Kinachokwenda kufanyika kwenye miamala ya simu, ni Serikali kuuchukua tena uchumi sadifu wa kati kwa walala hoi kwamba hawastahili kuwa nao

Kinachokwenda kufanyika kwenye miamala ya simu, ni Serikali kuuchukua tena uchumi sadifu wa kati kwa walala hoi kwamba hawastahili kuwa nao

Hao watu wa chini unaowasema ndio chanzo cha Serikali kutowajibika kwa wananchi. Hawa ndiyo wanakuwa watu wa kwanza kuunga mkono Serikali kwa kila kiti, hata inapowaonea watu...
Mkuu, Sio vema tuwaache wamezwe mdomoni mwa simba, hata kama kuna mahali wanamakosa, tuendelee kuwatetea mkuu
 
Kitu kigumu kabisa kwa wasomi wa Tanzania, ni kufikiri vizuri na kuona mwisho wa mawazo yao

Hizi ni kodi za hovyo kuwahi kutokea, Kuwa na simu siyo ufahari, kutuma pesa iende mahali siyo ufahari
 
Wafanye wawe masikini ili uwatawale, marehemu katusomesha huyu kaja kutuzika kabisa
 
Mimi kwa mtazamo wangu wale watu ambao wanaona hii issue ni ngumu kwao warudi tu kwenye Yale maisha ya zamani kabla issue ya simu ama miamala kuja. Maana sidhani Kama Kuna ulazima wa kutumia simu kwenye Jambo lolote.

Ambao hawataki wafungie simu zao makabatini na wenye kutaka wakubaliane na hali halisi. Muhimu hapa ni hii Kodi tunayokatwa itumike Kama ilivyokusudiwa. Bunge na mamlaka husika ziifuatilie kwa ukaribu Sana. Sio tukatwe kodi halafu ziishie kufaidisha watu binafsi kwa kuzidokoa.
Unategemea hilo bunge ambalo 'halikuchaguliwa' na wananchi lifanye kazi hiyo!!
Hilo la kurudi kwenye utoto, ni hoja isiyo na mashiko na kama ingewezekana kuacha kutumia simu kwa miamala basi serikali itakuwa ya kwanza kukosa mapato (kukusanya kwa cash)
 
Sijui ni kivipi mtu anapofika kwenye level fulani ya maisha hutaka kuilazimisha akili yake kuwa na wengine wote wako kama yeye

Badala ya kurudisha akili zake kule alikotoka ili ayapime maisha aliyopitia na hatimaye aone pia wale ambao bado wako huko wanapitia ugumu uleule aliowahi kuupitia yeye kabla hajafika hapo alipo, hata akichaguliwa/bahatika kuwa katika nafasi Fulani ya uongozi, Aumize kichwa chake jinsi ya kuisaidia jamii masikini,

Kusaidia Jamii kama kiongozi, hauhitaji utoe pesa mfukoni mwako

Ni kuweka sera wezeshi ambazo zitaifanya jamii hii masikini kufikia uwalau maisha ya kufurahia uwepo wao hapa duniani

Jamii yetu bado masikini sana, bahati mbaya kabisa, Kuzaliwa kwetu katika jamii ambayo haikuwahi kuona shida, isitufanye kutotambua kwamba shida zipo

Kinacho kwenda kufanyika sasa kwenye sera ya makato ya miamala ya simu, ni kwenda kuzidisha ukali wa maisha kwa jamii kubwa ya watu wa maisha ya chini na kuathiri uchumi wao mdogo unaotegemea jasho jingi ili mtu apate mlo wa siku

Naishauri serikali, Kwa sababu tunajamii kubwa ambayo inaishi kwa kutegemea maisha ya kubangaiza, na kwa sababu tozo hiyo ya miamala na laini ya simu ni mpango wa serikari ipate kodi ili kuendeleza miradi na ujenzi wa barabara vijini

Badala ya kodi hiyo kuingizwa kwenye huduma hizi mhimu na kuifanya huduma hii iwe na makato makubwa kiasi cha kufanya wazee wetu kule vijini wakose msaada kutoka kwa vijana wao wanaowatumia vijisenti vya kujipatia mahitaji yao

Kodi hii ihamishiwe upande wa abiria wanaosafiri kwa mabasi kwenda mikoani, usafiri wa Treni, meli, na ndege, na kodi yake iwe ni kila abilia atakatwa kodi ya sh 1,000 tu kwa kila abiria anayetumia usafiri wa basi kwenda mkoani,

Serikali itafute namna ya kulipa hiyo kodi, ni au iunganishwe kwenye tiketi, msafiri badala ya kulipa 10,000 alie 11000,

Itawaokoa wengi ambao hata hawajui ni lini watapanda basi, ndege, meli wala treni kwa maana hawana huo uwezo, lakini wanasimu na hawapigi simu wao, zaidi husubiri wapigiwe tu na kutumiwa pesa kidogo

Tatizo ni kuwa mnajali mno maslahi ya vyama. Hivi wale 19 hadi sasa ngapi zimeshafujwa?

Mkisikiaga wengine wakiambiwa hakutakikani chokochoko basi muwe mnaelewa kuwa ndiyo kama huku kudai kilicho haki.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Hao watu wa chini unaowasema ndio chanzo cha Serikali kutowajibika kwa wananchi. Hawa ndiyo wanakuwa watu wa kwanza kuunga mkono Serikali kwa kila kiti, hata inapowaonea watu.

Hili rungu likae hapo hapo, limbonde kila mtu kichwani, ili akili iliyolala iamke. Wasipopata maumivu hao unaowaita watu wa chini, siku zote wataendelea kuwa kikwazo cha mabadiliko yanayohitajika ili kuwa na uongozi unaowajibika kwa umma.

Hata wakati marehemu, kwa udikteta tu, alipoamua kuwaonea wenye pesa, akawa anawabambikia kesi, anawateka, anawapoteza, kundi kubwa la waliokuwa wakifurahia, ni hilo kundi la watu maskini.
Umeweka hoja yako kwa umakini na weledi mkubwa sana, ili dhahabu ing'ae basi lazima ipite kwenye moto mkali ..kwa hiyo ili akili za hawa masikini wenzangu wanaojiona wanyonge wakipigwa na hili rungu basi kwa wakati mwingine akili zitakaa sawa. kongratis uliejibu hoja[emoji108]
 
Mkuu, Sio vema tuwaache wamezwe mdomoni mwa simba, hata kama kuna mahali wanamakosa, tuendelee kuwatetea mkuu
Utetezi wenye nguvu ni ule wenye kuungwa mkono na umma. Utetezi mwingine wowote hauwezi kuwa na impact ya kuweza kuleta mabadiliko.

Kama watu wanaguswa na haya madhira, nina hakika ndani ya wiki moja Serikali inaondoa hizi tozo dhulumati.

Kwa mfano, wananchi tunaweza kuamua kuwa hatutatumia huduma yoyote ya fedha kupitia simu kwa wiki 1 ili kuishinikiza serikali iondoa tozo dhulumati. Halafu tukasema, kwa siku tatu, hakuna atakayepiga simu, mawasiliano yatakuwa kwa sms, whatsap. Hivi unajua watakaokuwa wa kwanza kusaliti hizo jitihada? Ni hao hao watu wa hali ya chini.

Unamsaidia mtu ambaye na yeye anaonesha kwa vitendo kuwa anahitaji kusaidiwa. Hivyo ni vrma machungu yamguse kila mtu, machungu yachochee umoja dhidi ya dhuluma ya serikali kwa wananchi wake.
 
Ni taifa la kujitolea kwa kila khali, lakini kwa bahati mbaya kabisa utasikia, Fedha zimepotea, fedha bilioni ngapi zimeibiwa sjui na nani, sijui taasisi fulani inajilipa posho ngapi kwa siku

Hii ndio inayoliza walipa kodi
Wewe ni moja ya watu humu mliojifanya hamuoni umuhimu wa katiba mpya sasa hivi unajifanya kulalamika.unalalamika nini sasa?.Wacha ukamiliwe wakazitumie wenye nchi wewe endelea kukodoa macho hadi akili zitakapokujia.
 
Wewe ni moja ya watu humu mliojifanya hamuoni umuhimu wa katiba mpya sasa hivi unajifanya kulalamika.unalalamika nini sasa?.Wacha ukamiliwe wakazitumie wenye nchi wewe endelea kukodoa macho hadi akili zitakapokujia.
Mkuu, unaushahidi?

na hata kama unaushahidi, huwezi kunilazimisha nistoe maoni yangu kisa niko kinyume na mawazo yako
 
Wewe ni moja ya watu humu mliojifanya hamuoni umuhimu wa katiba mpya sasa hivi unajifanya kulalamika.unalalamika nini sasa?.Wacha ukamiliwe wakazitumie wenye nchi wewe endelea kukodoa macho hadi akili zitakapokujia.
Na bahati mbaya sana sina akili ya kushikiwa
 
Sijui ni kivipi mtu anapofika kwenye level fulani ya maisha hutaka kuilazimisha akili yake kuwa na wengine wote wako kama yeye

Badala ya kurudisha akili zake kule alikotoka ili ayapime maisha aliyopitia na hatimaye aone pia wale ambao bado wako huko wanapitia ugumu uleule aliowahi kuupitia yeye kabla hajafika hapo alipo, hata akichaguliwa/bahatika kuwa katika nafasi Fulani ya uongozi, Aumize kichwa chake jinsi ya kuisaidia jamii masikini,

Kusaidia Jamii kama kiongozi, hauhitaji utoe pesa mfukoni mwako

Ni kuweka sera wezeshi ambazo zitaifanya jamii hii masikini kufikia uwalau maisha ya kufurahia uwepo wao hapa duniani

Jamii yetu bado masikini sana, bahati mbaya kabisa, tunao baadhi ya viongozi ambao tangu kuzaliwa hawaijui shida, na ndiyo maana imekuwa ni rahisi kwa viongozi kama hao kupiga makofi kwenye mijadara mingine inayoumiza walala hoi, Lakini Kuzaliwa kwetu katika jamii ambayo haikuwahi kuona shida, isitufanye kutotambua kwamba masikini wa masikini wapo, na shida zipo

Kinacho kwenda kufanyika sasa kwenye sera ya makato ya miamala ya simu, ni kwenda kuzidisha ukali wa maisha kwa jamii kubwa ya watu wa maisha ya chini na kuathiri uchumi wao mdogo unaotegemea jasho jingi ili mtu apate mlo wa siku

Naishauri serikali, Kwa sababu tunajamii kubwa ambayo inaishi kwa kutegemea maisha ya kubangaiza, na kwa sababu tozo hiyo ya miamala na laini ya simu ni mpango wa serikari ipate kodi ili kuendeleza miradi na ujenzi wa barabara vijini

Badala ya kodi hiyo kuingizwa kwenye huduma hizi mhimu na kuifanya huduma hii iwe na makato makubwa kiasi cha kufanya wazee wetu kule vijini wakose msaada kutoka kwa vijana wao wanaowatumia vijisenti vya kujipatia mahitaji yao

Kodi hii ihamishiwe upande wa abiria wanaosafiri kwa mabasi kwenda mikoani, usafiri wa Treni, meli, na ndege, na kodi yake iwe ni kila abilia atakatwa kodi ya sh 1,000 tu kwa kila abiria anayetumia usafiri wa basi kwenda mkoani,

Serikali itafute namna ya kulipa hiyo kodi, ni au iunganishwe kwenye tiketi, msafiri badala ya kulipa 10,000 alie 11000,

Itawaokoa wengi ambao hata hawajui ni lini watapanda basi, ndege, meli wala treni kwa maana hawana huo uwezo, lakini wanasimu na hawapigi simu wao, zaidi husubiri wapigiwe tu na kutumiwa pesa kidogo
Unapigwaaa mwingi kwel kwel..alisikika malisa godlisten, tindo, babati..n.k.
JPM mtamkumbukaaa tuu..iwe isiweee..
 
Mimi kwa mtazamo wangu wale watu ambao wanaona hii issue ni ngumu kwao warudi tu kwenye Yale maisha ya zamani kabla issue ya simu ama miamala kuja. Maana sidhani Kama Kuna ulazima wa kutumia simu kwenye Jambo lolote.

Ambao hawataki wafungie simu zao makabatini na wenye kutaka wakubaliane na hali halisi. Muhimu hapa ni hii Kodi tunayokatwa itumike Kama ilivyokusudiwa. Bunge na mamlaka husika ziifuatilie kwa ukaribu Sana. Sio tukatwe kodi halafu ziishie kufaidisha watu binafsi kwa kuzidokoa.
Eehh..kama walishindwaa kutumia kodi za nyuma kufanya hata mambo madogo tu mfano madawati kwa wanafunzi had jpm akaja na kuliondoa hilo tatizo kwa kiwango kikubwaa unazani hata wakikata elfu sana kwa kila raia wataweza kufanya jambo zaid ya kujilipa wao na familia zao..sahau hilo halipo..barabara zitabak kama zilivyo...na kila kitu kitakuwa business as usual..
 
Kweli nimeamini nchini Ina viongozi wahuni tu,nina hasira Sana basi tu.
Magu aligusa mafisadi mkalalamika kwamba anabambika kesii..anaonea watu..sasa hv mama anawagusaa nyie wanyonge hohe hahee..sasa sijui mtafanyajeee..kaz iendeleeeeeeeeee
 
Unapigwaaa mwingi kwel kwel..alisikika malisa godlisten, tindo, babati..n.k.
JPM mtamkumbukaaa tuu..iwe isiweee..
Laki moja ukitumiwa, ukienda kutoa unakatwa jumla ya sh 6000 badala ya sh 3250, huu ni wizi kwa serikali kwa wananchi wake
 
Mkuu haya ndiyo matatizo nilosema kwenye bandiko hili, Ukibahatika kuwa na maisha fulani hivi, usisahau pia kuwa kuna mtu hajafikia hayo maisha, bahati mbaya hii kodi inaenda kukusanywa kwa kiwango kilekile cha mtu wa chiiini zaidi, wa kati na wa juu kwa kiwango kilekile,

Kwa nini kodi hizi zisielekezwe kwa wasafiri wa ndege, meli, mabasi ya mikoa n.k?
Hivi tunatambua ata mb zilizotumia humu. Ni matumizi yasiyo yalazima?
 
JPM aliwezaje kuendesha nchi hii bila vitozo vya ajabuajabu?
 
Sijui ni kivipi mtu anapofika kwenye level fulani ya maisha hutaka kuilazimisha akili yake kuwa na wengine wote wako kama yeye

Badala ya kurudisha akili zake kule alikotoka ili ayapime maisha aliyopitia na hatimaye aone pia wale ambao bado wako huko wanapitia ugumu uleule aliowahi kuupitia yeye kabla hajafika hapo alipo, hata akichaguliwa/bahatika kuwa katika nafasi Fulani ya uongozi, Aumize kichwa chake jinsi ya kuisaidia jamii masikini,

Kusaidia Jamii kama kiongozi, hauhitaji utoe pesa mfukoni mwako

Ni kuweka sera wezeshi ambazo zitaifanya jamii hii masikini kufikia uwalau maisha ya kufurahia uwepo wao hapa duniani

Jamii yetu bado masikini sana, bahati mbaya kabisa, tunao baadhi ya viongozi ambao tangu kuzaliwa hawaijui shida, na ndiyo maana imekuwa ni rahisi kwa viongozi kama hao kupiga makofi kwenye mijadara mingine inayoumiza walala hoi, Lakini Kuzaliwa kwetu katika jamii ambayo haikuwahi kuona shida, isitufanye kutotambua kwamba masikini wa masikini wapo, na shida zipo

Kinacho kwenda kufanyika sasa kwenye sera ya makato ya miamala ya simu, ni kwenda kuzidisha ukali wa maisha kwa jamii kubwa ya watu wa maisha ya chini na kuathiri uchumi wao mdogo unaotegemea jasho jingi ili mtu apate mlo wa siku

Naishauri serikali, Kwa sababu tunajamii kubwa ambayo inaishi kwa kutegemea maisha ya kubangaiza, na kwa sababu tozo hiyo ya miamala na laini ya simu ni mpango wa serikari ipate kodi ili kuendeleza miradi na ujenzi wa barabara vijini

Badala ya kodi hiyo kuingizwa kwenye huduma hizi mhimu na kuifanya huduma hii iwe na makato makubwa kiasi cha kufanya wazee wetu kule vijini wakose msaada kutoka kwa vijana wao wanaowatumia vijisenti vya kujipatia mahitaji yao

Kodi hii ihamishiwe upande wa abiria wanaosafiri kwa mabasi kwenda mikoani, usafiri wa Treni, meli, na ndege, na kodi yake iwe ni kila abilia atakatwa kodi ya sh 1,000 tu kwa kila abiria anayetumia usafiri wa basi kwenda mkoani,

Serikali itafute namna ya kulipa hiyo kodi, ni au iunganishwe kwenye tiketi, msafiri badala ya kulipa 10,000 alie 11000,

Itawaokoa wengi ambao hata hawajui ni lini watapanda basi, ndege, meli wala treni kwa maana hawana huo uwezo, lakini wanasimu na hawapigi simu wao, zaidi husubiri wapigiwe tu na kutumiwa pesa kidogo
Kumtoza abiria hiyo Kodi Kuna tofauti gani na kutoza kwenye Simu.After all ukitoza kwenye nauli pesa haitafika yote serikalini
 
Mkuu, unaushahidi?

na hata kama unaushahidi, huwezi kunilazimisha nistoe maoni yangu kisa niko kinyume na mawazo yako
Acha kuweweseka wewe.sasa hivi baada ya hili kukugusa ndio unajifanya unatoa mawazo yako.Wale wengine waliokua wanatoa mawazo yao kuhusu katiba mbona hukuona nawao walikua wanatoa mawazo yao?.au ulidhani mambo ovyo nchi hii hayatakugusa.Na usijisahaulishe maana coment zako zakubeza ziko nyingi tu.Dunia duara.
 
Back
Top Bottom