Kinachoendelea Msumbiji, magaidi na Jeshi - Part 3

Kinachoendelea Msumbiji, magaidi na Jeshi - Part 3

Tuongeze nguvu kubwa sana huko kusini na usisahau mission za jeshi la Rwanda hua ni hatari wanaweza kupeleka hata kikosi cha siri kikawatrain magaidi au renamo wakapewa na vifaa wakatuvamia mchana kweupe lazima tukae tayari
Hili mbona liko wazi sana mkuu. Kwa fujo za Drc tu hapo Rwanda inavyokinukisha unadhan watashindwa hapo kusini walikojaa wazembe wazembe? Ni suala la muda tu. Acha hawa wanaojiita wanausalama wetu na wanajeshi waendelee tu kuwekeza akil zao kwenye salary slip kutwa kuchezesha mikopo tu mara leo Finca mara keshi Bayport mara keshokutwa Nmb.. wao kazi walishamaliza walipopata ajira tu 😂
 
Ni kweli mikoa ya mipakani huko Kusini haiko salama sana kutokana na Mgogoro wa huko Msumbiji. Jeshi letu linapaswa kuongeza nguvu nyingi zaidi kwenye upande huo ili kuimarisha ulinzi.

Aidha, tuondoe wanajeshi wetu waliopo huko Msumbiji, badala yake walinzi hao wajikite kulinda mipaka ya nchi yetu.
No kuondoa sio sawa,ningependekeza kuwe na maelewano na serikali ya Tz wanajeshi wetu waweke uthibiti Eneo la musumbiji la karibu na Tz Ili magaidi wasivuke kutoka huko kuja kwetu.

Hivyo majeshi yetu yawe upande wa Msumbiji na upande wa Tz,hapo kusini mwa Tz usalama unaimarika.Hao magaidi nihatari sana,maana wanafanyaga supprise attack always Usiku wanaua wanaiba then wanarudi kujificha huko Msumbiji.Dah! Natamani sana Jeshi letu liweke mkazo huko usalama nimdogo kwa raia.
 
achilia mbali makampuni hayo ya Rwanda lakini TOTAL wanaomba vikosi zaidi vikalinde uwekezaji wao lakini sharti viwe vikosi kutoka Rwanda tu
Siku zote mtu mwenye akili ndio huoewa priority kwakua matokeo ya kaz yake yako bayana. Sasa ulitaka waitwe wajinga wajinga wakalinde amani Msumbiji?

Na kama Nyusi kaomba Sadc waondoke, kwann hawa watanzania wabaki? Kwamba wamegoma au??
 
Siku zote mtu mwenye akili ndio huoewa priority kwakua matokeo ya kaz yake yako bayana. Sasa ulitaka waitwe wajinga wajinga wakalinde amani Msumbiji?

Na kama Nyusi kaomba Sadc waondoke, kwann hawa watanzania wabaki? Kwamba wamegoma au??
Hamna sehemu yoyote inaposema Nyusi kawaomba SADC waondoke. Kinachowaondoa SADC ni muda wao ulopangwa kuisha na huku ikiwa ni gharama sana kuendelea na oparesheni hii.

Tanzania kubaki hapo ni sababu ya kumbukumbu ya kilichowatokea mwaka 2022. Hamna taifa jingine la SADC lililowahi kuvamiwa na watu wake kuuawa mbali na Msumbiji na Tanzania.

Kama haitoshi, jeshi la RDF na SADC hapo nchini Msumbiji, hayakuwa yakipeana support. Mwanzoni kila mmoja alikuwa anafanya kazi mwenyewe bila kumpa ripoti mwenzake.

Ni baadae ndo' wakaanza kushirikiana, tena kidogo sana. Ni kana kwamba kila body ina misheni yake japo adui ni mmoja.
 
Kinachowaondoa SADC ni muda wao ulopangwa kuisha na huku ikiwa ni gharama sana kuendelea na oparesheni hii.

Tanzania kubaki hapo ni sababu ya kumbukumbu ya kilichowatokea mwaka 2022. Hamna taifa jingine la SADC lililowahi kuvamiwa na watu wake kuuawa mbali na Msumbiji na Tanzania.
Sasa kama muda umeisha, ni kipi kinaibakiza Tz hapo Kwenye foreign soil? Si warud mipakani mwao??
 
Mimi binafsi kwa Maoni yangu ni kwamba Jeshi la Tanzania (JWTZ/TPDF) linapaswa lijiondoe kutoka huko Msumbiji, badala yake Jeshi hilo lijikite kwenye Ulinzi wa Mipaka ya nchi yetu ya Tz. Iimarishe ulinzi ktk mipaka ya Tz na Msumbiji, lisijiingize kwenye Migogoro ya ndani ya nchi ya Msumbiji na hata ktk nchi zingine zote ambazo tunapakana nazo, tuache kufanya hivyo kwa sababu kuendelea kujiingiza kwenye hiyo Migogoro ndio chanzo Cha kuhatarisha usalama wa Wananchi wa nchi hii pamoja na mali zao.
Mbaya zaidi kwenye huo Mgogoro wa huko Msumbiji ni kwamba hata baadhi ya Viongozi wakubwa wa Serikali ya Msumbiji nao wapo nyuma ya Mgogoro huo, hao Wapiganaji wa hilo Kundi la RENAMO wamekuwa wakipata taarifa zote muhimu kutoka kwa INFORMERS wao ambao wapo ndani ya Serikali ya Msumbiji.
Je, mmeshawahi kujiuliza ni kwa nini Jeshi la Serikali ya Msumbiji halikuwa na Kambi nyingi za Jeshi ktk maene hayo ya Kaskazini kwa nchi hiyo ya Msumbiji, hususani kwenye hilo Jimbo la Cabo Delgado? Kwa nini kwenye Jimbo hilo kulikuwa na kambi chache sana za Jeshi na badala yake Kambi nyingi sana za Jeshi ziliwekwa upande wa Kusini mwa nchi hiyo?? Je, mnazijua sababu????
Hata pale Kampuni za kutoka Ulaya za Uchimbaji wa Gesi zilipoenda kuchimba Gesi kule Jimboni Cabo Delgado Serikali ya Msumbiji ilizijulisha na kuziruhusu Kampuni hizo kwenda huko wakiwa na Ulinzi wao binafsi, na pia Kampuni hizo ziliruhusiwa kwenda na Jeshi lao binafsi kwa ajili ya Ulinzi wao na hatimaye Kampuni hizo Walikodi Jeshi binafsi la Kujitegemea kutoka kwa Makaburu wa Afrika ya Kusini, Je, mmeshawahi kujiuliza ni kwa nini Serikali ya Msumbiji iliamua kufanya Maamuzi Kama hayo????

I remind you, "No research no right to speak ", Mgogoro wa huko Msumbiji una historia ndefu, haukuibuka tu hivi hivi from nowhere.
Natamani JWTZ iwe kisu kweli kweli!
Ipenye kila kichochoro kwa majirani na kuteka fursa zote za kiuchumi kwa njia Hali na batili.
Malengo ya majeshi, kabla ya ukoloni, yalikuwa na majukumu 2: kulinda himaya na kuiba rasilimali (ng'ombe, kuteka ardhi, n.k) kwenye himaya dhaifu.
 
Natamani JWTZ iwe kisu kweli kweli!
Ipenye kila kichochoro kwa majirani na kuteka fursa zote za kiuchumi kwa njia Hali na batili.
Malengo ya majeshi, kabla ya ukoloni, yalikuwa na majukumu 2: kulinda himaya na kuiba rasilimali (ng'ombe, kuteka ardhi, n.k) kwenye himaya dhaifu.
Hiki ndicho anafanya Kagame, sisi tulisha lemaa hakuna kitu tunafikiri. Anyway sio mbaya oia kulinda raia wako. Ila mwenzako anapofanya yake na jeshi lake kama rwanda, asionewe wivu
 
No kuondoa sio sawa,ningependekeza kuwe na maelewano na serikali ya Tz wanajeshi wetu waweke uthibiti Eneo la musumbiji la karibu na Tz Ili magaidi wasivuke kutoka huko kuja kwetu.

Hivyo majeshi yetu yawe upande wa Msumbiji na upande wa Tz,hapo kusini mwa Tz usalama unaimarika.Hao magaidi nihatari sana,maana wanafanyaga supprise attack always Usiku wanaua wanaiba then wanarudi kujificha huko Msumbiji.Dah! Natamani sana Jeshi letu liweke mkazo huko usalama nimdogo kwa raia.
Haya maelewano kwann hawa wakuu wa Vyombo vya usalama hawakuyaona toka awali wakayapendekeza toka mwanzo, mpaka kufikia hatua Msumbiji anavuivuka Tanzania na kwemda kuomba msaada Rwanda.

Kufikia hatua msumbiji anaacha umoja wa Sadc ambapo na yeye yupo (sina uhakika sana na hili) na kwenda kuomba msaada kwa nchi isiyohusika kabisaa??

Kuna nini kiliendelea hapa mpaka kupelekea hali hii iwe hiv??
 
Sure haihitaji hata cheti lakin kwan sisi nani katuzuia.
Unataka kusema Jw yeye hana anachotaka pale Drc. Halaf mbona hata Updf wako involved kwenye suala la Drc lakin kelele ni kwa Rwanda tu pekee??
Ingalikuwa hivyo, Raisi wa DRC asingeomba majeshi ya MONUSCO na yale ya EACRF yaondoke katika nchi yake ili awakaribishe SADC ambayo Tanzania imo ndani yake kwakuwa anawaamini zaidi.
 
Haya maelewano kwann hawa wakuu wa Vyombo vya usalama hawakuyaona toka awali wakayapendekeza toka mwanzo, mpaka kufikia hatua Msumbiji anavuivuka Tanzania na kwemda kuomba msaada Rwanda.

Kufikia hatua msumbiji anaacha umoja wa Sadc ambapo na yeye yupo (sina uhakika sana na hili) na kwenda kuomba msaada kwa nchi isiyohusika kabisaa??

Kuna nini kiliendelea hapa mpaka kupelekea hali hii iwe hiv??
Rwanda hata usipomwomba anakuja kukuomba yeye mwenyewe. Rejelea sakata la Benini na mipaka yake ya Burkina Faso.
 
Back
Top Bottom