Kisa kipi kilikufanya ujute sana?

Kisa kipi kilikufanya ujute sana?

COUNTERFEIT MONEY

Wakati bado nipo chuo kabla ya msala wa Receipt fake.. ilikua ni mwaka wa pili kama sikosei sem ya pili.

Hii story kama mhusika yuko humu JF atanijua rasmi mimi ni nani. Ila hakuna shida, cha kuogopa ni kifo pekee na bado kidgo kingenikuta!

Jamaa yangu mmoja nilikua naishi naye hostel nje kidgo ya chuo. Yeye kama ilivyo mimi hatukuwa na mkopo, na kwao hawakua vizuri kama ilivyo kwetu. Sema yeye alikua mtoto wa mjini kushinda mimi na alikua ameniacha parefu ki umri. Sema kuna vitabia flani hivi huwa vinafanya watu wanakua marafiki. Kwa namna yeye na mimi tulivyokua, ungeweza kutuita wazee wa michongo katika rejesta za kileo.

Kwa vile tulikua tunakaa room moja, vitu vingi kuhusu mimi vilikua wazi. Sina hela. Nimefulia. Sikua hata na confidence ya kusimamisha mwanamke nimtongoze. Akitaka tutoke out nitampeleka wapi? Kwa hela ipi? Kwaiyo nikawa ni mtu wa kutulia sana ndani na kuishi kikamilifu ndani ya ratiba za chuo na hostel. So unaweza ku imagine vile maisha yangu yalikua Boring!

Siku moja wakati tunapiga story za hapa na pale na jamaa akaniambia kuna mchongo wa siri anataka kunishirikisha. Nikatega sikio vizuri. Akaniambia kuna jamaa anamjua tukimpa kiasi fulani halali anaweza kututumia hadi mara nne yake ya bandia. Kwaiyo sisi kazi yetu ni kutafuta changes (Chenchi) tu ili tupate za halali.

Duh, wakati ananiambia mimi natetemeka. Nikamwambia mwanangu hii issue si inaweza ikatufanya tufungwe kabisa? Akaniambia "Ufungwe na nani?" .. "Tulia nikuoneshe", na mimi nikatulia.

Jamaa akaagiza mzigo, ukafika. Ilikua kama Mil 1 hivi ya Bandia. Nikamuona kwenye zile pande mbili za kuwekea hela kwenye Wallets; upande mmoja kaweka pesa halali kama 30K, na upande mwingine kaweka bandia kama 100K (Laki). Kaoga kamaliza, huyoooo kasepa!


Alikua ni mtu wa viwanja sana, sikumsikia wakati anarudi usiku. Kwaiyo kesho yake ahsubui namuona kakaa kwenye angle ya kitanda anahesabu hela, Duh. Ni kaki na buku be za kutosha. Mshenzi kashikisha watu zaidi ya elf 90 za bandia. Kabaki na 10 tu. Mimi tamaa ikawa imeanza kugonga mlango, nikawa sitaki kuifungulia. Unajua ukiwa umefulia sana vishawishi ni rahisi sana kukuzidi nguvu. Nikaendelea kujikaza huku jamaa yangu anazidi kuagiza mizigo na anapiga hela vibaya mno.

Mimi nampiga tu vi mizinga vya hapa na pale mwisho wa siku nikajikuta na mimi kanigawia fungu la kuchekecha. Ilikua kama laki 5. Laki 4 bandia, laki 1 halali.

Kama uko viwanja pesa za kwanza unatoa halali, halafu unatafuta mhudum mmoja mwenye tamaa unampiga vi ofa vya Beer huku ukiandaa mazingira ya yeye tu kukuhudumia. Akianza kuchangamka unamsukumia hizo noti mdogo mdogo kama hatasanuka ndio imeisha hiyo. Kazi inakua imebaki kuhesabu changes(Chenchi) nikifika hostel.

Shetani ni mjanja sana. Huwa anakulinda ukiwa unaanza magendo halafu baadae anakutelekeza ukisha kolea. Ndio kilichonikuta mimi, sikumaliza hata mwezi kwenye huo mchongo. Mungu huyu ni wa kumshukuru sana! Nisingekua naandika huu uzi hapa sasa hivi.

Kuna mahali nilikuja kusoma kuwa "Katika magendo yoyote yale, daima epuka kuwafanyia watu wenye hali za chini [kama masikini na wenye disabilities] kwa sababu ina create a very bad luck".Mfano mzuri ni watu wanaoiba vipochi vya wa Mama barabarani au sokoni, nadhani mnajua kinachowakuta wakidakwa! Na ndio kilichoniponza, kwa sababu nilikua desperate sana kupata hela haraka haraka nikaanza kuwafanyia hako ka mchezo mpaka boda boda na dereva taxi. Eh bhana eeh. Kumbe walikua wakifika sheli wanakataliwa pesa zao, wengine mpaka wanaitiwa polisi mimi sijui.

Wakawa wamejipanga siku wakimkamata huyo anayetoa pesa za bandia wanamuua. Mimi sikua nafahamu, nilikuja kugundua baadae huko. Sasa kuna boda wawili ambao nilikua napenda sana kuwatumia katika mishe zangu ambao nilikua nawapa pesa halali, hao ndio walikuja kuniokoa siku nimebananishwa nataka kumalizwa.

Siku yenyewe ilikua hivi. Mida ya jioni nimetoka zangu misele nikapita kijiwe kimoja kipya cha toyo nika scan sura za wajomba nikamuona mmoja kama boya boya hivi nikamchagua anipeleke maeneo karibu na Hostel (Huwa napenda kushukia kwa nyuma kidgo). Sasa kosa la kwanza, sikuwa na pesa ya halali hata moja kwenye wallet.

Sijui ilikuaje nikatumia zote huko nilipotoka halafu sikukagua kabla sijapanda boda. Ile nimeshuka si nikampa jamaa ten. Akaanza kuikagua akakuta ni bandia, akanikwida shati faster. Akasema wewe ndio tulikua tunakutafuta. Nikawa nabishana naye pale kwani vipi, kama ni bandia huenda hata mimi nimeshikishwa nikatoa wallet nikachomoa ten nyingine kumpatia alivyoicheck nayo ni bandia. Mama yangu!

Akapigia simu washkaji wa kijiweni na wao wakapigiana simu na wengine wakajaa pale. Mimi najifanys sielewi nimepanick najisachi kila mahali. Akaja jamaa mmoja akasema huyu mnamuhoji wa nini nikapigwa kofi moja la maana mpka nikajikuta niko chini. Nikaanza kulia kwa huruma. Wahuni wengine wanasema litafutwe tairi nichomwe. Ghafla mmoja kati ya wale jamaa naowatumiaga mara nyingi akawa na yeye amefika eneo la tukio. Hapo nimesha shikwa shikwa sana mpaka shati limechanika. Sura yangu imeanza kufanana kabisa na ya mwizi. Moyoni mwangu nimeshakubali kuwa leo ndio mwisho wangu!

Jamaa kuniona si ndio akawambia mbona huyu ni mwanafunzi wa chuo namchukuaga sana. Boda wengine wakakataa kata kata kuwa hakuna huyu ni jambazi hakuna kutetea. Wengine wakataka ninyang'anywe pochi waangalie ID. Ndio wakaona kweli mimi ni mwanafunzi. Hapo nimeshalia nimechoka, nawambia mimi sio mwizi jamani, mtaniua bure tu, nawaelewesha kuwa nilikua na shida nikaamua kuuza simu yangu ya kupangusa nahisi wale jamaa niliyowauzia ndio wamenifanyia huo mchezo hata mimi sielewi kama ni bandia.

Wakanichukua wakanipeleka kituo kidgo cha polisi hakikua sana mbali na pale. Nikaandika maelezo yangu na wao wakaandika maelezo yao. Sikumaliza hata siku tatu jamaa yangu akaja na wenzake wawili kuniwekea dhamana. Mambo yalikuja kuisha lakini baada ya hilo tukio na jamaa yangu akaachana na hayo mambo kabisa.

Bado nakumbuka vile nilikua najuta na kusali kule kituoni. Kumbe kufa ni kitu kidogo sana. Nikasema nikitoka hapa naenda nyumba za ibada kutoa sadaka ya shukrani. Washkaji walivyoisikia issue yangu, waliniambia nina bahati sana. Lazima kuna kusudi la Mungu katika maisha yangu ndio maana nimeponea kwenye tundu la sindano.
 
Kwenye Maisha tunajifunza kutokana na makosa na makosa yanaleta majuto kabla ya funzo.

Aidha ufanye kosa kwa siri au hadharani, ni lazima likugharimu kwa namna moja au nyingine na hivyo kupelekea majuto...
Umenikumbusha kisa kimoja sema hawakukamatwa, hizo documents huwa zinafanyiwa editing to na software za Adobe. Jamaaa alikuwa anataperi wazungu.

Hivyo anafanya malipo ya dollars 200 Kisha documents ya benk inafanyiwa editing inasoma $4000. Etc. Ilikuwa kwenye malipo ya gold serikalini.

Hivyo anaenda kulipa za gram 20 Kisha mzungu anaambiwa nimekusanya grams 2000, Ili amtumie pesa. Siku ya siku jamaaa katoroka na simu kuzima. Nilishangaa kuona Hadi list za NBC bank nazo zinafanyiwa editing.
 
Wakati bado nipo chuo kabla ya msala wa Receipt fake.. ilikua ni mwaka wa pili kama sikosei sem ya pili..

Hii story kama mhusika yuko humu JF atanijua rasmi mimi ni nani. Ila hakuna shida, cha kuogopa ni kifo pekee na bado kidgo kingenikuta...
Mmmmh we jamaa misala yako si ya kitoto[emoji848][emoji848]

Na kila mchongo lazima udakwe
 
Sitakuja kusahu aisee maana mie nilililelewa na mzazi mmoja bimkubwa, mshua enzi hizo mambo mengi hivyo bimkubwa akajitaa so mshua akaanzisha familia yake nyingine ambayo aliipa thamani kubwa halafu ukizingatia na mshiko mrefu wa dili zake za mbao.

Sasa bimkubwa akifight sana mpka nikamaliza chuo mwanzoni mwa 2000, mshua kule madogo walizingua wote kwenye elimu halafu kwetu hakuwa anahudumia chochote sio kwa kuambiwa ni kwa kuona kabisa, alikata networks baada ya muda mambo yakamuendea kombo hapo tayari nipo kwenye ajira.

Akaanza kunitafuta nimpe sapoti ya kiuchumi nilikuwa Nampa kimtindo bila kinyongo ila nguvu kubwa niliwekeza kwa bimkubwa, mshua akajua hilo akaenda kumkoromea bi mkubwa kuwa kwanini mie nampendelea sana yeye kuliko yeye mshua?

Hakika sintasau na hakika najutia maana hamaki niliyokuwa nayo nilienda kumuwakia mshua tena kwa facts aache kabisa kumzonga bi mkubwa ila baadae nilijutia sana maana mshua alikuwa mdogo sana hali hiyo ikapelea pressure kupanda ila Mungu ni mwema yupo poa ila alishakuwa mgonjwa mgonjwa ambapo moyoni najihisi hatia kuwa nahusika na ugonjwa wake.
Angevuta ingekuwa bonge la msala...Mungu ni mwema...
Mkuu nilicho gundua maugomvi ya wazazi jua kuna upande una makosa na sisi kama watt wao wana tusisha sana,Na wazazi nao wanatupotezea kitu si sahihi.
Baadae huko wanajirudi na kuona hatuwajali...
 
Miaka mingi nyuma ya ujana nikiwa field ile kwenye halmashauri moja hivi mimi na mpenzi wangu/girlfriend kutoka chuo kimoja.

Tukagombana nikamnunia kwa wivu akaniomba tutoke out nikakataa yeye na marafiki zake wakaenda saa sita usiku napigiwa simu na rafiki yake njoo....

I wish nisingemkatalia kutoka out R.I.P my angel naamini asingekutana na yaliyomkuta, ulinipenda sana nakiri sikujali hisia zako.

Kifo ni fumbo kubwa.

Tuwajali Sana wanaotupenda, life is too short.
Je!Umesha bahatika kupata mwingine wa kukupenda kama yule alietutangulia?
 
Ivi sisi watoto wa kiume na uwizi qu udokozi uko kwenye damu nn?

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Hamna uko peke yako mkuu.
Tofautisha watoto wa kiume na wanaume.
Mwanaume haibi bali anatafuta kwa nguvu zake na kula jasho lake.

Kuiba sio uanaume ni utoto au subiri dunia ya wanaume ikufunze madhara ya kuchukua kitu cha mwanaume kilichotafutwa kwa nguvu, damu, jasho na akili ndio utajua maana ya uanaume.
 
And Another!

Katika harakati za kutafuta Ugali nilijikuta nimeomba kujiunga na jeshi la JKT. Nikatupiwa Kigoma, kule Bulombora 821KJ.

Nikapigishwa jaramba na kulishwa vumbi huku nikitazama ziwa Tanganyika kwa ukaribu kabisa lililozungukwa na mawese ya kutosha. Ruka Juu, Kanyaga Chini kwa nguvu mpaka mguu utoke nje ya kiatu.


Mikesha ilivyozidi nikaona hapa nitakufa. Nikaanza harakati za kutafuta nafasi ya kulala vizuri maana zile Dakika 5 unazopewa za kulala hazitoshi kabisa. Nikaanza kutafuta machimbo. Wenzangu wakienda mkesha, mimi najipeleka porini. Siku nyingine nakutana na ma afande na wao wamedoji kwenda lindo wananitimua najikuta nimerudi kulala uvunguni.

Tabia yangu ya kujizoesha kulala ikaanza kunigharimu. Ikafika mahali nikawa siwezi kabisa kwenda kukesha hata siku moja. Nikaanza kuona hadi uvivu wa kwenda kulala mbali na anga letu. Nakumbuka nilikua Eagle Coy.

Siku hiyo nimelala uvunguni nakoroma kabisa, saa ngapi afande asiingie ndani kutafuta watoro. Si akaniskia navyokoroma kule chini ya kitanda. Dah sitasahau hiyo kipigo niliyopewa. Nakumbuka al manusura nipoteze jicho. Maana vile vitanda vimechomelewa kwaiyo kuna kama vichuma flani hivi kama nondo vimejitokeza kwa juu, alinibamiza kichwa kwenye kile kitanda ile nondo ikachubua kidogo pembeni ya jicho.

Sijui nilipata wapi ujasiri nikamsukuma pembeni nikasogeza kioo cha dirisha nikarukia nje nikaanza kukimbia huku nachechemea machozi yananitoka ya kutosha. Jamaa nadhani aliniangalia navyokimbia kwa tabu akanionea huruma akaamua kuachana na mimi huku akisema "Nitakuua Mbwa Wewe".

Nilivyofika walipo wenzangu kwenye mkesha nikapokelewa tena na adhabu za kubiringita na kukwepa ndege za kivita. Dah.. nilihisi mwisho wangu umefika, nikasema kwa sauti "Nakufa" huku machozi yanatoka ili hata jamaa anionee huruma lakini wapi. Yeye kakazana kunioshea na kunifanya mfano kwa wengine. Saiyo pumzi imekata, maumivu kila mahali, machozi yameshatoka mpaka yamekauka, siwezi kuongea tena. Ni kwa Neema za Allah pekee nilifanikiwa kuona tena Jua siku iliyofuata maana nilikua nahisi kabisa nakufa. Hali yangu ilikua mbaya sana!

Sikuwahi kujuta kwenye maisha yangu kama hiyo siku. Nililaani uamuzi wangu wa kwenda huko. Kile kitu kilinikaa sana moyoni kwa muda mrefu. Niliona kabisa huku sio kwangu. Course ilivyoisha, wakati wengine wanasikilizia kwenda JWTZ na Polisi, mimi nikaandaa nauli yangu, nikavizia ule muda tunaotumwa kwenda town...nikatorokea huko mazima na nikaapa sitarudi tena. Ikawa imeisha hiyo!

Kwa kweli mambo ya Jeshi yana watu wake. I was not one of them!
Hahahahaha 821kj, mtu unaenda kudoji ziwani unarudi mda wa mzabuni , ikifika muda wa bustani unazama tena ziwani. Balaa linakuja muda wa kufoleni ..watu wako na namba zao.
 
😂😂😂😂 Sijui nifanye Siri 🤔🤔au nimwage🤣🤣..wanaumeeee qu........e
Na wewe pia.

Uliyataka mwenyewe hakuna kitu kinakuja tuu we ulkua unadhani dunia hii n wewe tuu ndo ulikuwepo ndo ujipange sasa
 
Aise nikimkumbuka yule mwanamke naishia kujuta kwa nini nilimgegeda siku ile....ndio safari yangu ya arv ilipoanza[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kitu najutia ni kusoma chuo na life la chuo kwani nilikutana na maisha ya ovyo kabisa mazila ya kila aina nimegombana na watu wa karibu nimejuana na watu wengi hawana msaada .Nimekutana na watu wabaguzi



Yaani daily nilitamani kumaliza nihame baada ya kumaliza nikaondoka hata mwezi sijakaa nikapata mishe nikarudishwa tena huku dar nakutana na watu wale wale yaani sipendi nimeandika barua nihame mji imeshindikana

Group la chuo nilileft kitambo tangu mwaka wa pili ikawa nawasiliana na CR maana mtu wangu wa karibu sana.
Ni kama nakupata hivi. Tunafanana. Una ulemavu wowote?
 
Niliiba Matofali ya mwalimu Nyerere palee mwitongo wkt huo nikiwa na Mjomba wangu!!ila mjomba ndo aliniingiza mkenge Basi bana askari ana akili sana alijifanya haja tuona kabisaaa!!..... tukaenda tukarudia mara kibao!! kwa akili za utoto nilidhani ni kawaida.

kuumbe mwenzngu yule anaiba na mie namsaidia kuiba!! ........na uzuri ni kwamba Julius alikuwepo wakati huo!!! ...akatukamata kiulainiiii!!

tukapelekwa kwa julius Live.......mengi yalifanyika pale .........ila yule Mzee alikuwa ni wa ajabu sana narudia tena, sijakosea alikuwa wa ajabu mnoooo sana tuuu!!... .......lkn to cut long story short ndo ukawa mwanzo wa mie kusaidiwa shule tena nzuri sana abroad nilishangaa mpaka leo hapa nilipo bado nashangaa!! ......na marehemu kazi hii ilifanywa na Rais huyo huyo!..... hapo ni kwa kifupi sana nimeitoa hii!
Tobaaa kumbe we ni mhenga eeeh? Nimeghairi kukutongoza. Ni bibi kabisa
 
Mkuu ni mengi sana kwanza washkaji tulitoka advance tukaaa getto moja tulikuwa tunapendana ila tuligombana yaani mikosi mpaka leo hatuko pamoja

Mwanangu mmoja alikuwa mtu wa karibu alitaka kujiua kisa kuachwa na demu wake na kuolewa akadisco nikawa sina mtu was karibu na alivyodisco akarudi kwao mbeya yaani balaa

Mpaka nafika mwaka wa tatu crew yetu niliku2a alone na getto naishi mwenyewe hamna sapot wau tumegombana wengine wamecarry yaani mpaka [emoji310] graduation hakuna Ile hamsha hamsha
Uliishi maisha ya ukiwa sana
 
yaani wewe ni mi mi kabisa mkuu-mimi jana tu nimetoka kuwakiana na mmoja hapo Bungoni....kila kitu nalipa kuanzia ada,nguo,sikukuu,chakula etc,..halafu anawapigia simu rafiki zangu eti sihudumii mtoto.

mbaya sana
Nina mengi ya kuandika juu ya hili kifup Wewe n mm kabisa

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom