JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,780
- 6,607
Baadhi ya Wanawake wa Kijiji cha Shirimatunda, Kata ya Mnadani, Wilaya ya Hai wamekazimika kukimbia makazi yao kutokana na kuibuka kwa wimbi la Wanaume wanaofanya vitendo vya ubakaji.
Matukio hayo yanadaiwa kutokea katika maeneo ya mtoni wakati Wanawake wakifuata maji, ambapo wanaofanya tukio hilo wanajulikana kwa majina ya ‘Teleza’
Wanawake wa Kijiji hicho wametoa malalamiko yao hayo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Stephen Kagaigai wakati alipofanya ziara wilayani humo kukagua miradi ya maendeleo. Baada ya kupata malalamiko hayo, Kagaigai amemuagiza RPC wa Kilimanjaro, Simon Maigwa kushughulikia tatizo hilo.
Mtendaji wa Kata ya Mnadani ajili ya ziara ya Sembuli Mkilaha amelikiri kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi na kuyafikisha kwenye mamlaka husika ya wilaya hiyo.
Naye, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amesema ataunda kamati kuhakikisha wanaofanya vitendo hivyo dhidi ya Wanawake wanakamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Matukio hayo yanadaiwa kutokea katika maeneo ya mtoni wakati Wanawake wakifuata maji, ambapo wanaofanya tukio hilo wanajulikana kwa majina ya ‘Teleza’
Wanawake wa Kijiji hicho wametoa malalamiko yao hayo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Stephen Kagaigai wakati alipofanya ziara wilayani humo kukagua miradi ya maendeleo. Baada ya kupata malalamiko hayo, Kagaigai amemuagiza RPC wa Kilimanjaro, Simon Maigwa kushughulikia tatizo hilo.
Mtendaji wa Kata ya Mnadani ajili ya ziara ya Sembuli Mkilaha amelikiri kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi na kuyafikisha kwenye mamlaka husika ya wilaya hiyo.
Naye, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amesema ataunda kamati kuhakikisha wanaofanya vitendo hivyo dhidi ya Wanawake wanakamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.