Kirusi kipya cha HIV kimegunduliwa Uholanzi

Kirusi kipya cha HIV kimegunduliwa Uholanzi

Pacbig

JF-Expert Member
Joined
Oct 15, 2017
Posts
1,095
Reaction score
2,087
Nimeikuta hii habari kwenye ukurasa wa Millard Ayo. Kirusi hicho ni hatari zaidi ya kile cha mwanzo.

Kinashambulia kinga za mwili mara mbili zaidi ya kile cha awali. Mpaka sasa hakuna dawa wala chanjo ya hicho kirusi.

Corona inasuasua, hapa tusipokuwa makini tutapatikana.
===
Wakati dunia ikipambana usiku na mchana katika kuhakikisha kinapata uvumbuzi wa kutibu kirusi kinachosababisha UKIMWI, nchini Uholanzi kirusi cha aina nyingine chagundulika.

Kirusi hicho kilichopewa jina la 'VB Variant' kwa maana ya Virulent Subtype B kinasadikika kuwa na nguvu za kushambulia kinga mara mbili ya Virusi vya kawaida vilivyozoeleka.

Katika utafiti uliochapishwa hivi majuzi katika jarida la 'Journal Science' watalaam wanasema kuwa kirusi hicho kina uwezo wa kujizalisha kwa haraka zaidi hivyo kufanya mashambulizi ya kinga za mwili kuwa mara dufu.

Pia, wametanabaisha kwamba uwezo wake wa kuambukiza baina ya mtu na mtu ni mwepesi zaidi.

Kirusi hicho ambacho mpaka sasa hakina kinga wala tiba, kimeshashambulia zaidi ya watu 109 huko Uholanzi.

Kirusi hicho kinajulikana kwa kupima kwa vipimo vya kawaida vya kupima maambukizi ya virusi vya UKIMWI vya kawaida.

Nawasihi Watanzania wenzangu, tuzidishe uaminifu na kuchukua tahadhari zaidi kuepukana na kirusi hicho hatari.

Tutumie kinga pale inapobidi na tukapime ili tujue hali zetu. Kama utapatikana na ugonjwa, utaanza dozi mapema na kupunguza kasi ya mashambulizi ya virusi hivyo.


TANZANIA BILA UKIMWI INAWEZEKANA.
 
Okay.... Vax Vax
Sasa hii chanjo sijui ant Vaxx mtaikataa.

Yes tunajua ni biashara watu wanaingiza mzigo wao sokoni. But the question is nayo tutaipinga?
 
Nimeikuta hii habari kwenye ukurasa wa Millard Ayo. Kirusi hicho ni hatari zaidi ya kile cha mwanzo.

Kinashambulia kinga za mwili mara mbili zaidi ya kile cha awali. Mpaka sasa hakuna dawa wala chanjo ya hicho kirusi.

Corona inasuasua, hapa tusipokuwa makini tutapatikana.View attachment 2107848View attachment 2107849
Kumbe hata huyo Milard Ayo huwa hajiongezi kabla ya kutoa habari? Na kwanini haweki “source” ya habari zake? Kwasababu hiyo “variant” ya HIV inatibika.

“The new variant has been found mainly in The Netherlands and it is more infectious, but it can be detected with existing tests and responds to treatment”

 
Okay.... Vax Vax
Sasa hii chanjo sijui ant Vaxx mtaikataa.

Yes tunajua ni biashara watu wanaingiza mzigo wao sokoni. But the question is nayo tutaipinga?
Watu wamekataa Chanjo ya Covid- 19 ni vile tu wameiona Covid ni mdebwedo.

Ikija chanjo ya Ukimwi, hakuna hata atakayebaki ndani. Ugonjwa ule umekaa pabaya na watu wataona wamepata chance ya kujiachia.
 
Watu wamekataa Chanjo ya Covid- 19 ni vile tu wameiona Covid ni mdebwedo.

Ikija chanjo ya Ukimwi, hakuna hata atakayebaki ndani. Ugonjwa ule umekaa pabaya na watu wataona wamepata chance ya kujiachia.
Hahaha nataka niwaone watu wabishi
 
nini sasa hii, watu walishauzoea uliopo, wanajiachia tu....hizi shida sasa
 
Inajulikana kwamba HIV haina dawa kwa maana ya tiba, sasa sijui kwa nini kijana Ayo kaandika "hadi sasa haijapatikana dawa...."
 
Inajulikana kwamba HIV haina dawa kwa maana ya tiba, sasa sijui kwa nini kijana Ayo kaandika "hadi sasa haijapatikana dawa...."
Hizi ARV sio dawa?
 
Back
Top Bottom