Kinga kwa Rais aliyeko madarakani na wastaafu ni kichocheo cha uvunjaji haki, Iangaliwe upya

ni kweli kabisa,hapo bado maraisi wanaoishi kama ndezi katikati ya mbwa mwitu baada ya kuachishwa madaraka,akina Yahaya Jameh wanaficha magari hadi porini,akina Mugabe umaarufu umetoweka ghafla baada ya kuondolewa madarakani kabila kila leo anakaliwa kooni nk,bado hapa kwetu wanahofia nini kitatokea siku katiba ikibadilika,matokeo wanatumia nguvu kubwa kuvuruga mchakato wa katiba mpya,siku zinabadilika sana,sura ya ulimwengu inabadilika sana kadri siku zinavyokwenda
 
Hata viongozi wa upinzani waliopiga bilioni za mafisadi wanafaa kushtakiwa
Nakubaliana nawe 100/%
Vita vya UFISADI ukiangalia VYAMA na HURUMA hutaviweza.
Wote hoa kikaango ni kimoja tu MAFISADI lazima waadhibiwe.
 
Sikatai mina maono. Na maono yangu kama Mtanzania ni kuona nchi ILIYOSTAWI.
UMMASKINI tuuzamishe baharini kabisa kabisaaaaa.
Maendeleo ya vitu huku umasikini wa watu unaongezeka?

Maendeleo ya vitu huku ajira hakuna na watu wanapunguzwa makazini?

Maendeleo ya vitu huku watu wanamaliza vyuo na hawana pa kwenda?

Maendeleo ya vitu huku watumishi wa umma wamesahalika?

Maendeleo ya vitu huku mazao ya wakulima yanakosa masoko?

Maendeleo ya vitu huku uchumi unalalamikiwa?

Maendeleo ya vitu huku watu kila siku wanatekwa au kupotezwa?

Maendeleo ya vitu huku chaguzi zinavurugwa?

Lazima tu-balance haya mambo vinginevyo tunatengeneza bomu litakalokuja kutulipukia.
 
Ndo hapo sasa. Tunahitajika kutoa MAONI,USHAURI nini KIZURI ili kuepusha timing bomb la kuwa na watu amabao HAWANA AJIRA na wala HAWATAKI KUJIAJIRI.
Naamini masomo ya UFUNDO POLYTECHNICS yakisamabazwa.
Wengi WATAJIAJIRI. Badalaya ajira ya OFISINI.
 
Vipi tukianza na hawa tena na shahidi mnaye
 

Attachments

  • FB_IMG_1474786887887.jpg
    35.2 KB · Views: 37
  • FB_IMG_1484944703142.jpg
    23.7 KB · Views: 37
  • FB_IMG_1492698982281-1.jpg
    6.2 KB · Views: 33
Hata viongozi wa upinzani waliopiga bilioni za mafisadi wanafaa kushtakiwa
akili ndogo hiii. hapa tunaongelea rais kushtakiwa sio maana anakinga ya rais hao ulio wataja wewe hata leo waweza kwenda kuwashtaki hawana kinga popote kana una ushahidi nenda acha uzwazwa.
 
Itapendeza sana siku nikiona Bush wa pili, aliekua rais wa America, ndio ntaelewa the world is fairly
 
Nakuelewa. Sidhani kama wanaogopa katiba mpya ila nafikiri vipengele ndani ya katiba vikirekebishwa hamna mtu asiyetaka katiba yenye maendeleo si katiba ya miaka ya UJAMAA.
 
Mkuu hapo umekosea. Heshima si utumwa. Ni vizuri tuiheshimu taasisi ya URAISI hata kama hukubalini naye.
Ni MTANZANIA mwenzetu na wala si hivyo usemavyo.
Tujadili hoja badala ya matusi na kubezana. Ama vipi mkuu?
Correct!, hawa jamaa ni ngumu kuwajua, ni popo au ndege? ,nisamehe Kutumia lugha hiyo.
 
kuna mambo ambayo yako nje ya uwezo wetu kuamua. Yako ndani ya uwezo wa Muda.
huo wakati utafika, Kuna umuhimu wa viongozi kuchagua kuwa waadilifu leo kwa faida ya baadae.
wakati huo utafika siku rasilimali tunazojivunia zitakapopungua au kuisha na hakuna manufaa kwa wananchi.
 
Tanzania hatuna shida sana na Viongozi wetu wastafu kama hizo nchi. Naomba wimbi la kushitaki viongozi waliobariki/walioua raia wasio na hatia kule Iraq, Cossovo, Libya, Palestine, Nagasaki, Syria, Yemen, Soweto, Vietinam n.k wapelekwe The Hague
Hapa Wanapita tu, na ndio uhalisia wenyewe
 
Sidhani kama walikuwa wakiongoza Tz kweli ama labda walikuwa na nchi zao binafsi ...Ni vigumu kumlingsnisha JPM wa miaka 2.5 na wale wa 20 kwa pamoja
Umesema yote kwa UKWELI KABISA
 
Hata hivyo. Siku ipo watajibu.Kama Zuma anashitakiwa kwa manunuzi ya sulaha ya miaka ya 90?
Tunaweza.Nia ipo naamini kabisa.
 
Ulianza vyema but ulivyoanza kusifiaaa umepotezaaa radha
 
Ni kweli kabisa, unakuta askofu ana 8 bil kwenye ndoo chumbani hii ni hatari!
 
Mm naona ulianza vzr mwanzoni..ila ulipoanza tu kuiporomoshea misifa serikali ya awamu hii nikashangaa na kukuona mchumia tumbo!..hii serikali ndo itakuwa ya kwanza kustakiwa kutokana na vitendo vyake vya kibabe na maamuzi ya kukurupuka!Ufisadi mkubwa unaendelea kichinichini..kujenga uwanja Chato...kununua ndege zisizo na faida!..kashfa ya kutengeneza passport mpya!..haya yote ni uamuzi wa kukrupuka wa mtu moja!..mauaji na utekaji..haya yote yatafukuliwa awamu zijazo..Hakuna kupona hivi sasa wanachimba makaburi yao ili waje wazikwe...hili lipo wazi ..apende asipende..pingu na msoto wa jela unamsubiri kama anavyotesa wengine..yeye atauonja moto mkali zaidi na vibaraka wake!
 
Inatia moyo.
Ila kwa nchi za ukanda wa Africa Mashariki ni Muujiza na ndoto.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…