kushuka kwa Bei ya mbolea sokoni,. Mfano mbolea ya DAP msimu uliopita ilikuwa inauzwa shillingi laki moja na 40 lakini msimu huu inapatikana kwa elfu 70 tu, hii imewasha Taa ya Matumaini katika mioyo ya mamilioni ya watanzania wanyonge ambao wanategemea kilimo kuendeshea maisha yao,kwani hatua hii itafanya wakulima kuongeza uzalishaji na hivyo kuinuka kiuchumi na kupunguza umaskini wa Kaya.
Ukija katika Elimu unakuta mh Rais Samia kachukua uamuzi wa kufuta Ada na kufanya Elimu kuwa bure Hadi kidato Cha sita, hatua hii imewafuta machozi na jasho na kuwatua mzigo wazazi wengi waliokuwa wanahangaika kutafuta Ada kwa ajili ya kusomesha watoto wao,lakini pia hatua hii ya mama yetu mpendwa mama Samia imewasha na kuamsha Matumaini kwa wanafunzi wanaotoka katika familia duni nafasi ya Kuendelea na masomo yao bila kikwazo chochote kile,
Lakini pia mama yetu shupavu na Mama wa shoka amehakikisha ujenzi wa shule mpya nchini kwote na ujenzi wa vyumba vya madarasa zaidi ya elfu nane nchini,Hali iliyopelekea na kutoa nafasi kwa wanafunzi wote wanaofaulu kupata Nafasi ya kwenda shule kwa wakati bila kukaa nyumbani Kama ilivyokuwa zamani ambapo wanafunzi wengine walikuwa wanakwenda muhula wa pili na hivyo kuwa nyuma kimasomo ukilinganisha na wenzao waliotangulia tangia mwezi January.
Ukija katika Afya,Unakuta mama wa shoka kipenzi Cha watanzania Tumaini la wanyonge na chaguo la watanzania Mama Samia ameimarisha Sana secta ya Afya kwa kuhakikisha ujenzi wa zahanati na vituo vya Afya mbalimbali nchini,mfano majuzi hapa takribani vituo vya Afya 234 vimejengwa nchini kwote,lakini pia ameimarisha upatikanaji wa vifaa Tiba , madawa na hata wataalamu wa Afya nchini kwote Kama ambavyo tumeshuhudia utoaji wa ajira za Afya miezi michache iliyopita ambapo zilitoka pamoja na zile za ualimu,
Hatua hii imesaidia na kusogeza huduma Karibu kabisa ya mtanzania na kupunguza adha ya kusafiri umbali mrefu kutafuta huduma. Lakini pia huduma za kibingwa zinapatikana na hivyo kupunguza zile safari za kupeleka wagonjwa nje ya nchi ambapo watanzania masikini wasio na uwezo wa kupeleka wagonjwa wao nje ya nchi waliishia kuwapoteza na kubaki na majonzi na uchungu mioyoni mwao ya kupoteza wapendwa wao kwa kukosa tu fedha, Sasa Hali Ni ya Matumaini Sana kwetu watanzania kutokana na juhudi za Rais Samia kuimarisha secta ya Afya
Ndugu zangu kila eneo utakalo kwenda iwe Ni suala la demokrasia au usambazaji wa maji, au umeme unakuta Rais Samia kafanya kazi kubwa Sana ya kugusa maisha ya watanzania, Ni ngumu kumaliza yote aliyoyafanya Rais Samia maana hapa patajaa kabisaa
Watanzania tukubali kuwa taifa Letu halitaongozwa na Malaika kwa kuwa hatuna Malaika miongoni Mwetu, Na katika Ubinadamu wake Rais Samia Anastahili pongezi kubwa Sana kutoka kwetu watanzania, Anastahili kuungwa mkono na kila mtanzania mwenye mapenzi mema na nchi hii, Anastahili kuombewa na kila mtanzania ili mwenyezi Mungu amjalie Afya njema na nguvu za kututumikia watanzania.
Watanzania tunataka Nini Tena ambacho Rais Samia hajafanya? Nini ambacho Hakipo katika mipango ya Rais Samia ambacho tunaona kina umuhimu kwetu? Nini na wapi ambako hajagusa kiutendaji? Mimi naona kagusa na kufanyia kazi kila eneo linalo gusa maisha ya mtanzania mnyonge, kila eneo kaweka mkono wake wa upendo na huruma kwa mtanzania mnyonge na kila eneo kalitazama kwa macho ya utayari
Kazi iendeleee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu
