Kina Mangi njooni tubadilishane uzoefu. Tushirikiane.


Wahindi kwny maduka yao customer care ni ya kisenge tu,sema tu jamaa wamefanya biashara kwa muda mrefu wana connections na financial displine ya kutosha.
 
Wahindi kwny maduka yao customer care ni ya kisenge tu,sema tu jamaa wamefanya biashara kwa muda mrefu wana connections na financial displine ya kutosha.
Kuna ukweli hapo ila kataa kubali hawa jamaa walikuwa wanatoboa sababu ya kukwepa kodi, hasa bandarini, kuna wahindi mwanza pale walikuwa na stationery kama tatu mjini kati rimpepa zile walikuwa wanauza karibu nusu bei na walikuwa wanauza balaa mpaka magu, ukerewe, Geita, Bukoba, mara visiwani huko wanatuma mizigo, saivi ukioneshwa ndio wenyewe utapinga mpaka unaingia kaburini

Zipo factors nyingi zinazochangia mafanikio kwenye biashara ila zipo nyingine zimejificha sio rahisi watu wazishtukie japo utajaribu kumuiga kila kitu.
 
Yeah ila kuna mikoa hawawezi kabisa kufungua hata genge la nyanya chungu bila kwenda kwa fundi.
Naonaga waha wakija mjini toka Kigoma wana anza na kaduka kadogoooo na analala humo humo dukani utamuona tu na kajiko kake ka mafuta ya taa na gunia lake la dagaa ambalo ametoka nalo kigoma ndo msosi wake huo na likiisha baada ya muda anapiga simu Kigoma linaletwa jingine kwa treni,ila baada ya miaka 3 au 4 unasikia amejenga ana ka usafiri..

Ila pia kwa mitishamba wako vzr sana.
 
Mnapambana vp na madeni
Hakuna kitu inakera kama madeni aisee kwenye biashara. Unapoanza biashara yako watu watakuja na Cash kwawingi na kukupa moyo, kadri siku zinavyosonga mbele wakishazoeleka wanaanza sasa kuja kukopa. Ukizingatia mtaji wako ni mdogo unategemea uukuze kwa kuzungusha hela yako, ila kila ukipiga hesabu unakuta hela asilimia kubwa iko mikononinmwa mwatu kuliko uliyo nayo mkononi.

Muhimu ni kuwa strict na biashara yako, ni heri uwe na mauzo kidogo kuliko kujiona unauza bidhaa nyingi sana kwa siku kumbe kwa mkopo.

Weka msimamamo wa kutokopesha kabisa, wakiliewa hilo wataanza kuja wenyewe. Unaweza legeza masharti kwa wateja wachache sana, ambao unajua ni waaminifu na hulipa kwa wakati.
 
Hahaha waha ndio wafanyabiashara mashuhuri huko Geita, Kahama, Bukoba mpaka Mwanza wanasifika kwa uchakarikaji na kiukweli wanafanya kazi haswa ila mitishamba utamuua ukimuambia aache

Halafu ni Mentality tu ya hovyo Watanzania tunaendekeza tayari watu wana imani kubwa kwamba bila ndumba hawatoboi kama huko Njombe ndio balaa sababu kule wana uchawi mpaka wa kuhamisha mazao kwenye mashamba ya watu.
 
Sawasawa kabisa mkuu,hpo kwny kukwepa kodi hao ndio ma master,sisi weusi kukwepa kodi tunasingiziwa tu bado hatujakomaa vzr.

Nadhani ndio maana kuanzia wakina Gachuma,Mengi etc na matajiri wengineo wenye ma co. watu wao wa finance(Top) ni wahindi tu nadhani watakua wanawakubali kwny kufanya manuva huko kwny kodi.
 

Hahah huo uchawi wa kuhamisha mazao kwenye mashamba ya watu sijawahi kuusikia,na unafanya kazi fresh kwny mashamba ya watu?
 
Hahah huo uchawi wa kuhamisha mazao kwenye mashamba ya watu sijawahi kuusikia,na unafanya kazi fresh kwny mashamba ya watu?
Hahaha babu kule kuna uchawi wa rejareja tena sio huo tu sababu huo mpaka mbeya upo, kuna uchawi mpaka wa kuhamishiwa mkojo, yaani mpo vilabuni huko mnakunywa mataputapu kuanzia mchana mpaka usiku ila huwa kuna wazee hawaamki kwenda chooni kuanzia mwanzo wa gambe mpaka mwisho πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

Hiyo kazi wanapichikiwa vijana πŸ˜…πŸ˜…
 
Hongera sana mkuu
 
Unapoamua kufanya biashara unapaswa kujitengenezea territory yako au uwe affiliated kwenye network fulani, unahitaji connection tra, manispaa, polisi, serikali ya mtaa, sekta za kifedha bila kusahau madalali wa mizigo ya kupigwa nk. Ukifanikiwa kujipenyeza kwenye network sahihi, hakika utafanikiwa.
 
Hiyo biashara siyo kabisa yaani duka liliisha mpaka Leo nina super glue, uzi wa kushonea nguo, pins kibao ndani.
Ila kuna biashara hata ukitoa laki 2 hautetereki wala kugusa mtaji.
😁😁😁😁 niuzie super glue moja mkuu
 
hili la vijana kukaa nje linahusu sana asee yaan kwa mfano saloon unakuta watu wamejaa wanapiga story yaan ukiingia hv wote macho kwako....yaan saloon za kihvo huwa siingii hata iweje
 
Mm Sina starehe ila napenda kuwa na uhuru na pesa yangu aisee..wengine tuko radhi kwenda mkoa mwingine kula bata✌🍷
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ manengelo maisha yenyewe mafupi na pesa haijai so unachagua biashara ya akili na siyo ya kujibana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…