Kilevi hiki ni hatari kwa taifa japo kina faida kwa wanasiasa

Kilevi hiki ni hatari kwa taifa japo kina faida kwa wanasiasa

Wajanja wa nchi hii wametuletea kilevi hatari kwa taifa letu, kiasi kimekolezwa na kesi za akina Magoma zinazoipotezea muda mahakama zetu.

Wakati bodi ya vilevi hairuhusu baa kuuza pombe saa za kazi lakini bodi hii TCRA inaruhusu walevi wake wanshinde kutwa nzima eti wasikilize uchambuzi na kesi za mpira wa Simba na Yanga ambako kuna wapiga kura pendwa wengi, kunogesha kilevi hiki kimeongezewa na mamilioni ya ya shilingi za goli! Leo hii uswahilini watu wamekuwa mateja wa Simba na Yanga, panapouzwa magazeti ni ubishi wa kilevi hiki kipya.

Tanzania viongozi wetu hufurahia umasikini na ujinga wetu kwani ndio unaowapa kura ili washike madaraka kupitia kutudanganya na visima vya maji yasiyo salama karne hii! Kwa pombe hii Tanzania itabaki kuwa mtazamaji huku wenzetu wanachanja mbuga, lete pombe nyingine.
Huu ni ushirikina wa serikali ya CCM
 
Miaka ya nyuma asubuhi ilikuwa uchambuzi wa siasa, usiku saa mbili kasoro michezo, dakika 15-30, sasa hivi asubuhi, mchana,jioni, usiku ni michezo.

Generation ya wachambuzi wa siasa ime-phase out, imeondoka na akina Jenerali Twaha.

I bet kwa sasa wachambuzi bora wa michezo ndio wanaolipwa vizuri kuliko wa siasa
Ni aibu tupu
 
Wajanja wa nchi hii wametuletea kilevi hatari kwa taifa letu, kiasi kimekolezwa na kesi za akina Magoma zinazoipotezea muda mahakama zetu.

Wakati bodi ya vilevi hairuhusu baa kuuza pombe saa za kazi lakini bodi hii TCRA inaruhusu walevi wake wanshinde kutwa nzima eti wasikilize uchambuzi na kesi za mpira wa Simba na Yanga ambako kuna wapiga kura pendwa wengi, kunogesha kilevi hiki kimeongezewa na mamilioni ya ya shilingi za goli! Leo hii uswahilini watu wamekuwa mateja wa Simba na Yanga, panapouzwa magazeti ni ubishi wa kilevi hiki kipya.

Tanzania viongozi wetu hufurahia umasikini na ujinga wetu kwani ndio unaowapa kura ili washike madaraka kupitia kutudanganya na visima vya maji yasiyo salama karne hii! Kwa pombe hii Tanzania itabaki kuwa mtazamaji huku wenzetu wanachanja mbuga, lete pombe nyingine.
Double kiki, smart gin?
 
Katika nchi yenye matukio na ujinga mwingi,starehe ya mwananchi wa kawaida zimebaki chache tu ,mpira ni mojawapo.... mtu unaona kuliko kuwa serious muda wote,bora upoteze mawazo huku. Lkni kama ilivyo desturi ya serikali zenye chembechembe za udikteta siku zote,na huku wameamua kuji-insert kwenye conversation kupitia "goli la mama"

Tanzania is a "total state" ,serikali itakuongoza hadi kwenye familia yako mwenyewe.Watch!
Totalitarian state
 
Back
Top Bottom