Kisarawe: DC Petro Magoti ameutaka Msikiti unaotoa elimu ya dini kwa watoto 96, kuwarudisha walipowatoa sababu ya Mazingira Mabovu ya malazi

Hao watoto watakuwa wamemaliza darasa la saba na hawakufaulu kwenda sekondari,ndio maana wazazi wakawapeleka huko.Serikali inatakiwa kuja na majibu kwa watoto wa namna hiyo kwa nchi nzima.
 
Siku chache zilizopita yalitokea Dodoma n Longido. Kuna uwezekano hii Biashara ipo sehemu nyingi nchini! Kwa Nini hili linatokea na lengo lao Nini! Wazazi wanelewa wanachokifanya! ?
 
Siku chache zilizopita yalitokea Dodoma n Longido. Kuna uwezekano hii Biashara ipo sehemu nyingi nchini! Kwa Nini hili linatokea na lengo lao Nini! Wazazi wanelewa wanachokifanya! ?
Dr.Gwajima wizara ya maendeleo ya jamii na watoto, akishirikiana na wizara ya mambo ya ndani wafanye msako nchi nzima kubaini vituo kama hivi, itawasaidia watoto na wazazi wao pia. Watoto hawawezi kufahamu madhara ya hili jambo, ila wazazi walaumiwe na kuonywa.
 
Mzee hata hili bado, unatumia. Hituba ya Kitwana Kombo ya miaka 40 kasoro iliyopita?! Hivi wewe unaweza kumpeleka mjukuu wako wa miaka 13,14 kwenye program kama hii Kwa Mazingira Yale! Nioneshe Chuo au Shule ya Biblia yenye Wanafunzi Watoto!?
 
Sheikh ametoa ushauri bora kabisa.

Namshauri Rais Mama Samia atengue uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Petro Magoti na amrudishe huko UVCCM huku kwenye uongozi atakuja kumfitinisha dhidi ya Uislam na Waislam kwa ujumla.

Petro Magoti anachangia kuzua taharuki na kuvuruga amani ya nchi ya Tanzania. Tanzania watu wa imani zote wanaishi kwa maridhiano na kwa amani.

Ila chokochoko za Kidini zinaweza kuivuruga amani ya nchi.
 
Afadhali hii inanhata kivuli , zipo za chini ya miti au juani! Lakini sio Shule za Bweni!
 
Inasikitisha sana,huyu Mzee kuendelea kutumia hii hotuba,kufanya reference ya jambo tofauti! Ndugu zetu Waislam watieni baadhi ya Waislamwrnsenu tongotongo kumekucha! Wengi wenu mnawapeka watoto kusoma Shule za Kanisa au Shule za Kiislam zenye Mazingira Bora Kabisa! Kuna kundi dogo bado wako.o nyuma!
 

Tanga palikua na vyuo rasmi vya kiislam kwa miaka mingi. Havikua na shida.
Shida ilianza pale walipoibuka wanaharakati wanaochanganya dini na siasa na kuwafundisha watoto wadogo bila kujali maisha yao ya baadae katika dunia yenye ushindani mkubwa wa sayansi . Hata kwenye mihadhara mashehe wenye elimu kubwa ya Darasani/Dunia wanaheshimika zaidi kwa uwezo wao wa kufafanua mambo ya dini Kizazi hiki hata huko Uarabuni hapo huko kidini zaidi ya uchumi ndio maana Saudi Arabia hawajitengi na Taifa dhalimu la Marekani kwa sababu ya kuangalia laslahi yao.

Hakuna mtu atamchagua shekhe mkuu asiye na elimu ya kidunia. Huku ni kuwadanganya hao watoto na kuja kuwatumia kujitoa Mhanga.

Hii hata kwa Wakristo ipo umaskini na kukosa Elimu sahihi ya dini ni mtaji mkubwa sana wa watu matapeli wenye tamaa ya mali. Watu wanauza pipi na maji na chumvi makani makanisani .

Tofauti ya Wakrsto na Waislam ni kwamba Waislam wanafanya kwa siri na hawaweki hadharani ili atu wajue nini malengo yale.

Wakrsto wanaweka wazi kwenye tv hata kama ni mazingaumbwe . Mtu ataenda kwa hiyari yake mwenyewe bila kushawishiwa kwa pesa kisirisiri zaidi yeye atauza mali zake na kuwapelekea.

Hatuoni hizo kozi au shule zikitangazwa kuwa zitagunguliwa lini na masomo yake ni yapi na wanafuata mtaala upi na nana anasimamia hiyo mitaala kama ni BAKWATA au ni Wizara ya Elimu au ni nani?
Kwa nini inakua ni siri . Watoto wanatokewa Kenya kuja kusoma Porini kama Maisha Plus . Kuna jambo nyuma yake na halina tija kwa Taifa zaidi ya kakikundi ka watu kujinufaisha kisasa na kiuch
Hakuna Mtanzania anayebaguliwa na serikali kwa sababu ya dini n hakuna dini 8nyopendelewa na serikali .
Hizo ni propaganda zinazoratibiwa na Mahaidi na fedha nyingi sana zinatolewa kwa sababu ya hizo propaganda .

Magaidi siku zote huwa na watu ndani ya mifumo ya utawala.

Hii nchi imetawaliwa na watu wa dini Mbili kubwa yaani Waislam na Wakatoliki tu., na madaraka ya Rais ni makubwa sana. Memorandum of Understanding haikuwa kwa ajili ya Wkristo peke yao ,huo ni upotoshaji unaotumiwa na mawakala wa ugaidi kufakanisha jamii kwa malengo ya kuleta chuki kwenye jamii. Hakuna Kanisa linalojengwa na seriakali wala Msikiti lakini ni Wazi kuwa kwa upande wa uislam serikali hua inwatafutia mpaka wafdhili kwa ajili ya kujenga misikiti. Na hakuna shida kwa sababu ni maamuzi na maombi yao.

Hakuna Hospitali au shule ya Kanisa au Bakwata inayojengwa na serikali kwa sababu serikali yenyewe haina fedha za kujenga shule zake.
Sasa hiyo MoU ya kuwapendelea wakristo peke yao na kuwatenga Waislam inatoka Wapi?
Fedha Mtriloni yanayoruhusiwa kuingia kusaidia uislam toka uarabuni zingetumiwa kuleta miradi ya maendeleo kwenye taasisi za dini za kiislam leo hii hakuna mtoto wa kitanzania angesoma shule ya Kata mana shule zingejenhwa kila kona ya nchi na mahospitali .
Kuna watu wanajinufaisha sana na masuala ya Ugaidi kupitia dini ya kiislam na wapo mpaka ndani ya serikali ndio maana fedha zinazoingizwa na Waarabu hazifanyi shughuli za maendeleo ya taasisi za dini na mbaya zaidi zinatumika kuhujumiana na kukusanya watoto wa maskini kwenye mazingira magumu na picha zinatumwa kuombamisaada.

Haiingii akilini kuwa waislam hawana uwezo wa kujenga shule bora na mahospitali wakati katika Mabilionea kumi Tanzania hakuna Mkristo hata mmoja wote ni Waislam.

MoU ilikua ni makubaliano kati ya Serikali na Taasisi za dini zinazotoa huduma kwenye jamii kuwa pale penye mradi wa dini sehemu fulani basi serikali isiweke huduma kama hiyo kushindana na taqsisi hiyo iliyoanzisha na waumini wenyewe kwa michango yao au sadaka zao bali serikali iweke utaalamu wake au fedha za kuboresha huduma hiyo. Hii ni kwa dini yoyote hata kama ni Upagani alimradi kuna huduma inatolewa inayopaswa kutolewa na serikali.

Mfano Hospitali ya Kanisa kama KCMC ni hospitali ya rufaa kanda ya Kaskazini kulingana na ukubwa wake. Inahumia watu wa dini zote na inaajiri watu wa dini zote na wanapona au kufa watu wa dini zote bila ubaguzi. Na kama kuna ubaguzi ni mtu binafsi lakini sio sera wala mpango wa kanisa wala serikali. Halikadhalika hospitali ya Ndanda,Nyangao ,Bugando n.k. Maeneo hayo wakakubaliana kuwa serikali isijenge tena Hospitali kwa sababu hizo za kanisa zitakufa kutokana na ukweli kuwa hawana ruzuku ya kutoa huduma bure kama serikali. Wakati huo huduma za afya zilikua ni bure kwenye hospitali za Serikali. Hivyo ili zile za binafsi na taasisi za umma zitolewe bure kwa watu maskini ni vyema serikali ikatoa fedha au kupeleka madaktari wake pale ili wananchi maskini wapate huduma ya afya bure. Huo ukawa msingi wa MoU.

Hata Waislam wakijenga Hospitali eneo fulani bado serikali ingepeleka Dawa na wataalam na ruzuku ili ihudumie wananchi wake. Kwa sasa Bima ya afya imekwenda mbali zaidi mpaka hospitali ya mtu binafsi na Famasi bila kujali ni wa dini gani?
Wakristo wanachanga sana kujenga na kuanzisha Miradi yao wenyewe jambo ambalo waislam hawakatazwi kufanya hivyo.

Ushahidi upo wazi Chuo cha Kiislam cha Morogoro wanafunzi wake wanapata milopo sawa na wa SAUT na UDSM . Hayo ndiyo matunda ya MoU. Lakini ukiwaskiliza mawakala wa Ugaidi wakiwa wanasimilia na kupotosha MoU utafikiri ni lijitu likubwa linalogawa pesa na chakula kwa Wakristo. Sijui aliweka Lowasa akiwa waziri mkuu sijui nini !! Kuwajengea tu watu roho mbaya na chuki bila sababu. Hivi Waziri mkuu anaweza kufanya MoU ambayo haiwezi kuvunjwa na Rais. ?
Yaani Rais alikua Muisam wakati huo JK aone waziri mkuu anafanya lakubaliano ya kugandamiza dini yake halafu na yeye ayakubali halafu baadae atume watu watu waseme kuwa wakrsto wanapendelewa. Hivi unajua kuwa hakuna fedha zinazoweza kutoka na kwenda kokote kama Rais hajakubali?
Lowasa alitumwa tu nenda kawasikilize lakini maamuzi yoyote ya mkataba wa kudumu yanakuwa ni ya Rais.

Kule Moshi kuna Waumini wa dini ya Kikristo juzi wamechanga fedha wakakarabati barabara ya maeneo yao . Seeikali ilitoa wataalam toka Tarura sasa hapo wamependelewa au wameipendelea serikali yao badala ya kuandamana na kuishinikiza ifanye majukumu yake.

Iko hivi : Ubepari ni Unyama ; Kuna watu toka ndani na nje ya nchi ,walioko madarakani na nje ya madaraka wao wanatafuta mafanikio yao kwa namna yoyote hata kama jamii itaangamia. Hawa ndio wanaofadhili vita na ugaidi duniani . Wapo Wakristo kwa upande wa magharibi na wapo Waislam kwa upande wa nchi za Kiarabu. Hawa hawajali mila ,tamaduni na desturi za Mafrika zaidi ya malengo yao na mila zoa. Kwa mfano mimi binafsi sinufaiki na chochote kama Mkrsto kwenye taasisi na miradi ya dini ya Kikristo zaidi ya michango isiyokoma katika miradi hiyo.

Sasa akitokea gaidi mmoja akaanza kuafarakanisha watu na kuwadanganya kuwa wakrato kama dini wananufaika na miradi hiyo ni muongo mkubwa sana. Hiyo miradi ina mpaka ufisadi ndani yake na mikopo mikubwa toka kwenye mabenki. Hakuna Mkrsto anyepunguziwa gharama za matibabu ya figo kwa sababu tu ni mkristo . Hakuna. ! Ukiugua uwe ni mkrsto uwe ni muislam utalipia gharama za matibabu bure.

Juzi kuna Taaisisi Moja ya kiislam ilitoa ngombe zaidi ya elfu tatu kwa ajili ya kuchinja kwenye idi. Ng'ombe elfu 3 ni karibu bil.2. Sasa hapo kupanga ni kuchagua. Kama watu wanapanga zaidi ya peponi kama vile wanaiandaa wao basi waache. Kuna watu wanatoaga maburungutu ya pesa wakati wa sikukuu ya Iddi . Ni maamuzi yao na imani yao kuhusu kesho yao sasa kuwapangia kuwa wajenge hospitali haiwezekani mana anayesimamia taasisi hiyo ana malengo yake.
Kuna wakrsto wanatoa laki tano ili wakamuone Nabii . Na Wanafurika kama nyuki lakini ukiwaambia wajenge shule ya kanisa hawaoni kuwa kuna kubarikiwa na kuleta maendeleo ya jamii nzima leo na kesho. Nabii anachukua pesa anakwenda kununua Hammer na Helkopta binafsi . Kesho anaongiza Waumini kulalamikia MoU inawapendela Wakatoliki .

Ubinafsi ni kitu kibaya sana.

Leo hii ungenipa Urais hospitali na shule zote za dini na serikali zingekua sawa ili kila mtu achague mwenyewe pa kwenda.

Wanasiasa wanachota fedha za umma bila kujali dini zao halafu wanazitumia kuweka machawa wa kueneza propaganda za kuwahawa watu kuwa umaskini wetu umetokana na dini fulani kupendelewa. Badala ya kuwawajibisha Wanasiasa na Watawala kwa kushindwa kuleta maendeleo tunasema kuwa serikali inapendelea dini fulani. Cha ajabu huyo anayeeneza hayo ni Chawa wa serikali hiyo inayopendelea dini moja na eneo analotoka tangu uhuru hakuna diwani wala mbunge wa chama cha upinzani na yeye mwenyewe ni chama kilichotawala tangu uhuru na MoU imewekwa na serikali yake na rais wa Dini yake.

Hqpo ndipo chuki zinapojegwa bila sababu.
 
The best,
Hapakuwa na historia ya kweli ya uhuru wa Tanganyika hadi mimi niliponyanyua kalamu na kuiiandika.

Nimepokea hadi sasa nishani nne kwa kazi yangu hii ya mwisho mwezi April mwaka huu.

Niko hapa JF nasomesha historia mpya ya Mwalimu Nyerere na TANU na nimechaguliwa hapa JF Mwandishi Bora mara mbili mfululizo 2021 na 2022.

Au hulijuwi hili?
 
Ungeweza kumpeleka mwanao akaishi kwenye mazingira hayo?
Magni...
Hayo ni mazingira ya kawaida sana kwa familia nyingi nchini petu.

Kuna picha nyingi za shule mbovu au hujaziona?

Shule hizi hazijavamiwa usiku wa manane na DC wala Kamati ya Usalama.
 

Unapoteza Muda wako.

MTU mlalamishi hakosi visingizio
 
Kama umeangalia video hakuna aliyeachishwa shule hata mmoja wapo ambao bado wako primary na waliomaliza lasaba wakafeli, ninachopinga mimi ni watu kuleta dhana potofu tu.

Mkuu wa wilaya kapafungia kwakuwa mazingira hayafai watoto kuishi ambapo hajafanya vibaya lakini anasahau kuna shule za serikali zina mazingira mabovu kuliko hayo
 
Magni...
Hayo ni mazingira ya kawaida sana kwa familia nyingi nchini petu.

Kuna picha nyingi za shule mbovu au hujaziona?

Shule hizi hazijavamiwa usiku wa manane na DC wala Kamati ya Usalama.
Mkuu hapo ni familia!? Hizo.Shule mbovu wanalala au kuishi hapo! Mbona unajenga hoja nyepesi sana Kwa level Yako! Ndio maana huwa tunakuambia unasukumwa na Udini! Ukitaka kujenga hoja yoyote ya uduni wa maisha ya Waislam ..unarejea ....kuwa ndio waliompokea Nyerere, mara walimpa nyumbaya kuishi
Mara ulete Hotuba ya Kitwana Kondo, au kurejea MOU ...Je Mazingira ya Elimu Kwa Sasa yapoje?!
 
Nafkiri DC hana shida wala tatizo na elimu ya dini kutolewa kwa vijana, kwani ni jambo jema,yeye amejikita katika mazingira mabaya katika eneo husika kwa watoto husika,pia kituo kutokusajiliwa na serikali kukaguliwa wala kufahamika hata na Sheikh wa Mkoa ili kukidhi vigezo, hata Sheikh mwenyewe kakiri mapungufu ni makubwa.kwa hiyo hatua alizochukua ni sahihi kabisa, kwani huwa lolote la hatari kama mlipuko wa magonjwa au baya lolote huwa likitokea serikali ndio inabeba lawama, na kumbuka hakuna jambo sensitive duniani kama linalohusu watoto haswa jambo baya linapotokea, so ni jukumu la serikali kulinda na kuzuia kabla jambo baya halijatokea. Bravo Jasusi PM
 
Umefunga mjadala...nyongeza ...Mazingira Kam hayo yanachochea sana Watoto kufirana!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…