Kisa kipi kilikufanya ujute sana?

Kisa kipi kilikufanya ujute sana?

FUJO ZA WANAFUNZI NA WANAKIJIJI


Dah miaka hiyooo. Nipo sekondari O-level mkoa fulani hiviii waliosoma hapo wataikumbuka hii story maana nilikua aina ya wale wanafunzi ambao anafahamika shule mzima na nilikua nataniwa na kila mtu.

Kulikua na shida kubwa sana ya maji katika mji huo hivyo kulazimika wanafunzi wa shule za boarding za hapo kuwa na kawaida ya kutoka nje ya shule kutafuta maji huko mitaani yaani ilikua ni ubabe na vurugu maana kilichokua kinahitajika ni maji yawe ya kisima salama, kisima cha wazi/shimo ama hata ya mfereji lakini maji yafike shule kwa matumizi binafsi na matumizi ya jikoni endapo darasa lako litakua na zamu na kipindi hiki hata ratiba za darasani hazikua sawa maana wenye zamu ya jikoni wakizingua basi uji mnakunywa saa sita mchana😂😂😂😂😂 au kula wali saa sita usiku kosa maji yamechelewa ilikua kawaida.
Kipindi hicho ilikua inafika hatua mtu ukimaliza kula inabidi uilambe sahani yako kwani hakukua na maji ya kuoshea, tulikunywa maji machafu yaani machafu unayoyajua wewe yaani ile ndoo mnayoingia nayo bafuni(nadhani mnajua hali ya maliwato za shule za bweni za serikali) ndio hiyo mnaitumbukiza kisimani mnachota maji kwa matumizi yooote kuanzia kunywa, kuoshea, kufulia, kupikia,nk hapo kutumia maji chooni ilikua anasa zaidi ya makaratasi na magodoro🤨🤨🤨.
Basi nilikua na kakundi kangu tunajikuta manundaaa hatuogopi mbuzi yeyote baada ya chakula cha jioni tumeenda kunyanyua vyuma ikabidi tushuke kitaa kusaka maji na kuoga hukohuko ilikua mida ya saa mbili usiku no body caring about the so called night prepo.
Sasa kufika kwenye kisima cha wazi kikubwa zaidi hatukukuta foleni tukajichotea maji na kuoga. Wakati tunaoga kuna majamaa wawili ambao ofcourse tulikua tunafahamiana nao (kutokana na harakati zetu chafu na uhuni za mtaani) walikua wanaishi jirani kabisa na kisima na walikua wamelewa, sasa wakaanza kututolea maneno machafu sana na ninaamini hawakututambua kutokana na kulewa.
Kikatuuma sana wana tulikua 6 tukaamua tukiwashe, ukumbuke ni usiku sasa hiyo inaenda saa nne basi tukawachezeshea kichapo na walipiga kelele kinoma nadhani hadi wanakijiji wengine wakasikia. Ili kuonesha sisi ni wababe zaidi tukaanza kurusha mawe mazito kwenye paa la nyumba ya washkaji ASALALEEEEH kumbe wanakijiji wamejikusanya waje kutoa msaada.

Sasa kutokana na jeuri ya wanafunzi wanapokua wanafuata maji kijijini kulikua na chuki imejengeka kwa wanakijiji juu ya wanafunzi ni vile tu walikua wanakosa namna ya kulipiza sasa na sisi ndio tukawa tumeingia king wenyeweee. Ebwanaee, baada ya kumaliza hilo timbwili letu kuwapiga majamaa na kufanya vurugu tukaamua tusepe sasa njia ilikua ni ile ya imesongwa na nyasi so mnavyopita mnakaa kama msululu kama bata na wanae mimi nikiwa wa mwisho kabisa nikiwa nimebeba maji nusu ndoo na tochi mkononi.
Ghafla tunakutana na nyomi la wananzengo mzee mwenye jiwe, fimbo na silaha nyingine za jadi kumbe wanatulia timing basii nilichosikia ni WEZI WENYEWE HAWA HAPAAA KAMATAAA.

Ilikua ni nyuma geuka, mimi nikawa wa kwanza nilikimbia nikapaa kile kisima ambapo hadi leo sijui niliwezaje mbele kulikua na matuta yale ya majaruba nikajikwa nikaanguka, hapo ujue wanakijiji wametuungia na kelele za weziiii weziiiiii🔥🔥🔥🔥🔥🔥.
Ile nataka kuinuka nikasukumwaa na mwenzangu nikarudi chiniiii wanakijiji hawa hapaaa, usiombe babaangu, ndani ya sekunde kadhaa nilikua nakiona kifo hiki hapa nilipiga kelele ambazo sijawahi kupiga maishani mwangu nikijitetea kuwa mimi sio mwizi bali ni mwanafunzi wa hiyo shule.

Nashkuru kuna mzee mmoja pale wenye hekima akaingilia kati nisiendelee kupigwa japo wanakijiji kila mmoja alikua na hasira na tabia chafu za wanafunzi mfano kuchota maji kibabe wakikuta foleni( yaani unaweza kuwa na kisima kwako ila tukifika tunakusubirisha kuchota hata ya kupikia), kuiba mazao ya bustani kama miwa na matunda, kuiba mademu zao, nk ambazo nyingine hata mimi nilikua nazo basi nikawa nimepelekwa sehemu kuna taa nahojiwa pale ratiba inayofuatia ni kupelekwa polisi kwa uharibifu tulioufanya na wakati huohuo kuna baadhi ya raia wenye hasira wananipa ngumi au makofi ya kuvizia, sisahau mshkaji mmoja yuliwahi kula demu wake namkumbuka vizuri kabisa alinipa kichwa cha pua aisee nikaishia kuona nyotanyota.

Lakini akatokea mwana ambaye alikua tunafanya nae michongo flani haramu akateteaa pale uwongo na ukweli nikaachiwa kwa mkwara mzito, hapo nahisi maumivu kila sehemu.
***********
Sasa wale wenzangu wengine walifanikiwa kufika shule na kugonga kengele ya dharula(ile shule ni moja ya shule inayoheshimu lengele za dharula yaani mtu anaweza asikimbilie kengela ya chakula ila ya dharula usiku ni dk chache tu wapo assembly. Basi jamaa mmoja fala sana akatangaza kuwa nimedakwa na wanakijiji huko wananibaka na tunavyozidi kuchelewa watakuta nimekufa hivyo washuke fasta kuniokoa.

Mwanaaa usiombeeee, ofisi ya vifaa ikavamiwa wa kutoka na fyekeo, jembe, fito za mafagio, mwenye jiwe, na silaha yoyote alibeba shule nzima yenye 800+ students ikashuka village na hasira maana ujue hapo wanafunzi na wanakijiji hawapatani.
Aisee mimi nimeachiwa pale hata wanakijiji hawajatawanyika, nakatisha kona ya kwanza kusepa nachechemea taratibu nipo na mwana aliyenitoa kwenye msala nakutana na wale vimbelembele wa skaut aisee wataka waanze na yule mshkaji nikawapooza nikamwambia mshkaji potea jeshi la kazi limefika hapo ukumbuke wanakijiji bado hawajatawanyika pale walipokua wakinihoji na wanafunzi wanazidi kuja wananiuliza hali yangu palee nikawaambia wabaya wote wapo hapo nyuma kama vipi tuwaibukie.

Kilichotokea huwa sipendi kukumbuka kilitembea kichapo hapo yaani palichafuka, yule mshkaji aliyenipiga kichwa cha pua aisee sikumuacha tulilipana palepaleee nadhani ndie aliyejeruhiwa zaidi maana wana walikua wananiuliza nioneshe aliyenipiga wote wamewekwa mtu kati alitia huruma sana maana alipasuliwa kweli kuna jamaa alimkata na jembe kichwani ameloa damu kichwa choteee. Basi mida ya saa saba operation ya kuniokoa ikaisha tukakusanyana wale wote tuliokua kwenye kisanga tukatunga story moja na kama tulijua, polisi hawa hapa shule tukabebwa hadi kituoni tukahujiwa kila mmoja peke yake na tukatoa story inayofanana.

Pamoja hayo yote ila ni shule ninayojivunia kwa shule zote na levels zote za kielimu nilizopitia ma huwa naimiss sana.
Sengerema secondary
 
Pole sana Mkuu,kuoa ni kama kamali. Ila mimi sitoicheza hiyo kamali.
Ndoa ni jambo la kheri,

Mke ni mama wa watoto wako,

Mke hukupa msimamo na heshima kwenye jamii

Mke ni mtu muhimu mwenye kujua shida zako kwa ukaribu zaidi kuliko hata wazazi waliokuzaa

Mke mratibu wa mipango mingi na mwenye kukukumbusha mambo mengi

Oa kijana kila mtu na mapito yake vitu vingine visikuchanganye

Mimi sijutii kuoa Bali najutia kumuoa huyu
 
Tulichapwa bakora siku ya kumaliza necta form six

Siku hiyo sitosahau nilikula mijeledi kama yesu msalabani bila kosa ndo nikaamini sio kila anayeenda jela ana makosa

Ilikua hivi Nakumbuka ilikua Alhamisi ile tunamalizia mtihani wa mwisho msimamizi akatuambia mkimaliza mtihani muende uwanjani msiondoke kwanza tukasema poa tulikua tunahisi sijui walimu wanakuja kutupongeza basi tukapiga pepa pale mpaka...
Pole sana ndugu,Mjita alikuponza.
 
Majuto mengine yanatokana na tamaa. Sielewi hata ile akili tuliitoa wapi, Ila mm na mwanangu Shedrack tulipanga tuibe nguruwe wa shule tukauze. Kipindi hicho tupo O level, kwenye shule ya kanisa (seminary)...
Ooh aise pole San mkuu
 
Mkuu wapi ulielezea weka link[emoji3][emoji3][emoji3]

Check na hiyo mkuu [emoji3][emoji3][emoji3]
 
Nipo darasa la tatu hasubuhi mama kaniandaa kwa ajili ya kwenda shule vizuri tu na chai nimekunywa na nauli kanipa na pesa ya kutumia pia..

Sasa sijui alizubaa vipi? Si nikachukua/nikaiba pesa shs 400 tena mezani iliwekwa sijui ya nini? Poa nikasindikizwa mpaka kituoni nikapanda basi nikaenda shule baadae niliporudi.. ikagundulika kama ni mimi niliechukua pesa banah wewe.. mama alinitandika sana..

Nilipigwa sana yaani hakuna mfano wa kichapo kilee ukiringanisha na umri ule mdogo na moto nikaunguzwa kidogo mkononi.. ila ilinisaidia baada ya pale sijawahi kuiba tena yaani niliachana na habari ya kuchukua kitu cha mtu popote palee hata mtu akidondosha pesa/kitu na nimeona ntamuokotea na kumpa pesa yake.. ilinisaidia sana..

Cha ajabu nilipofika form 1 .. ilikuwa siku ya malipo mama na dada walikuwa wametoka kazini siku ya kupokea mshahara.. kufika home wakaweka mabegi yao mda huo mimi sipo nipo zangu kiwanjani nacheza mpira.. kumbe banah wameficha pesa zao za mshahara kwa sababu hawataki Baba apate pesa sijajua kama walikuwa na utaratibu wa kumpa pesa au laaah

Nimerudi zangu sina lile wala hili nimeoga zangu na kwenda tena nje kupiga story.. baadae nikaitwa kwa ajili ya chakula nikala..

Baba alivyorudi nilikuwa nimeshalala nikaamshwa na kuanza kuulizwa kuhusu pesa zingatia mda wote mama na dada hawakuniuliza kuhusu pesa kama ingekuwa kweli wameibiwa wangeniuliza kabla ya baba kurudi “ nikajua hapa wanataka kunisingizia tu..

Kikaanza kichapo daah nilipigwa sana bila sababu alaf ilikuwa usiku saa nne inaenda saa tano cha haibu zaidi baba akaanza kunitembeza kwa marafiki zangu kuwauliza kuhusu kuniona na pesa au laah.. marafiki zangu wanasema huyo kwanza sio mwizi wala hachukui cha mtu na leo hakuwa na pesa wala nini! Yaani nilipigwa sana kama mtu ambaye amechukua pesa lazma angesema tu cha ajabu nilikuwa napigwa na mwiko mpaka ukavunjika nikawa napigwa na bakora yaani ingekuwa sio wazazi wangu walllah sijui ingekuaje!!

Mambo yakaishaga maisha mengine yakaendelea sasa nimekua nimemaliza shule na nikaanza kazi sasa lile tukio linajirudia rudia kichwani nikafikilia ngoja nimuulize mama ilikuaje zile pesa mliibiwa kwenye daladala au ilikuaje!!

Mama nikimuulizaga ananiambia tu mwanangu naomba unisamehe sana na anakuaga na huzuni sana kila nikimuulizaga hayo mambo.. yaani analengwagwa mpaka na machozi najisikiaga vibaya sana na nimeachaga kumuuliza tena na kwa moyo wangu wote nimemsamehe sana ila natamani siku aniambie ukweli wa lile jambo lilikuaje!! Nahisi siku moja atanambia tu nimewasamehe ila likinijia kichwani huwa linanisumbua sana kichwa.. daaah baba alinipigaga sanaa kama sio mwanae vilee

Wababa msitoe hadhabu kwa watoto wenu kabla ya kuchunguza kosa..
 
Back
Top Bottom