Kiongozi aliyehujumu na kuua kiwanda cha TIPER ni wa ovyo kuwahi kutokea Tanzania

Kila Kitu hapa Ni Dili tuuu yaani mpaka laana hii itutoke sijui lini
 
Zambia wanakula raha tu
 
Swadakta !! Umefanya vizuri kuwafahamisha Hao vijana wasiojua nini mwalimu Nyerere alichokifanya katika nchi hii wao siku zote ni kubeza utawala wa Nyerere eti hakujua kutengeneza Uchumi !!
 
sisi wananchi ndo wa hovyo kupitiliza, chumvi tu packet moja tunachagua mtu wa hovyo
 
Utasikia.. watanzania wanahitaj elimu, maji, umeme na huduma za afya 😂😂😂 That's they songs always 🤣🤣🤣🤣
Fikiria tu tumeshindwa kuzalisha mafuta ya alizeti, vijiti vya kuchokonolea meno, ngano, nguzo za umeme nk wakati ardhi ya kutoa raw materials ipo kubwa tu, nani anayehujumu uzalishaji wa malighafi nchiniu
 
nakumbuka kipindi cha mkapa tulikua tunanunua petrol lita sh 500 yalikua yakichakatwa hapo kigamboni
 
unasema ilikua smallest refinery lakini ilikua inatutosheleza kwa mahitaji ya ndani mafuta yalikua sh 500 kwa lita
 
uko sahihi kabisa kuna mzee mmoja alikua anafanyakazi mule ndani alinisimulia alisikitika sana kuwa sasa tiper watakua wanafanya storage tu
 
Ni wakati muafaka kwa serikali kufikiria kufufua kiwanda hiki au kutafuta wawekezaji kujenga kiwanda kipya cha kusafisha mafuta.
Kwa serikali ipi..hii ya sa100 ya wapiga dili...tegemea maumivu hao jamaa na genge lao la wezi wanawawza upigaji tu.

#MaendeleoHayanaChama
 
Wacha porojo mzee wetu, kile kiwanda hakikfungwa kwa sababu kilikuwa hakitoshelezi, bali kilifungwa kwa msukumo wa IMF. Kiwanda kilipojengwa mwaka 1965 kilikuwa kinatosheleza kabisa mahitaji ya nchi ambayo wakati huo ilikuwa na watu kama milioni 14 tu, ila kadri siku zilivyoenda, idadi ya watanzania iliongezeka na mahitaji ya mafuta pia yaliongezeka ndipo TPDC ikaanza kuwa inaagiza mafuta nje. Kilipojengwa mwaka 1963 haikuwa na maana kitakuwa hivyo hivyo bali ilitegemewa kuwa kitakuwa kinapanuliwa kadri mahitaji yanapoongezeka, ila waswahili tukakikalia kama ndiyo kimefikia mwisho, na kuanza kulalamika kuwa hakitoshlezi badala ya kufikiria namna ya kukipanua. Basi wajanja wakatuambia tuuze, nasi tukaingia kichwa kichwa tu kwa vile tulikuwa wavivu wa kufikiri.

Tungejua kuwa tunahitaji kupanua viwanda vyetu kadri mahitaji yanavyoongeza tusingekiuza. Hata Uwanja wa ndege wa DAR tulianza na terminal 1 tu, kufikia katikati ya miaka ya sabini ikawa haioteshelezi tukajenga terminal 2, na hivi majuzi tumeongezea tena terminal 3 ili kukua kuendana na mahitaji. Siyo kwamba kwa vile terminal 1 haitoshelezi basi tuuze tusiwe na uwanja tena.
 
lakini tiper ingekuwepo ingesaidia kupunguza gap japo kwa icho kidogo wanachozalisha na tungekua na mafuta ya kutosha tofauti na huu uhuni unaofanyika sasa
 

Thanks kwa historia
 
Hivi kufufua ATCL na kununua mandege tena kama wanavyo sema wananunua cash na kujenge REFINERY ya uwezo mkubwa hapo lipi LINGEKUWA jambo bora na lenye TIJA KUBWA kwa TAIFA?
 
NYERERE alijenga Viwanda vya Kutosha Wakaja Wanyang'anyi Wakavipora Vyote Leo Kiwanda cha Tanganyika Packers Pamekuwa KANISA
Leo Kiwanda cha URAFIKI wachina Wanauza MAUA

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app

Nyerere hakujenga viwanda bali alidhulumu wakoloni, wazawa na Wa Asia viwanda vyao
Tanganyika packers haikujengwa na wa Tz
Urafiki ilijengwa na China [emoji630]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…