Tetesi: Kinara wa kukwamisha Rais Magufuli asiwe Mwenyekiti wa CCM ni Rajab Luhwavi, NKM CCM Bara

Tetesi: Kinara wa kukwamisha Rais Magufuli asiwe Mwenyekiti wa CCM ni Rajab Luhwavi, NKM CCM Bara

Status
Not open for further replies.
Lizaboni jambo usilolojua ni kwamba CCM ni kama nyati aliepigwa risasi kadhaa (ndio haya matukio yote)na UKAWA.Kilichopo sasa hivi ni mwindaji UKAWA anafuatilia matone ya damu ajichinjie mzoga wake.Ni suala zima la timing tu
Duh! Endeleeni kujifariji. Hiyo UKAWA ya Lowasa itakayoiangusha CCM?
 
Watashindwa kumzuia Magufuli kushika chama.!
 
Mkulu lizaboni ktk ubora wake.
Nimezoea kuona unaandika mistari miwili ikizidi mitatu
Hapa utakuwa umeguswa sana
 
Taarifa za kiintenjensia kutoka kwa kamanda wa dodoma kuhusu hili zinasemaje? Wataandamana tena kama jana?
 
Raisi wa JMT na mwenyekiti wa CCM JPM 2016-2030
 
Taarifa za kiintenjensia kutoka kwa kamanda wa dodoma kuhusu hili zinasemaje? Wataandamana tena kama jana?
 
Lizaboni jambo usilolojua ni kwamba CCM ni kama nyati aliepigwa risasi kadhaa (ndio haya matukio yote)na UKAWA.Kilichopo sasa hivi ni mwindaji UKAWA anafuatilia matone ya damu ajichinjie mzoga wake.Ni suala zima la timing tu
UKAWA ilishakufa, sema Chadema na wanachama wake wapya ambao ni James Mbatia na Seif Sharif
 
Labda katumwa aiue ccm. Maana kwa sasa ccm bila JPM hakuna chama. Leo JPM akiondoka ccm inabaki mabua.
 
Chama kimezaliwa upya. Wasaliti wanapaswa kwenda kutafuta maficho yao CHADEMA
leo umeandika vizuri ila unanikera unapoweka chadema,ukawa. wajumbe wa MM wataamua jinsi ya kufanya ila tusubiri mwanga utokee..
 
Mkuu Lizaboni, miaka 5 iliyopita huyu Ruhwavi pia iliwahi kuamuriwa akamatwe na polisi na kufikishwa mbele ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi kwa kukiuka kifungu namba 13 ya kutowasilisha fomu ya maelezo ya mali au madeni.

Sababu ya kuamuru kukamatwa kwake ni kitendo chake cha kusepa na asijulikane akipo.
Yatakuwa majipu ya mwanzo kbsa kutumbuliwa na JPM
 
Wadau amani iwe kwenu.

Hivi karibuni, tumeshuhudia harakati kadhaa za baadhi ya wanasiasa wa ndani na nje ya CCM wakipaza sauti zao kutaka Rais Magufuli asiwe Mwenyekiti wa Chama hicho ili kumrithi Dr Jakaya Kikwete ambaye anatarajiwa kustaafu rasmi wadhifa huo Julai 23.

Awali kulikuwa na figisu figisu nyingi kuwa chama hakina fedha za kuendeshea Mkutano Mkuu ili tu lengo lao litimie. Thanks kwa jitihada zilizofanywa na Katibu Mkuu Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti Bara Philip Mangula ambao wamehakikisha kuwa fedha zinapatikana na mkutano Mkuu unafanyika Julai 23.

Hata hivyo, tunapoelekea Julai 23, yapo Mambo kadhaa yanaendelea ndani ya CCM ambayo kwa hakika yanaweza kuvuruga utamaduni ambao imejiwekea wa kukabidhiana madaraka ya Uenyekiti pindi Rais anapomaliza muda wake. This time, zipo harakati za chini kwa chini zinazoendeshwa ili Kikwete aendelee kuwa Mwenyekiti na Magufuli abaki kwenye cheo cha Urais tu.

Binafsi baada ya kuona kuwa vuguvugu hilo linazidi, ikabidi niingie chimbo ili kumnasa anayeinjinia mkakati huo. Hakika nilichokibaini kinanishtua sana. Mchawi sasa kajulikana. Ni Rajab Luhwavi, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara ambaye ametwaa madaraka hayo tarehe 9 Julai 2015 mara Baada ya Mwigulu Nchemba kujiuzulu nafasi hiyo wakati wa mchakato wa kumpata Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM. Mtakumbuka kuwa Luhwavi alikuwa Msaidizi wa Rais kwenye Masuala ya Siasa kabla ya nafasi hiyo kumuachia Martin Shigela Julai 2015.

Hoja za Luhwavi kutaka Magufuli asiwe Mwenyekiti wa CCM ni za kitoto sana. kwamba, Magufuli hakijui chama na hivyo yeye pamoja na genge lake wanaamini kuwa atakiharibu badala ya kukiimarisha. Hofu yao imeongezeka hasa kutokana na (kwa mtazamo wao) teuzi alizofanya Rais mpaka sasa kutozingatia kigezo cha Ukada wa CCM.

Hofu nyingine ya Luhwavi ni kupoteza madaraka ndani ya CCM. Luhwavi anaamini kuwa ikiwa Magufuli atakuwa Mwenyekiti wa CCM, hatakuwa na wadhifa wowote ndani ya chama na kwamba hata hiyo nafasi ya Unaibu Katibu Mkuu ataipoteza.

Pia Luhwavi ana hofu kubwa ya kufikishwa Mahakamani kutokana na kufuja fedha nyingi zilizotengwa wakati wa kampeni. Inaelezwa kuwa Luhwavi alikihujumu chama kwa kupeleka fedha kidogo kwenye majimbo ya uchaguzi tofauti na ilivyoidhinishwa na chama. Inadaiwa kuwa kwa baadhi ya mikoa, fedha hizo hazikwenda kabisa na hivyo kufanya baadhi ya wagombea kujigharamia hali iliyochangia kushindwa kwao.

Nani anampendekeza Luhwavi awe Mwenyekiti wa CCM? Hili lipo dhahiri. Luhwavi anataka Jakaya Kikwete aendelee kwenye wadhifa huo. Matarajio ya Luhwavi ni kwamba, ikiwa Kikwete ataendelea kuwa Mwenyekiti wa CCM, atamteua yeye (Luhwavi) kuwa Katibu Mkuu kujaza nafasi ya Katibu Mkuu wa sasa Abdulrahman Kinana ambaye ametangaza kuachia nafasi hiyo baada ya Mkutano Mkuu wa Julai 23.

Mpaka sasa, Luhwavi amezunguka kwenye mikoa kadhaa ya Tanzania Bara kuhamasisha wajumbe wa Mkutano Mkuu wasiridhie hoja ya Magufuli kuwa Mwenyekiti wa CCM. Inasemekana kuwa mpunga wa kutosha umetembea kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu ili wamkwamishe Rais Magufuli.

Hata hivyo, inaonekana dhahiri sasa kuwa mkakati wa Luhwavi na Timu yake umegonga mwamba. Mwenyekiti wa sasa Jakaya Kikwete amesema hataongeza hata sekunde moja na kwamba dhamira yake ya kwenda kulala usingizi baada ya Magufuli kushinda Urais iko pale pale. Hana mashaka hata kidogo na Rais na anawabeza wale wanaodhani kuwa Magufuli hana uzoefu wa kutosha kuongoza chama. Kwamba, kama amechaguliwa kuwa Rais wa nchi, atashindwaje kuongoza chama?

Nani walio nyuma ya harakati hizo? Nitaendelea kuwajuza kwa kadri tunavyokaribia Julai 23. Stay with me. Niwapongeze tu na kuwatia moyo baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa mikoa ya Njombe, Iringa, Dar es Salaam, Tanga, Manyara, Kilimanjaro, Mbeya na Dodoma ambao wamenipa ushirikiano wa kutosha wakati ninafuatilia jambo hili mpaka mchawi amejulikana. Mikoa hii ni miongoni mwa mikoa ambayo Luhwavi alitembelea kufanikisha mkakati wake.

Duuh ameumbuka aisee noma kama ni kweli sijui atakimbilia kule nae au anastay tuned
 
Niliwahi kupinga wapi? Nimesema kwenye uzi huu kuwa nilipoona kelele zinazidi, niliamua kuingia chimbo na haya ndo niliyoyabaini
Mwambie Sirro amwachie Baba Askofu wetu sasa. Maana haya waneno yalisemwa na Baba Askofu mkamsaka eti mchochezi sasa yanaanza kudhihirika kweli yapo. Mbona Sirro anaendelea kumsumbua Baba Askofu? Alichokisema Baba Askofu ndicho ulichokiandika hapa. Tofauti zetu ni Kwamba wewe umetaja jina la engineer, wakati Baba Askofu hakutaja mtu aliye nyuma ya njama hizo. Lakini Kwa ujumla ujumbe wenu una mahudhuhi yale yale.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom