Kinga kwa Rais aliyeko madarakani na wastaafu ni kichocheo cha uvunjaji haki, Iangaliwe upya

Kinga kwa Rais aliyeko madarakani na wastaafu ni kichocheo cha uvunjaji haki, Iangaliwe upya

ni kweli kinga ya rais iondolewe kwani ikiondolewa itaögeza tadirifu na umakini wa kazi kwani ataluwa akijua kuwa akifanya madudu anaweza kustakiwa
 
Waheshimiwa wana Bodi!
Naheshimu sana utaratibu wa Jf jinsi walivyopanga majukwaa yao humu. Ila ukweli ni kuwa jukwaa ambalo linatembelewa na watu wengi, wenye peo mbalimbali, hasi na chanya, hoja nzito na pia dhaifu ni Jukwaa la Siasa anayebisha apinge.

Hoja hii najua inastahili kuweka jukwaa la Sheria lakini mimi nimeiweka humu kwa sababu nilizotaja hapa juu. Naomba Moderator wanisamehe kwa hili na wasiiondoe hoja hii kwani ina maana kubwa sana kwa jamii inayoamka ya Watanzania.

HOJA
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (matoleo yote tangu tupate uhuru mpaka sasa ) sinawakingia kifua viongozi wakuu wa nchi (Marais - Waliopo madarakani na wastaafu) kutoshtakiwa mahakamani.

Hapa majuzi Rais wetu mstaafu Benjamini Mkapa kaenda kutoa ushahidi mahakamani kwenye kesi ya Costa Mahalu inayohusu uhujumu uchumi. Nilipatwa na mshtuko kidogo kwani ukizama ndani zaidi unaona kuwa na Rais alieoko madarakani anakuwa shahidi muhimu kwenye hii kadhia kwani yote yalifanyika akiwa waziri wa mambo ya nje.

Sasa najiuliza na wale mnaojua sheria naomba michango yenu ili baade iwe rejea kwenye kutoa maoni ya katiba mpya na katiba ilitolee ufafanuzi jambo hili.

Endapo mahakama itagundua kuwa Mkapa kasema uongo vipo vifungu vya kumtia hatiani mtu anayeongea uongo mahakamani Je kwa Mkapa au Kikwete itakuwaje ?

Je, Mtu mwenye kinga ya kushtakiwa ana sifa za kumtetea mtu mahakamani

Je, Mtu anaweza kuhukumiwa kutokana na ushahidi wa mtu asiye kuwa na sifa ya kushatakiwa

Naomba kuwasilisha
 
Hapa tusubiri wanaojua Sheria na Katiba ya nchi inasemaje wafike.


MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
Uk 49, kifungu cha 46,kifungu kidogo cha (1). Kinsema.

During the president's tenure of office in accordance with this Constitution it shal be prohobited to institute or continue in court anya criminal prceedings against him whatsover against him.

Mliofikiwa na wakusanya maoni ya katiba, mmelijadili hili?

Naomba kuwasilisha!
 
Uk 49, kifungu cha 46,kifungu kidogo cha (1). Kinsema.

During the president's tenure of office in accordance with this Constitution it shal be prohobited to institute or continue in court anya criminal prceedings against him whatsover against him.

Mliofikiwa na wakusanya maoni ya katiba, mmelijadili hili?

Naomba kuwasilisha!

Umenikumbusha siku ile ya 27/11/12 jioni wakati tunajadili maoni ya katiba mpya pale Msewe-Ubungo, mkazi moja wa umri wa miaka 26 aluipohoji mamlaka, madaraka, na kinga ya rais. Katika kinga ya rais alihoji hivi .." hivi leo rais Kikwete akibaka asishtakiwe kwa kutii kinga ya rais, ni upuuzi" basi ilimlazimu mwenyekiti wa kikao kumtahadharisha kuhusu maneno yake mengi, na kisha kumkatiza asiendelee kutoa maoini.


My take: Kwa kinga hii, hata kama rais atampa mimba mtoto wa darasa la tano hatashtakiwa kamwe. Hii kinga lazima iondolewe
 
Uko nchi gani. Mbona suala hili linaongelewa sana
 
KINGA Sio kwa rais tu hata MABALOZI....... Mbona watu wanahoji sana madaraka na kinga ya rais au kwa vile ni KIKWETE yupo madarakani?
 
Mjuni na Googrich. Nilikuwa nakumbushia tu wadau nalijua hilo vizuri.
 
Watanzania tulitenda dhambi kubwa kwa kuendelea kuiacha sheria inayomlinda rais dhidi ya makosa aliyofanya katika uongozi wake. Yapo makosa makubwa ambayo marais wetu wamekuwa wakifanya mfano kuliingiza taifa kwenye mikataba ya ulaghai, kushiriki wizi wa fedha za uma kwa kuwashinikiza mawazi, kuagizavyombo vya dola kuzuia harakati za kidemokrasia,kufanyika utekaji na mauwaaji ya wanahabari nk.

Sheria hii haina tija kwa Taifa na sheria mfilisi. Ni kupitia kwa Raisi kikwete tumeshuhudia raslimali zetu zinatoroshwa na wahusika kufichwa na ikulu, the list of shame nayo iko kwenye mafaili ikulu,fedha zetu ziko uswis,ikulu imetughib kwa tume,gosh!.... Sheria za namna hii originally zilitumiwa na wakoloni only for protection purposes.

Sheria za namna hii zinamshawishi rais kuiba,kuuwa,kutawala kiimla. Haya ndio yanayotokea sasa.

Hicho ni kichaka cha watawala,ufike wakati rais tumsimamishe kizimbani,tumfilisi na atumikie kifungo kwa makosa yake.
 
ndio mkuu. ila pia tuwe waangalifu. kuna watu wabaya ambao watabanwa na rais akiwa madarakani ambao watataka kumkomesha pindi akitoka ikulu kwa kumfungulia makesi feki ili kumsumbua.
 
tunatokosea sana tunapokuwa na raisi ambaye tunamchukulia kama mungu mtu akiwa madarkan na akitoka madarakan. wabaya wetu wanalijua hili na wanalitumia dhidi yetu.
 
Katiba Mpya inataka Rais apunguziwe madaraka ya kuteua. Sawa lakini mfumo wa watu kuingia holela katika idara hata wasipoweza kufanya kazi (siyo wasizoziweza-tofautisha hapa) ni hatari.

(Mfano mwepesi ni kumpa Mchaga ajira huria namna hiyo, nchi itaingizwa biashara na mwenendo usio na mwelekeo sahihi kama ukabila, wizi wa fedha na hata maangamizi ya makabila mengine. Siyo kuwa mchaga hawezi kazi bali akiipata anafanya mambo mengine yenye madhara kwa raia wengine (sasa hivi nimenunua butter ya karanga kutoka Super Market ya Mchaga amefungua makopo yale na kuongezea madawa ya kupoteza fahamu)).

Kasoro iko katika namna Rais anavyochaguliwa na kinga anazopewa. Rais anachaguliwa na wananchi halafu katika ndoto za ujinga wote wananchi wanashangilia kuwa wana demokrasia ya kuchagua mpaka Rais wao.Lakini Rais huyo huyo akishaingia Ikulu anakuwa kama Mungu-Mtu, wananchi waliomchagua hawawezi kumfukuza na hashauriwi na yeyote katika kazi zake isipokuwa akina-Rweyemamu. Na kama Bunge likijazwa mahela ya kwenda mpaka Dubai kukutanisha wapendanao basi hata ukasirike namna gani kuhusu tabia ya Jakaya Ikulu unapoteza wakati wako. Sana sana ukionyesha wazi chuki zako kwa Jakaya unajipalia makaa utaishia kama Ulimboka au Kibanda.

Mahela yamejaa Uswiss lakini Rais hata aibe na wewe ukapata data zote huna chombo cha kumsikiliza raia wa kawaida kuhusu tabia ya wizi wa Rais. Mahakama yote anateua yeye, na Jaji Kiongozi ni Mstaafu aliyepewa Ruzuku na Rais huyo huyo kurudi kazini.Ukifungua madai Jaji Kiongozi anakubana, jinai huwezi kwa sababu Rais hashitakiwi kwa jinai, na Yeye Rais ndiyo Mwendesha Mashitaka Mkuu wa jinai, ndiyo anamteua DPP.

Hivyo -------- yeyote akishapata kura za wananchi kuwa Rais kaula na hana kikwazo mpaka miaka mitano ipite. Wakati wa kutoa mapendekezo kuhusu Katiba Mpya mimi niliwahi kupendekeza kwenye mtandao wa Tume husika kuwa:

!.Kuwe na utaratibu Rais kufukuzwa na wale waliomchagua. Sheria zote za ajira nchini zinasema hivyo, kila mwajiriwa atafukuzwa na mamlaka iliyomwajiri.

2. Rais asitokane na Chama cha Siasa kwa sababu majukumu yake ni ya Kitaifa siyo ya kisiasa wala kimkoa. Hivyo Rais achaguliwe na ushirika wa nyanja zote zinazounganisha wana siasa wote na asasi zote zinazoweka mskumo katika nchi. Tukishindwa kueleka huko basi Rais achaguliwe na Bunge kama ambavyo anafukuzwa na Bunge.

3. Rais anapokurupuka kwa wiki mbili kwenda kuomba kura kwa watu wasiomjua kuna hatari ya Rais huyo huyo kurudi huko akigawa pesa za walipakodi kwa wakulima wa korosho kama shukrani kwa kumsaidia kuingia Ikulu.

4.Utawala wa ki-Demokrasia ndiyo unaotokana na wananchi moja kwa moja na hapa wananchi ndiyo wanaweza kuonyesha tofauti kati ya ubora wa mawazo yao. Hata ndani ya nyumba tofauti za kimawazo zipo lakini baba huwa hazitakiwi kumfanya mbaguzi. wote ni watoto na huyo ni Mama yao. Na mtoto mmoja akimpenda kaka yake na mama yake na kumchukia HUYO ZURIAT haina noma, nyumba itadumu tu. Hivyo watawala wa kisiasa ndiyo wachaguliwe na wananchi. Na hapa ilitosha kabisa Mmasai kuchagua Mbunge wake Monduli kwa sababu anamjua, siyo mkazi wa Mpanda kumchagua mtu wa Kilosa aliyepita siku moja tu akijinadi kwake, ni urongo huo. Waziri Mkuu akitokana na Chama Chenye Majority Bungeni ndiyo utaratibu unaotumika na kwingine. Waziri Mkuu wa namna hiyo atakuwa makini kuhakikisha Chama chake hakiingii migogoro ya uchumi na raia kwa ujumla kwa sababu chama kitapoteza umaarufu.

5. Raia wamshitaki Rais mahakamani na Mahakama iwe na uwezo wa kumpa mdai hukumu dhidi ya Rais, halafu hukumu hiyo apewe Spika wa Bunge kwa ajili ya kuona hukumu inatekelezwa kwa kiwango cha hata kumwondoa Rais madarakani. Hapo Rais atawaheshimu hata raia wa nchi yake.

Mkiendelea na utaratibu wenu wa sasa itakuwa Rais anateua Mawaziri halafu wahuni na mafisadi waliomweka Rais madarakani wanaharibu na waziri husika anajiuzulu halafu Rais anateua Mawaziri wengine. Huo ndiyo huitwa mzunguko wa umaskini.
 
umechelewa kumpelekea warioba

Nilimpelekea Warioba wakafunga page! Nikalazimika kupitia personal page ya Jakata nayo wakaikorofisha lakini nikatumia duru ngumu nikapeleka lakini ndiyo hao wanapeta!
 
JAJI mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania,Raymond Mwaikasu, amewataka wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kuondoa kinga inayomlinda rais wakati anapostaafu ili aweze kufikishwa mahakamani pindi inapobainika amevunja katiba wakati wa utawala wake.

Jaji Mwaikasu alitoa wito huo jijini Dar es Salaam jana alipozungumza na viongozi wa dini walipokutana kujadili mwenendo wa Bunge Maalumu la Katiba linaloendelea mjini Dodoma.

Alisema kuondolewa kwa kinga hiyo kutasaidia kudhibiti baadhi ya watu wanaotarajia kuingia madarakani kwa ajili ya kujinufaisha binafsi badala ya kulinda katiba.

Chanzo: Tanzania Daima la 27/3/2014
 
Back
Top Bottom