mkerewe halisi
JF-Expert Member
- Apr 11, 2015
- 299
- 152
Kingunge anasahau kamati iliyomchinja lowassa ndio iliyomchinja malecela akiwa makamu mwenyekiti wa chama taifa na yeye kingunge hakupaza sauti kumlilia!
Kinachoonekana sasa ni mbinu mbadala ya kundi LA mafisadi wanaomzunguka lowasa kutaka wasisahaulike kwenye utawala mpya
Pia kasahau kutuambia yeye na mwalimu walitumia busara gani kumfunika lowassa!
Kinachonifurahisha Mimi ni kuona wale walioitwa mafisadi na wale wasio mafisadi yaani kwa lugha nyepesi unaweza kusema Nuru na Giza wakiungana pamoja kupata ccm moja-hii imekaaje ndugu du!!!!!!!!!!!!!!!Sometyms the end justify the means. Kwa kukiuka hizo taratibu tumeweza kumpata mgombea asie na makundi wala si fisadi kama maamvi. Hata kama mapungufu si kama ya edo au membe. I pray to God awe na speed ile ile na in three years nchi itapata mwelekeo.
Katikati ya Maneno ya huyu Mzee Edo hatoki CCM anachotaka Tingatinga akapige magoti ili kuonyesha nguvu yake na yeye ahakikishiwe maslahi yake hizi ni siasa chafu
Kama Kingunge asingekua na mgombea angeheshimika sana lakini kwa sasa atadharaulika sana hakuna atakaye msikiliza, huyu ni mnafiki.
Yeye alihusika sana kuweka utaratibu mbovu wa kuingia CCM alishauri kwa JK enzi hizo kwamba ili kua Mwanachama lazima mtu asome miezi 3 yeye na JK walikua miungu mtu tena alikua mnoko sana kuwasema vibaya wenzake kwa JK. Enzi zimebadilika Ubungo haitarudi tena mikononi mwake atulie wakati umepita, alisaidia sana kujenga makundi ndani ya CCM kwa maslahi binafsi.
Kamati ndogo ya maadili ile ya watu 5 ndiyo inafanya kazi ya kushauri lakini kamati ya Usalama na maadili inaruhusiwa kupunguza kwa sababu inaongozwa na Mwenyekiti wa Chama, kwa hiyo hakuna uhalali wa kusema hayo, lugha nzuri ya kumwambia huyu Mzee ni kwamba aache kuropoka muda wake umekwisha.
Kabisa mkuu.huyu mzee anajidhalilisha tu,eti utaratibu umrkiukwa yani kamati ya maadili ipeleke jina kwenye vikao vya uamuzi ambavyo vimeshajaa wachumia tumbo?nani hajui watu wanalipwa kwa kumfanyia kazi lowasa?dharau za kutisha chama atwambie kingunge zimeanza lini?wapi kwenye katiba yao pameandikwa MTU kwanza chama baadae?ukiwa na mzee wa namna hii huwezi kwenda kuomba ushauri.
hahahaa et ukiwa na mzee kama huyu huwez kuomba ushauri..hahahaaa
kwa kifupi sana
wakati wa kikao cha maadili kujadili report za watia nia kusomwa membe na lowasa wote walikatwa majina ...report zao zilikuwa mbaya sana..tena mbaya mno...ila ya lowasa ilikuwa mbaya zaidi kuliko.....mtu aliyeongoza kwa kuw ana alama za juu kwenye maadili ni Makongoro,magufuli, makamba, migiro na huyo amina... kamati ikaazimia kuchuku majina hayo kwa sababu walizozijua wao...baada ya mda mweneyekiti akaonekana kutoridhika na hiyo tano bora..akamwita mstaafu wa awamu ya tatu na ya pili na pia kina malecela...akalamimika kuwa tano bora yote imejaa watu ambao wao wazee wastaafu waliwataka..yeye kama mwenyekiti hana mtu...iweje tano bora awe na mtu mmoja tena mwanamke..mvutano kidogo ukatokea...mwenyekiti akapewa uhuru wa kuamua anachotaka...ndipo akasema namuondoa mmoja na kuweka mwingine...akaliondoa jina la Makongoro na kuweka la membe..wazee wastaafu wakashangaa sana ...ili amani ya yerusalemu iendelee kudumu wakakubaliana na mawazo ya mwenyekiti japo kwa shingo upande...
wakarudi chumba cha mkutano wakawaeleza wajumbe wa maadili juu ya mabadiliko hayo ...minong'ono ikatokea mle ndani..gafla mwenyekiti akafunga kikao.... na kutoka na hiyo tano bora iliyochachuliwa kwa kuondolewa makongoro na kumwingiza membe...hii ni kwa kifupi sana hivyo ndivyo ilivyokuwa...badae huko mbele nikipata mda ntaeleza kwa nini lowasa alikatwa tena kwa kutumia ''collecting ink''...
Kwisha habari yao hamna jipya tena, mbona wengine wameridhika na matokeo, yeye ni nani katika nchi hii, mgombea amepatikani basi tuendelee na mambo mengine
Watu wanam-puuza/dharau/kejeli Kingunge kwa sababu ya kuegemea kwake kwa Lowassa! Ila katikati ya mstari anafikisha ujumbe kuwa ccm hawako wamoja kama wanavyodhani! Kuna wale waliokuwa na matarajio makubwa na pengine walishaahidiwa kwa namna fulani, lakini wakakatwa na "Kitengo" katika hatua za mwanzo kabisa bila hata kupewa haki ya kusikiliwa! Hawa hawajasema chochote hadharani, na pengine hawana guts za kusema, ila ndani wana maumivu na hakuna mwenye kujua gizani watafanya nini kulipiza kisasi! CCM wasijidanganye, panapofuka moshi...............!
Huyu mzee anajisahau!Mzee anatapatapa, asome alama za nyakati, wenzie hiyo chapter imeshafungwa ndio maana Sophia Simba alishiriki mapokezi ya John Magufuli.