Kisutu: Kesi ya Erick Kabendera yaendelea. Jamhuri yaweka kisiki Erick kushiriki msiba wa mama yake mzazi

Kisutu: Kesi ya Erick Kabendera yaendelea. Jamhuri yaweka kisiki Erick kushiriki msiba wa mama yake mzazi

Mkuu usiandike ili uonekana ya kuwa na ww umeandika rudi nyuma tangia awamu ya kwanza hadi ya nne na unitajie mahabusu m1 tu aliyerusiwa kutoka magereza kwenda kuhudhuria msiba wa mama, baba, mke au mtoto wake.

Au tangia tupate uhuru hakuna mahabusu aliyefiwa na wazazi wake? Hata kwa nchi tunazozisifia kuwa zina demokrasi hakuna mahabusu ambae kesi yake ni unbaillable ambae amewahi kutolewa magereza na kwenda kuhudhuria mazishi.

Sent using Jamii Forums mobile app

Kama huyo mtu anatuhuma za msingi sawa, sio hizo siasa za kishamba na kukomoana. Ni nani asiyejua kuwa Kabendera anakomolewa?
 
Hizo sheria zinazobadlika unazisema za nyumban kwenu au?
Kama jambo hulielewi bora ukae kimya

Sent using Jamii Forums mobile app
Unawezavipi jitofautisha kati ya civilized and educated society and uncivilized and uneducated society kama unamiliki sheria zilizopitwa na wakati.
Unamshikilia mtu miaka 7 ushahidi haujakamilika then hukumu inatoka alipe fine laki 5,nini hii,hio miaka 7 hizo gharama za kumtunza kwa miaka 7 si zimezidi hio laki 5 pia huyu mtu angechangia ngapi kuinuia uchumi si zaidi ya hio laki 5?.Thus haya mambo kwenye modern na civilized society huwezi yakuta.
 
Sikuona sababu ya haya maombi.
huku ni kuonyesha unyonge kama mwanzo mama yake alipoonyesha unyonge kuom,ba msamaha wakatio ni jambo la kisheria.
ukwlei ni kuw akesi ipo mahakamni basi wapambane huko huko hakuna sababu ya kutafuta huruma.
hata kama ni ya kubambikia, apige moyo konde apapambane.
 
Akome kiranga ,wako wapi wale waliomtumia na kumvimbisha kichwa?,

Vijana msicheze na Dola
Erick Kabendera mwandishi wa Kujitegemea wa Habari za uchunguzi inaendelea leo Mahakama ya Kisutu.

Kabendera anashtakiwa kwa Makosa matatu ikiwemo kukwepa Kodi, Utakatishaji Fedha na kujihusisha na genge la uhalifu.


UPDATES

MAHAKAMA YAOMBWA KABENDERA KUMUAGA MAMAKE


HOJA SITA ZA UPANDE WA UTETEZI KWANINI KABENDERA APEWE RUHUSA KUSHIRIKI MAZIKO YA MAMA YAKE

Jopo la mawakili wa Mwandishi wa habari wa kujitegemea Erick Kabendera, wakiongozwa na Wakili Jebra Kambole wamewasilisha hoja sita mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu Janet Mtega kwa mshitakiwa kupatiwa ruhusa chini ya ulinzi ili aweze kushiriki Katika maziko au kutoa heshima za mwisho kwa mama yake aliyefariki hivi karibuni.

1. Kutoa heshima za mwisho ni haki ya msingi ya binadamu. Wakili ameeleza kuwa Kabendera ana haki ya kuwa na kuheshimu familia pamoja na haki ya faragha hivyo kuna umuhimu kwa Kabendera kushiriki Katika kutoa heshima za mwisho kwa mama yake.

2. Erick Kabendera anatakiwa adhaniwe kuwa hajatenda kosa mpaka pale mahakama itakapothibitisha kuwa ametenda kosa na kumzuia kushiriki mazishi itakuwa ni adhabu ya Kinyama kwa Kabendera.

3. Tangu Mshitakiwa amekamatwa hajaonesha nia ya kutoroka au kutaka kufanya vurugu hivyo hakuna uwezekano wa mtuhumiwa kutoroka Kama atapatiwa ruhusa

4. Mashitaka anayokabiliwa nayo mshitakiwa hayahusiani na uvunjifu wa amani hivyo Mahakama itilie maanani ombi Hilo

5. Kama Mahakama ilitoa amri aende mahabusu hivyo Mahakama Ina uwezo wa kuamua ombi hilo kwani kama mshitakiwa pia aliweza kupelekwa mahakamani haitashindikana kumpeleka kanisani kumuaga mama yake.

6. Ruhusa ya Kabendera kuhudhuria mazishi Jamhuri haiwezi kuathirika



MAJIBU YA UPANDE WA SERIKALI

Jamhuri yampa pole nyingi kwa msiba wa mama yake mzazi, Bibi Verdiana Mjwahuzi. Pia Jamhuri imepinga hoja za utetezi wakidai Mahakama haina Mamlaka wala DPP hajaipa mamlaka ya kutoa maamuzi hayo.

Wakili wa Serikali, Simon Wankyo amesema...

"Hata sisi tuna masikitiko makubwa na tunampa pole nyingi Kabendera kwa kufiwa na mama yake mzazi, lakini mahakama isifungwe mikono kwa maombi yaliyowasilishwa ya kutaka mshtakiwa kushiriki Msiba.”

Mheshimiwa Hakimu katika macho ya kisheria mahakama yako haina mamlaka ya kusikiliza maombi hayo kwa sababu kesi hii ni ya uhujumu uchumi, licha ya kuwa hata sisi tuna masikitiko makubwa lakini tunaiomba Mahakama yako isifungwe mikono.”



Pia soma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kupel
Kitu gani kinasababisha upelelezi kutokukamilika?.
Kama kweli waliona makosa kwake,kwa Nini wasioneshe ushahidi usio na Shaka ili kijana ahukumiwe?.
Kuna Nini kinachowazungusha upelelezi haujakamilika?.
Au walimkamata kimakosa?.
Mkuu wa majaji,Roho wa Mungu akuongoze usimamie hili,mtu akikamatwa tia miezi miwili au mitatu, upelelezi Kama Bado tupilia mbali.


Sijui!
 
huyu mtu ni mshitakiwa mama yake akizikwa hatapata tena nafasi ya kumuona zaidi ya kutembelea kaburi lake ni vema aruhusiwe apate nafasi ya mwisho kutoa heshima kwa mama yake hakuna mtu ajuaye kesho yake
 
Umeshasema mshtakiwa kwa maana bado hajakutwa na hatia.
Vipi ikitokea akaachiwa huru kwa kukosekana ushahidi wa kumtia hatiani.
Usiwe unajitoa ufaham tu mwenzio amefiwa na bi mkubwa wake!

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwaiyo atolewe mahabusu akafanye mambo ya jamii? Je ilishawahi kutokea nchini au Kabendera ni special?
 
Kwani alizaliwa peke yake? Lini mshitakiwa aliwahi ruhusiwa kwenda kwenye mazishi? Au hii iwe special kwa huyu, mwandishi habari? Wakulima je? Wafugaji je?
Tusiishie kusikitika, tuepuke kujiingiza kwenye mambo ya kujitakia. Kulikuwa na kila njia ya kuachana na hayo lakini naona alijivunia ushujaa.
Once a fool always a fool, may the pit of hell open up and shallow you and your jiwe
 
Mkuu tetea uovu maana uko mezani kwa mfalme na sahani yako imejaa mlo wa kutosha, na namna nzuri ya huo mlo ili uweze kushuka utakavyo ni pamoja na kujenga hoja ya kuutetea huo uovu. Hata akina Mwigulu, Nape, Januari nk walikuwa wanatetea uovu enzi za JK wakiwa mezani kwenye mlo kama ww. Ila hiyo warmup inayowakuta hivi sasa akili imewarudia.
Mungu akubariki na akupe maisha marefu, umeongea ukweli mtupu, shukurani kabisa mkuu
 
Back
Top Bottom