Kinachoendelea Msumbiji, magaidi na Jeshi - Part 3

Kinachoendelea Msumbiji, magaidi na Jeshi - Part 3

Acha kuhemuka wewe, war is a big business, interest ni pesa tuu na kuyapa majeshi yake utayari, mission kama hizo askari wanalipwa big money kwa mwezi wanalipwa mpa 2000$ na serikali pia inalipwa , ila akili yako tayari unaona unavamiwa wewe unaanza msako wa waha na watu wa wako wa mipakani, akili za hovyo sana
SteveMollel shusha story kuna sehemu nimepaelewa sana ukishusha itakua tamu sana sehemu ya 4
 
Kumbe Boko Haram bado wapo? Nina muda siwasikii ama wamedhibitiwa?
Nguvu ya Boko Haram imepungua baada ya kugawanyika na kutengeneza makundi madogo madogo yanayopambana yenyewe kwa yenyewe kwa kutofautiana itikadi na maono, mfano kundi la ISWAP.

Waliamini Shekau anatoka kwenye mstari na yampasa kudhibitiwa.

Mapambano yao ndo' yakapelekea kujeruhiwa kwa Shekau na hata pia kifo chake.
 
Upo sahihi kabisa, ilipaswa hiyo Burundi na Rwanda iwe mikoa ya Tanganyika kisha huko kusini Cabo Delgado na Niassa irudishwe mikononi mwa Tanganyika maana hapo awali hiyo ilikuwa sehemu ya Tanganyika. Ila sasa angalia viongozi wako. Hii nchi ina viongozi wa hovyo sana, inasikitisha!
Natamani JWTZ iwe kisu kweli kweli!
Ipenye kila kichochoro kwa majirani na kuteka fursa zote za kiuchumi kwa njia Hali na batili.
Malengo ya majeshi, kabla ya ukoloni, yalikuwa na majukumu 2: kulinda himaya na kuiba rasilimali (ng'ombe, kuteka ardhi, n.k) kwenye himaya dhaifu.
 
Nadhani alifanya kipindi cha JPM nadhani hawakufikia muafaka baina yao, saizi kuna huyu mzurulaji ata kama ni wewe utamwambia nini?
SAsa hapo kosa lake ni lipi kaka? Maana kama Tanzania ingekua bado na ile diplomatic influence iliokuaga nayo miaka yoote, trust me Nyusi asingeshindwa kutu consult kwanza sisi kwa kuheshim mipaka yetu kabla hajaingiza jesho la nchi ambayo ana uhakika kabisa tunahasimiana nayo huko Drc.
Yan leo hii viatu vya akina Mahiga anavaaa mtu mjinga mjinga kama February unategemea haya yasitokee??
 
Ukichunguza kwa umakini Sana utagundua kwamba yale maeneo karibia yote yenye vurugu kule Msumbiji yana historia kongwe sana kuhusiana na suala la vurugu za kisiasa, hata kabla ya Taifa hilo la Msumbiji halijapata uhuru wake kutoka kwa mkoloni wao Ureno. Kambi nyingi sana za Makundi ya kisiasa ya Wapigania Uhuru wa nchi hiyo ya Msumbiji ziliwekwa katika ukanda huo wa Kaskazini mwa nchi hiyo, maeneo ambayo hadi leo hii bado yanaendelea kukumbwa na vurugu. Makundi ya Wapigania Uhuru ya vyama vya Siasa vya FRELIMO na RENAMO vilikuwa na Kambi zao nyingi za wazi na za siri kubwa ktk maeneo hayo yenye vurugu kwa sasa. Baada ya kufanikisha suala la kuuangusha utawala wa mkoloni wao Ureno, maeneo hayo tayari yalikuwa yamevurugwa vibaya sana na vita vya ukombozi, miundombinu yote ya kujenga uchumi kama vile viwanda viliharabiwa kabisa na mapigano ya vita.
Mbaya zaidi, hata chama cha Siasa cha FRELIMO kilipofanikiwa kushika madaraka ktk nchi hiyo ya Msumbiji, haikukishirikisha Chama cha RENAMO ktk kuitawala nchi hiyo ya Msumbiji, badala yake vyama hivyo viligawanyika na kuwa vyama vinavyohasimiana, vikapigana vita tena wao kwa wao ili kugombea kupata udhibiti wa madaraka ktk nchi hiyo, hatimaye Chama cha RENAMO kilizidiwa nguvu na kushindwa vita. Chama cha FRELIMO kutokana na msaada mkubwa waliopata kutoka kwa Mwl. J. K. Nyerere na CCM yake, walifanikiwa kuhodhi na kudhibiti mamlaka na madaraka yote ya nchi hiyo ya Msumbiji, na RENAMO kikawa Chama kikuu cha Upinzani dhidi ya FRELIMO.
Mbaya zaidi tena, utawala wa FRELIMO ulikichukulia Chama cha RENAMO kama Kundi la Waasi wala siyo Chama cha Siasa, Matokeo yake Wanachama na Wapiganaji wa RENAMO wakakimbilia msituni na kuweka Kambi zao nyingi za Siri kwenye huo Upande wa Kaskazini mwa nchi hiyo ya Msumbiji.

Serikali ya Msumbiji Kama ililitelekeza kabisa kwa muda mrefu eneo hilo lililopo Kaskazini mwa nchi hiyo kwa sababu ililiona kama eneo lenye maficho ya Waasi wa RENAMO, hata huduma za kijamii zilikuwa duni sana kwenye maeneo hayo. Wananchi wengi wa upande huo wa Kaskazini mwa nchi waliona kama Serikali ya Msumbiji imewatenga na haikuwa inawajali. Serikali ilijichimbia mizizi kwenye eneo la Kusini mwa nchi hiyo ya Msumbiji na kuigawa nchi ktk mapande mawili ya Kaskazini na Kusini. Serikali hiyo ya Msumbiji ilirudi tena kwa kasi upande wa Kaskazini mwa nchi hiyo baada ya Ugunduzi wa Nishati ya Gesi kwenye maeneo hayo ya Kaskazini, hapo ndipo ukawa mwanzo mpya wa kuibuka kwa Vurugu hizi zinazoendelea hivi sasa ktk eneo hilo la Kaskazini mwa nchi hiyo ya Msumbiji.

Suala la Dini au Udini ktk vurugu hizo za huko Msumbiji linatumika tu na wahusika kama "SCAPEGOAT" ili kuweza kupata msaada wa kijeshi na wa silaha za kupigania vita.
Kaka upo vizuri pia tuandalie makala mpya tuenjoy
 
Migogoro mingi ya kibinadamu iliyopo barani Afrika chanzo chake hasa ni kutokana na Serikali zilizopo kwenye hizi nchi zetu kushindwa kuongoza Watu (Wananchi) vizuri. Serikali zilizopo kwenye nchi zetu hizi nyingi sana kama siyo zote ni za Kidikteta, Wala haziwajibiki kwa Wananchi matokeo yake zinazalisha mivutano na Migogoro dhidi ya wananchi.
Magaidi wanajua demoracia?
 
Mambo haya hayapendwi sana, mkuu. Sisi tunataka umbea wa mastaa.
Shusha sehemu ya 4 kuna Ile sehemu ya zile barua za wanajeshi wa Rwanda na picha zao Fb pale kuna kiulizo bado ukiweza fukua fukua zaidi utuletee kilichokua kinasababisha wanakufa ni nini? Kwanini kabla ya kufa walikua wanaandika zile barua za KUACHIA password za Bank?
 
Shusha sehemu ya 4 kuna Ile sehemu ya zile barua za wanajeshi wa Rwanda na picha zao Fb pale kuna kiulizo bado ukiweza fukua fukua zaidi utuletee kilichokua kinasababisha wanakufa ni nini? Kwanini kabla ya kufa walikua wanaandika zile barua za KUACHIA password za Bank?
Nitakapopata wasaa, nitaendelea tena kaka japo kuna za sehemu zingine zinaningoja kupost.
 
Kuondoka Kwa vikosi vya SADC msumbiji ni ombi la rais Nyusi na mkuu wao wa majeshi waliwaarifu jamaa waondoke na ukumbuke vikosi vya Rwanda wanaishi kama wafalme kule maana hakuna wanachokosa kuanzia posho nono, vifaa vya kisasa yaani hata wakiwa doria mtaani wanajeshi wa Rwanda wanavifaa vya kisasa na bora zaidi kuliko hata wanajeshi wetu, lazima kazi ifanyike kubwa na serikali ya msumbiji Kwa sasa imeshaanza kuwalipa wanajeshi wa Rwanda hadi mishahara Kwa siri, na achilia mbali makampuni hayo ya Rwanda lakini TOTAL wanaomba vikosi zaidi vikalinde uwekezaji wao lakini sharti viwe vikosi kutoka Rwanda tu
Imeisha hiyo..
Kwa hili swala tumezingua sana kama nchi usalama wa hayo maeneo ni muhimu sana kwa amani yetu kama nchi.
 
Nafikiri, JW washamsoma PK Muda mrefu sn na wanajua nani yupo nyuma yake ( western countries), wanajeshi wa PK Wana vifaa vingi sn vya kisasa, KP anaiba madini mengi sn DRC na kuwapa watu wa western ili wamsapoti na kumkingia kifua ( hapa amepata Kwa kujificha), bahati mzuri Russia hayupo sn nchi za Africa Nina uhakika angekuwa DRC , TZ au msumbiji angempiga mapema sn kama anachofanya Ukraine.

PK si wakumuingia hovyo anaweza kukuharibia kabisa nchi au ukaingia ktk vita isiyoisha, hapa anayetafutwa ili adhoofike ni TZ na JW wanalijua hilo, kugunduliwa Kwa gas mtwara na Lindi ni target Yao kubwa sn.

JW wabaki msumbiji hii itawasaidia kujua mbinu zote za PK ili asiwafundishe (magaidi) na kuwapa silaha ili kutusumbua na pia wabaki mipakani na silaha nzito kwa kulinda na kutoa support.

NB: siku tukisikia majeshi ya TZ yanafukuzwa msumbiji na utawala wa msumbiji, silaha nzito hasa zipelekwe mipakani maana ambush inaweza Anza Muda wowote
 
Back
Top Bottom