Kinana akerwa na Utitiri wa Traffic barabarani. Atoa maagizo mazito kwa Afande IGP Camilius Wambura

Kinana akerwa na Utitiri wa Traffic barabarani. Atoa maagizo mazito kwa Afande IGP Camilius Wambura

Wata mjibu. Kama waliweza kumjibu Mh. Rais, sitoshangaa hata Kinana akajibiwa kwamba wao wana intelijensia. Asiwaingilia.
 
Sisiem kwa ngenga hawajambo maneno na matendo mbingu na ardhi.
 
Hili aliongea kinana yuko sahihi sana, ni aibu kwa nchi ya Tanzania kila mita 10 unakuta traffic tena wana uliza maswali yale yale ya kijinga, eti fire extinguisher, driving license, insurance, wanaangalia tairi, wengine wako na list ya makosa 48 wana tazama, wengine wana jificha porini na tochi, huu nu upuuzi sana.

Utadhani nchi yetu iko vitani, kila mita 10 traffic police, ni kero kubawa sana , wengine hadi wanaomba maji ya kunywa kinyume na maadili kazi zao, ilitakiwa kutoka Arusha hadi Dar walai usimame mara moja au hakuna, kuwe na one stop traffic checking ,na after checking watoe certificate/kibali kuwa tume kagua mazaga zaga yote baada ya hapo safari inaanza hadi ufikapo kusiwe na utitiri huu wa kijinga.
 
Akijibu malalamiko hayo Kinana amesema “Nampongeza Rais kwa kumtea IGP mpya, nina hakika ni IGP mwadilifu, mchapakazi na hodari lakini namuomba na kumshauri atazame wingi wa Trafiki mijini, kila baada ya muda mfupi unasimamishwa na Trafiku, wenye magari hawaendeshi kwa raha, hivyo nimsihi IGP afanye tathimini kuhusu uwepo wa Trafiki wengi kwenye miji yetu, wamekuwa wengi sana kila ukitembea kidogo unasimamishwa, kilomita moja unakuta Trafiki”
Mwenye mamlaka na yeye anaomba badala ya kutoa maagizo
 
Kama daktari mmoja wagonjwa 80, mwalimu mmoja wanafunzi 40, trafiki mmoja magari mangapi? tuanzie hapo kwanza.....
Magari yanaweza kuwa mengi pia,jiulize ni magari mangapi yenye makosa ya barabarani yanayofika vituoni?Je,wingi wa Traffic Police kumesaidia kwisha kwa ajali za barabarani zinazotokana na ubovu wa vyombo,miundo mbinu ya usafirishaji?Je,vyombo vingapi visivyofaa kuwa barabarani na bado vinatembea?Madereva wangapi wenye sifa stahiki wapo barabarani?
Je,hakuna technology inayoweza kufanya kazi wafanyazo askari hawa wanaopamba barabara zetu kwa suti zao nyeupe?
Ah,acha niishie hapo kwa sasa maana jamaa wapo pale kukusanya na bei elekezi zinafahamika,ila TAKUKURU na Watanganyika wametulia tuli.
 
Sio magari tu, Bodaboda pia.
Vituo vidogo vimejaza pikiki balaa
 
Tatizo la dot.com tunalaamu tu bila ya Kuja na mbadala, sasa wewe una comment hapa hii sio suluhu!,sasa tell us how to remedy this
Suluhu zilishatolewa, na wanazijua. Waliambiwa wa'digitize' mifumo yote inayohusu usalama barabarani na matukio yote yawe recorded na kuwa reported in real time! Badala yake wamedigitize tozo peke yake. Digitization inatakiwa iende kwenye maeneo yote.

Na tungeweza kufanikiwa hili kama tungekuwa na nishati ya uhakika kwa kukamilika Bwawa la umeme la Mwalimu Nyerere huko Rufiji! Lakini, wale wanao lipinga Bwawa hilo wanatushauri tutumie nishati ya haja kubwa zetu (rejea hotuba ya Balozi wa Uholanzi nchini Wieb De Boer aliponukuliwa na ITV- tazama kuanzia dakika 7 sekunde 42) kuwa na nishati!


Sina hakika kama tuna elewana hapa!
 
Tatizo kubwa hao Traffic wamewekwa kuwa chanzo cha mapato serikalini na kwao wenyewe.
Hawa wamewekwa kuwa chanzo cha mapato kwa wanaowapangia vitengo.

Mitaani tunalazimishwa ulinzi shirikishi wakati watu tunaowalipa kutulinda kwa kodi zetu wamegeuka majambazi wakutupora, tena kwa kutumia rasilimali zinazogharamiwa na kodi zetu.

Kuna hawa askari polisi wanaotumia pikipiki. Wao ni kufukuzana na watu mchana mitaani kupora mali za watu. Tukio la uhalifu litokeapo usiku hakuna askari wa kusaidia.

Jeshi la polisi linahitaji major overhaul.
 

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinanana amemshauri Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Camilius Wambura kufanya tathimini ili kuona uwezekano wa kupunguza idadi ya Askari wa usalama barabarani ambao wanalalamikiwa na Wananchi kusababisha kero.

Kinana ametoa ushauri huo jana akiwa katika mwendelezo wa ziara yake katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ambapo Wananchi wa maeneo mbalimbali ya Mikoa ya Songwe na Mbeya wamelalamikia idadi kubwa ya Askari wa barabarani ambao wamekuwa wakiwasimamisha mara kwa mara, kutaka fedha ambazo hata hivyo hawatoi stakabadhi yoyote.

Malalamiko hayo ya Wananchi yaliendelea kuibuka hata katika kikao cha ndani cha Wanachama wa CCM Mkoa wa Songwe ambapo mmoja ya wanachama hao, dereva wa magari ya kubeba abiria, ametoa malalamiko mbele ya Kinana akidai wamechoka kusimamishwa mara kwa mara na Trafiki na kila wanaposimama wanatoa sh. 2,000 kwa kila kituo.

Akijibu malalamiko hayo Kinana amesema “Nampongeza Rais kwa kumtea IGP mpya, nina hakika ni IGP mwadilifu, mchapakazi na hodari lakini namuomba na kumshauri atazame wingi wa Trafiki mijini, kila baada ya muda mfupi unasimamishwa na Trafiku, wenye magari hawaendeshi kwa raha, hivyo nimsihi IGP afanye tathimini kuhusu uwepo wa Trafiki wengi kwenye miji yetu, wamekuwa wengi sana kila ukitembea kidogo unasimamishwa, kilomita moja unakuta Trafiki”
Anakereka mzigo wake unapekuliwa sana unapopita
 

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinanana amemshauri Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Camilius Wambura kufanya tathimini ili kuona uwezekano wa kupunguza idadi ya Askari wa usalama barabarani ambao wanalalamikiwa na Wananchi kusababisha kero.

Kinana ametoa ushauri huo jana akiwa katika mwendelezo wa ziara yake katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ambapo Wananchi wa maeneo mbalimbali ya Mikoa ya Songwe na Mbeya wamelalamikia idadi kubwa ya Askari wa barabarani ambao wamekuwa wakiwasimamisha mara kwa mara, kutaka fedha ambazo hata hivyo hawatoi stakabadhi yoyote.

Malalamiko hayo ya Wananchi yaliendelea kuibuka hata katika kikao cha ndani cha Wanachama wa CCM Mkoa wa Songwe ambapo mmoja ya wanachama hao, dereva wa magari ya kubeba abiria, ametoa malalamiko mbele ya Kinana akidai wamechoka kusimamishwa mara kwa mara na Trafiki na kila wanaposimama wanatoa sh. 2,000 kwa kila kituo.

Akijibu malalamiko hayo Kinana amesema “Nampongeza Rais kwa kumtea IGP mpya, nina hakika ni IGP mwadilifu, mchapakazi na hodari lakini namuomba na kumshauri atazame wingi wa Trafiki mijini, kila baada ya muda mfupi unasimamishwa na Trafiku, wenye magari hawaendeshi kwa raha, hivyo nimsihi IGP afanye tathimini kuhusu uwepo wa Trafiki wengi kwenye miji yetu, wamekuwa wengi sana kila ukitembea kidogo unasimamishwa, kilomita moja unakuta Trafiki”
Biashara zake za meno ya tembo zinacheleweshwa na Trafiki kufika sokoni
 
Waje na mbadla wake. Tuwe na camera , watu wakutane na bill zao mwisho wa mwezi.
 
Kinana anabanwa kusafirisha dili zake ?
Akae kwa kutulia, nchi inahitaji ulinzi hii.
 
Barabara nzuri za lami lakini usafiri hauna tija. Traffic wanatumia gari binafsi Bagamoyo - Msata kumulika magari toka kichakan. Je chaoi na cha serikali kipi kikubwa. Tume ya Kipolisi ilifanyie kazi. Tanrods wanaweka 50km limit kila pahala. Kivuli?. Haina raha tena kwenda mikoani kwa gari binafsi. Bora nitumie mabasi.


Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinanana amemshauri Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Camilius Wambura kufanya tathimini ili kuona uwezekano wa kupunguza idadi ya Askari wa usalama barabarani ambao wanalalamikiwa na Wananchi kusababisha kero.

Kinana ametoa ushauri huo jana akiwa katika mwendelezo wa ziara yake katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ambapo Wananchi wa maeneo mbalimbali ya Mikoa ya Songwe na Mbeya wamelalamikia idadi kubwa ya Askari wa barabarani ambao wamekuwa wakiwasimamisha mara kwa mara, kutaka fedha ambazo hata hivyo hawatoi stakabadhi yoyote.

Malalamiko hayo ya Wananchi yaliendelea kuibuka hata katika kikao cha ndani cha Wanachama wa CCM Mkoa wa Songwe ambapo mmoja ya wanachama hao, dereva wa magari ya kubeba abiria, ametoa malalamiko mbele ya Kinana akidai wamechoka kusimamishwa mara kwa mara na Trafiki na kila wanaposimama wanatoa sh. 2,000 kwa kila kituo.

Akijibu malalamiko hayo Kinana amesema “Nampongeza Rais kwa kumtea IGP mpya, nina hakika ni IGP mwadilifu, mchapakazi na hodari lakini namuomba na kumshauri atazame wingi wa Trafiki mijini, kila baada ya muda mfupi unasimamishwa na Trafiku, wenye magari hawaendeshi kwa raha, hivyo nimsihi IGP afanye tathimini kuhusu uwepo wa Trafiki wengi kwenye miji yetu, wamekuwa wengi sana kila ukitembea kidogo unasimamishwa, kilomita moja unakuta Trafiki”
 
Trafic wanadai hela toka kwa madereva kwa nguvu hasa Dar.
 
Kinana anasahau kuwa traffic ni chanzo kipya na cha kuaminika cha mapato ya serikali?
 
Back
Top Bottom