Kipengele cha kuwabeba Polisi wasishtakiwe katika Muswada mpya chafutwa na Serikali

Kipengele cha kuwabeba Polisi wasishtakiwe katika Muswada mpya chafutwa na Serikali


Serikali imefuta Ibara ya 24 iliyokuwa inapendekeza kifungu kipya 47A kwa lengo la kutoa mamlaka kwa polisi kufanya operesheni za kificho kwa madhumuni ya kuzuia utendaji wa makosa.

Akitoa taarifa mbele ya Bunge, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Eliezer Feleshi amesema kwamba katika Muswada huo wa Sheria ya Marekebisho mbalimbali na 7 uliopitishwa hapo jana, kifungu hicho tata kimeondolewa rasmi.

Awali tangu kuzuka kwa taarifa za kupelekwa kwa muswada huo kwa hati ya dharura, kuliibuka kwa maswali na sintofahamu kwenye mitandao ya kijamii ikihoji mantiki ya kuwakingia kifua askari polisi endapo watafanya jinai na kuhalalisha mauaji ya raia.

Maoni ya wananchi hao yanakuja ikiwa siku chache tangu Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuonesha kushangazwa kwake na hatua ya jeshi la Polisi nchini kupitia mkuu wake IGP Simon Sirro kutangazia umma kwamba jeshi hilo limeunda tume kuchujichunguza kwa madai ya mauaji ya mfanyabiashara wa madini mkoani Mtwara Mussa Hamisi (25).

Hivi karibuni kumekuwa na mlolongo wa matukio ya ukiukwaji wa kanuni na taratibu za Jeshi la Polisi jambo linalotajwa kuitia doa serikali, licha ya matamko kadhaa ya viongozi wa nchi kutaka jeshi hilo lijitafakari.
Bila kuwaingiza wapinzani Bungeni, TANZANIA HAITOBOI. Hapa watahangaika tuna kucheza danadana na kufanya kazi kwa matukio badala ya kubadili sheria mbovu nyingi tu zilizopo sasa hivi. Sheria hizi zinachelewesha maendeleo hasa katika eneo la biashara. Wafanyabiashara wanaogopa kila kukicha na kufanya eneo/sector kubwa ya kujiajiri kudhorota.

Kimsingi KATIBA MPYA ndio jibu. Waamuzi ni wao. Tanzania ipo katika mkanyiko!
 
Msichokijua,
Hiki kpengele ni mahsusi kwenda kumshughulikia yule afande alomshikia bunduki Nape[emoji4]
 

Serikali imefuta Ibara ya 24 iliyokuwa inapendekeza kifungu kipya 47A kwa lengo la kutoa mamlaka kwa polisi kufanya operesheni za kificho kwa madhumuni ya kuzuia utendaji wa makosa.

Akitoa taarifa mbele ya Bunge, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Eliezer Feleshi amesema kwamba katika Muswada huo wa Sheria ya Marekebisho mbalimbali na 7 uliopitishwa hapo jana, kifungu hicho tata kimeondolewa rasmi.

Awali tangu kuzuka kwa taarifa za kupelekwa kwa muswada huo kwa hati ya dharura, kuliibuka kwa maswali na sintofahamu kwenye mitandao ya kijamii ikihoji mantiki ya kuwakingia kifua askari polisi endapo watafanya jinai na kuhalalisha mauaji ya raia.

Maoni ya wananchi hao yanakuja ikiwa siku chache tangu Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuonesha kushangazwa kwake na hatua ya jeshi la Polisi nchini kupitia mkuu wake IGP Simon Sirro kutangazia umma kwamba jeshi hilo limeunda tume kuchujichunguza kwa madai ya mauaji ya mfanyabiashara wa madini mkoani Mtwara Mussa Hamisi (25).

Hivi karibuni kumekuwa na mlolongo wa matukio ya ukiukwaji wa kanuni na taratibu za Jeshi la Polisi jambo linalotajwa kuitia doa serikali, licha ya matamko kadhaa ya viongozi wa nchi kutaka jeshi hilo lijitafakari.
Wangeua sn na kupita watu kupita kiasi
 
Bila kuwaingiza wapinzani Bungeni, TANZANIA HAITOBOI. Hapa watahangaika tuna kucheza danadana na kufanya kazi kwa matukio badala ya kubadili sheria mbovu nyingi tu zilizopo sasa hivi. Sheria hizi zinachelewesha maendeleo hasa katika eneo la biashara. Wafanyabiashara wanaogopa kila kukicha na kufanya eneo/sector kubwa ya kujiajiri kudhorota.

Kimsingi KATIBA MPYA ndio jibu. Waamuzi ni wao. Tanzania ipo katika mkanyiko!
Kweli tupu
 
Wapiga kura wanawawajibishaje hao wawakilishi wao??

Ni nani anaetoa muongozo wa namna ya kuwawajibisha hao wawakilishi??

Ni mambo gani ambayo wapiga kura watawawajibisha wawakilishi wao kwayo??

Baada ya uwajibishwaji, ni nini kitafuata?? Kama uwajibishwaji maana yake ni kufukuzwa ubunge, je tunachagua mbunge mwengine AMA la??

Ndani ya jimbo moja, je wananchi watawawajibisha wapiga kura mara ngapi ndani ya kipindi cha miaka 5??
Kifungu hicho kilikuwa kimewekwa vizuri. Mfano, kama wananchi wanaona mwakilishi hao hawatembelei kujua matatizo yao, "hawawakilishi kikamilifu" basi kifungu kilikuwa kinatoa utaratibu wa kuweza kumwondoa huyo mwakilishi wao na nafasi yake kuchukuliwa na mgombea mwenza aliyepata kura zinazofuatia kwa wingi. Kumbuka maana ya phrase "uwakilishi wa wananchi bungeni" na pia kumbuka phrase "hawawakilishi kikamilifu". Otherwise, tunakuwa na aina ya wawakilishi wanaojiwakilisha wenyewe na wala hawana mpango na wananchi wao kwa sababu wanajua wakati wa kupiga kura watashinda tu.
 
Wabunge lazima wawe na aibu kuwa wanategemea kila kitu RAIS awape mungozo wa nini kina faida kwa wananchi katika maamuzi yao! Mnakula mshahara mkubwa bila Kufanya kazi mnayostahili kufanya ; you should be ashamed!! HONGERA Rais kwa marekebisho hayo ya sheria!
KUNA WABUNGE NCHI HII? KILA KITU NDIO, HATA YAKILETEWA MSWADA KUA BAADA YA MIAKA MITANO WATAENDA JELA WATAPITISHA TU
 
Kifungu hicho kilikuwa kimewekwa vizuri. Mfano, kama wananchi wanaona mwakilishi hao hawatembelei kujua matatizo yao, "hawawakilishi kikamilifu" basi kifungu kilikuwa kinatoa utaratibu wa kuweza kumwondoa huyo mwakilishi wao na nafasi yake kuchukuliwa na mgombea mwenza aliyepata kura zinazofuatia kwa wingi. Kumbuka maana ya phrase "uwakilishi wa wananchi bungeni" na pia kumbuka phrase "hawawakilishi kikamilifu". Otherwise, tunakuwa na aina ya wawakilishi wanaojiwakilisha wenyewe na wala hawana mpango na wananchi wao kwa sababu wanajua wakati wa kupiga kura watashinda tu.
Mkuu Magobe maswali yangu hujanjibu.

Ila shukran. Nimeshapata majibu
 
Unapaswa kujiuliza kilipitaje kwenye baraza la mawaziri.
Yaani waandae wenyewe, wapeleke bungeni kipitishwe alafu wake kukifuta wenyewe. Hapo nani.mwenye tatizo?
Wamesoma. Upepo malalamiko nje kuhusu huo mswada umreashtusha.
 
Back
Top Bottom