Kila nikijaribu kutaka kufanya Maendeleo kwa wazazi wangu ninashindwa

Kila nikijaribu kutaka kufanya Maendeleo kwa wazazi wangu ninashindwa

Ipo hivi; ukiwaambia wazazi wako, nao wanawaambia ndugu zako, kwahiyo inakua sio Siri Tena, sasa roho za ndugu zako hauwezi kujua kama wanafurahia au wanaona uwivu wewe kufanikisha suala lililowashinda wao, kwahiyo usiri ni lazima ili ufanikishe jambo lolote lile
 
Usitoe Taarifa ya zoezi unalotarajia kulifanya. Ukiwaambia wazazi wako hizo Taarifa hawakai nazo wanaeneza Kwa watu wengine ambao Kuna wabaya na wema. Hivyo wabaya wanaanza kukunenea mabaya na kukuhamisha kwenye reli hivyo huwezi kufikia malengo. Andaa pesa, jikamilishe uende na vifaa na ufanye kazi ndani ya wiki Moja na uondoke chap, ukizubaa utakufa.
 
Mambo ya ovyo kama vile starehe japo uwa situmii pombe Ila bebez na kununua vitu visivyo kuwa na maana yote imekuwa nyingi mno na uwa lust inakuwa kubwa kila nikianza kupata pesa hasa nikiwaambia tu home kuwa next month ntakuwa huko
Tatizo ni wewe , jiwekee mazingira ya kubadilika kitabia na kujifunza kunyamazia mambo yako.
 
Sijajenga ila wazazi wangu wana nyumba yao ila ni kama pagale tu coz haija kamilika sehemu kubwa na ule mtaa wanao ishi wamezungukwa na watu wenye pesa karibu wote………..Huwezi amini!!!! Kwetu ndio imekuwa mfano wa kaya masikini kwa pale mtaani

Shida yangu kubwa ni kubadili mazingira ya pale japo kwa kiasi kidogo tu ili nipunguze ile picha ya kudharaulika pale mtaani ila ndio hivyo tena mabalaa yamekuwa mengi sana
Shukuruni kwa mlichonacho. Usiangalie jirani au mtu mwingine atasemaje, ukiangalia vigezo hivyo hutoboi.
 
Pole sana jitahidi sana kumwomba Mungu na kuweka nia bila kuitangaza utafanikiwa
 
Hapo ni ishu ya negative energy ipo kwa wingi kwenye kijiji au ukoo wako ndo inanyonya hio energy yako uliyonayo thus ukidream kutoboa inakuvuta down.
Pia Pana ishu za madhabau za kiukoo na maagano ambayo mababu waliweka so unachofanya wewe ni kama unajaribu kublock ile chain waliyoiweka, kublock chain hio inatakiwa uwe vizuri kiroho.
 
Kafungue hata fixed account kwa kipindi flan let's say hata 3yrs, then jiwekee akiba kadri uwezAvyo , muda ukifika katoe pesa yako zama ndichi kafanye maendeleo,,, pia zingatia usiwe unawaambia sana watu mipango yako mfano kujenga, kufungua biashara nk,,,kuna watu wana mikosi na laana
usiwe unawaambia sana watu mipango yako mfano kujenga, kufungua biashara nk,,,kuna watu wana mikosi na laana
 
tatizo linaanzia kichwani kwako,una elimu ya chuo kikuu hujui kupangila mambo bado unaamini huenda umerogwa.
Ushauri
Rudi darasani tafuta chuo kinachofundisha kuelewa sio kukariri kisha njoo kitaa tukupe elimu ya mtaa halafu tutakufundisha namna ya kufanya jambo kubwa kwa kuanza kufanya kidogo halafu utatoboa.
Kuwa na elimu ya chuo kikuuu sio kuwa na elimu ya utambuzi wa mambo ya kiroho.
 
Hii siyo kuhusu mabalaa.

Na hapo kwenye kumaliza pesa hovyo nafikiri ni unacompensate kwa ulivyovikosa wakati you were broke.

Kuna details hautoi hapa
 
Kama una mawazo ya kuufuta ama kupunguza umaskini wa familia/ukoo wako, hutoboi. Mizimu ya babu, maaika wa Mungu na kanuni zote za kiuchumi zinakataa. Wewe ndiye ulioaswa kusaidiwa na wazazi kupambana na maisha mpk utoboe. Na siyo kinyume chake.
Hizi jitihada za kuondoa umaskini katika ukoo ndo zitakuwa anguko lake.. mm nampa H/W akiweza afanye. Achunguze ni nani hasa katika familia yao ananufaika na umaskin wa ukoo mzima uliopo

Mana katika familia hizi wapo watu wananufaika n umaskini huo hatakama na wao ni maskini vilevile. Na hao huwa hawatoki mbali, ndo hao hao kwemye masuala ya maana na mendeleo michango hawatoi na wanakuaga wazito kwelikweli kushiriki mambo ya maendeleo hata kimawazo tu
 
Ninatoka familia duni sana ambayo kipato chao,mlo wao na ata makazi yao ni duni sana

Nina wakubwa zangu Ila na wao wote wana familia zao na wao pia hali zao zipo chini sana kiuchumi, kwahiyo pale nyumban nimebaki mimi na wadogo zangu wengine ambao na wao bado wanasoma

Mimi ndio mtu wa kwanza kufika elimu ya Chuo Kikuu kwa home na ata kiukoo kwa ujumla japo kiuchumi bado sipo vizuri sana

Ila sasa kila nikiwapigia simu wazaz wangu kuwa mwezi unaokuja nitakwenda kuwakarabatia nyumba yao na ata kuwawekea umeme na pamoja na maji. Zile pesa zote nilizo changa zinaishia kwenye mambo mengne tena ni ya ovyo sana

Ninajiona kama nina jukumu kubwa sana la kubadili hali ya pale home coz nikiwaangalia ndugu zangu sifikirii kama ata wana mawazo hayo,ila sasa hali ninayo kumbana nayo ndio Kama hiyo

Msaada pleasee,kuna nguvu za giza zinaniandama au ni maroho ya umaskini?
Ombea hio mipango yako
 
Hii siyo kuhusu mabalaa.

Na hapo kwenye kumaliza pesa hovyo nafikiri ni unacompensate kwa ulivyovikosa wakati you were broke.

Kuna details hautoi hapa
Yeah Upo sahihi sana!!!! Ni kweli kuna vitu uwa natamani sana kuvifanya hasa nikiwa broke so,nikipata tu pesa nakimbilia kwenye hayo mambo mwisho wa siku pesa yote inakuwa inakwisha kwenye mambo ya ovyo sana
 
Hizi jitihada za kuondoa umaskini katika ukoo ndo zitakuwa anguko lake.. mm nampa H/W akiweza afanye. Achunguze ni nani hasa katika familia yao ananufaika na umaskin wa ukoo mzima uliopo

Mana katika familia hizi wapo watu wananufaika n umaskini huo hatakama na wao ni maskini vilevile. Na hao huwa hawatoki mbali, ndo hao hao kwemye masuala ya maana na mendeleo michango hawatoi na wanakuaga wazito kwelikweli kushiriki mambo ya maendeleo hata kimawazo tu
Na huyo sio mwngine nahisi ni Kaka yangu ambaye anapenda sana starehe kama kunywa pombe na sio kufanya mambo ya maana
 
Ninatoka familia duni sana ambayo kipato chao,mlo wao na ata makazi yao ni duni sana

Nina wakubwa zangu Ila na wao wote wana familia zao na wao pia hali zao zipo chini sana kiuchumi, kwahiyo pale nyumban nimebaki mimi na wadogo zangu wengine ambao na wao bado wanasoma

Mimi ndio mtu wa kwanza kufika elimu ya Chuo Kikuu kwa home na ata kiukoo kwa ujumla japo kiuchumi bado sipo vizuri sana

Ila sasa kila nikiwapigia simu wazaz wangu kuwa mwezi unaokuja nitakwenda kuwakarabatia nyumba yao na ata kuwawekea umeme na pamoja na maji. Zile pesa zote nilizo changa zinaishia kwenye mambo mengne tena ni ya ovyo sana

Ninajiona kama nina jukumu kubwa sana la kubadili hali ya pale home coz nikiwaangalia ndugu zangu sifikirii kama ata wana mawazo hayo,ila sasa hali ninayo kumbana nayo ndio Kama hiyo

Msaada pleasee,kuna nguvu za giza zinaniandama au ni maroho ya umaskini?
Ushaur wangu kwako. Fanya maendeleo yako wekeza vya kutosha. Katika maisha usimuahidi kitu ndugu au mzazi, we mfanyie surprise tu. Kumbuka wewe ndie unawaona wanaishi maisha duni kwasababu ushaona uli.wengu wa nje ila wao ndio maisha yao hawana shida nayo. Kama kuna mtu analoga hilo boma lisiendelee chochote utakachofanya watakutarget wewe. So jiwekeze kwanza vya kutosha. Pili ukipokea mshahara au kipato chochote kitolee sadaka huwa zinalinda dhidi ya mwaribifu. Kuwa makin usibadili life style wakati unajipanga wewe yaan kununua magari kuwaonyesha una hela kabla hujawekeza watakufanyia mabaya. Kama una hela nunua viwanja nunua majumba kimya kimya mpaka wakija wakukute uko kwenye point of no return. Ndio unabadilika mazima.
 
Ushaur wangu kwako. Fanya maendeleo yako wekeza vya kutosha. Katika maisha usimuahidi kitu ndugu au mzazi, we mfanyie surprise tu. Kumbuka wewe ndie unawaona wanaishi maisha duni kwasababu ushaona uli.wengu wa nje ila wao ndio maisha yao hawana shida nayo. Kama kuna mtu analoga hilo boma lisiendelee chochote utakachofanya watakutarget wewe. So jiwekeze kwanza vya kutosha. Pili ukipokea mshahara au kipato chochote kitolee sadaka huwa zinalinda dhidi ya mwaribifu. Kuwa makin usibadili life style wakati unajipanga wewe yaan kununua magari kuwaonyesha una hela kabla hujawekeza watakufanyia mabaya. Kama una hela nunua viwanja nunua majumba kimya kimya mpaka wakija wakukute uko kwenye point of no return. Ndio unabadilika mazima.
Uhakika mzee hapa umeuwa sana ila kwenye kuwasaidia ninahisi ninapaswa kukarabati hiyo nyumba yao basi halaf vingine watamalizia na wengine au wao wenyewe
 
Back
Top Bottom