Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
"INFLUENCES POWER" au sisi wabongo husema ana nguvu ya ushawishi mkubwa sana katika kuleta wateja kwenye biashara yoyote ile tokana na umaarufu wake.Chief kwanza nikupongeze kwa hiki ulichokiandika. Pili ni kwamba watanzania wengi hawajui impact aliyokuwa nayo msanii hasa kwenye masuala ya biashara, Diamond ni msanii Mkubwa na ana influence kubwa kwa jamii. Kitendo alichofanya cha kupost video na kauli alizozitoa kina athari kubwa kwa Taasisi husika katika kupata abiria na kuongeza pato la uendeshaji wa huduma za taasisi hiyo. Diamond inabidi awe mfano kwa wasanii wengine katika kuheshimu biashara za watu binafsi na hata za taasisi za kiserikali.
Ningekuwepo pale airport ningemwambia Diamond... "GERARA HERE"
UpunguwaniKakutongozea mamaako au ?
Hata akihama bado Tanzania itaendelea kuwepo na dunia itazunguka tu, nakutolea mfano thabiti hata akina Lionel Mess huwa wanawajibishwa sana kisheria ikiwa hawakufuata sheria na kanuni za nchi.Mimi ningekuwa daimond ningehama nchi na ningebadili uraia,mbona wakati anauza mitumba basata hawakumsumbua?yani tuna baraza la kufungia nyimbo peke yake.
Si lazima kila mwenye mafanikio ajitangaze, USIKARIRIWewe usiye na laana ya baba umefanikiwa lipi kumzidi yeye ,waswahili bwana wivu cjui utaisha lini
Heeeh... Yaani bado unasisitiza kuwa ATCL wamemfungia diamond maisha?[emoji23][emoji23][emoji23] Kwanza lazima uelewe waliomfungia si ATCL ni Basata.
Pili HAWAJAMFUNGIA MAISHA. NI KWA MUDA USIOJULIKANA. AMBAO INAWEZA HATA KUWA SIKU TANO KAMA HUELEWI.
kwa nini watanzania wengi hawaelewi kiswahili au wanashindwa kuelewa kilichoandikwa ?
Nilivyoisoma post yako nikakumbuka kuwa Tanzania inaongoza kwa unafiki duniani ikabidi nutulie tu.
Mahaba ya ushabiki kwa mtu asiyejielewa akiongozwa na kiburi cha pesa ndiyo yanatusumbua kupagawa kiasi hicho chote Chifu.
Ni kwer kabisa mkuu...Hata hapa kwenye huu Uzi tayari wengi wameichukia ATCL ni dhahili kwamba chanzo ni msanii diamond...yeye mambo mengine anafanyaga ujinga lakin serekali inatambua umuhimu wake inaamua kupotezea lakini yeye kafanyiwa hivo kakimbilia Instagram...Duh....kweri wamemkosea lakini inapaswa afate masharti ..huyo alierekodiwa keshadhalilishwa kwa upande flani hivi...Natamani ungemuelewa walau kidogo mleta mada ..ingekusaidia sana .
.. Iwe tickets za wcb ziliuzwa kwa watu wengine au wcb walichelewa Ujinga alioufanya domo nikuipaka kinyesi taasisi nyeti ya serikali " kisha akakipost kinyesi chake kwenye mitandao ya kijamii ... huu ni uzwazwa mkubwa Sana ambao unapaswa kukemewa " diamond alipaswa kuwasilisha malalamiko yake katika uongozi wa ATCL ama kwenda kufungua kesi na kudai fidia .. nasio kufanya upuuzi alioufanya " ambao unapelekea kuchafua brand ya ATCL kibiashara " ... diamond ni kioo cha jamii anafuatiliwa na watu wengi inapotokea akawa na conflict na taasisi nyeti kama ATCL ni rahisi " sana kuifanya tasnia hiyo isiaminike pia itaingia hasara kwakukosa wateja " .... diamond akiwa kama icon alipaswa " kuweka uzalendo mbele nakuficha madhaifu ya ATCL asiyaonyeshe kwenye public..
.
.kisha angefuata protocol ambayo ilikuwa ni kwenda kufikisha malalamiko yake ama maoni katika uongozi husika " ..... so ule alioufanya ni ujinga " unaoweza kuligharimu shirika na kulifilisi " pia amechangia kutaka kuwavunja moyo " wafanya kazi wote wa ATCL na Raisi wa nchi ambao wamekuwa wakitumia ma billions ya fedha kuhakikisha kwamba " taasisi hii ya usafiri wa anga inaleta matumaini upya nchini na kulipatia taifa faida
Mwambieni huyo jamaa Yenu apunguze misifa itamuharibia Maisha yake
Natumai huo ni mwanzo tu " kuna vikwazo vingi toka serikalini ambavyo sio vya kupendeza " vinavyo mfuata.
Sana " yule mzee kadhalilishwa sana binafsi sikupenda alichofanyiwaNi kwer kabisa mkuu...Hata hapa kwenye huu Uzi tayari wengi wameichukia ATCL ni dhahili kwamba chanzo ni msanii diamond...yeye mambo mengine anafanyaga ujinga lakin serekali inatambua umuhimu wake inaamua kupotezea lakini yeye kafanyiwa hivo kakimbilia Instagram...Duh....kweri wamemkosea lakini inapaswa afate masharti ..huyo alierekodiwa keshadhalilishwa kwa upande flani hivi...
Asante mkuu " Unausimamia vyema Ukweli ..mwambie huyoMahaba ni utumwa sana katika sayari tunayoishi.
Ukikua utajitambua Chifu.
Taasisi ya umma haikosolewi? Hao wanaoongoza hiyo taasisi si ni binadamu kama wewe kwamba hawafanyi makosa?Natamani ungemuelewa walau kidogo mleta mada ..ingekusaidia sana .
.. Iwe tickets za wcb ziliuzwa kwa watu wengine au wcb walichelewa Ujinga alioufanya domo nikuipaka kinyesi taasisi nyeti ya serikali " kisha akakipost kinyesi chake kwenye mitandao ya kijamii ... huu ni uzwazwa mkubwa Sana ambao unapaswa kukemewa " diamond alipaswa kuwasilisha malalamiko yake katika uongozi wa ATCL ama kwenda kufungua kesi na kudai fidia .. nasio kufanya upuuzi alioufanya " ambao unapelekea kuchafua brand ya ATCL kibiashara " ... diamond ni kioo cha jamii anafuatiliwa na watu wengi inapotokea akawa na conflict na taasisi nyeti kama ATCL ni rahisi " sana kuifanya tasnia hiyo isiaminike pia itaingia hasara kwakukosa wateja " .... diamond akiwa kama icon alipaswa " kuweka uzalendo mbele nakuficha madhaifu ya ATCL asiyaonyeshe kwenye public..
.
.kisha angefuata protocol ambayo ilikuwa ni kwenda kufikisha malalamiko yake ama maoni katika uongozi husika " ..... so ule alioufanya ni ujinga " unaoweza kuligharimu shirika na kulifilisi " pia amechangia kutaka kuwavunja moyo " wafanya kazi wote wa ATCL na Raisi wa nchi ambao wamekuwa wakitumia ma billions ya fedha kuhakikisha kwamba " taasisi hii ya usafiri wa anga inaleta matumaini upya nchini na kulipatia taifa faida
Mwambieni huyo jamaa Yenu apunguze misifa itamuharibia Maisha yake
Natumai huo ni mwanzo tu " kuna vikwazo vingi toka serikalini ambavyo sio vya kupendeza " vinavyo mfuata.
Hahaa mindset za watu wengi sana wanadhani kuwa kufanikiwa nikuwa na ukwasi tu pekee " huu ni ujuha" ... kwa mantiki hiyo waliyonayo basi tunaweza kusema kuwa che Guevara" na wana harakati wengi sio watu waliowahi kufanikiwaKufanikiwa siyo kuwa vizuri kiuchumi, je mahusiano yako na jamii inayokuzunguka katika maisha uishiyo inaakisi au inazaa matunda mema kwa kumpendeza Mungu?
Kila mwenye pesa anaishi maisha ya furaha(ametawaliwa na amani nzuri rohoni mwake)?
Weka hapa ushahidi kama alichelewa airport....Tupe ushahidi kama kweli aliwahi airport?
Hahaaa inamaana round hii bashite hana cha kuwafanya BASATA ??Dah...hili ni somo jingine tena...hasa kwa wale wote wasiotaka kuelewa nguvu ya aliyempiga Goliath...[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Muwage mnasoma nakuelewa basiii "" gosh mnachosha ".... wapi nimesema kwamba taasisi ya serikali haikosolewi "!?Taasisi ya umma haikosolewi? Hao wanaoongoza hiyo taasisi si ni binadamu kama wewe kwamba hawafanyi makosa?
Management yake ndio inabidi ilaumiwe,Diamond ni mwanamuziki makubwa mwenye hadhi kubwa kama waziri au balozi,yote haya yasingetokea kama angekuwa na meneja uhusiano mzuri,ambaye angekuwa amefatiria ishu ya tiketi mapema,na kumwepusha Mond na balaa hili LA kutoa maneno ya ovyo na kurekodiwa,au angewaona basata au viongozi wa ATCL mapema na kusawazisha mambo,kabla hayajaharibika.Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) limetangaza kumfungia msanii Diamond Platnumz na mwenzake Rayvanny kufanya maonesho yoyote ndani au nje ya nchi kwa muda usiofahamika. Si hivyo tu, bali pia wamelifutilia mbali Tamasha la Wasafi Festival ambalo limekuwa gumzo kubwa katika siku za hivi karibuni.
Sababu zinazotolewa na Basata, ambazo zina ushahidi wa wazi, ni kwamba msanii huyo amekiuka maelekezo aliyopewa na Basata, ya kuacha kuperform wimbo wa Nyegezi (Mwanza) uliofungiwa na Basata kwa kile kilichoelezwa kwamba ni kukiuka maadili ya Kitanzania.
Tukio la Diamond kupigwa pini na Basata, limekuja muda mfupi baada ya Mbongo Fleva huyo kusababisha hali ya sintofahamu katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza baada ya video kusambaa kwenye mitandao ya kijamii, ikimuonesha 'bwa mdogo' huyo akiwatemea mbovu wafanyakazi wa uwanja huo, kwa kile alichodai kwamba wamemchezea rafu kwa kuuza tiketi alizozifanyia booking mapema na kusababisha ashindwe kusafiri kurejea Dar baada ya kumalizika kwa shoo yake jijini Mwanza.
Madai hayo yalililazimu shirika la ndege la ATCL kutoa tamko rasmi na kukanusha madai ya Diamond ambapo taarifa ilieleza kwamba hakuna aliyeuza tiketi yake isipokuwa yeye ndiye aliyefanya makosa kwa kuchelewa kufika uwanja wa ndege hivyo kwa mujibu wa kanuni na taratibu, alipoteza sifa za kusafiri na ndege hiyo hivyo kuomba kupangiwa siku iliyofuatia.
Kabla ya ATCL kutoa ufafanuzi huo, watu wengi waliotazama video hiyo, waliamini kwamba kweli ATCL wamefanya uzembe, wamepiga dili kwa kuuza tiketi ya Diamond na kundi lake kwa watu wengine, kwa lugha nyepesi Diamond aliwaaminisha watu kwamba ATCL si waaminifu kwa wateja wake na ndiyo maana wameuza tiketi ambazo zilishafanyiwa booking kwa watu wengine.
Ikumbukwe kwamba ATCL ni shirika la serikali na serikali ya awamu ya tano imewekeza nguvu kubwa kulihuisha shirika hilo lililokuwa mahututi kwa kununua ndege mpya na kulifanya sasa angalau liwe na uhai baada ya kudoda kwa muda miaka mingi. Tayari ndege tano zimeshafika nchini na zinafanya kazi na matarajio ni kuleta mashine kubwa zaidi, Airbus mapema mwezi huu.
Wakati serikali ikihangaika kuhakikisha ATCL inapata wateja wa uhakika na kujiendesha kwa faida, anatokea 'mwehu' mmoja na kuibua tuhuma ambazo zinawafanya wateja wapoteze imani na shirika hilo na hivyo kulikosesha wateja na mapato.
Diamond ambaye kwa heshima na taadhima, alialikwa wakati moja kati ya ndege hizo ikiwasili nchini, badala ya kuwa balozi wa kuwahimiza watu wengine watumie huduma za ATCL, yeye anahujumu kwa kuibua tuhuma za uongo zenye lengo la kuikosesha ATCL wateja na mapato.
Fyekelea mbali ili siku nyingine ajifunze kuwa na adabu na uzalendo! Siku zote serikali inaweza kuwa inajua kwamba unafanya makosa lakini kwa sababu hugusi maslahi yake, ikakuacha uendelee kukosea! Ndiyo, kwani Diamond ameanza kuidharau Basata leo kwa kuimba Nyegezi? Upo ushahidi wa mpaka video akiwa Zanzibar na kwingineko, alionekana akiwaimbisha mashabiki kijanja.
Kama ishu ingekuwa ni hiyo tu, Basata wangeweza kuweka pamba masikioni au kuitana kishkaji, Mngereza alikuwepo kwenye uzinduzi kule Mtwara, kwa hiyo kwao siyo adui tena bali mlezi, wangeweza kunena kwa lugha moja wakayamaliza ili kuepusha hasara ya mamilioni ambayo sasa ataipata kwa kufungiwa.
Diamond, man up! Don't mess with the government!
We jamaa wakati anauza mitumba alikuwa na nguvu ya ushawishi kwa jamii?? Hata hizo taratibu za ndege alikuwa anazijua?? Ndege alikuwa akiziona angani tu na kusikia muungurumo wakeMimi ningekuwa daimond ningehama nchi na ningebadili uraia,mbona wakati anauza mitumba basata hawakumsumbua?yani tuna baraza la kufungia nyimbo peke yake.