Kinachoendelea Msumbiji, magaidi na Jeshi - Part 3

Kinachoendelea Msumbiji, magaidi na Jeshi - Part 3

Hiyo mbinu ya Winning hearts and Mind strategy ina fanikiwa vipi wakati jamii ina fahamu matatizo yote hayo yana sabibshwa na kikundi hicho ndio maana serikali imeingia vitani kuwaondoa
Pale mwenye nyumba haaminiki; hana uwezo, mengine post na. 9 imejibu.
Ya Crystal Ventures ndio mishe za 'vijana' wanapotumwa kufanya nje ya himaya.
Vp kuna mwenye clue yoyote ya mishe za SUMA JKT?
 
Huu uzi wa SteveMollel ni Kati ya nyuzi bora sana humu jf katika miaka ya hivi karibuni; ila naamini huyu mwamba yupo au ni mtaalamu wa maswala ya ulinzi na ujasusi.
Imagine ukusanyaji huu wa taarifa na picha halisi za matukio je ni uwezo wa mtu wa kawaida ambae sio TISS au MI ya TPDF?
Bro tulia Sisi tuendelee na story usianze habari kufukua mwandishi ni nani sijui nini yasije yakawa yale ya yoga na Dark Days SteveMollel lete sehemu ya 4
 
- Shambulizi la kigaidi mji wa Macomia mwezi jana.

- Oparesheni ya SADC na jeshi la Rwanda.

- Interest ya Kagame katika vita za wengine.


Wa kwanza kufika hapa Msumbiji ni jeshi la Rwanda. Kwa makubaliano ya siri yalowekwa na raisi wa Msumbiji, Felipe Nyusi, na raisi wa Rwanda, Paul Kagame, polisi 300 na wanajeshi 700 wanaingia nchini kuanzia tarehe 9 July, 2021.

View attachment 3008214

Kikosi hiki maalum kinaongozwa na jenerali Innocent Kabandana (pichani) kabla ya hapo baadae kuja kupandishwa cheo kuwa Lt. General kwa oparesheni kubwa yenye matunda hapa nchini Msumbiji.

View attachment 3008215

Siku sita baadae, tarehe 15 July, ndo' kikosi cha SADC kinaingia hapa. Kikosi hiki kina jumla ya wanajeshi 2,200 wengi wao wakitokea Afrika Kusini ambapo ndo' pia anatokea kamanda wa kikosi hiki cha SADC, jenerali Xolani Mankayi. (pichani)

View attachment 3008216

Kwa pamoja, makamanda hawa wawili, Innocent Kabandana (wa Rwanda) na Xolan Mankayi (wa SADC) wanashirikiana na kamanda mwenyeji, Cristovao Chume (pichani), kupanga misheni ya kupambana na magaidi wa Ansar al-sunna.

View attachment 3008217

Jeshi la Rwanda linakabidhiwa mji wa Palma na Mocimboa de Praia na lile la SADC linapewa miji kama vile Nangende, Mueda na Muidumbe.

View attachment 3008218

Kuanzia hapo, magaidi ya Ansar al-sunna yakaepuka kufanya mashambulizi makubwa kwenye miji mikubwa, badala yake wakawa wanashambulia kidogo na kukimbia (small hit-and-run raids), haswa vijiji vidogo visivyo na ulinzi ama kambi ndogo za jeshi zisizokuwa chini ya uangalizi.

Oktoba 2022, magaidi wanavamia maeneo mapya kabisa ambayo hayakuwahi kushambulia hapo kabla. Maeneo ya kusini mwa Cabo Delgado kama vile Namumo, Balama na Montepuez na sio tena kaskazini kama vile Palma na Mocimboa de Praia.

View attachment 3008219

Baadae magaidi wanakuja na mkakati maalum. Wakiendelea kushambulia kule kusini, wanafanya tukio kubwa kaskazini kwa kuvuka mpaka wa Tanzania na kushambulia vijiji vya Kitaya na Michenjele kule Mtwara.

Wanaharibu, kuteka na kuua.

Lengo lao kugawa 'attention' ya vikosi hivi vipya ndani ya Msumbiji, vigawanyike kuzingatia kaskazini na pia kusini mwa Cabo ili wapate mwanya wa udhaifu kushambulia zaidi.

View attachment 3008221

Bahati mbaya mpango huu hauzai matunda na mpaka kufikia ukomo wa mwaka 2022, oparesheni ya kuwadhibiti inafanikiwa kuwapunguza kwa idadi kubwa sana.

Ripoti ya UN Security Council inasema kati ya magaidi 2,500 mpaka 3,000 walipoteza maisha kwenye oparesheni hii.

Matokeo yake tunakuja kuuuona mwaka 2023 kama mwaka tulivu zaidi tofauti na miaka ya nyuma tangu pale 2017. Kwa sasa ni wastani wa matukio 11 kwa mwezi ukilinganisha na hapo 2022 kulipokuwa na wastani wa matukio 36 kwa mwezi.

View attachment 3008224

Ndani ya mwaka huu (2023), Ansar al-sunna wanabadili mbinu na kuanza kutumia 'winning hearts and minds' strategy. Mbinu ya kushinda na kuvutia mapenzi ya watu kwa kutembelea jamii maeneo ya Macomia na Mocimboa ili kufanya nao biashara na kuwaambia wao si watu wabaya.

Hivyo mambo yanatulia kidogo.

View attachment 3008226

Lakini kwenye kimya hiki, kinakuja kishindo kikubwa sasa kuanzia mwanzo wa mwaka 2024.

Mwaka unaanza kwa tabu.

Siku ya tarehe 21 January, magaidi wanashika kijiji cha Mucojo na kuweka sheria kali kwenye mavazi, haswa kwa wanawake, na wanapiga marufuku uuzwaji na unywaji wa pombe, lakini chini ya wiki mbili wanadhibitiwa na kuondoshwa.

View attachment 3008229

Wiki moja mbele, tarehe 31, wanashambulia msafara wa wanajeshi na kusababisha vifo vya wanajeshi wawili.

February 9, wanashambulia eneo la Mazeze na kuchoma makanisa yaliyokuwa yanahifadhi watu.

View attachment 3008230

Lakini kilele cha mwaka huu ni siku ile ya Ijumaa, tarehe 10 mwezi wa tano katika mji wa Macomia.

View attachment 3008232

Siku hiyo, kwenye majira ya alfajiri, magari yalobebelea wanaume zaidi ya mia mbili wenye silaha za moto, yanavamia Macomia kupitia magharibi (Xinavane), kusini (Bangala) na mashariki (Nanga) ili kuwakuta wanajeshi wa Msumbiji katikati.

View attachment 3008233

Swala la kufumba na kufumbua, mvua ya risasi inaanza kushuka kila kona.

Kujiokoa roho zao, watu wanakimbilia huko porini na mashambani.

View attachment 3008234

Simu inaita upesi kwa jeshi la Rwanda pamoja na la SADC kuwa Macomia hali ni tete na unahitajika msaada wa haraka sana.

Magari yalobeba wanajeshi wa RDF na SADC yanatoka mji wa Pemba, mji mkuu wa jimbo la Cabo Delgado, na kuanza safari ya kwenda kuokoa jahazi huko Macomia.

View attachment 3008236

Baada ya mapambano makali, mabwana wanazidiwa na kuondoka lakini baada ya dakika arobaini na kitu, wanarudi tena na mapambano yanazuka upya.

View attachment 3008237

Ni mpaka tarehe 12 May, baada ya siku mbili, ndipo jeshi la Msumbiji na washirika wake wanafanikiwa kuurejesha mji wa Macomia mikononi.

View attachment 3008238

Serikali ya Msumbiji, kwa ajenda wanayoijua wao wenyewe, wanaficha maswahibu yalotokea katika huu mji lakini shida huwezi kufumba macho na mdomo wa kila mtu.

Waliokuwapo wanasema waliona miili ya watu kuanzia kumi mpaka ishirini na tatu. Wanajeshi kadhaa waliuawa, maduka kadhaa yaliporwa na pia 'ambulance' moja ilibebwa.

View attachment 3008240

Hivyo kwa hali hii, tofauti kidogo na hapo nyuma, hatuwezi tukasema hali ni shwari hapa jimboni Cabo Delgado.

Sasa kwenye nyakati hizi za mashaka, 'members' wa SADC, hususani Afrika ya Kusini, Botswana na Lesotho, zinaondoa majeshi yao hapa nchini Msumbiji.

Kama haitoshi, oparesheni yenyewe ya SADC inatarajiwa kufikia mwisho rasmi tarehe 15 July mwaka huu.

View attachment 3008241

Just imagine.

Lakini ajabu upande wa pili, kwa wenzetu wa Rwanda, ambaye si hata mwanachama wa SADC, mambo ni kinyume kabisa na hawa wengine.

View attachment 3008242

Kwanza jeshi hili, kwa namna ya pekee, limejichimbia kwenye mioyo ya wanamsumbiji, wanajeshi wake wanaaminika zaidi ya wenyeji wao linapokuja kwenye swala la uadilifu na ufanisi.

Mara kadhaa, wanajeshi wa Msumbiji wanaleta shida kwa wananchi. Wanafanya uonevu. Wanaiba. Wananchi wanaita wanajeshi wa Rwanda kuja kuwatetea na kweli wanaupata msaada.
(pichani wananchi wa Msumbiji wakiwa wamebebelea picha za Kagame na Nyusi)

View attachment 3008243

Lakini pili, wakati wengine wanabeba mabegi kuondoka hapa nchini Msumbiji kama tulivyoona hapo juu, Rwanda ndo' kwanza anasogeza kiti chake apate kuketi vizuri.

Jenerali Karuretwa (pichani), kiongozi wa ushirikiano wa kijeshi kimataifa nchini Rwanda, anasema;

"Kuondoka kwa majeshi ya SADC nchini Msumbiji kunatufanya tuchukue hatua fulani ... tutawapa mafunzo wanajeshi wa Msumbiji ili kuyachukua maeneo yaliyoyoachwa na jeshi la SADC na pia tutaongeza idadi ya wanajeshi kucover maeneo zaidi."

View attachment 3008244

Mbali na fungu la pesa linalotoka Umoja wa Ulaya (EU) kwenda kwa Rwanda, jenerali Karuretwa anasema kuguswa kwa Rwanda katika oparesheni za kutunza amani ni matokeo ya mauaji ya kimbari, mwaka 1994.

Kama watunza amani wa Umoja wa Mataifa wasingeliwatelekeza, basi wangelinusurika na kikombe kile cha mauaji, hivyo wanaujua umuhimu wa kuitunza amani.

Ikumbukwe mbali na Msumbiji, Rwanda wana jeshi lao kule jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) tangu walipopeleka kikosi chao cha kwanza Januari, 2014 baada ya makubaliano ya Kagame na Raisi Faustine Touadera.

View attachment 3008245


Mpaka kufikia sasa wanajeshi wa Rwanda katika nchi hiyo ni zaidi ya alfu moja, wakiwa hapo kwa makubaliano rasmi ya kuisaidia nchi hii maskini barani Afrika kupambana na waasi wanaoitaka serikali kwa udi na uvumba.

View attachment 3008246

Achilia mbali hapo, tarehe 15 April 2023, Raisi Kagame anafunga safari mpaka nchi ya Benin kukutana na Raisi Patrice Talon ambaye katika kikao anamuahidi kumpatia msaada wa jeshi kupambana na magaidi wanaotokea mipaka ya kaskazini.

View attachment 3008247

Sasa yote haya Rwanda anayafanya kwa gharama ya kitu gani?

Ananufaika vipi na wanajeshi wake waliotapakaa Afrika kupambana na kifo uso kwa uso?

Bila ya shaka kuna mchezo Rwanda anaucheza na mchezo huo unamwingizia zaidi kuliko vile anavyopoteza. Na hii inamfanya autake mchezo zaidi na zaidi.

Kwenye mchezo huu, mbali na kocha mwenyewe bwana Kagame, kapteni si mwingine bali kampuni ya CRYSTAL VENTURES Ltd (CVL). Kampuni yenye thamani ya zaidi ya dola milioni 500 za kimarekani.

View attachment 3008249

Kampuni hii iliyoanzishwa 1995, ni mkono wa kuume wa chama tawala hapa Rwanda (RPF) na inashikilia karibia kila nyendo ya kiuchumi katika nchi hii kwa kupitia makampuni yake madogo madogo yanayosimama kama matawi.

View attachment 3008251

Mkono wa kampuni hii unagusa kuanzia sekta ya kilimo, madini, ujenzi na hata ulinzi.

Kuanzia 2014, wawakilishi wa kampuni hii wanaambatana na serikali yao kwenda nchini Afrika ya kati, nchi ambayo Rwanda imepeleka wanajeshi wake kupambana na waasi, na tokea hapo wamekuwa wakifungamana na Afrika ya kati kwa makubaliano kadhaa.

Mojawapo ni lile la mwezi wa 9, 2021 ambapo tawi la CVL, Vogueroc, linaidhinishwa na serikali ya Afrika ya kati kufanya uvumbuzi wa migodi ya dhahabu na almasi nchini humo.

THERE'S NO FREE LUNCH.

Hata kule nchini Msumbiji mkondo ni huohuo.

Habari ni zilezile.

Mpaka muda huu unaposoma hapa, tayari makampuni matatu ya CVL; Macefield Ventures, NPD Ltd na Strofinare, yapo kwenye ardhi ya nchi hiyo kwa shughuli mbalimbali chini ya makubaliano ambayo wanayafahamu Felipe Nyusi na Kagame.

View attachment 3008256

Taratibu, shughuli za ujenzi na ulinzi binafsi katika nchi hii, vinaanza kuhodhiwa na makampuni ya Rwanda.

View attachment 3008257

Wataishia wapi na ingali wanazidi kujitanua hivi sasa wakiachwa peke yao na SADC?

Na nini hatma ya Ansar al-sunna mbele ya mabwana hawa wa Rwanda na sisi Tanzania tuliopakana nao?

Bila shaka tutalibakiza jeshi letu hapo Msumbiji, hata kama ni kwa gharama kubwa, lakini yatakayojiri huko mbeleni bado hatujajua.

Ngoja na tuone.
Baada ya kusoma makala yako mkuu maoni yangu ni haya;

kwanza nimeanza kuelewa chanzo cha hawa magaidi sababu si dini kama tunavyoaminishwa hii ni michezo michafu inayochezwa na baadhi ya serikali ili kujihakikishia wanabaki madarakani ila pia wanahodhi njia za kiuchumi.

hawa wanaoitwa magaidi kwa kisingizio cha dini ya uisilamu wanatumiwa tu kufanikisha malengo ya watu bahati mbaya dini ya uislam inajinasibu sana na vita vya kulinda imani na udhaifu huo unatumiwa vyema na hawa viongozi makatili..

nini tanzania ifanye?
kwa upande wetu tuendelee kuimalisha mifumo yetu ya ulinzi hasa ya ndani ila pia ni wakati wa sisi pia kudeal na hawa bwea wanaotuchukulia poa mimi naamini tunaweza kuwadhibiti vizuri tu kwa hali iliyopo msumbiji hakuna mwekezaji atakuja kuwekeza hapo mtwara kwenye gas yetu hii.. ila tunajua ni nani yupo behind this kwa hili ilipaswa na sisi tuwatekenye hawa wahuni hizi tabia zetu za kijamaa sometime zina tuumiza kama nchi.

leo hii wamejaa waamiaji haramu kila pembe ya nchi na kuna fununu wahamiaji kutoka nchi fulani wao wanajisogeza zaidi karibu na uongozi wanatafuta nini huko tushtuke.. naona walijaribu njia ya magaidi wakafail na wameona njia nyepesi kufikia lengo lao ni kupitia kujipenyeza kwenye uongozi tushtukeeee!

ikiwa SADC itafunga operation zake kule msumbiji na kuwaacha majeshi ya rwanda pekee tutegemee matatizo zaidi mimi naona tunazungukwa pande zote na adui huku sisi tukiwa mtu kati..

namaliza kwa kusema upande wangu naona kwa hiki kinachoendelea target kuu ni Tanzania kinachofanyika kwanza kwa sasa ni kudhoofisha mipaka yetu ambayo ilikuwa imara kwenye ulinzi wa nchi yetu.

kuna nchi inajikuta ni israel ya Africa sasa kabla tatizo halijawa kubwa na sisitunapaswa kuchukua hatu lasivyo tutakuja kushtuka tupo uchi. tutaishia kutupa taulo kwa aibu!
 
Baada ya kusoma makala yako mkuu maoni yangu ni haya;

kwanza nimeanza kuelewa chanzo cha hawa magaidi sababu si dini kama tunavyoaminishwa hii ni michezo michafu inayochezwa na baadhi ya serikali ili kujihakikishia wanabaki madarakani ila pia wanahodhi njia za kiuchumi.

hawa wanaoitwa magaidi kwa kisingizio cha dini ya uisilamu wanatumiwa tu kufanikisha malengo ya watu bahati mbaya dini ya uislam inajinasibu sana na vita vya kulinda imani na udhaifu huo unatumiwa vyema na hawa viongozi makatili..

nini tanzania ifanye?
kwa upande wetu tuendelee kuimalisha mifumo yetu ya ulinzi hasa ya ndani ila pia ni wakati wa sisi pia kudeal na hawa bwea wanaotuchukulia poa mimi naamini tunaweza kuwadhibiti vizuri tu kwa hali iliyopo msumbiji hakuna mwekezaji atakuja kuwekeza hapo mtwara kwenye gas yetu hii.. ila tunajua ni nani yupo behind this kwa hili ilipaswa na sisi tuwatekenye hawa wahuni hizi tabia zetu za kijamaa sometime zina tuumiza kama nchi.

leo hii wamejaa waamiaji haramu kila pembe ya nchi na kuna fununu wahamiaji kutoka nchi fulani wao wanajisogeza zaidi karibu na uongozi wanatafuta nini huko tushtuke.. naona walijaribu njia ya magaidi wakafail na wameona njia nyepesi kufikia lengo lao ni kupitia kujipenyeza kwenye uongozi tushtukeeee!

ikiwa SADC itafunga operation zake kule msumbiji na kuwaacha majeshi ya rwanda pekee tutegemee matatizo zaidi mimi naona tunazungukwa pande zote na adui huku sisi tukiwa mtu kati..

namaliza kwa kusema upande wangu naona kwa hiki kinachoendelea target kuu ni Tanzania kinachofanyika kwanza kwa sasa ni kudhoofisha mipaka yetu ambayo ilikuwa imara kwenye ulinzi wa nchi yetu.

kuna nchi inajikuta ni israel ya Africa sasa kabla tatizo halijawa kubwa na sisitunapaswa kuchukua hatu lasivyo tutakuja kushtuka tupo uchi. tutaishia kutupa taulo kwa aibu!
Critical insight, mkuu.
 
Migogoro mingi ya kibinadamu iliyopo barani Afrika chanzo chake hasa ni kutokana na Serikali zilizopo kwenye hizi nchi zetu kushindwa kuongoza Watu (Wananchi) vizuri. Serikali zilizopo kwenye nchi zetu hizi nyingi sana kama siyo zote ni za Kidikteta, Wala haziwajibiki kwa Wananchi matokeo yake zinazalisha mivutano na Migogoro dhidi ya wananchi.
Thanks for this insight, brother.
 
Hatari ya ugaidi kutoka Msumbiji ni tishio kubwa kwa usalama wa Tanzania. Serikali yetu inapaswa kuchukua hatua za haraka na za makusudi ili kupunguza hatari hii, ikiwa ni pamoja na kuimarisha usalama wa mpaka, kupambana na ufadhili wa ugaidi.
Jeshi la Tanzania litaendelea kubaki huko hata pale wengine wa SADC watakapokuwa wamejiondoa.
 
Baada ya kusoma makala yako mkuu maoni yangu ni haya;

kwanza nimeanza kuelewa chanzo cha hawa magaidi sababu si dini kama tunavyoaminishwa hii ni michezo michafu inayochezwa na baadhi ya serikali ili kujihakikishia wanabaki madarakani ila pia wanahodhi njia za kiuchumi.

hawa wanaoitwa magaidi kwa kisingizio cha dini ya uisilamu wanatumiwa tu kufanikisha malengo ya watu bahati mbaya dini ya uislam inajinasibu sana na vita vya kulinda imani na udhaifu huo unatumiwa vyema na hawa viongozi makatili..

nini tanzania ifanye?
kwa upande wetu tuendelee kuimalisha mifumo yetu ya ulinzi hasa ya ndani ila pia ni wakati wa sisi pia kudeal na hawa bwea wanaotuchukulia poa mimi naamini tunaweza kuwadhibiti vizuri tu kwa hali iliyopo msumbiji hakuna mwekezaji atakuja kuwekeza hapo mtwara kwenye gas yetu hii.. ila tunajua ni nani yupo behind this kwa hili ilipaswa na sisi tuwatekenye hawa wahuni hizi tabia zetu za kijamaa sometime zina tuumiza kama nchi.

leo hii wamejaa waamiaji haramu kila pembe ya nchi na kuna fununu wahamiaji kutoka nchi fulani wao wanajisogeza zaidi karibu na uongozi wanatafuta nini huko tushtuke.. naona walijaribu njia ya magaidi wakafail na wameona njia nyepesi kufikia lengo lao ni kupitia kujipenyeza kwenye uongozi tushtukeeee!

ikiwa SADC itafunga operation zake kule msumbiji na kuwaacha majeshi ya rwanda pekee tutegemee matatizo zaidi mimi naona tunazungukwa pande zote na adui huku sisi tukiwa mtu kati..

namaliza kwa kusema upande wangu naona kwa hiki kinachoendelea target kuu ni Tanzania kinachofanyika kwanza kwa sasa ni kudhoofisha mipaka yetu ambayo ilikuwa imara kwenye ulinzi wa nchi yetu.

kuna nchi inajikuta ni israel ya Africa sasa kabla tatizo halijawa kubwa na sisitunapaswa kuchukua hatu lasivyo tutakuja kushtuka tupo uchi. tutaishia kutupa taulo kwa aibu!
Ukichunguza kwa umakini Sana utagundua kwamba yale maeneo karibia yote yenye vurugu kule Msumbiji yana historia kongwe sana kuhusiana na suala la vurugu za kisiasa, hata kabla ya Taifa hilo la Msumbiji halijapata uhuru wake kutoka kwa mkoloni wao Ureno. Kambi nyingi sana za Makundi ya kisiasa ya Wapigania Uhuru wa nchi hiyo ya Msumbiji ziliwekwa katika ukanda huo wa Kaskazini mwa nchi hiyo, maeneo ambayo hadi leo hii bado yanaendelea kukumbwa na vurugu. Makundi ya Wapigania Uhuru ya vyama vya Siasa vya FRELIMO na RENAMO vilikuwa na Kambi zao nyingi za wazi na za siri kubwa ktk maeneo hayo yenye vurugu kwa sasa. Baada ya kufanikisha suala la kuuangusha utawala wa mkoloni wao Ureno, maeneo hayo tayari yalikuwa yamevurugwa vibaya sana na vita vya ukombozi, miundombinu yote ya kujenga uchumi kama vile viwanda viliharabiwa kabisa na mapigano ya vita.
Mbaya zaidi, hata chama cha Siasa cha FRELIMO kilipofanikiwa kushika madaraka ktk nchi hiyo ya Msumbiji, haikukishirikisha Chama cha RENAMO ktk kuitawala nchi hiyo ya Msumbiji, badala yake vyama hivyo viligawanyika na kuwa vyama vinavyohasimiana, vikapigana vita tena wao kwa wao ili kugombea kupata udhibiti wa madaraka ktk nchi hiyo, hatimaye Chama cha RENAMO kilizidiwa nguvu na kushindwa vita. Chama cha FRELIMO kutokana na msaada mkubwa waliopata kutoka kwa Mwl. J. K. Nyerere na CCM yake, walifanikiwa kuhodhi na kudhibiti mamlaka na madaraka yote ya nchi hiyo ya Msumbiji, na RENAMO kikawa Chama kikuu cha Upinzani dhidi ya FRELIMO.
Mbaya zaidi tena, utawala wa FRELIMO ulikichukulia Chama cha RENAMO kama Kundi la Waasi wala siyo Chama cha Siasa, Matokeo yake Wanachama na Wapiganaji wa RENAMO wakakimbilia msituni na kuweka Kambi zao nyingi za Siri kwenye huo Upande wa Kaskazini mwa nchi hiyo ya Msumbiji.

Serikali ya Msumbiji Kama ililitelekeza kabisa kwa muda mrefu eneo hilo lililopo Kaskazini mwa nchi hiyo kwa sababu ililiona kama eneo lenye maficho ya Waasi wa RENAMO, hata huduma za kijamii zilikuwa duni sana kwenye maeneo hayo. Wananchi wengi wa upande huo wa Kaskazini mwa nchi waliona kama Serikali ya Msumbiji imewatenga na haikuwa inawajali. Serikali ilijichimbia mizizi kwenye eneo la Kusini mwa nchi hiyo ya Msumbiji na kuigawa nchi ktk mapande mawili ya Kaskazini na Kusini. Serikali hiyo ya Msumbiji ilirudi tena kwa kasi upande wa Kaskazini mwa nchi hiyo baada ya Ugunduzi wa Nishati ya Gesi kwenye maeneo hayo ya Kaskazini, hapo ndipo ukawa mwanzo mpya wa kuibuka kwa Vurugu hizi zinazoendelea hivi sasa ktk eneo hilo la Kaskazini mwa nchi hiyo ya Msumbiji.

Suala la Dini au Udini ktk vurugu hizo za huko Msumbiji linatumika tu na wahusika kama "SCAPEGOAT" ili kuweza kupata msaada wa kijeshi na wa silaha za kupigania vita.
 
Kagame tunamchukulia poa sana.
CDF kwenye hotuba yake ilitakiwa Uhamiaji waanze msako na Ikulu ianze temesha watu
Acha kuhemuka wewe, war is a big business, interest ni pesa tuu na kuyapa majeshi yake utayari, mission kama hizo askari wanalipwa big money kwa mwezi wanalipwa mpa 2000$ na serikali pia inalipwa , ila akili yako tayari unaona unavamiwa wewe unaanza msako wa waha na watu wa wako wa mipakani, akili za hovyo sana
 
Jeshi la Tanzania litaendelea kubaki huko hata pale wengine wa SADC watakapokuwa wamejiondoa.
Mimi binafsi kwa Maoni yangu ni kwamba Jeshi la Tanzania (JWTZ/TPDF) linapaswa lijiondoe kutoka huko Msumbiji, badala yake Jeshi hilo lijikite kwenye Ulinzi wa Mipaka ya nchi yetu ya Tz. Iimarishe ulinzi ktk mipaka ya Tz na Msumbiji, lisijiingize kwenye Migogoro ya ndani ya nchi ya Msumbiji na hata ktk nchi zingine zote ambazo tunapakana nazo, tuache kufanya hivyo kwa sababu kuendelea kujiingiza kwenye hiyo Migogoro ndio chanzo Cha kuhatarisha usalama wa Wananchi wa nchi hii pamoja na mali zao.
Mbaya zaidi kwenye huo Mgogoro wa huko Msumbiji ni kwamba hata baadhi ya Viongozi wakubwa wa Serikali ya Msumbiji nao wapo nyuma ya Mgogoro huo, hao Wapiganaji wa hilo Kundi la RENAMO wamekuwa wakipata taarifa zote muhimu kutoka kwa INFORMERS wao ambao wapo ndani ya Serikali ya Msumbiji.
Je, mmeshawahi kujiuliza ni kwa nini Jeshi la Serikali ya Msumbiji halikuwa na Kambi nyingi za Jeshi ktk maene hayo ya Kaskazini kwa nchi hiyo ya Msumbiji, hususani kwenye hilo Jimbo la Cabo Delgado? Kwa nini kwenye Jimbo hilo kulikuwa na kambi chache sana za Jeshi na badala yake Kambi nyingi sana za Jeshi ziliwekwa upande wa Kusini mwa nchi hiyo?? Je, mnazijua sababu????
Hata pale Kampuni za kutoka Ulaya za Uchimbaji wa Gesi zilipoenda kuchimba Gesi kule Jimboni Cabo Delgado Serikali ya Msumbiji ilizijulisha na kuziruhusu Kampuni hizo kwenda huko wakiwa na Ulinzi wao binafsi, na pia Kampuni hizo ziliruhusiwa kwenda na Jeshi lao binafsi kwa ajili ya Ulinzi wao na hatimaye Kampuni hizo Walikodi Jeshi binafsi la Kujitegemea kutoka kwa Makaburu wa Afrika ya Kusini, Je, mmeshawahi kujiuliza ni kwa nini Serikali ya Msumbiji iliamua kufanya Maamuzi 'ya ajabu' Kama hayo????
Kwa Nini Jeshi la Msumbiji halikuhusishwa kwenye ulinzi kwenye maeneo hayo yenye machimbo ya Gesi huko Cabo Delgado badala yake liliruhusiwa Jeshi binafsi la kukodishwa kutoka nchini Afrika ya Kusini??

I remind you, "No research no right to speak ", Mgogoro wa huko Msumbiji una historia ndefu, haukuibuka tu hivi hivi from nowhere.
 
Acha kuhemuka wewe, war is a big business, interest ni pesa tuu na kuyapa majeshi yake utayari, mission kama hizo askari wanalipwa big money kwa mwezi wanalipwa mpa 2000$ na serikali pia inalipwa , ila akili yako tayari unaona unavamiwa wewe unaanza msako wa waha na watu wa wako wa mipakani, akili za hovyo sana
Turekebishane kwa lugha ya staha tu, mkuu.
 
Ukichunguza kwa umakini Sana utagundua kwamba yale maeneo karibia yote yenye vurugu kule Msumbiji yana historia kongwe sana kuhusiana na suala la vurugu za kisiasa, hata kabla ya Taifa hilo la Msumbiji halijapata uhuru wake kutoka kwa mkoloni wao Ureno. Kambi nyingi sana za Makundi ya kisiasa ya Wapigania Uhuru wa nchi hiyo ya Msumbiji ziliwekwa katika ukanda huo wa Kaskazini mwa nchi hiyo, maeneo ambayo hadi leo hii bado yanaendelea kukumbwa na vurugu. Makundi ya Wapigania Uhuru ya vyama vya Siasa vya FRELIMO na RENAMO vilikuwa na Kambi zao nyingi za wazi na za siri kubwa ktk maeneo hayo yenye vurugu kwa sasa. Baada ya kufanikisha suala la kuuangusha utawala wa mkoloni wao Ureno, maeneo hayo tayari yalikuwa yamevurugwa vibaya sana na vita vya ukombozi, miundombinu yote ya kujenga uchumi kama vile viwanda viliharabiwa kabisa na mapigano ya vita.
Mbaya zaidi, hata chama cha Siasa cha FRELIMO kilipofanikiwa kushika madaraka ktk nchi hiyo ya Msumbiji, haikukishirikisha Chama cha RENAMO ktk kuitawala nchi hiyo ya Msumbiji, badala yake vyama hivyo viligawanyika na kuwa vyama vinavyohasimiana, vikapigana vita tena wao kwa wao ili kugombea kupata udhibiti wa madaraka ktk nchi hiyo, hatimaye Chama cha RENAMO kilizidiwa nguvu na kushindwa vita. Chama cha FRELIMO kutokana na msaada mkubwa waliopata kutoka kwa Mwl. J. K. Nyerere na CCM yake, walifanikiwa kuhodhi na kudhibiti mamlaka na madaraka yote ya nchi hiyo ya Msumbiji, na RENAMO kikawa Chama kikuu cha Upinzani dhidi ya FRELIMO.
Mbaya zaidi tena, utawala wa FRELIMO ulikichukulia Chama cha RENAMO kama Kundi la Waasi wala siyo Chama cha Siasa, Matokeo yake Wanachama na Wapiganaji wa RENAMO wakakimbilia msituni na kuweka Kambi zao nyingi za Siri kwenye huo Upande wa Kaskazini mwa nchi hiyo ya Msumbiji.

Serikali ya Msumbiji Kama ililitelekeza kabisa kwa muda mrefu eneo hilo lililopo Kaskazini mwa nchi hiyo kwa sababu ililiona kama eneo lenye maficho ya Waasi wa RENAMO, hata huduma za kijamii zilikuwa duni sana kwenye maeneo hayo. Wananchi wengi wa upande huo wa Kaskazini mwa nchi waliona kama Serikali ya Msumbiji imewatenga na haikuwa inawajali. Serikali ilijichimbia mizizi kwenye eneo la Kusini mwa nchi hiyo ya Msumbiji na kuigawa nchi ktk mapande mawili ya Kaskazini na Kusini. Serikali hiyo ya Msumbiji ilirudi tena kwa kasi upande wa Kaskazini mwa nchi hiyo baada ya Ugunduzi wa Nishati ya Gesi kwenye maeneo hayo ya Kaskazini, hapo ndipo ukawa mwanzo mpya wa kuibuka kwa Vurugu hizi zinazoendelea hivi sasa ktk eneo hilo la Kaskazini mwa nchi hiyo ya Msumbiji.

Suala la Dini au Udini ktk vurugu hizo za huko Msumbiji linatumika tu na wahusika kama "SCAPEGOAT" ili kuweza kupata msaada wa kijeshi na wa silaha za kupigania vita.
Nimefuatilia comments zako kwenye Uzi wa SteveMollel kuna picha naiona kwako inanitisha sana.

Vipi mnanufaika nini na ugaidi wenu?
 
Mimi binafsi kwa Maoni yangu ni kwamba Jeshi la Tanzania (JWTZ/TPDF) linapaswa lijiondoe kutoka huko Msumbiji, badala yake Jeshi hilo lijikite kwenye Ulinzi wa Mipaka ya nchi yetu ya Tz. Iimarishe ulinzi ktk mipaka ya Tz na Msumbiji, lisijiingize kwenye Migogoro ya ndani ya nchi ya Msumbiji na hata ktk nchi zingine zote ambazo tunapakana nazo, tuache kufanya hivyo kwa sababu kuendelea kujiingiza kwenye hiyo Migogoro ndio chanzo Cha kuhatarisha usalama wa Wananchi wa nchi hii pamoja na mali zao.
Mbaya zaidi kwenye huo Mgogoro wa huko Msumbiji ni kwamba hata baadhi ya Viongozi wakubwa wa Serikali ya Msumbiji nao wapo nyuma ya Mgogoro huo, hao Wapiganaji wa hilo Kundi la RENAMO wamekuwa wakipata taarifa zote muhimu kutoka kwa INFORMERS wao ambao wapo ndani ya Serikali ya Msumbiji.
Je, mmeshawahi kujiuliza ni kwa nini Jeshi la Serikali ya Msumbiji halikuwa na Kambi nyingi za Jeshi ktk maene hayo ya Kaskazini kwa nchi hiyo ya Msumbiji, hususani kwenye hilo Jimbo la Cabo Delgado? Kwa nini kwenye Jimbo hilo kulikuwa na kambi chache sana za Jeshi na badala yake Kambi nyingi sana za Jeshi ziliwekwa upande wa Kusini mwa nchi hiyo?? Je, mnazijua sababu????
Hivi mnaelewa hata mnaandika nini? Kwa sass TZ haina matatizo kwenye mipaka yao wanajeshi wapo tuu makambini sio busy, mission kama hizi wanalipwa pesa nyingi sana wanajeshi wanaokwenda na kuwapa experience ya vita na mambo mengine, acheni wajeshi wapige pesa au mnataka wawe busy kuwavua uniform za jeshi mitami na kuwatandika wanavijiji kwa utemi tuu na ulevi
 
Hivi mnaelewa hata mnaandika nini? Kwa sass TZ haina matatizo kwenye mipaka yao wanajeshi wapo tuu makambini sio busy, mission kama hizi wanalipwa pesa nyingi sana wanajeshi wanaokwenda na kuwapa experience ya vita na mambo mengine, acheni wajeshi wapige pesa au mnataka wawe busy kuwavua uniform za jeshi mitami na kuwatandika wanavijiji kwa utemi tuu na ulevi
Huyo mhuni anaandika kwa code
 
Hivi mnaelewa hata mnaandika nini? Kwa sass TZ haina matatizo kwenye mipaka yao wanajeshi wapo tuu makambini sio busy, mission kama hizi wanalipwa pesa nyingi sana wanajeshi wanaokwenda na kuwapa experience ya vita na mambo mengine, acheni wajeshi wapige pesa au mnataka wawe busy kuwavua uniform za jeshi mitami na kuwatandika wanavijiji kwa utemi tuu na ulevi
Hoja yako haina mashiko hata kidogo.
Je, unakijua kitu au sababu iliyoiponza Kenya kuhusiana na mashambulizi ya kigaidi kutoka kwa Al-Shabaab???
 
Nimefuatilia comments zako kwenye Uzi wa SteveMollel kuna picha naiona kwako inanitisha sana.

Vipi mnanufaika nini na ugaidi wenu?
Unatoa comments kutokana na msukumo fulani fulani uliopo nje ya uwezo wako. Isipokuwa tambua tu kwamba Mimi Ninatoa Maoni yangu hapa nikiwa na moyo thabiti kabisa wenye nia njema kwa nchi hii ili tusije kuingia kwenye shimo ambalo hatutaweza kujinasua endapo kama tutatumbukia humo.

Aidha, Mimi siyo Mwislamu Wala sina maslahi yoyote yale huko kwenye dini hiyo ambayo inanasibishwa na hao Wapiganaji wa huko Msumbiji.
Nimetoa Maoni yangu haya nikiwa ni mtu mwenye mitizamo na fikra huru kabisa, ambapo sijaegemea upande wowote usiostahili, Bali ni kueleza ukweli na uhalisia wa mambo jinsi yalivyo.
 
Back
Top Bottom