Kilimo kinalipa kama ukikifanya kama kazi

Kilimo kinalipa kama ukikifanya kama kazi

Labda vuli isinyeshe, mvua za vuli zikinyesha, mwezi pili watu wanavuna na bei inaporomoka ghafla.
Sio mikoa yote inayolima vuli, kumbuka mwaka huu karibia maeneo yote ya nchi mvua zilikua hafifu
 
Sema mwaka huu wakulima wa mahindi wanachekelea. Miaka mingine kwa hayo mavuno ungeishia kupata laki 7 au 8 ambayo ni sawa na bureee.
 
Natoa ushuhuda wangu wa kilimo cha mahindi nilichofanya msimu wa 2022

Niliandaa shamba ekari 3 kwa tsh 180,000.

Nilinunua mbegu aina ya Dk mifuko 7 ya kilo 2 kwa garama ya tsh 91,000.

Gharama za kupandà ni tsh 60,000.

Palizi 180,000.

Jumla ya garama zote ni tsh 511,000.

Mavuno niliyopata ni gunia 22.

Bei ya gunia moja kwa sasa ni elfu 95.

Siwezi kuuza sasa hivi kwa sasa nitayahifadhi mpaka mwaķani mwezi wa pili.

NB:
Mbegu zimeìngia chache sababu shamba lina mazao mengine kama michungwa, minazi na miģomba
Vijana tuacheni kulalamika kilimo kinalipa ukiwa makini

kaka kilimo chako unakifanyia wapi?
 
Nina ekari kumi zangu ila sijaona manufaa ya kilimo..nip3ni maarifa mkuu
cha msingi elewa kila shughuli hapa duniani inalipa kulingana na wakati wake. wakulima wa mahindi msimu huu wanajinasibu kwa sababu ya hali ya hewa ilikuwa mbovu na wengi wameangukia pua kwenye mahindi, wachache waliotoboa ndio wanatusisimua hapa kuwa kilimo cha mahindi kinalipa.

"Usiingie shambani kwa kusisimuliwa na shuhuda za watu". Ingia shambani kwa sababu umejiandaa kukutana na hali zote mkuu
 
Mshukuru Mungu umevuna kipindi ambacho mahindi yapo bei nzuri. Ungekutana na bei ya gunia elf 30 mpaka 40 ndo ungefahamu kama kilimo kinalipa kweli au ni story tu.
Hakuna nyakati gunia lingeuzwa kwa bei ya 30 au 40 kwa miaka 10 nyumaila serikali ndio ilikuwa inawaminya wakulima kwa kufunga mipaka kwa kigezo cha kuepusha taifa na njaa ikimnufaisha mfanyakazi,biashara, bila kujali mkulima nguvu,muda na gharama anayotumia kwa msimamo wa Sasa wa serikali hata vijijini tutaanza kuona nyumba za bati na wale wa mijini waidai serikali ongezeko ktk kile walichokuwa wanamdhurumu mkulima ili kubalance maisha.

Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu kwa heka moja kwa makadirio yako alitakiwa apate gunia ngapi mkuu? Tupe uzoefu wako mkuu.
nakazia tu ekari moja huwa ni around 13 up 18 hili ni kadirio kwa mkulima mzoefu gunia 22 ekar tatu daah hapana aise maana yake kalma ekar moja na nusu
 
cha msingi elewa kila shughuli hapa duniani inalipa kulingana na wakati wake. wakulima wa mahindi msimu huu wanajinasibu kwa sababu ya hali ya hewa ilikuwa mbovu na wengi wameangukia pua kwenye mahindi, wachache waliotoboa ndio wanatusisimua hapa kuwa kilimo cha mahindi kinalipa.

"Usiingie shambani kwa kusisimuliwa na shuhuda za watu". Ingia shambani kwa sababu umejiandaa kukutana na hali zote mkuu
kweli mkuu aingie uwanja wa vita akutane na hali halisi kilimo kina changamoto asikuambie mtu,naongea kama shahidi kwa yaliyo nikuta mwaka huu ekar nne cjavuna

ekari 4 kukodi 100000 *4=40 0000
kulima na trekta kila ekar 45000

mbegu mifuko 12 kila mfuko 12000elfu

palizi kwa kila ekar elfu 44000


bado dawa na dharura mkuu shkuru umepata hcho kidogo
 
Back
Top Bottom