Kimara, Dar: Polisi wawakamata kwa uzururaji Daktari chriscyrilo na Daktari Shindo Kilawa

Kimara, Dar: Polisi wawakamata kwa uzururaji Daktari chriscyrilo na Daktari Shindo Kilawa

Hivi huu utaratibu wa kukamatana bila kuambiwa kosa, kupitia serikali ya mtaa, bila ya taarifa ya kuitwa polisi au mahakamani ni utaratibu wa askari wa Tanzania pekee? Sheria inasemaje kwani wakikuhitaji kwenda polisi either kwa mahojiano au vyovyote vile?
Tuna sheria za aina yake...
 
Return Of Undertaker, Kumbe ni makamanda? Siku nyingine tafuta Uzi Wa makamanda halafu uwataarifu makamanda wenzenu,mana kwa raia Wa kawaida kama sisi yanakuwa hayatuhusu
 
Ndugu kuna utaratibu wa kisheria wa namna polisi anavyotakiwa kufanya ili kumkamata mtu. Utaratibu huo usipofuatwa polisi wanageuka kuwa watekaji tu na wasiojulikana. Na mambo haya ya kukamatana kienyeji ni kawaida sana ambapo polisi wenyewe walibainisha ukamataji huo kuwa ni watu wasiojulikana
Hii nchi inamaajabu mengi Sana, msomi na mjinga huwezi kuwatofautisha, inawezekanaje mtu tunayemuona angalau alimaliza darasa la saba anaandika tarifa ya watu kutekwa na wasiojulikana

Halafu hiyohuyo ndani ya tarifa zake hizo anahitimisha kuwa watu waliokuwa wametekwa na wasiojulikana Wapo kituoni na wameachiwa, hatuoni kwamba huo ni uduni wa mtoa tarifa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi huu utaratibu wa kukamatana bila kuambiwa kosa, kupitia serikali ya mtaa, bila ya taarifa ya kuitwa polisi au mahakamani ni utaratibu wa askari wa Tanzania pekee? Sheria inasemaje kwani wakikuhitaji kwenda polisi either kwa mahojiano au vyovyote vile?
Haya ndio makosa na matokeo ya kuajiri watu wenye elimu duni kufanya kazi yenye kuhitaji kureason! Hata polisi wa kikoloni hawakuwa na ubazazi huu uliopo Sasa! Hakika, jeshi la polisi ni la kuvunjiliwa mbali na kusukwa upya kitaalaamu!
 
Korona itaondoka na wengi, swali la kizushi aliyesikia watekaji wakijitambulisha kuwa ni askar wa jeshi la polisi ni Nani? Na alikuwa wap mpak akaiona hyo gar kuwa ni defender??? Bas tuanze na huyo ili kuharakisha upelelezi na madaktar wapatikane mapema iwezekanavyo
Naifananisha hii ishu na scenario ya Prof Assad. Mtu kaenda shambani simu haipatikani kuna mwanasiasa(kapuni) akasema ametekwa.

Kutekwa imekuwa kama mbinu ya upinzani kuipaka nchi matope. Japokuwa kuna tatizo pia namna gani polisi wanawakamata watuhumiwa. Labda hili nalo linaleta shida kwa wananchi.

Hasa ukiangalia Eric na wale jamaa wa lhrc walivyokamatwa inaleta picha mbaya.
 
Nionavyo Mimi hawa vijana wetu wanafanya fujo sana, hawafuati sheria wala utaratibu.

Mimi ninafikiria mamlaka hasa IGP awatangazie wananchi kwamba hawa watu wanapokuja kumkamata mtu wafuate sheria na utaratibu.


Ndiyo wakati mwingine mtu anakamatwa mjini sio nyumbani basi waoneshi vitambulisho na kuwaruhusu mtuhumiwa aongee na wakili wake kwamba amekamatwa na askali flani namba flani na anaelekea kituoni.


Kwa kweli huu ujinga ujinga umepitwa na wakati tena ni ushamba tu.

Wanapokataa kuonesha vitambulisho maana yake wanapoteza utambulisho wao, kwa hiyo wanakuwa hawana tofauti na majambazi, wezi na magaidi.

Je Jeshi la polisi linafuga magaidi?.


TUNAOMBA UFAFANUZI KWA IGP AU JESHI LA POLISI KUHUSU UTARATIBU WA KUMKAMATA MTUHUMIWA NA HAKI ZAKE KAMA RAIA NA HAKI YA POLISI KAMA AFISA MTIMZA WAJIBU.


Kwa kweli huu utaratibu wa kuja na madifenda na kuwakamata watu na kisha ndugu na jamaa hawajui walipo, baadaye kwa aibu mnakuja kusema mnawashikilia.

Tuanhisi Hofu

Tuanhisi hatuko salama.

Tunahusi kunyanyaswa.

Tunahisi jeshi letu halifanyi kazi zake kiutaratibu..



Any way tukikumbuka ya Tundu Lissu mpaka leo hakuna aliyekamatwa na wala hakuna kinachoendelea tunawaza kama Mbunge akiwa bungeni anapigwa risasi na Polisi wapo, Usalama wapo na hakuna kinachoendela.

Nachelea wananchi hatuko salama na hata nchi ipo mashakani.
 
Ni makada/waamini/ wafuasi wa chama gani cha siasa hapa Tanzania?
 
Back
Top Bottom