TANZIA Kipa wa zamani wa Simba, Yanga na Songea auawa kwa kuchomwa moto na Wananchi wenye hasira kali

TANZIA Kipa wa zamani wa Simba, Yanga na Songea auawa kwa kuchomwa moto na Wananchi wenye hasira kali

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Golikipa wa zamani wa timu za Majimaji ya Songea, Simba Sc na Yanga Sc, Doyi Moke raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo amefariki Dunia baada ya kuchomwa moto na Wananchi wenye hasira kali

Screenshot 2025-03-07 094430.png
Inaelezwa asubuhi ya Machi 6, 2025 Doyi ambaye alikuwa tayari amepatwa na matatizo ya akili na amekuwa akitembea barabarani kama ‘chizi’ alitoka kwake akielekea nyumbani kwa mwanaye ambapo mahali alipoenda huko Bukavu kuna wafungwa ambao walitoka gerezani na walishakuwa na tabia ya kuwaingilia watu ndani na kuwaibia vitu.

Kwa hiyo Wananchi waliamua kujichukulia Sheria mkononi kutokana na kitendo cha wafungwa hao kufanya vitendo hivyo ambapo inaelezwa kuwa Wananchi walikutana na Doyi ambaye alikuwa anatoka kwa mwanaye na kumjumuisha miongoni mwa wahalifu hao.

Wananchi hao walimfunga minyororo sambamba na watu wengine watatu na kumchoma moto kama inavyoonekana pichani.
 
Ni dhambi kuuwa, isipokuwa kwa haqqi. Waislamu jijini dar, najua huko ndiko Waislamu wengi kuliko wasio na dini, basi jiepusheni na bendera fuata upepo ukiona mtu anauliwa au kuchomwa moto basi msishiriki dhambi hiyo, hawa wenzetu hawajui ya dhambi, wao kuuwa wanaona kama ni uanaume. In short wafanyao ni watu wasio na imani wala huruma ni makatili sana sana.

Allah atujaalie mwisho mwema
 
Maisha ya kisenge sana.

Ndiyo sababu naishi reckless in terms of dini
Mandojo naye alikufa hivyo hivyo ,kuna mzee mtaani aliykuwa baba wa rafiki yangu aliuawa hivyo hivyo.

Kuna jamaa kipind cha nyuma alikuwa chizi anaitwa Ally upolichi hapa Tanga ni maarufu ,alikuja kuuliwa mtaa wa pili wakidhani ni mwizi
..Tena vifo vyao vibaya sana.

Kiufupi maisha yanafikirisha sana ni pata potea.
 
RIP nyanda ya [emoji460].
[emoji22][emoji22]
 
Wakati watani wa jadi wa soka la Bongo, Simba na Yanga, wakitarajiwa kushuka dimbani katika dabi inayonadiwa kwa kaulimbiu ya HAINA KIPENGELE, kuna taarifa mbaya na ya huzuni kwa nyota wa zamani wa timu hizo mbili. Huyu ni Mabruki Doyi Moke, kipa wa zamani wa Simba na Yanga aliyeishi kwenye mitaa ya Kariakoo kuanzia 1999 hadi 2003.

Moke, raia wa DRC kutoka Bukavu ameripotiwa kuuawa asubuhi ya Machi 6, mwaka huu huko kwao Bukavu.
Sababu za kifo chake zinatajwa ni kuchomwa moto na wananchi waliojichukulia sheria mkokoni wakidhani ni mhalifu. Katika siku za hivi karibuni matukio ya wananchi kujichukulia sheria mkononi huko Bukavu nchini DRC yamekuwa mengi sana.

Sababu kubwa inatajwa kuwa ni kupambana na wimbi la uhalifu kufuatia wafungwa wote kutolewa jela na waasi wa M23 baada ya kuliteka eneo hilo.

Wafungwa hao sasa wamegeuka kuwa wahalifu mitaani na wananchi hawana namna zaidi ya kuwakamata na kuwachoma moto.

Kwa hiyo wananchi walimkamata Doyi Moke kimakosa wakidhani mhalifu na kumchoma moto. Hii ni habari ya kuhunisha sana.
1741334514098.png


CHANZO: MwanaSpoti
 
Mandojo naye alikufa hivyo hivyo ,kuna mzee mtaani aliykuwa baba wa rafiki yangu aliuawa hivyo hivyo.

Kuna jamaa kipind cha nyuma alikuwa chizi anaitwa Ally upolichi hapa Tanga ni maarufu ,alikuja kuuliwa mtaa wa pili wakidhani ni mwizi
..Tena vifo vyao vibaya sana.

Kiufupi maisha yanafikirisha sana ni pata potea.
Hata bondia Thomas mashari
 
Back
Top Bottom