Kiranga alikuwa anasali Kanisa Katoliki. Ilikuwaje akaanza kuamini hakuna Mungu?

Mkuu, dunia na vyote vilivyomo alivyoviumba Mungu ni mali yake, kama ni mali yake ANA MAMLAKA YA KUFANYA CHOCHOTE, sisi viumbe hatuna uwezo wa kupingana nae.

Mfano wewe ukiwa na mali, unakuwa na mamlaka ya kufanya chochote utakacho.

Hoja zako ni maswali fikirishi, kuna maswali mengine majibu yake anayo Mungu pekee(kwanini hivi, kwanini vile n.k)

Kuna maswali mengine huwezi kumuuliza baba au mama unayaacha.

Kama binadamu tunachotakiwa kufanya ni kuacha kutenda dhambi, kuyashika na kuyaishi mafundisho ya kweli ya kumtii Mungu na kutenda mema.
 
So Mungu hana kosa
Bado najifunza, Je kwa uwezo wake wote imekuwaje basi aweke option ya namna hiyo? Yaan labda nitoe mfano wa kidunia hapa, kwamba unavyakula umeandaa kingine kiwe na Sumu na kingine kizima; kisha umwambie mtoto wako kwamba Tafadhali tumia Chakula cha kwenye Sahani, cha kwenye Sufuri kina sumu ukila utakufa; Kulikuwa kuna ulazima gani Mti ambao unaleta uharibifu uwekwe kwa option? ni kweli ni maamuzi yake lakini huoni kuweka maamuzi kama hayo kuna ukakasi kaka? Kumbuka unaambiwa Mungu ni upendo, mungu ni wa Haki; je Upendo upi hasa, au Mungu ana upendo wa peke yake kabisa? kwamba akikuwekea mtego ukanasa mwenyewe ndio upendo wake?

Almight God and All knowing God hapa pekee ndipo pananipa utata wa kuwa na mashaka na kufanya imani yangu kwake isiwe thabiti sana.
 
Mkuu, kwa mfano huo huo umekatazwa kula kwanini ule?
 
mafundisho ya kweli ya kumtii Mungu
Hapa Pia ndio ambapo panaongeza Kunichanganya; Kuna Dini Nyingi, kuna Mafundisho mengi kuhusu Mungu na mengine yanakinzana yenyewe kwa yenyewe; Ivi ni fair kweli kaka kwamba Kuna mchanganyo mkubwa sana kwenye Dini, halafu sisi tuwe na option ya kuchukua huku tukiwa hatuna Standard za moja kwa moja kutoka kwake kwamba Dini gani tuchague, Halafu hapo hapo ukikosea Ndio Unachomwa moto (Au kupewa adhabu fulani huku mbeleni, kwa kadiri nilivyofundishwa)
 
Mkuu, kwa mfano huo huo umekatazwa kula kwanini ule?
Watu wako Tofauti, na COncern yangu hapo sio Suala la kula; Baba Mwema hatakiwi kuweka option ya hivyo ili iweje, Kuna Ulazima gani wa kuweka option za namna hiyo Huku ukiwa na uwezo wa kuweka option zilizo njema?; Baba mwema anahakikisha anamlinda Mtoto wake; Kama mtoto atapata shida basi apate shida za kutafuta mwenyewe si za Option ambazo ziliwekwa na baba; Huku baba akiwa na uwezo wote wa kuhakikisha kwamba Anaweka option zilizo salama.

Hatutengenezi matatizo, tunatengeneza Solution; Solution ya kwanza ni kuhakikisha kwamba hatutoi Machaguo yenye matatizo na kuwapa watu.

Anyway nashukuru kwa maelezo yako; nadhani itoshe tu hapo; nitaendelea kujifunza taratibu; kwa sasa nikomee hapa ndugu. Asante sana.
 
Unakosea sana kumuangalia Mungu katika kofia moja peke yake (kama Baba).

Mungu ni Mungu, hebu fikiria Mungu anayemiliki mbingu na viumbe vyote unavyovijua na usivuovijua ( hapa nalenga uone ukubwa wake kama Mungu)


Mungu ameamua kuweka utaratibu wake kwa wanadamu (Kumbuka Mungu hapangiwi), wa kutaka kung'amua ni wangapi watakaomtii ( yale aliyosema yasifuatwe) na watakaokaidi utaratibu wake.

Ukifikiria kwa ukubwa wa Mungu na ukuu wake unapoteza kabisa hoja ya kuhoji kwanini kuna mema na mabaya.


Hapa duniani kuna viongozi tuu ambao hawajaumba chochote walitamani waabudiwe na wasikilizwe amri zao, vipi kuhusu Mungu muumbaji wa vyote vile, Je yeye hasatahili kuweka utaratibu kwa viumbe vyake alivyoviumba mwenyewe!!
 
Unajua mkuu, jinsi uwazavyo ni tofauti na Mungu jinsi anavyofanya utendaji wake.
Namna ya unavyoelezea maneno au mtazamo wako, unauelezea kwa namna ya kidunia ni tofauti kabisa na namna ya utendaji wa Mungu.

Mungu aliumba kila mmea wa matunda wa chakula ili kiumbe me na ke(Binadamu) wale kwa wakati huo, MUNGU ALITOA/ALIWAPA KATAZO KIUMBE ME na KE "KULENI MATUNDA YOTE ILA MATUNDA YA MTI WA UJUZI WA MEMA NA MABAYA MSILE KWAMAANA MKILA MTAKUFA HAKIKA"

Katazo hilo Binadamu akaliasi na kula tunda, hapo kosa ni la binadamu kuasi agizo la Mungu na kusababisha matatizo.

UMEWAHI KUJIULIZA VIPI KAMA WANGELITII HILO KATAZO NA WASINGEKULA MATUNDA YA MTI HUO KUNGEKUA NA HAYA MATATIZO?
 
Nimehitaji unipe formation haujanipa mpaka sasa mkuu
jibu lako nimekupa kupitia hoja ya SNDANGUJA

Inawezekana unashindwa kuliona jibu kwasababu mawazo yako yanapinga kua SNDANGUJA ni habari ya kutungwa, hayupo kihalisia ila hauwezi kuthibitisha hayupo

Kama umefikia level hiyo basi natumaini utakua umeliona jibu la swali lako.
 
Mkuu, usitafute kuchagua dini gani, tafuta kumtii Mungu na kutotenda dhambi.
 
Kitu kimoja mkuu ambacho wewe unakikwepa kwa muda mrefu kukijibu, ni kitu kimoja tu:

Wewe unasema hakuna uwepo wa Mungu na vitu vyote vilivyopo katika ulimwengu huu havijaumbwa na Mungu, ok fine. Kama unavyosema hakuna uwepo wa Mungu na vitu vyote havijaumbwa na Mungu.

Naomba unifahamishe hivi vitu vimetokea wapi? how do they formed?
 
Nilikujibu hivi

Nimekuambia kutokua na majibu sahihi ya swali haimaanishi jibu lisilo sahihi nikipewa siwezi kulijua

Sio mungu tu ambaye nasema hayupo, kuna unicorns, Flying Spaghetti, spiderman, batman, harrypoter, teapot orbiting the sun nk. Swali lolote nitakaloshindwa kujibu kuhusiana na hao niliowataja, je itathibitisha viumbe hao wapo?

Wewe unakubali kua nicorns, Flying Spaghetti, spiderman, batman, harrypoter, teapot orbiting the sun wapo/vipo kihalisia? unaweza kuthibitisha wapo/vipo?

Bila shaka najua utapinga kua hukazaliwa jana

Lakini unathibitisha vipi kua alien mwenye super intelligent hakukuzaa jana katika umbile hilo hilo ulilonalo kisha kaku edit ubongo uwe unakumbuka kumbukizi za nyuma zinazokuonesha ulikuwepo kabla ya hiyo jana?

Kama unaweza ku disprove hayo madai (kitu ambacho najua huwezi) basi hautakiwi kupinga kua haukuzaliwa jana. Kushindwa kwako kutathibitisha kua wewe ulizaliwa jana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…