Benjamini Netanyahu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2014
- 95,871
- 116,627
Wewe utapata hasara gani?Ushujaa gani unautaka mbele ya sheria. Ukiwa mwizi ukakamatwa, legea usije ukafa kwa kipondo. Subiri huyo mwingine utamsikia na haki yake.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wewe utapata hasara gani?Ushujaa gani unautaka mbele ya sheria. Ukiwa mwizi ukakamatwa, legea usije ukafa kwa kipondo. Subiri huyo mwingine utamsikia na haki yake.
Kwanini Mkuu???Wale jamaa(Seth na Rugemalira) ukiangalia picha zao sa hivi wanafanana na wale manabii wa enzi za yesu.
Picha zao tafadhari,kapige hukohuko walikoWale jamaa(Seth na Rugemalira) ukiangalia picha zao sa hivi wanafanana na wale manabii wa enzi za yesu.
Nani ana shida na wewe CCM?Mimi nilikuwa Kiherehere wa CCM kabla yako kwa taarifa yako KAMWE! sintorudi CCM
Yapo wapi!DPP Sylvester Mwakitalu leo amemuachia huru mfanyabiashara Herbinder Seth baada ya kukiri makosa na kulipa faini.
Mzee Ruge bado amekomaa, tusubiri tuone nini kinaendelea.
Source: Darmpya Blog
Una uhakika kijana?Huyo ndio DPP sio kama yule Biswalo Mganga aliyekuwa anataka Rushwa.
[emoji2][emoji2][emoji2]Ruge kafanana na Burning Spear
Nani kuilipa Standard chartered Malaysia, ni Harbinder au awamu ya serekali zinazo kuja na interest kuongezeka.
Leo 16/06/2021 12:45
Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania (DPP), Sylvester Mwakitalu amesema, mfanyabishara Herbinder Seth anayekabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi, amekubali na kukiri makosa na kulipa faini na leo kama atakamilisha utaratibu ataachiwa huru na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Wakati hapo Jana mahakamani alitokea Seth peke yake je kila mmoja ana msimamo wake? Tusubiri leo baadae
👇🏽👇🏽👇🏽👇🏽
15/06/2021
Serikali yaafiki maombi majadiliano na Seth
Dar es Salaam. Upande wa mashtaka katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Mtendaji wa PAP, Harbinder Seth, umeieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa wamepitia barua iliyoandikwa na mshtakiwa huyo na kufikia makubaliano kwa kile alichokiomba. Seth aliandika barua hiyo Juni 10, kwenda kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), akiomba kukiri mashtaka yake na kupunguziwa adhabu.
Barua hiyo ilijadiliwa kwa siku mbili na upande wa mashtaka na ule wa utetezi na kisha kutolewa mrejesho.
Wakili wa Serikali Mkuu, Marterus Marandu akisaidiana na Ladslaus Komanya jana alitoa maelezo hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi.
Wakili Marandu alitoa maelezo hayo wakati kesi hiyo ilipoitwa kwa ajili ya upande wa mashtaka kuwasilisha mrejesho wa kile walichozungumza kati yao na Seth kwa ajili ya kuimaliza kesi hiyo.
“Kesi imekuja kwa ajili ya kutoa mrejesho wa barua iliyoandikwa na mshtakiwa huyu (Seth), niseme barua tumeshazipitia kwa pamoja na tumefikia mahali pa kukubaliana kuhusu kile ambacho mshtakiwa alikuwa anakiomba na baada ya hapo, tumekubaliana kuendelea na shauri hili,” alidai wakili Marandu na kuongeza:
“Kwa muktadha huo, upande wa utetezi kama hawatakuwa na pingamizi, naomba shauri hili lije mahakamani hapa kesho ( Juni 16) kwa ajili ya usikilizwaji,” alidai Marandu.
Baada ya kueleza hayo, Wakili wa Seth, Melchisedeck Lutema alikubaliana na maelezo ya upande wa mashtaka na kueleza kuwa huo ndio ukweli na ndio msimamo wa pande zote mbili za majadiliano waliyofanya.
Hakimu Shaidi baada ya kusikiliza maelezo ya pande zote alikubaliana na ombi hilo na kuahirisha kesi hadi Juni 16 itakapoitwa kwa ajili ya usikilizwaji au majadiliano ya kuimaliza kesi.
Hata hivyo, jana Seth alikuwepo mahakamani peke yake, wakati upande wa mashtaka walipowasilisha mrejesho huo.
Itakumbukwa Juni 10, Mahakama hiyo ilikubali upande wa mashtaka kufanya mazungumzo na mshtakiwa huyo ya kuimaliza kesi hiyo. Mahakama hiyo ilirihusu majadiliano hayo baada ya upande wa mashtaka kuwasilisha ombi mahakamani hapo la kutaka kufanya majadiliano na Seth na kisha kutoa mrejesho wa kile walichozungumza kwa ajili ya kuimaliza kesi.
Mbali na Seth, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ambao hawajaandika barua ya kukiri mashtaka yao kwa DPP ni aliyekuwa Mwanasheria wa kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), Joseph Makandege na Mkurugenzi wa VIP na mmiliki mwenza wa zamani wa kampuni ya IPTL, James Rugemalira.
Katika kesi ya msingi, Seth na wenzake wanakabiliwa na mashtaka 12 likiwemo la kutakatisha fedha na kuisababisha Serikali hasara ya Dola za Marekani 22,198,544.60 na Sh 309,461,300,158.27.
Hoja hapa ni kwann watozwe faini na DPP? Mahakama si zipo?Acha wivu koo ulitaka wafie hukohuko mkuu vipi bwana!!?
Apelekwe mahakamani. Kwanini atozwe faini na DPP?Ulitakaje?
Tuwekee hapa tuoneWale jamaa(Seth na Rugemalira) ukiangalia picha zao sa hivi wanafanana na wale manabii wa enzi za yesu.
vip mzee, ulitaka singasinga afie jela, si bora ametoa ayo mabilioni Kama FainiAisee
Kwaiyo Bora angeachwa afie jela??? We una akili kuliko team nzima serikalini?!Huu ujinga bado unaendelezwa? Mama sasa hasomeki.
EeeenHeee!Wale jamaa(Seth na Rugemalira) ukiangalia picha zao sa hivi wanafanana na wale manabii wa enzi za yesu.
We unadhani waliemuachia Ni wajinga Kama wewe??!Singa singa intown....sasa ile mitambo pale pameota nyasi....yale ma HOF engines yatahitaji mpunga ww kutosha kuyaamsha na kuyawasha au kuyauza ... Kuna hatari ya kesi inakuja kati ya GOVT na SETH + RUGE na hichi ndicho yule jamaa alikikwepa akaamua kuwahifadhi akiamini kwa mateso na kukosa uhuru natural death itasema nao...