Kinana: CCM imevunja rekodi ukusanyaji wa maoni juu ya Rasimu ya Katiba Mpya

Kinana: CCM imevunja rekodi ukusanyaji wa maoni juu ya Rasimu ya Katiba Mpya

Mkuu angalia usemi
wako kwa sababu katika usemi huu wewe ndiyo unaonekana 'mshamba'.

Maoni ya wananchi wote yalikusanywa na Tume ya Jaji Warioba kupitia
Mabaraza ya Katiba ambayo yaliundwa, kusimamiwa na kuendeshwa na Tume ya
Mabadiliko ya Katiba mojawapo ya mabaraza hayo ni mabaraza ya kata,
wilaya n.k. ambayo yalilalamikiwa na CHADEMA kuwa yamejaa wanaCCM pekee
badala ya wananchi wote.

Mabaraza ya CCM ni mabaraza ya taasisi ambayo yanaundwa na taasisi
yenyewe. Haya ni sehemu ya pili ya aina ya mabaraza kama yalivyoainishwa
katika Sheria ya Mabadiliko ya Katiba Sura ya 83. Haya ni pamoja na
Asasi na makundi ya watu wenye mwelekeo na malengo yanayofanana hii ina
maana kwamba hata walevi au wafungwa wanaweza wakaanzisha baraza lao la
katiba kama tume ya Jaji Warioba itaona umuhimu wa kuwepo.

CCM kama Taasisi iliyoundwa na wanachama na pia kuwepo kwake kisheria
kunategemea wanachama ndiyo maana imekusanya maoni ya wanachama wake
kama Taasisi.

Hii ndiyo inapelekea kuwepo kwa hoja ya Jaji Warioba aliposema kuwa
hawatachukua maoni ya "jukwaani wala ya kwenye helikopta" kwa cover la
Taasisi pamoja na kwamba kauli yake hiyo ni debatable.

ukweli mchungu kwa chadema. hakika chadema hawapendi kujua ukweli labda kwa vile viongozi wao na wafuasi wao wengi wao ni vihiyo
 
Labda hayo maoni kinana alikuwa anakusanya serengeti na Ngorongoro wakati akiwa anavuna tembo kama kawaida yake
 
Chama
kilichokusanya maoni ya wanachama wao kwa uwazi ni chadema tu na
sivinginevyo, vingine ni kuforge data kwa kwenda mbele!

kuna haja ya chadema kuelimishwa ili wajue maana ya taasisi. maana wengi wao hata wanachoongea hakijulikani
 
Badala ya kusema mimi
ninapotosha, ingekuwa vizuri ukaelewa kilichoko kwenye bandiko langu.

Wapi nimesema maoni ya CCM yamekusanywa kutoka kwenye Mabaraza ya Katiba
ambayo yaliundwa, kusimamiwa na kuendeshwa na Tume ya Mabadiliko ya
Katiba. Legally, Mabaraza yanayosimamiwa na kuendeshwa na Tume ya
Mabadiliko ya Katiba niya wananchi wote yanayotokana na wajumbe
waliochaguliwa na wananchi wote kupitia mitaa, kata, wilaya n.k

Sasa wewe unataka CCM ionyeshe jinsi ilivyokusanya maoni ya wanachama
wake wapi?. Hapa JF?.

Kwanza ukiangalia hata hiyo video haionyeshi hotuba nzima ya Katibu Mkuu
wa CCM kwa maana kuwa hatufahamu baada ya kutoa hayo maelezo aliendelea
kusema nini zaidi, lakini kikubwa zaidi anayetakiwa kujua njia ambazo
CCM walitumia kupata mapendekezo yao ni Tume ya Jaji Warioba kupitia
vidhibiti ambavyo Tume ya Jaji Warioba inazitaka taasisi mbali mbali
kukamilisha.

mkuu, hawa chadema nafikiri wamepungukiwa kwa kiasi kikubwa sana uelewa juu ya ukusanyaji wa maoni ya taasisi. pia hawajui kama kinachhojadiliwa sasa ni rasimu ya katiba na si maoni ya wananchi juu ya katiba mpya. chadema walichokifanya si kukusanya maoni ya wanachama wao bali walikuwa wanawaambia wananchi nini msimamo wao juu ya rasimu hiyo.
 
Chama kilichokusanya maoni ya wanachama wao kwa uwazi ni chadema tu na sivinginevyo, vingine ni kuforge data kwa kwenda mbele!

Ndivyo ambavyo CCM hupiga bao kirahisi bila wapinzani kujua, Kwani kabla hata chopa kuanza kuruka CCM Ilikuwa na vikao vyake vya mabaraza ya kata na nililishuhudia kule visiwani, Mabaraza ya Kata ya CCM yameanza kabla ya mabaraza ya Tume ndiyo maana wengi walioyasikia walidhani ni yaliyoundwa na Tume
 
Labda hayo maoni kinana
alikuwa anakusanya serengeti na Ngorongoro wakati akiwa anavuna tembo
kama kawaida yake

hizo kejeli zenu zinadhihirisha namna gani mlivyo watupu kwenye jambo hili. by the way, kama nyie si members wa ccm, iweje mjue kuwa haijakusanya maoni ya taasisi?
 
Duuuuuh kweli CCM ina wenyewe na wenyewe ndo waliotoa maoni!!..Zidumu fikra za mwenyekiti..Hiki chama ni michosho miyeyusho isiyo na mwisho!! Kimekaa kiuwizi uwizi tuuu na kitapelitapeli..Inafikia hatua mpaka wanaanza kujiibia wenyewe..Hayo maoni walikusanya wapi? lini? kwa kutumia nini?? na waliwatumia watu gani?? Upuuzi huu unaofanywa na wahuni wachache ndani ya CCM kuvuruga kila jambo haukubaliki tena!!
 
Ndivyo ambavyo CCM
hupiga bao kirahisi bila wapinzani kujua, Kwani kabla hata chopa kuanza
kuruka CCM Ilikuwa na vikao vyake vya mabaraza ya kata na nililishuhudia
kule visiwani, Mabaraza ya Kata ya CCM yameanza kabla ya mabaraza ya
Tume ndiyo maana wengi walioyasikia walidhani ni yaliyoundwa na
Tume

mkuu, yaani hapo ndipo ccm inadhihirisha kuwa ni chama makini na kongwe. pia kina mfumo na viongozi thabiti toka mabalozi wa nyumba kumi hadi mwenyekiti Taifa. ccm wanajua sheria inasemaje na ndo maana walijipanga mapema
 
Hayo maoni ya Kinana atakuwa aliyatoa kwa TEMBO maana hakuna sehemu nyingine yalipopatikana ambayo iko wazi!!
 
Duuuuuh kweli CCM ina
wenyewe na wenyewe ndo waliotoa maoni!!..Zidumu fikra za
mwenyekiti..Hiki chama ni michosho miyeyusho isiyo na mwisho!! Kimekaa
kiuwizi uwizi tuuu na kitapelitapeli..Inafikia hatua mpaka wanaanza
kujiibia wenyewe..Hayo maoni walikusanya wapi? lini? kwa kutumia nini??
na waliwatumia watu gani?? Upuuzi huu unaofanywa na wahuni wachache
ndani ya CCM kuvuruga kila jambo haukubaliki tena!!

wewe kwa vile umeajiriwa kutoa maoni ya chadema humu jf ndo unajidanganya kuwa ccm ni ya wachache. kumbuka mchakato wa chadema umeanzia kwa mabalozi na sasa ni ccm Taifa. hapo mmepigwa bao la kisigino. nyie sijui mtakaa lini vikao vya taifa maana viongozi wenu wanafurahia tu kuruka kwa chopa na kujichotea mamilioni ya fedha
 
CCM wao walichagua njia ya kukusanya maoni siyo kwenye mikutano ya nje bali mikutano ya ndani kwa maana hiyo kwa kiasi kikubwa ni wanachama wa CCM pekee waliohudhuria hiyo mikutano ndiyo wanaofahamu vizuri process yao ya ukusanyaji wa maoni.

Kuna thread ililetwa hapa JF ya tamko la Nape kuhusu utaratibu wao katika ukusanyaji wa maoni kupitia wanachama wao kama taasisi.


OK, lets assume you and CCM are right. Kwa utaratibu walioutumia CCM, naomba ufafanuzi wa statement: CCM YAVUNJA REKODI UKUSANYAJI WA MAONI

Kama hiyo ndio njia waliyoitumia (kujifungia vyumbani), wamevunja rekodi ya nani? Iliyokuwa imewekwa na nani? Kulinganisha na ya nani? Kwa data zipi? Hebu waache longo longo za kujitafutia cheap populariy.
 
Hayo maoni ya Kinana atakuwa aliyatoa kwa TEMBO maana hakuna sehemu nyingine yalipopatikana ambayo iko wazi!!
Mkuu, wee endelea tu na porojo zako. Wenzako wako serious katika hili. Ccm ni chama ambacho kina watu makini sana na kinafanya kwa mujibu wa sheria. Thanx Jaji Warioba kwa kuwapasha ukweli CHADEMA. walithani kwa kuruka na chopa ndo kukusanya maoni kumbe walikuwa wanajipotezea muda bure
 
Nimeamini Chadema chama kubwa na ndio chama pekee cha upinzani maana kila anaepinga magamba hapa JF anaonekana ni chadema. LONG LIVE CHAMA DUME CHADEMA
 
Mkuu, wee endelea tu na porojo zako. Wenzako wako serious katika hili. Ccm ni chama ambacho kina watu makini sana na kinafanya kwa mujibu wa sheria. Thanx Jaji Warioba kwa kuwapasha ukweli CHADEMA. walithani kwa kuruka na chopa ndo kukusanya maoni kumbe walikuwa wanajipotezea muda bure
Kweli CCM ina watu makini kama mwenyekiti wao kwa kuhongwa suti na vyandarua na kutoa dhahabu na tanzanite yetu. Pia kina watu kama kinana ambao wako makini katika ukamati wa tembo bila tembo kupiga kelele, watu makini kama Nchemba kwa kupiga bomu mabomu na bila kukamatwa, wako wengi naomba niishie hapo.
 
OK, lets assume you and CCM are right. Kwa utaratibu walioutumia CCM, naomba ufafanuzi wa statement: CCM YAVUNJA REKODI UKUSANYAJI WA MAONI

Kama hiyo ndio njia waliyoitumia (kujifungia vyumbani), wamevunja rekodi ya nani? Iliyokuwa imewekwa na nani? Kulinganisha na ya nani? Kwa data zipi? Hebu waache longo longo za kujitafutia cheap populariy.
CCM imevunja rekodi yake yenyewe iliyoweka mwaka 1977 wakati wa mchakato wa uundwaji wa kariba ya sasa.
 
mjomba umeshaambiwa vikao hivyo vya ndani unavyodai viliwahusu wana ccm wachache sana na vilikuwa siyo vya kutoa maoni kama unayodai bali vya kuwakaririsha mistari ya kwenda kusema mbele ya tume na wengine wakashindwa hata kusema wakafikia kusoma mbele ya wajumbe wa tume na wengine kuishia kutimuliwa. ccm haijawahi kuita wanachama watoe maoni yao
Mkuu kumbuka kuna aina mbili ya mabaraza ya katiba ambapo aina moja ni Mabaraza ya Katiba ambayo yaliundwa, yakasimamiwa na kuendeshwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba na aina ya pili ni Mabaraza ya Katiba ya Asasi, Taasisi na Makundi ya Watu wenye Malengo yanayofanana.

Maelezo yako naona kama unachanganya kati ya wajumbe wa mabaraza yaliyosimamiwa na Tume ya mabadiliko ya katiba ambapo wajumbe wengi wanasemekana walikuwa ni viongozi na wanachama wa CCM ambapo inadaiwa walifanyishwa vikao na kukaririshwa vipengere ambavyo walitakiwa wakavitoe kwenye vikao vya mabaraza hayo kama wajumbe.

CCM pia ni taasisi ambayo inaangukia kwenye aina ya pili ya mabaraza ya katiba ambayo muundo na uratibu na uendeshaji wake unatokana na jinsi inavyoona unafaa katika kuichambua rasimu ya Katiba. Wajumbe wake wanaweza wakawa pia ni kati ya wale waliokuwa pia kwenye kundi la kwanza lakini maoni yao katika kundi hii yanachukuliwa niya kitaasisi kama zilivyo Asasi na Vikundi vingine.
 
Kweli CCM ina watu makini kama mwenyekiti wao kwa kuhongwa suti na vyandarua na kutoa dhahabu na tanzanite yetu. Pia kina watu kama kinana ambao wako makini katika ukamati wa tembo bila tembo kupiga kelele, watu makini kama Nchemba kwa kupiga bomu mabomu na bila kukamatwa, wako wengi naomba niishie hapo.
Mkuu, hiyo mioasho yenu haitawaondolea CHADEMA aibu na ujinga mliouonesha wakati wa mchakato wa kupata maoni ya Taasisi juu ya rasimu ya katiba mpya. Hakika CHADEMA mmejiaibisha sana na inaonesha ni namna gani chama kimekosa watu muhimu wa kuwashauri viongozi wao
 
OK, lets assume you and CCM are right. Kwa utaratibu walioutumia CCM, naomba ufafanuzi wa statement: CCM YAVUNJA REKODI UKUSANYAJI WA MAONI

Kama hiyo ndio njia waliyoitumia (kujifungia vyumbani), wamevunja rekodi ya nani? Iliyokuwa imewekwa na nani? Kulinganisha na ya nani? Kwa data zipi? Hebu waache longo longo za kujitafutia cheap populariy.

Mkuu Kwa maneno ya Viongozi wa CCM, rekodi walioivunja ni hii hapa,
Jaji Warioba alisema Idadi ya wananchi wanaohudhuria na kutoa maoni katika mikutano nayo imeongezeka. Kwa mfano, idadi ya wananchi waliohudhuria mikutano ya awamu ya kwanza walikuwa 189,526. Awamu ya pili ni 325,915 wakati wananchi waliohudhuria mikutano ya awamu ya tatu ni 392,385. Aidha, wananchi waliotoa maoni kwa kuzungumza katika mikutano ya awamu ya kwanza walikuwa 17,127. Awamu ya pili walikuwa 12,334 wakati wananchi 21,512 walizungumza katika awamu ya tatu;
Tume ya Mabadiliko ya Katiba

Wakati wao CCM wanadai wamefanya jumla ya Mabaraza 18,879, huku washiriki wakiwa 2,618,753 ambayo hayo yamefanyika kuanzia 15/07/2013 up to 24/08/2013 when compare to above figure.
 
Back
Top Bottom