Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
hiyo statement ndio ushahidi wako? Je nikisema kuwa CHADEMA baada ya kusikia maneno ya PM wametumia vijana wao kufanya hili tukio. Mtu anaweza kujipachika jina lelote na cheo chochote.Umesikia kauli ya Pinda liwalo na liwe? umejaribu kuifafanua ili kuelewa kwa kina?
Taarifa iliyonifikia hivi punde ni kuwa jemedari Dr. Ulimboka ametekwa majira ya saa sita usiku na watu watatu waliokuwa na silaha za moto na kumpeleka kusikojulikana! Inasemekana alipigiwa simu na jamaa mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja la 'Abeid' ambaye tangu mwanzo amekuwa akiwasiliana naye na kujiita afisa wa serikali na kudai kuwa alitaka aonane naye face to face kwa ajili ya reconciliation.
Wadau,
Habari ndiyo hiyo.
"Jamani this is iserious nimepigiwa simu sasa hivi na watu wa legal and human rights center wameniambia wametoka kumchukua Dr Ulimboka kule Mabwepande amepigwa vibaya sana na ni emergency wanampeleka MOI sasa hivi please tunaomba mtume habari hii kila mahali please!
Ni habari ya uhakika sana nimeomngea na Patience Mlowe wa Legal and Human Rights center"".
By Dr. Riwa
Haya waliokuwa wakisema udikteta wa kutisha watu kwenye utawala huu hakuna hii ni nini sasa, Wanataka kutufikishawapi hawa watu
Naunga mkono hoja...wana JF, je inawezekana kuanzisha michango hapa kwa ajili ya matibabu ya huyu dr Ulimboka na ikiwezaka nje ya nchi. kama masanja aliweza kufanikisha michango kwa ajili ya Sajuki, kwa nini JF yenye wanachama zaidi ya 80,000 washindwe?
Kila member wa JF achangie kiasi kidogo cha 1000/ tu. Nani anaweza kuratibu hii kitu?????????????//
Naamini njia zao zingine ziligonga mwamba na wameamua kubadilisha tu njia za ubabe, wameona sumu inadunda wameanza kuwadunda sasa. Ila kwa nini Dr. Ulimbooka alikubali kutoka usiku ule wote na alikuwa anajiamini nini? Kwa kweli naye hakufikiria vyema, Japo si mda wake sasa kulaumu ila watu wengine wajifunze wasije kukubali kukutana na mtu yeyote usiku hata kama iweje. Kwa sasa ngoja tuone madaktari watachukua hatua gani kulingana na hili tukio la kusikitisha sana
Huyu nae naanza kumuona ni mpumbavu tu, je yeye anauhakika gani kama ndio serikali imehusika, hizi statement mchwara ndio zina kuja kuwaponza hawa wanasiasa mchwara.[TABLE="width: 100%"]
[TR]
[TD]Serikali inawajibika kutueleza: Dkt. Ulimboka kutekwa, kupigwa na kuumizwa - Zitto Kabwe
27/06/2012
1 Comment
Ujumbe amenitumia Daktari yupo pale MOI
‘Kaka Zitto,hali ya Dr.Ulimboka yuko unconscious,multiple ribs fracture na kwenye mikono pia amevunjika pamoja na taya,yuko icu wanamstabilise kwanza kwasababu hapumui vizuri,the situation here is really bad, I agree with you this is outright outrageous'
Nimechukizwa sana na habari za kutekwa, kupigwa na kuumizwa vibaya kwa Dr Ulimboka, Kiongozi wa Madaktari Nchini. Mambo kama haya tumezoea kuyasikia kwenye nchi za kidikteta na kuongozwa kiimla ambapo watawala badala ya kutumia njia ya kidemokrasia na kisheria kushughulikia wanaoamini ni maadui zao katika utawala, hutumia wahuni katika Taasisi za usalama kuteka raia, kuwatesa, kuwafunga na hata kuwaua.
Sitaki kuamini kwamba Tanzania imefikia huko. Nimezungumza na baadhi ya madaktari walio karibu na Dokta Ulimboka na kujulishwa kwamba majeruhi huyu wa vitendo vya hovyo kabisa kutokea hapa nchini alikamatwa jana usiku mnamo saa sita na watu wasiojulikana na kupelekwa katika msitu wa MagwePande na kujeruhiwa vibaya. Habari hizi bado hazijathibitishwa na vyanzo huru lakini ndio zilizopo hadi hivi sasa.
Serikali kama mlinzi wa usalama kwa raia inaWAJIBU kueleza tena kwa haraka ni nini kimetokea kwa kijana huyu msomi na kiongozi wa wataalamu wenzake. Serikali INAWAJIBIKA kueleza katika nyakati kama hizi ambapo kuna mgogoro kati yake na madaktari imekuwa wapi kuhakikisha usalama wa viongozi wa madaktari ili kuepusha watu wanaoitwa 'agente provocateure' kuweza kuhatarisha hali ya amani ya nchi na hata kupelekea kuweka hali ya vitisho kwa madaktari wetu.
Serikali INAWAJIBIKA kueleza kama sasa imeamua kutumia njia za kihuni kumaliza matatizo na wananchi wake.
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Source: wavuti - wavuti
Habari zinazoletwa na magwanda humu ndani huwa za kutatanisha, mara "atekwa", mara yuko "polisi", mara kaokotwa "mabwepande" yuko taabani.
Hivi huwa hamjui kusema kweli?
Isitoshe, kama kweli hili la mwisho la kuwa kala kichapo mpaka kawa taabani limefanyika, basi hapo itakuwa kuna watu wenye uchungu wameupokea ushauri wangu nilioutoa jana humuhumu JF, huu hapa:
hiyo statement ndio ushahidi wako? Je nikisema kuwa CHADEMA baada ya kusikia maneno ya PM wametumia vijana wao kufanya hili tukio. Mtu anaweza kujipachika jina lelote na cheo chochote.
Angekamatwa ingejulikana ni kwa sababu zipi na amepelekwa wapi, unasema amekamatwa kwa mahojiano zaidi,unajua amekamatwa na nani na anahojiwa kuhusiana na nini?
Kama ni kweli hii habari basi lazima nitamke wazi kwamba serikali haiwezi kufanya jambo la kipuuzi kama hilo wakati madhara ya upuuzi kama huo yapo wazi. Kwa vyovyote vile, hiyo inaweza kuwa ni ama hujuma dhidi ya serikali, au hujuma dhidi ya kiongozi wa nchi au mchezo wa kitoto uliofanywa na madaktari wenyewe, au wabaya wa Ulimboka mwenyewe.
MCHEZO WA KITOTO WA MADAKTARI:
Kikundi kidogo cha madaktari wenyewe wanaweza ku-engineer mpango wa kipuuzi kama huo ili kutafuta huruma ya wananchi. Michezo ya kitoto kama hii inafanywa sana na huwa inaaminiwa na wale wasio na uwezo wa kuchanganua mambo.
HUJUMA DHIDI YA SERIKALI:
Watu wenye maslahi tofauti dhidi ya serikali wanaweza kufanya upuuzi kama huo ili kujenga picha kwamba serikali iliyopo ni ya kidhalimu inayoweza kufanya lolote dhidi ya raia wake wanaotetea maslahi yao. Watu wanaoweza kufanya haya ni wale wenye maslahi ya kisiasa...ni Political Sabotage.
HUJUMA DHIDI YA RAIS:
Ulingo wa siasa ni ulingo uliojaa uadui baina ya mtu na mtu. Katika hilo, mtu au kikundi cha watu wanaweza kufanya upuuzi kama huo ili kumuumbua kiongozi mkuu wa nchi.
MAADUI BINAFSI WA Dr. ULIMBOKA MWENYEWE: Hawa wanaweza kutumia opportunity ya Dr. Ulimboka kuwa ndani ya mgogoro ili ionekane kwamba waliomdhuru ni watu wa serikalini.
MOJA kati ya hizo inaweza kuwa ndio sababu sahihi lakini there's no way kwamba serikali inaweza kufanya utoto kama huo. Ki