Mhe, Kinana asante sana, nawe afande IGP Wambura sikia kilio hiki cha Watanzania.
Matrafiki karibia wote hawako barabarani kiusalama wa laia na mali zao.
Bali ni usalama wa matumbo yao wenyewe!
Yaani mtu inafikia huna kosa lolote, lakini unaambiwa kwamba unatuachaje-achaje hapa! Kwao gari bovu siyo chukizo tena ila rasilimali yao kubwa.
Hali imezidi kuwa mbaya mpaka ma-RTO na Ma-DTO wameona kuwa ofisini hakulipi, nao wameingia mzigoni.
Hatukatai mtu kufanya maendeleo yake binafsi. Lakini siyo kushindana kununua magari na kujenga nyumba kwa pesa za kuwapora laia.
Waheshimiwa, nakubaliana kwamba wapunguzwe barabarani, lakini na watakaosalia wafuatiliwe, mbona huwa wanachukuwa pesa waziwazi mno? Kwani Takukuru ya nchi hii huwa kazi yao nini hasa. Mbona ni rahisi kuwakamata waovu hawa?
Hivi takukuru hata kutegesha camera kwenye vijiwe vyao nako kumewashinda?
Au ndiyo nanyi fungu linawafikia? Sasa kama ninyi hamfanyi hivyo nani huwa anawadhibiti watu hawa?
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinanana amemshauri Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP)...