Kipindi cha kuingia mwaka mpya ni msimu wa wahubiri uchwara kuvuna pesa!

Kipindi cha kuingia mwaka mpya ni msimu wa wahubiri uchwara kuvuna pesa!

raslimali

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2014
Posts
1,958
Reaction score
1,744
Fungulia tu hizo redio zao usikie habari za makongamano na ibada za kubariki,kukomboa, kutakasa n.k mwaka mpya ujao. Ukiwa mpumbavu fulani unajipeleka halafu unaambiwa toa sadaka au panda mbegu kwa ajili ya mwaka mpya uwe wa mafanikio. Pesa zile zinaingia mfukoni kwa mhubiri. Hivi watanzania tumefika kiwango kibaya namna hii kwenye afya ya akili hata utapeli ulio wazi kabisa hatuwezi kuung'amua?? Hili ni janga.
 
Upumbavu umewajaa kichwani watanzania
Nani atalinusuru taifa letu na huu utapeli? Serikali yetu imefika wakati sasa iwe serious na isiwafumbie macho watu wanaojificha kwenye kichaka cha dini kuwaibia kondoo wasiojielewa. Hawa ni matapeli kama matapeli wengine. Kumtaja Yesu au Biblia siyo kigezo cha kuhalalisha uhalifu. Serikali isisubiri mpaka uhai wa watu upotee ndipo ije na jitihada za zima moto. Yanayoendelea hivi sasa ni kutengeneza taifa la mataahira kupitia huu upumbavu wa wezi waliojificha kwenye kichaka cha ukristo. Tusisubiri mpaka watu wafe bali hapa tulipofika tayari watu wameuawa kiakili na kila siku wanaendelea kuuawa. Serikali please take action. Taifa linaangamia. You will be answerable kama mnaachia hii holelaholela kwenye taifa letu.
 
Back
Top Bottom