Pacbig
JF-Expert Member
- Oct 15, 2017
- 1,095
- 2,087
Nimeikuta hii habari kwenye ukurasa wa Millard Ayo. Kirusi hicho ni hatari zaidi ya kile cha mwanzo.
Kinashambulia kinga za mwili mara mbili zaidi ya kile cha awali. Mpaka sasa hakuna dawa wala chanjo ya hicho kirusi.
Corona inasuasua, hapa tusipokuwa makini tutapatikana.
===
Wakati dunia ikipambana usiku na mchana katika kuhakikisha kinapata uvumbuzi wa kutibu kirusi kinachosababisha UKIMWI, nchini Uholanzi kirusi cha aina nyingine chagundulika.
Kirusi hicho kilichopewa jina la 'VB Variant' kwa maana ya Virulent Subtype B kinasadikika kuwa na nguvu za kushambulia kinga mara mbili ya Virusi vya kawaida vilivyozoeleka.
Katika utafiti uliochapishwa hivi majuzi katika jarida la 'Journal Science' watalaam wanasema kuwa kirusi hicho kina uwezo wa kujizalisha kwa haraka zaidi hivyo kufanya mashambulizi ya kinga za mwili kuwa mara dufu.
Pia, wametanabaisha kwamba uwezo wake wa kuambukiza baina ya mtu na mtu ni mwepesi zaidi.
Kirusi hicho ambacho mpaka sasa hakina kinga wala tiba, kimeshashambulia zaidi ya watu 109 huko Uholanzi.
Kirusi hicho kinajulikana kwa kupima kwa vipimo vya kawaida vya kupima maambukizi ya virusi vya UKIMWI vya kawaida.
Nawasihi Watanzania wenzangu, tuzidishe uaminifu na kuchukua tahadhari zaidi kuepukana na kirusi hicho hatari.
Tutumie kinga pale inapobidi na tukapime ili tujue hali zetu. Kama utapatikana na ugonjwa, utaanza dozi mapema na kupunguza kasi ya mashambulizi ya virusi hivyo.
TANZANIA BILA UKIMWI INAWEZEKANA.
Kinashambulia kinga za mwili mara mbili zaidi ya kile cha awali. Mpaka sasa hakuna dawa wala chanjo ya hicho kirusi.
Corona inasuasua, hapa tusipokuwa makini tutapatikana.
===
Wakati dunia ikipambana usiku na mchana katika kuhakikisha kinapata uvumbuzi wa kutibu kirusi kinachosababisha UKIMWI, nchini Uholanzi kirusi cha aina nyingine chagundulika.
Kirusi hicho kilichopewa jina la 'VB Variant' kwa maana ya Virulent Subtype B kinasadikika kuwa na nguvu za kushambulia kinga mara mbili ya Virusi vya kawaida vilivyozoeleka.
Katika utafiti uliochapishwa hivi majuzi katika jarida la 'Journal Science' watalaam wanasema kuwa kirusi hicho kina uwezo wa kujizalisha kwa haraka zaidi hivyo kufanya mashambulizi ya kinga za mwili kuwa mara dufu.
Pia, wametanabaisha kwamba uwezo wake wa kuambukiza baina ya mtu na mtu ni mwepesi zaidi.
Kirusi hicho ambacho mpaka sasa hakina kinga wala tiba, kimeshashambulia zaidi ya watu 109 huko Uholanzi.
Kirusi hicho kinajulikana kwa kupima kwa vipimo vya kawaida vya kupima maambukizi ya virusi vya UKIMWI vya kawaida.
Nawasihi Watanzania wenzangu, tuzidishe uaminifu na kuchukua tahadhari zaidi kuepukana na kirusi hicho hatari.
Tutumie kinga pale inapobidi na tukapime ili tujue hali zetu. Kama utapatikana na ugonjwa, utaanza dozi mapema na kupunguza kasi ya mashambulizi ya virusi hivyo.
TANZANIA BILA UKIMWI INAWEZEKANA.