Kiranga anatoa sadaka na anaamini stori za majini lakini haamini uwepo wa Mungu

Kiranga anatoa sadaka na anaamini stori za majini lakini haamini uwepo wa Mungu

Unajuaje Mungu hajaweka wazi na si kwamba Mungu hayupo?

Kama Mungu hayupo, halafu mtu akaamua tu kujudanganya akakwambia Mungu hajulikani wazi kwa sababu kaamua kutojiweka wazi kwa sababu zake, ukaamini hilo, utajuaje ukweli kwamba Mungu hayupo wakati umetanguliza imani potofu?

Unajuaje hatujui sababu za Mungu kuumba ulimwengu unaoruhusu dhambi kwa sababu Mungu kaamua kutoziweka wazi, na si kwa sababu Mungu hayupo?

Kama unaamini uwepo wa Mungu usiyemuelewa vizuri, unajuaje kwamba huyo Mungu yupo kweli na habari za uwepo wake si hadithi za watu tu tumedanganyana kwa sababu zetu za kidunia hii tu?
Hapa twende kwenye baselines. Mimi Mungu simwamini kinadharia tu, nimemwona kwenye maisha yangu mara nyingi sana.

Kimsingi Mungu anaeleweka kirahisi sana mara baada ya kumwamini. Zamani nilikuwa napata changamoto maswali ya namna hii yanapoulizwa na yale ya waislamu kuhusu Yesu. Ilikuwa doubtful moment.

Lakini nikaamua kumuomba Mungu anipe ufahamu kuhusu yeye. Nilifanya study ya dini hizi mbili kubwa hapa Tanzania. Nikapata ufahamu wa kuelewa namna ambavyo Yesu ni Mungu, nikaelewa kuhusu the trinity of God, nikaelewa kuhusu the righteousness of God, the love of God, ukuu wa Mungu, msamaha wa dhambi na hata uzima wa milele.

Mimi ninakuunga mkono kuhoji na kujiuliza maswali haya na mengine mengi. Ni watu wachache sana wanapata nafasi ya namna hii. Actually hata waislamu wanapohoji na ku doubt ninawaelewa.

Ila kwa uzoefu wangu, utapata majibu ikiwa moyoni unayodhamira ya dhati kupata majibu. Unyenyekevu utawezesha kupata ufahamu. Unaweza kuomba sincerely from your mind kwamba kama Mungu yupo basi ajidhihirishe kwako.

Nina uhakika atakupa ufahamu kumjua kama kweli unapenda kumjua.
 
Unalazimisha sana Mungu aonekane hayupo, kisa contradiction ndogondogo
Contradiction ambayo hujaweza kuisuluhisha si ndogo.

Ingekuwa ndogo ungeweza kuisuluhisha.

Kutoelewa hilo nayo ni ishara ya Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote kutokuwepo.

Angekuwepo, asingeruhusu ujinga uwepo mara tano kwako.

Ujinga wa kuamini uongo

Ujinga wa kuelimishwa unaamini uongo na bado kushindwa kuelewa.

Ujinga wa kushindwa kutatua contradiction.

Ujinga wa kushindwa kutatua contradiction, halafu kuiita ndogo.

And I bet utaendeleza ubishi kijinga katika mambo ambayo oengine huna hata uwezo wa kuyaelewa.
 
Hapa twende kwenye baselines. Mimi Mungu simwamini kinadharia tu, nimemwona kwenye maisha yangu mara nyingi sana.

Kimsingi Mungu anaeleweka kirahisi sana mara baada ya kumwamini. Zamani nilikuwa napata changamoto maswali ya namna hii yanapoulizwa na yale ya waislamu kuhusu Yesu. Ilikuwa doubtful moment.

Lakini nikaamua kumuomba Mungu anipe ufahamu kuhusu yeye. Nilifanya study ya dini hizi mbili kubwa hapa Tanzania. Nikapata ufahamu wa kuelewa namna ambavyo Yesu ni Mungu, nikaelewa kuhusu the trinity of God, nikaelewa kuhusu the righteousness of God, the love of God, ukuu wa Mungu, msamaha wa dhambi na hata uzima wa milele.

Mimi ninakuunga mkono kuhoji na kujiuliza maswali haya na mengine mengi. Ni watu wachache sana wanapata nafasi ya namna hii. Actually hata waislamu wanapohoji na ku doubt ninawaelewa.

Ila kwa uzoefu wangu, utapata majibu ikiwa moyoni unayodhamira ya dhati kupata majibu. Unyenyekevu utawezesha kupata ufahamu. Unaweza kuomba sincerely from your mind kwamba kama Mungu yupo basi ajidhihirishe kwako.

Nina uhakika atakupa ufahamu kumjua kama kweli unapenda kumjua.
Umemuonaje Mungu katika maisha yako na una hakika gani ni Mungu uliyemuona si kitu kingine?
 
Umemuonaje Mungu katika maisha yako na una hakika gani ni Mungu uliyemuona si kitu kingine?
Nina uhakika kwasababu nimekutana naye. Yesu, niko naye kila siku. Ni rafiki wa karibu. Sio nadharia, ni halisia.
 
Kiranga jeshi la mtu mmoja[emoji3][emoji3][emoji3][emoji91]
Nyuma yangu kuna ukweli usiopingika, fikra za kina, mawazo ya kidhahania na uthabiti wa kimantiki.

Nabishana na watu wengi hawajamsoma Anselm, hawajamsoma Aquinas, hawajamsoma Russell hawajamsoma hata Dawkins.

Wengine hata Kiingereza hawajui.

Hawajui classical arguments for or against the existence of God.

Ni kama nabishana hesabu na mtu anayegawanya kwa sifuri na kufanya kila namba iwe sawa na kila namba nyingine.
 
Sasa unasaidia kwa madhumuni yapi?
Nasaidia ninapoweza kwa kuwa napenda watu, napenda kuwa mtu wa msaada, na najua hakuna Mungu wa kusaidia mtu, watu ndio tunasaidiana wenyewe.

Ningeamini Mungu yupo, nisingesaidia sana. Ningesema tu Mungu atasaidia watu wake, wamuombe tu msaada.

Lakini, kwa kuwa najua Mungu hayupo, kazi ya kumsaidia mtu ni ya mtu. Mungu hawezi kusaidia, kwa sababu hayupo.

Na huu ni msaada mzuri zaidi, kwa sababu nautoa bila kutegemea kupata zawadi ya mbingu (ambayo sikubali kwamba ipo) wala kuogopa kwenda adhabuni motoni (ambapo sikubali kwamba kupo) na zaidi, bila kutaka kujipendekeza kwa Mungu (ambaye sikubali kwamba yupo)
 
Nasaidia ninapoweza kwa kuwa napenda watu, napenda kuwa mtu wa msaada, na najua hakuna Mungu wa kusaidia mtu, watu ndio tunasaidiana wenyewe.

Ningeamini Mungu yupo, nisingesaidia sana. Ningesema tu Mungu atasaidia watu wake, wamuombe tu msaada.

Lakini, kwa kuwa najua Mungu hayupo, kazi ya kumsaidia mtu ni ya mtu. Mungu hawezi kusaidia, kwa sababu hayupo.

Na huu ni msaada mzuri zaidi, kwa sababu nautoa bila kutegemea kupata zawadi ya mbingu (ambayo sikubali kwamba ipo) wala kuogooa kwenda adhabuni motoni (ambapo sikubali kwamba kupo) na zaidi, bila kutaka kujipendekeza kwa Mungu (ambaye sikubali kwamba yupo)
Let me save this
 
Nina uhakika kwasababu nimekutana naye. Yesu, niko naye kila siku. Ni rafiki wa karibu. Sio nadharia, ni halisia.
Hujaeleza unathibitishaje upo na Yesu na si ugonjwa wa akili tu unaokufanya ujione uko na Yesu?

Hata kichaa anaweza kujiona yuko na Yesu kila siku.

Kumbe ana matatizo ya akili tu.
 
Hujaeleza unathibigmtishaje upo na Yesu na si ugonjwa wa akili tu unaokufanya ujione uko na Yesu?

Hata kichaa anaweza kujiona yuko na Yesu kila siku.

Kumbe ana matatizo ya akili tu.
Mimi na wewe tumekuwa tukijadili hapa tangu juzi, unaweza kusema kwamba ninalo tatizo la akili? Yesu ninamfahamu, ni rafiki yangu wa karibu.

Umewahi kuziona akili? Unafahamu vipi kwamba hizi ni akili?
 
Mimi na wewe tumekuwa tukijadili hapa tangu juzi, unaweza kusema kwamba ninalo tatizo la akili? Yesu ninamfahamu, ni rafiki yangu wa karibu.

Umewahi kuziona akili? Unafahamu vipi kwamba hizi ni akili?

Kuamini kuwapo kwa Mungu asiyethibitishika na ambaye dhana ya kuwapo kwake ina contradiction, hata baada ya kuelimishwa vizuri mara kadhaa, ni aina fulani ya matatizo ya akili.

Kwa nini kuona kuwe jambo la msingi?

Wewe unaamini uwepo wa Mungu, ushawahi kumuona?

Akili zinapimwa kwa logical consistency.

Wewe unaamini uwepo Mungu wa contradiction.

Una matatizo ya akili.

Ndiyo maana unasema unakaa na Yesu.
 
Kuamini kuwapo kwa Mungu asiyethibitishika na ambaye dhana ya kuwapo kwake ina contradiction, hata baada ya kuelimishwa vizuri mara kadhaa, ni aina fulani ya matatizo ya akili.

Kwa nini kuona kuwe jambo la msingi?

Wewe unaamini uwepo wa Mungu, ushawahi kumuona?

Akili zinapimwa kwa logical consistency.

Wewe unaamini uwepo Mungu wa contradiction.

Una matatizo ya akili.

Ndiyo maana unasema unakaa na Yesu.
Mimi Mungu nimemuona na ninamuona kila siku. Ndani yake naishi na kuwa na uzima wangu.

Sijakuuliza unapima vipi akili, nimeuliza akili ni nini? Umewahi kuziona?
 
Mimi Mungu nimemuona na ninamuona kila siku. Ndani yake naishi na kuwa na uzima wangu.

Sijakuuliza unapima vipi akili, nimeuliza akili ni nini? Umewahi kuziona?
Thibitisha Mungu umemuona kwanza na kwamba hii habari si uongo au ujinga wako tu.
 
Nasaidia ninapoweza kwa kuwa napenda watu, napenda kuwa mtu wa msaada, na najua hakuna Mungu wa kusaidia mtu, watu ndio tunasaidiana wenyewe.

Ningeamini Mungu yupo, nisingesaidia sana. Ningesema tu Mungu atasaidia watu wake, wamuombe tu msaada.

Lakini, kwa kuwa najua Mungu hayupo, kazi ya kumsaidia mtu ni ya mtu. Mungu hawezi kusaidia, kwa sababu hayupo.

Na huu ni msaada mzuri zaidi, kwa sababu nautoa bila kutegemea kupata zawadi ya mbingu (ambayo sikubali kwamba ipo) wala kuogopa kwenda adhabuni motoni (ambapo sikubali kwamba kupo) na zaidi, bila kutaka kujipendekeza kwa Mungu (ambaye sikubali kwamba yupo)
Kuna siku utamtaka sana Mungu na itakuwa too late kwako. Yesu anakupenda na yupo tayari kukusamehe dhambi na kukupa uzima wa milele.
 
Kuna siku utamtaka sana Mungu na itakuwa too late kwako. Yesu anakupenda na yupo tayari kukusamehe dhambi na kukupa uzima wa milele.
Acha mahubiri.

Thibitisha Mungu yupo.
 
Thibitisha Mungu umemuona kwanza na kwamba hii habari si uongo au ujinga wako tu.
Utajuaje kama nitakaokupa ndio uthibitisho?

Mimi nipo na Yesu wakati wote, unataka uje kwangu umuone kama uthibitisho?
 
Mahubiri ni muhimu.

Utajuaje kama nitakaokupa ndio uthibitisho wa uwepo wa Mungu?

Swali zuri.

Nina vigezo vitatu.

Weka hoja ambayo ina clear and logical evidence, haiwezi kuwa contradicted na haina logical inconsistency kuhusu uwepo wa Mungu tuichambue.

Mpaka sasa, hoja zote kuhusu uwepo wa Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, hazina clear and kogical evidence, zina contradiction na logical inconsistencies.

Karibu, nakusubiri.
 
Back
Top Bottom