Kinondoni, Dar: Hamza Mohammed, Polisi Watatu na mlinzi mmoja wauawa katika Majibizano ya Risasi

Kikubwa wamemuuwa ndiyo ila mtuhumiwa kama yule kumuuwa bila kutengeneza mazingira ya kumuhoji may be wapo watu nyuma yake ukapata pakuanzia police wamefamba.

Hatukatai chuma ni hatari ila kama taifa tuna snipers ilifaa watumie uzoefu wao kumletea majeruhi ili wamkamate hai asaidie upelelezi.
 
Sinema ya kumfunga mbowe hii kigogo akiwa Master plans
 

Mimi nikiwaza Askari Watatu na Mlinzi mmoja wa SGA wapo Mochwali inauma sana. Sasa sijajua, yule askari aliyepigwa pale nje ya Ubalozi wa Ufaransa, akijaribu kumuua huyo Mhalifu kwenye Kibanda sijui kapona? Maaana alipigwa Risasi na Hilo lijamaa.
 
Kulingana na hyo clip huyo kijana alikuwaga na akili ka zimeruka jeuri na msumbufu ndio akapelekwa Egypt kusoma dini na aliporudi Tanzania akawa anataja mambo ya jihadi
Itupie basi tuione
 
Jambo moja na la ajabu sana ni hili.
[emoji1484]
-Yule jamaa katoka wapi na siraha zile pasi kushukuliwa?.
-Kuna kitu kimejificha kutokana na tukio hilo?.
-Ametumwa kupima ulinzi wetu ukoje?.
-Kwa nini bakuwa na habari na raia waliokuwa jirani?.
-
Na tushukuru Mungu hakuhangaika na ile daladala iliyokuwa mbele yake alipokuwa anajipiga piga kifua tungekuwa saizi tunaongea mengine hapa.
 
Walikuwa wanawasema vibaya alishabaab, vita yao na wakenya lakini mmatumbi kutoka tandale na mitaa fulani anaingilia ishu yao,,,haya sasa kumekucha mammae,,,na walivyo waoga [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] Mungu atunusuru kwaakweli.
Kabisa mkuu tuombe MUNGU atunusuru.
 
Kuna askari mmoja ameenda kifara fara pale kwenye banda na kibastola chake halafu akawa anatoa ishara kwa wenzake huku kageukia huko huko kwa wenzake badala amwangalie adui..acha ale shaba ya mguu; akaanza kuruka ruka!!!!
 
Alikuwa na maamuzi ya kweli ktk maangamizi na kasomea Misri mambo ya Dini
 
Kuna askari mmoja ameenda kifara fara pale kwenye banda na kibastola chake halafu akawa anatoa ishara kwa wenzake huku kageukia huko huko kwa wenzake badala amwangalie adui..acha ale shaba ya mguu; akaanza kuruka ruka!!!!
Pale hata mimi nilishangaa amemuachia adui mgongo je angepigwa ya kisogo
 
Siyo alshababu?
 
Umewaza mbali, kudos sana,kumbe kungekuwa na utaratibu wa kumpiga na risasi ya usingizi,mda ana zinduka angetoa siri nyingi kama mfano Alshabab wamemtuma au vinginevyo.
Huwa nafuatilia sana zile police chase kwenye majiji ya Marekani,jinsi police wao wanavyofukuzia majambazi na kuwakamata wakiwa hai,gari zisizopungua tano zinafukuza gari moja ya jambazi,hewani kunakuwa na helcopter mbili moja inaenda kwa chini kidogo ikisaidia kufukuza nyingine inakuwa juu sana ikiwa inawawezesha polisi waliopanda kuona sehemu kubwa ya barabara za jiji husika,wakikaribia gari la mhalifu Wanajaribu kushoot matairi,lakini hatimaye huwa wanahakikisha wemkamata akiwa hai ilo atoe Siri za operation zake.
 
Itakie mema nchi yako,hakuna furaha katikati ya umwagaji damu.
Mkuu nasikitika sana kwa haya yanayotokea tena sana tu.Mimi ni Mkristo ninaye amini ktk kuishi kwa Amani na Upendo,lkn Dhuluma inafanya watu watafute haki kwa njia nyingine.Ndio maana Ktk Biblia kuna sehemu imeandikwa hivi "Haki huinua Taifa". Hivyo viongozi wetu wajitafakari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…