kilimbamula
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 1,792
- 853
Sasa aone utamu wa kuvuruga taratibu na mchakato.
Kingunge ulishiriki kuvuruga mchakato wa katiba pendekezwa... Sasa usilalamike, muosha uoshwa.
Hivi alikatwa mtu mmoja tu au zaidi ya watu 30??????
Hivi alikatwa mtu mmoja tu au zaidi ya watu 30??????
Ni kweli...alichofanyiwa EL si sahihi ila hiki kitendo huitwa "Necessary Evil"....ilikuwa haiepukiki kwa maslahi mapana ya taifa...full stop
Ukichoka hata TUNGULI zinachoka.amechokA KWELI MZEE WETU AMECHOKA MWILI NA akili
Why only Lowasa mbona wagombea wengine 33 hawasemei?
Mzee kingunge ameongeza kuwa Lowassa yupo tayari kushirikiana na Chama kusaidia Chama kupata ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi mkuu, lakini yaliyotokea lazima yazungumzwe kwa uwazi ndani ya vikao vya Chama ili watu watoe madukufuku yao.
Kingunge anadai Mkutano Mkuu umetamka Mgombea ni Magufuli, lakini ili kupata ushindi - chama kitahitaji nguvu na ushirikiano wa ndugu Lowassa na kuongeza kuwa anaamini Ndugu Magufuli atafurahia suala hilo na ataandaa mazingira mazuri ya kuipata sapoti hiyo.
Anadai Kabla ya Uchaguzi inabidi CCM kufanya mazungumzo ili wakubaliane na kukosoana lakini mwisho wa siku watoke tukiwa wamoja ili kupambana na adui.
Bro wewe kama mtanzania mwema uliwahi kutoa taarifa hii kwenye chombo chochote chenye mamlaka ya kushughulikia maovu haya au umechukizwa tu na taarifa ya mzee kingunge?
Ukifanya mambo ya hovyo utasulubiwa tu, mbona Zitto alisulubiwa ilihali ni kipenzi cha wengi? na sasa katulia tu? Kingunge kapauka kisiasaKingunge ameamua kusema Ukweli na ukweli pekee ndio unaweza kuwaweka huru wanaCCM. Japokuwa simuungi Mkono Lowassa lakini hakutendewa haki kabisa.
Kama kweli Lowassa na wenzake wenye nguvu na ushawishi ndani ya CCM waliokuwa wanagombea walikuwa hawafai, ilikuwa ni busara sana kuwapa nafasi wajumbe wa Kamati kuu, Halmashauri Kuu au Mkutano Mkuu kuamua hilo na sio kuwakata majina yao kwenye kamati ya Maadili kinyume kabisa na kanuni, taratibu na Katiba ya CCM.
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.