Kitabu cha baba wa taifa katika mjadala Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam 26 Mei, 2022

Kitabu cha baba wa taifa katika mjadala Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam 26 Mei, 2022

Baba yangu as i said, mimi binafsi nakuheshimu sana kwanza kwa UMRI wako na hata kwa maandishi yako; sijapingana kabisa na historia yako unayo iandika na wala sijasema kwamba kile nilicho kisoma shuleni kuhusu historia ya Tanganyika/Tanzania ndio cha kweli, laa hasha! Nilicho kisema ambacho naendelea kukisisitiza ni kwamba, somo la historia huwezi ku prove ukweli wake, nimejerea mambo kadhaa kwamba hata historia ya Mapinduzi ya Zanzibar kile tulicho fundishwa shuleni ni tofauti na tunacho ambiwa na wazee wa Kizanzibar ambao wapo hai to date, nimemtolea mfano mzee Visram Kassam, huyu ni mwandishi mkongwe, nimeanza kuzoma makara zake tokea mwaka 1984 alipokua akiandika gazeti la Mzalendo those years, ameendelea kuwepo akilini mwangu hadi sasa nikiwa na umri wa utu uzima; now coming back to your articles, mimi sijui na sina hakika kama unayo yasema ni ya kweli au na wewe umeongeza CHUMVI, sina proves kwasababu ile ile tu, HISTORIA huwezi kuithibitisha, ni mambo ya mtu kuweka kumbukumbu zake na mwingine anaweza kuzipotosha atakavyo na hasa kama mlengwa unamchukia au unampenda sana, kwa unayemchukia, the law of nature says, "hutayasema mazuri yake hata kidogo, utataka yasijulikane" mfano wako ni kwamba kwenye maandishi yako, huwezi kuzungumzia kabisa kitendo cha Nyerere kunyang'anya shule na taasisi za dini yake ili hata wasio wa dini yake (nimekwepa kusema Waislam ili twende sawa ) ili Watanzania wasome; hilo hakuna sheikh ambaye atalizungumza, lakini ungependa kuwaweka watu unao wapenda (may be wengine nao waliwaficha ili tusiwajue ) ili wajulikane na hapa ndio shida ya somo la historia inapokuja kwangu, NO PROVES. Ingekua ni sayansi, it doesnt matter whether we are friends or not, ukweli wake UPO Maabara. Can site one of the example; mhe rais wa awamu ya tano alipingana sana na actions za kudhibiti CORONA nchini mwake, hadi sasa hivi watu wanamzodoa kwa maneno, lakini tuwaulize kivitendo, alicho kikataa Magufuli, leo wanafanya nini tofauti na alicho kisema Magufuli? Well, dunia anafanyaje sasa tofauti na alichokua anasimamia Magufuli? Hiyo ndio sayansi, unampenda au unamchukia haijalishi, ukweli upo!
Mazindu...
Mimi nazugumza historia ninayoifahamu ya uhuru kwa ''facts.''

Mathalan nakuaambia kuwa katika mswada wa kitabu cha Kleist Sykes ameandika vipi waliasisi African Association mwaka wa wa 1929 na kawataja ndani ya mswada hawa wafuatao kuwa ndiyo waasisi: Cecil Matola (President), Klesit Sykes (Secretary), Mzee bin Sudi, Zibe Kidasi, Ibrahim Hamisi, Seleiman Majisu, Ali Said Mpima, Rawson Watts na Raikes Kusi.

Hii ni ''fact'' haina ubishi na haiwezi kuingia kwenye hayo unayosema kuwa huwezi kuwa na ithibati.

Kleist kaandika na nimekupa ushahidi wa rejea ya seminar paper Idara ya Historia Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam ba kitabu cha John Iliffe.

Sasa hiyo chumvi itatoka wapi?
Kwa Iliffe au kwangu?

Taarifa hii hakuna katika kitabu walichohariri Temu na Kimambo, ''A History of Tanznaia,'' (1969) wala katika kitabu cha Chuo Cha CCM Kivukoni (1981)wala katika wasifu wa Julius Nyerere (2020) kitabu kilichoandikwa na Prof. Shivji at. al.

Kuhusu elimu zipo ''facts.''

Serikali iliivunja EAMWS wakati wanajiandaa kujenga Chuo Kikuu mwaka wa 1968 na jiwe la msingi Nyerere ndiye aliyeliweka.

Katika miaka ya 1970 Organisation of Islamic Conference (OIC) walitaka kujenga Chuo Kikuu Tanzania, serikali ikakataa kutoka kibali OIC wakaenda kujenga chuo hicho Mbale, Uganda.

Halikadhalika shule za Kanisa zilitaifishwa lakini Waislam hawakupewa nafasi ya kusoma.
Kulikuwa na mfumo ndani ya Wizara ya Elimu ambao watendaji wa Kanisa walijipanga katika nafasi zote kuzuia Waislam wasisome.

Uko ushahidi.

Ndipo nakuambia usijadili kitu ambacho huna ujuzi nacho.
Usidhani mimi niko hapa kufanya maskhara.

Hizi nilizokuwekea hapa ni "facts," ukisoma kitabu cha Sykes utajifunza mengi.
Ndiyo maana kitabu hiki kimechapwa mara nne toka 1998 na sasa kinakwenda toleo la tano.

Usiwe na haraka ya kuja hapa kujadiliana na mimi kwani wewe haya hayakuhusu wa kuwajibu Waislam ni serikali iseme kuwa Mohamed Said ni muongo hakuna ukweli katika haya anayoandika.
 
Lofchie huyu aliyeandika kile kitabu 'Zanzibar background to revolution'?
Biti...
Ndiyo yeye huyo.

Alifika Zanzibar siku za mwanzo za mapinduzi na Balozi wa Marekani aliomba asaidiwe katika utafiti wake.

Huyu jamaa aliyetaka niweke, ''vipicha na Wazungu,'' nia yake ilikuwa kunikejeli.

Uzoefu ni kuwa hawa jamaa zetu wakiona una kitu ambacho wao hawana wanachofanya ni kukukejeli.

Fanya utafiti utaona.

Mwalimu wangu wa aliyenifunza mlango wa Mnakasha Sheikh Haruna alikuwa akisema, ''Hata kama utakejeliwa endelea kumjibu anaekukejeli kama vile huzioni zile kejeli zake na usiache kumsomesha kwani kejeli ni kukubali kuwa yeye hakuwezi hana la kutoa ila kebehi.''

Ndiyo nikachagua hivyo ''vipicha'' moja nikiwa Northwestern University, Chicago, Minneapolis na nyingine University of Iowa, Iowa City na Prof. Michael Lofchie.

Kashindwa hata kuniambia ahsante.
 
Biti...
Ndiyo yeye huyo.

Alifika Zanzibar siku za mwanzo za mapinduzi na Balozi wa Marekani aliomba asaidiwe katika utafiti wake.
Kitabu chake ndiyo kimoja kati ya references muhimu sana kuhusu mapinduzi ya Zanzibar.

Nimewahi kukisoma kitabu chake.
 
Kitabu chake ndiyo kimoja kati ya references muhimu sana kuhusu mapinduzi ya Zanzibar.

Nimewahi kukisoma kitabu chake.
Biti...
Hiyo ndiyo miamba yenyewe inayoaminika Marekani kwa siasa za Afrika.
Alipokuja Zanzibar alikuwa mwanafunzi ana miaka 25.
 
Mazindu...
Mimi nazugumza historia ninayoifahamu ya uhuru kwa ''facts.''

Mathalan nakuaambia kuwa katika mswada wa kitabu cha Kleist Sykes ameandika vipi waliasisi African Association mwaka wa wa 1929 na kawataja ndani ya mswada hawa wafuatao kuwa ndiyo waasisi: Cecil Matola (President), Klesit Sykes (Secretary), Mzee bin Sudi, Zibe Kidasi, Ibrahim Hamisi, Seleiman Majisu, Ali Said Mpima, Rawson Watts na Raikes Kusi.

Hii ni ''fact'' haina ubishi na haiwezi kuingia kwenye hayo unayosema kuwa huwezi kuwa na ithibati.

Kleist kaandika na nimekupa ushahidi wa rejea ya seminar paper Idara ya Historia Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam ba kitabu cha John Iliffe.

Sasa hiyo chumvi itatoka wapi?
Kwa Iliffe au kwangu?

Taarifa hii hakuna katika kitabu walichohariri Temu na Kimambo, ''A History of Tanznaia,'' (1969) wala katika kitabu cha Chuo Cha CCM Kivukoni (1981)wala katika wasifu wa Julius Nyerere (2020) kitabu kilichoandikwa na Prof. Shivji at. al.

Kuhusu elimu zipo ''facts.''

Serikali iliivunja EAMWS wakati wanajiandaa kujenga Chuo Kikuu mwaka wa 1968 na jiwe la msingi Nyerere ndiye aliyeliweka.

Katika miaka ya 1970 Organisation of Islamic Conference (OIC) walitaka kujenga Chuo Kikuu Tanzania, serikali ikakataa kutoka kibali OIC wakaenda kujenga chuo hicho Mbale, Uganda.

Halikadhalika shule za Kanisa zilitaifishwa lakini Waislam hawakupewa nafasi ya kusoma.
Kulikuwa na mfumo ndani ya Wizara ya Elimu ambao watendaji wa Kanisa walijipanga katika nafasi zote kuzuia Waislam wasisome.

Uko ushahidi.

Ndipo nakuambia usijadili kitu ambacho huna ujuzi nacho.
Usidhani mimi niko hapa kufanya maskhara.

Hizi nilizokuwekea hapa ni "facts," ukisoma kitabu cha Sykes utajifunza mengi.
Ndiyo maana kitabu hiki kimechapwa mara nne toka 1998 na sasa kinakwenda toleo la tano.

Usiwe na haraka ya kuja hapa kujadiliana na mimi kwani wewe haya hayakuhusu wa kuwajibu Waislam ni serikali iseme kuwa Mohamed Said ni muongo hakuna ukweli katika haya anayoandika.
Facts gani wee mzee? Facts za michongo kama Walowezi, Maaskari wa kulipwa makatili na vibaraka wakubwa wa Wajerumani aka mercenaries hadi wakapewa majina ya Kijerumani na wakakubali kubaki nayo hayo majina ya Kijerumani wakayafanya ya ukoo hadi leo hii; Wahamiaji Wamanyema na Wazulu ndiyo unataka kutuambia walikuwa na uchungu sana na Tanganyika kuliko Wazawa wenyewe wa nchi hii? Huo Uzulu na «umbuyane» wa hao wajomba zako uliishia wapi, na kwanini hadi leo wameng’ang’ania jina «Sykes» kama la ukoo na mengineyo kama «Kleist» waliyopewa na Wajerumani kama Askari dhalinu na vibaraka wao dhidi ya Wazawa?
 
Madhalimu Mamluki wa Kijerumani wameletwa Tanganyika na Wajerumani toka kwao Msumbiji kuja kuendeleza Utawala wa Kijerumani wa kuwakandamiza, kuwanyanyasa, kuwaua, kuwabaka, kuwafunga, kuwadhalilisha Wazawa leo hii wawe mashujaa na wakombozi wa Tanganyika?
 
Taja nchi 10 za Kisslamu duniani halafu zinao wasomi wengi. Kwa asili uislamu una aleji na ELIMU, hilo linajulikana, sema kama unataka kubishana tu mzee wangu. Libya ya Gadaff ilifadhili elimu from the scratch to higher level, nambie Walibya wangapi walikua na degree walau moja? Nenda kote Qatar, Saudia kote huko kunako itwa Mataifa tajiri ya Waarabu, angalia think tank wao ni kina nani? Sio Wazawa mzee. Njoo mikoa ya pwani hata sasa hivi, angalia idadi ya watoto wanao maliza form 4 hasa wa kike ni wa ngapi? Na hili nalo Nyerere anahusika kwenye hu ulimwengu wa elimu bure? Kumsingizia mtu ni DHAMBI kubwa, hata kama sio wa dini yako. Mwinyi akiwa rais alizifanya shule karibu zote za Nyerere kua day schools ili watoto wengi wasome, idadi ya waislamu kipindi hicho walikua wangapi? Mlipenda zaidi madrasa na sio elimu dunia, kuweni wakweli mzee
Kwa hiyo kwenye namba ya wakristo wasomi na wewe upo?
 
Facts gani wee mzee? Facts za michongo kama Walowezi, Maaskari wa kulipwa makatili na vibaraka wakubwa wa Wajerumani aka mercenaries hadi wakapewa majina ya Kijerumani na wakakubali kubaki nayo hayo majina ya Kijerumani wakayafanya ya ukoo hadi leo hii; Wahamiaji Wamanyema na Wazulu ndiyo unataka kutuambia walikuwa na uchungu sana na Tanganyika kuliko Wazawa wenyewe wa nchi hii? Huo Uzulu na «umbuyane» wa hao wajomba zako uliishia wapi, na kwanini hadi leo wameng’ang’ania jina «Sykes» kama la ukoo na mengineyo kama «Kleist» waliyopewa na Wajerumani kama Askari dhalinu na vibaraka wao dhidi ya Wazawa?
Golds...
Sijui kwa nini kila unaponiandikia inakupendeza kunivunjia heshima kwa lugha ambazo si za kiungwana.

Ningeweza kukunyamazia nikakuacha kama ulivyo na nikawajibu wengine walio na adabu na heshima zao.

Lakini kuna mambo umeyaleta hapa ningependa uyafahamu kama mchango wangu kwa jamii inayonizunguka khasa kwa kuwa mimi ni kitukuu cha Mmanyema mamluki aliyeingia Germany Ostafrika akitokea Belgian Congo kuja German Osta Afrika kuwasaidia Wajerumani kushinda vita dhidi ya Abushiri bin Salim Al Harith na Mtwa Mkwawa.

Hivi ni vitu vinavyofikirisha sana na ni ukweli ambao siwezi kuukataa.

Babu yangu mkuu ambae mimi ni kitukuu chake jina lake ni Muyukwa.
Muyukwa alikuwa askari katika Boma la Wajerumani Shirati, Musoma.

Akiwa Shirati alioa mwanamke wa Kitusi akazaliwa babu yangu akampa la jina la Rashid Abdallah Popo kutoka jina la baba yake Mwekapopo.

(Miaka mingi baadae babu yangu akabadili jina akawa Salum Abdallah lakini akaja kujulikana zaidi kwa jina la ''Baba Popo,'' kwa ajili ya kuwa na mtoto aliyempa jina la Humud Popo).

Rashid alipopata mtoto akampa jina Humud Popo, hili Popo jina la baba yake kama nilivyoeleza hapo juu.

Wazee wangu hawa wamechanganya majina yao ya Kimanyema na majina ya Kiarabu ukipnda majina ya Kiislam.

Mwanae mmoja baba yangu mdogo alimpa jina la Kimanyema, ''Numbi'' na la Kiarabu ukipnda la Kiislam, Farjallah na hili ni jina la babu yake mzaa mama, bibi yangu Zena bint Farjallah mwanamke wa Kimanyema.

Mama yake Bi. Zena bint Farjallah ni Mmanyema jina lake Safia bint Farjallah.
Humud na yeye akaja kujulikana zaidi kwa jina la Popo kuliko jina ka Humud.

Katika nyakati zao hawa wazee wangu wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika walikuwa watu maarufu Tabora na Dar es Salaam.

Babu yangu akiwa mmoja wa waasisi wa TANU na Tanganyika Railways African Union Tabora na ana historia ya kuvutia sana kwani aliongoza migomo mitatu (general strike) 1947, 1949 na 1960.

Huyu ni mtoto wa Mamluki wa Kimanyema kutoka Belgian Congo aliyezaliwa Shirati na akashiriki katika siasa za African Association Dar es Salaam katika miaka ya 1930s akifanya kazi Tanganyika Railways hadi alipohamishwa kwenda Tabora akiwa fundi mfua chuma katika Locomotive Shed ailiyotolewa Dar es Salaam na kupelekwa Tabora mwaka wa 1947.

Kwa nini babu yangu hakupewa majina ya Kijerumani na Wajerumani siwezi kufahamu.

Siwezi kufahamu pia kwa nini yeye aliwapa wanae wawili wa kiume majina ya Kiarabu ukipenda ya Kiislam akachanganya na ya Kimanyema.

Mtwa Mkwawa jina lake la Kiarabu ukipenda la Kiislam ni Abdallah.
Katika mashujaa wa Maji Maji Songea Mbano jina lake ni Abdulrauf na Mkomanile ni Khadija.

Haya majina ni katika jamii zinavyoingiliana kwa namna nyingi kiasi una Mwafika anaitwa Fredrick Mwakitosi, Alexander Ngowi nk.

Hawa wameng'ang'ania majina yasiyo yao ya Wazungu na sote ndivyo tulivyo.
Hili si jambo kwa hakika la kumshughulisha mtu yeyote.

Mimi ni Mohamed Said Salum Abdallah na nikipenda naweza kuyaongeza majina ya babu zangu ya Kimanyema hayo niliyoyaweka hapo juu.

Ukoo wa Sykes.

Aliyekuja Germany Ostafrika kama mamluki ni Sykes Mbuwane kutoka Mozambique na akaoa mwanamke wa Kinyaturu Pangani jina lake Kwema akazaliwa mtoto ambae Wajerumani walimsajili kwa jina la Kleist jina la Kijerumani na ukipenda jina la Kikristo lakini baba yake akampa jina la Abdallah.

Pamoja na Sykes Mbuwane alikuwa Chief Mohosh Shangaan ambaye baadae alikuja kujulikana kama Afande Plantan na yeye alikuwa na watoto Thomas, Schneider baba yake akampa jina Abdillah, Machado akapewa jina Ramadhani na hawa wote wamezaliwa Mozambique chini ya utawala wa Wareno.

Hii ndiyo sababu ya jina la Ramadhani Machado Plantan.

Koo zote hizi mbili ya Sykes na Plantan watoto wao waliishi na majina yao hayo ya Kizungu na wameacha alama katika historia ya uhuru wa Tanganyika kwa yale waliyoyafanya katika TAA na TANU na pengine wangelala katika makaburi yao kwa amani ila kwa mimi baada ya kuona historia ya kizazi kizima chetu itapotea ndiyo nikaandika historia hii.

Bahati mbaya wewe historia hii inakuudhi kuwa kwa nini iwe Wazulu na Wamanyema watu ambao hawa asili ya nchi hii wawe mbele katika historia ya uhuru wa Tanganyika kuliko wenye nchi yao.

Sasa tunafanyaje katika hili.

Tuaweza kusema kukataa Kleist Sykes Mzulu aliasisi African Association na Al Jamiatul Islamiyya?
Tunaweza kukataa kuwa Mzee bin Sudi Mmanyema aliasisi African Association na Al Jamiatul Islamiyya?

Tunaweza kukataa kuwa Affande Plantan alikuwa Mkuu wa German Constabulary Tanganyika?
Tunaweza kukataa kuwa Thomas Pantan alikuwa President wa African Association.

Tunaweza kukataa kuwa Abdul na Ally Sykes walikuwa waasisi na wafadhili wakubwa wa TAA na TANU na ndiyo waliompokea Julius Nyerere?

Tunaweza kukataa kuwa Denis Phombeah Mnyasa kutoka Nyasaland alikuwa kiongozi wa TAA na kadi yake ya TANU ni No. 5?

Tunaweza kukataa Dome Okochi Budohi Mluya kutoka Kenya alikuwa kiongozi wa TAA na kadi yake ya TANU ni No. 6?

Ninachoweza kufanya ni kukupa pole kwani utake usitake hii ndiyo historia ya uhuru wa Tanganyika toka ilipoundwa African Association 1929 hadi ulipopatikana uhuru 1961.

Katika picha hiyo hapo chini wote unaowaona hapo ni Wamanyema ila Julius Nyerere:

1653764509766.png

Kulia: Haruna Iddi Taratibu, Saadan Abdu Kandoro, Julius Kambarage Nyerere, Sheikh Mohamed Yahya Ramia na Idd Faiz Mafungo Dodoma Train Station 1955/56​
 

Attachments

  • 1653767971923.png
    1653767971923.png
    59.8 KB · Views: 10
Madhalimu Mamluki wa Kijerumani wameletwa Tanganyika na Wajerumani toka kwao Msumbiji kuja kuendeleza Utawala wa Kijerumani wa kuwakandamiza, kuwanyanyasa, kuwaua, kuwabaka, kuwafunga, kuwadhalilisha Wazawa leo hii wawe mashujaa na wakombozi wa Tanganyika?
Gold...
Mimi siwezi kukana kuwa wazee wangu walikuwa askari katika jeshi la Wajerumani na wakapigana dhidi ya Abushiri na Mkwawa.

Hii ni kweli tupu.

Lakini katika kusoma kwangu kote na kutafiti historia ya Afrika na Wajerumani hadi kufika Zentrum Moderner Orient, (ZMO) Berlin moja ya vituo vikubwa duniani katika utafiti wa historia sijakuta popote pale kuwa kuwa German East Africa askari wa Kijerumani walishiriki katika kubaka.

Hayo mengine yalikuwapo katika kiwango kile kinachofahamika katika historia kuwa walifungwa watu na wengine wakanyongwa.

Haya yote ni katika changamoto za ukoloni Afrika na kwengineko.

1653767022731.png

Zentrum Moderner Orient (ZMO), Berlin
 
Sasa hapo MS umekiri kuwa mababu zako walikuwa washiriki wa Wakoloni madhalimu wa Kijerumani, na walilietwa Tanganyika kama Mamluki wa Wajerumani kutoka Msumbiji na kwingineko kwa nia moja tu ya kuwanyanyasa na kuwakandamiza Wazawa wa Tanganyika, kwa faida ya Wakoloni. Isitoshe hao Wajomba zako walinufaika kwenye nafasi yao hiyo walyojipatia kwa njia dhalimu kiasi cha kujijengea sifa kubwa katika jamii; Kiuchumi, kisiasa, kidini, na kadhalika, sababu waliletwa Tanganyika na Wajerumani wawe Mabwana by proxy dhidi ya Watanganyika na Waafrika wenzao.
 
Abdul Sykes alitoroka nyumbani na kwenda vitani kupigana upande wa wakoloni wa kijerumani...Hii inaonyesha ni jinsi gani alivyokuwa anauhusudu ukoloni na uzungu.....hakuwa mzalendo
 
Sasa hapo MS umekiri kuwa mababu zako walikuwa washiriki wa Wakoloni madhalimu wa Kijerumani, na walilietwa Tanganyika kama Mamluki wa Wajerumani kutoka Msumbiji na kwingineko kwa nia moja tu ya kuwanyanyasa na kuwakandamiza Wazawa wa Tanganyika, kwa faida ya Wakoloni. Isitoshe hao Wajomba zako walinufaika kwenye nafasi yao hiyo walyojipatia kwa njia dhalimu kiasi cha kujijengea sifa kubwa katika jamii; Kiuchumi, kisiasa, kidini, na kadhalika, sababu waliletwa Tanganyika na Wajerumani wawe Mabwana by proxy dhidi ya Watanganyika na Waafrika wenzao.
Gold...
Hili halina shaka kuwa waliingia nchi ya Waafrika wenzao kuwasadia wakoloni wakiwa askari walioaminiwa silaha.
Vipi mimi nikatae ukweli huu ulio wazi kabisa?

Knachonifariji ni kuwa watoto wao na ndiyo hawa akina Salum Abdallah, Kleist Sykes, Scheneider Plantan, Ali Juma Ponda Mzee bin Sudi na wengineo wakaja kuweka misingi ya kuwaondoa Wangereza katika ardhi ya Tanganyika.
 
Kwa hiyo kwenye namba ya wakristo wasomi na wewe upo?
Poor miinds always discuss personalities, strong once discuss issues; just for your interest; nimezaliwa na kukulia kwenye Uislamu hadi nikiwa na miaka 24, so najua ninacho kisema, naelewa each and everything about dini yangu. Nisingependa kwenda zaidi ya hapo; now kuhusu kama nimesoma au laa hilo nakuachia wewe.

Mwishoni nimalizie hivi; kwenye ukanda hu wa Africa, umewahi kumsikia nani kaenda kwenye nchi za Kiislamu kwenda kusoma walau degree ya kwanza, masters or PHD? Si hata Waislamu nao wanaendaga kwa wala nguruwe ili wakaongeze maarifa, usisahau hilo. Uislamu una aleji na elimu "dunia" period
 
Mazindu Msambule
Kidogo nina mawazo tafauti na wewe kuhusu hizo PhD za nchi za kiislamu. Mfano, mimi namfahamu Prof mmoja wa UDSM (Geography jina nimelisahau) alikuwa amesoma PhD yake Al Azhar University Cairo. Yeye ni mkristo na alikuwa anakizungumza kiarabu very fluently.

Kwani wewe unawajua PhD holders wote wa nchi hii na wapi waliposoma?
 
Mazindu Msambule
Kidogo nina mawazo tafauti na wewe kuhusu hizo PhD za nchi za kiislamu. Mfano, mimi namfahamu Prof mmoja wa UDSM (Geography jina nimelisahau) alikuwa amesoma PhD yake Al Azhar University Cairo. Yeye ni mkristo na alikuwa anakizungumza kiarabu very fluently.

Kwani wewe unawajua PhD holders wote wa nchi hii na wapi waliposoma?
Tunapofanya ujumuishi hua haina maana kwamba 100%; mfano debate iliopo hapa na mzee wangu ni kwamba, waislamu by nature sio wapenzi wa elimu dunia na nikataja mifano mingi tu ya maeneo yanayo kaliwa na waislamu na elimu zao, nikaenda hadi kutaja nchi za kiislamu nyingi pamoja na viongozi kadhaa wa kiislamu kama Mohamadi Gadaf; kwa kutaja hivyo, haina maana kwamba waislamu 100% hawasomi au hizo nchi zote za Kiislamu hakuna kabisa wasomi, wapo but ki uchumi walio nao havifanani na idadi yao. Kwa kusema hivo, weka rekori ya maprofesa 10 unao wajua, tena wawe waislamu tupu, akiwepo na profesa Asad, Lipumba nk, halafu angalia ni wangapi wameipatia elimu yao, jibu utalipata tu.
 
Tunapofanya ujumuishi hua haina maana kwamba 100%; mfano debate iliopo hapa na mzee wangu ni kwamba, waislamu by nature sio wapenzi wa elimu dunia na nikataja mifano mingi tu ya maeneo yanayo kaliwa na waislamu na elimu zao, nikaenda hadi kutaja nchi za kiislamu nyingi pamoja na viongozi kadhaa wa kiislamu kama Mohamadi Gadaf; kwa kutaja hivyo, haina maana kwamba waislamu 100% hawasomi au hizo nchi zote za Kiislamu hakuna kabisa wasomi, wapo but ki uchumi walio nao havifanani na idadi yao. Kwa kusema hivo, weka rekori ya maprofesa 10 unao wajua, tena wawe waislamu tupu, akiwepo na profesa Asad, Lipumba nk, halafu angalia ni wangapi wameipatia elimu yao, jibu utalipata tu.
Kwa kweli mimi sina rekodi ya nani amesoma na nani hakusoma, awe muislamu au mkristo. Huyo niliyekuambia ni kwamba tulikutana kwenye washa fulani ndiyo akanielezea.

Nenda nchi za kiarabu, China, Indonesia, na kadhalika ambazo zina idadi kubwa ya waislamu, hivi unadhani ndiyo kuna idadi ndogo ya wasomi? Na hayo maUniversity yao waliyo nayo nchini kwao wanafundisha akina nani?

Nadhani umesoma historia kwamba ustaarabu ulianzia kwenye maeneo ya Euphrates na Tigris (middle east), algebra yenyewe ilianzia Egypt kwenye mahesabu ya mto Nile... unadhani wote hao masomo wamesomea Ulaya ya enzi zile?
 
Poor miinds always discuss personalities, strong once discuss issues; just for your interest; nimezaliwa na kukulia kwenye Uislamu hadi nikiwa na miaka 24, so najua ninacho kisema, naelewa each and everything about dini yangu. Nisingependa kwenda zaidi ya hapo; now kuhusu kama nimesoma au laa hilo nakuachia wewe.

Mwishoni nimalizie hivi; kwenye ukanda hu wa Africa, umewahi kumsikia nani kaenda kwenye nchi za Kiislamu kwenda kusoma walau degree ya kwanza, masters or PHD? Si hata Waislamu nao wanaendaga kwa wala nguruwe ili wakaongeze maarifa, usisahau hilo. Uislamu una aleji na elimu "dunia" period
Mazindu...
Kwani kipimo cha watu kupenda elimu ni kwa watu kutoka taifa moja kwenda kusoma taifa lingine?

Kupenda elimu au kuwa na watu walioelimika ni kule kujaza vyuo vyako na wanafunzi.

Vyuo visiwe vitupu havina wasomaji.

Waingereza walitawala dunia hii kiasi wakawa wanajigamba wanasema jua halituwi katika himaya yao.

Kote walikotawala walijenga shule na wakasomesha watuliowatawala Kiingereza.

Dunia ikawa na wasemaji wengi wa lugha hii na Waingereza wakaifanyia juhudi kubwa lugha yao kuisomesha kwa kupeleka walimu na kupata walimu wa Kiingereza katika wenyeji.

Tanganyika ikawa moja ya nchi ulimwenguni walionufaika na msaada huu.

Mimi nimesomeshwa Kiingereza shule ya msingi na Peace Corps anaitwa Romenesko na sekondari na Mrs. Grant.

Mumewe pia akisomesha Kiingereza Chang'ombe Teachers College.

Hawa waliletwa huku na British Council.

Mimi nilipata "high grades," katika Kiingereza kati ya masomo manane niliyofanya mtihani wa Cambridge.

Nakueleza hili kukuonyesha juhudi ya Waingereza katika lugha yao vipi mimi Mswahili niliyesoma Kinondoni Primary School na si English Medium nimesomeshwa lugha ya kigeni nikaimudu kwa kupata Merit Pass English Oral.

Waingereza kwa ajili hii wakawa wanaweza kuchukua katika vyuo vyao vikuu wanafunzi kutoka dunia nzima na wakasomeshwa kwa lugha yao ya Kiingereza.

Mimi nimesoma huko na nilikuwa International Student darasa letu lina wanafunzi hadi kutoka China na nchi za Latin Amerika.

Namaliza kwa kukufahamisha kuwa Uingereza wamekuwa na uwezo mkubwa wa kuwa na vyuo vingi kwa miaka mingi sana.

Hii ndiyo maana si kama hakuna wanafunzi wanaokwenda kusoma Arabuni wapo tena kwa fani nyingi tu lakini ni wachache.

Mtume kasema itafuteni elimu hadi China.

Nina academic paper tatu nimewasilisha ndani na nje ya nchi kuhusu tatizo la elimu kwa Waislam Tanzania na sababu moja niliyoeleza ni hujma kutoka watendaji Wakristo ndani ya taasisi za elimu.

Ondoa hiyo "period," si adabu wala haipendezi watu mnapojadiliana.

Jitahidi tufanye mjadala ambao jamii itanufaika ba kuelimika jizuie na hizi lugha za "wala nguruwe," hazina maana.

Tunaweza sasa kusonga mbele kuanzia hapa labda kwa mimi kukuwekea ushahidi zaidi wa hujuma.
 
Back
Top Bottom