Mungu alituepusha na lile janga.
Ni kweli mkuu, inaonekana Mungu husikia maombi!
1. Mwendazake alipenda sana kuomba watu wamuombee! Kila mtu na Mungu wake, Mungu akaamua isiwe kesi, ikawa!
2. Mwendazake akaambiwe Korona inaua, akaamkia kanisani, kadhihaki mapadri, kwa kuwa alishaomba aombewe wakapiga maombi, Mungu akaamua isiwe kesi, ikawa!
3. Mwendazake akaambiwe hela ya rambirambi hailiwi, akawakejeli wahanga wa tetemeko la Kagera, kwa kuwa alishawasihi sana watu wamuombee, katikati ya maombolezo ya wafu wao wakaomba Mungu wao, huyo Mungu akaona isiwe kesi akaamua, ikawa!
4. Mwendazake akaambiwa usibomolee watu wa Morogoro road bila kuwafidia au kuwafuta machozi, alipoenda Mwanza akadokeza hawakumchagua. Kwa kuwa aliwaomba sana watu wamuombee kweli bwana, wakiwa wamelala nje na vitu vyao na watoto wao usiku wa Kawa wanaomba sana, Mungu wao akaamua basi, isiwe kesi, akaamua, ikawa!
5. Mwendazake akaambiwa mwanafunzi yeyote akifika chuo sio kilaza, akasema ah wapi! Wanafunzi walee wa UDOM wote vilaza, timua wote! Akasau aliwasihi sana watu wamuombee, wale wanafunzi wakiwa na wazazi wao nyumbani kwao wakapiga magoti mbele ya Mungu wao wakaomba. Mungu akaona isiwe kesi, akaamua, ikawa!
6. Mwendazake akaambiwa usifukuze watu kazi kisa kutofautiana majina ya vyeti vyao, wape nafasi wasahihishe dosari hizo, akasema fukuzilia mbali! Kazini wakaondoka! Lakini aliendelea kuomba watu wamuombee sana, wakiwa hawajui hatimaye yao na wataishije wakakumbuka kuomba, wakaomba na kufunga, Mungu sio athumani kajibu! Kesi ikaisha, ikawa!
7. Mwendazake akaambiwa kikokotoo ni kitanzi kwa wastaafu, akasema kikokotoo lazima kiwepo wapende wasipende! Na kweli kikawekwa, wastaafu wakaanza kujitundika bwana, wakaona twafa! Kwa kuwa aliomba mwenyewe wamuombee, wakaanza kuomba pamoja na familia zao, Mungu kasikia maombi yao, akaamulia kesi, ikawa!
8. Mwendazake akaambiwa wanafunzi wakipata mimba wakiwa shuleni, baada ya kujifungua huruhusiwa kuendelea na elimu yao, akasema sisomeshi wazazi mie! Ikawa mwiko kuendelea na masomo! Lakini muda mwingi aliomba watu wamuombee, haya wanafunzi wazazi na vichanga vyao na wazazi wao wakaanza kuomba kwa Mungu wao, kumbe Mungu husikia bwana, si akajibu maombi, kesi ikaishia hapo, ikawa!
9. Mwendazake akaambiwa biashara ya korosho inalipa huko Lindi na Mtwara! Akasema hewala! lazima serikali ihodhi biashara yote ya korosho, kaingiza JWTZ, kangomba wakakiona cha moto, na hela ya mfuko wa uendelezaji korosho akakomba yote! Wakulima na kangomba wakala hasara! Wanawake na Shangazi wa kimakonde wakaambiwa wakithubutu kusema kitu wakakiona cha mtema kuni! wakakaa kimya na jaka moyo! Ila alisahau kuwa anawasihi watu kumuombea sana, Si watu wa kusini na wafanyabiashara wakakumbuka kuomba, wakaamua kuomba bwana, haikupita muda Mungu akaingilia kati, kaamua kesi, ikawa!
10. Mwendazake aliambiwa fuata utaratibu wa kuchukulia hatua taasisi za fedha kama ukiukwaji upo wa undeshaji wa biashara hiyo. Akasema sina muda huo, hapa nikuvamia na kupora hela na vitendea kazi kwanza halafu utaratibu ufuate, kaingiza jeshi hela ikaporwa. Akasahau kila akiongea na watu aliomba wafu wamuombee. Wahanga wa biashara ya beaural de change na familia zoa hasa wa Arusha wakaomba na kufunga. Mungu bwana kawasikiliza akaona wana hoja, kaingilia kati na kesi kaamua, ikawa!
Kwa machache hayo, Mwendazake aliambiwa na kushauriwa kuyaendea taratibu mambo mengi mathalan, uchumi na uwekezaji, ustawi wa jamii, kuvunja mikataba bila utaratibu, uhuru wa viombo vya habari, usalama wa raia, uhusiano wa mataifa jirani, manunuzi ya ndege na wapunzani, demokrasia na uchaguzi nchini na kadhalika ila hakusikia.
Kila akiumiza watu akawa anawasihi na kuwahiza wamuombee. Idadi ya aliowaumiza ikawa kubwa, waombaji na wafungaji wakawa wengi, kila mmoja kwa imani yake na Mungu wake akaomba, Mungu akashindwa kuvumilia na kuhimili kishindo cha maombi, akaamua kesi! Ikawa!