Kitabu cha "ushahidi kuwa Mungu hayupo na uchawi haupo" kiko njiani

ndugu yangu, unachojaribu kufanya ni kutumia "logic"

swala la hili linaweza kuwa tofauti na logic unazojaribu kutumia hivyo jiandae kusikiliza mawazo mapya unaweza kubadiri mtizamo


Logic ndio yakufuatwa kinyume cha logic ni illogic, je tufuate illogic??!!.

Logic ni kwamba hakuna kitu chenye kutenda kinidhamu na kikose muumbaji au mtengenezaji wake aliyekiwekea hiyo nidhamu ili kikidhi haja kusudiwa.---- hiyo ndio point ya kutafakari.
 
Unajaribu kutumia limited thinking yako, sometimes inabidi kupanua wigo wa kufikiri kwa kusikiliza na wengine wanasemaje.
 
Daah kwa hiyo Dunia ilijitengeneza yenyewe bila kuwepo na kitu kingine chochote ambacho ndio kinamiliki...Dunia kwa jinsi ilivyo na viumbe vilivyopo inaonyesha kuna uwepo wa Mungu...
 
Unajaribu kutumia limited thinking yako, sometimes inabidi kupanua wigo wa kufikiri kwa kusikiliza na wengine wanasemaje.


Siku zote sifa ya moto ni kuunguza na kamwe huwezi kupanua fikra zako kwa kusema kwamba moto siku moja utaacha kuunguza na ndivyo hivyo kwamba kitu chochote kinachotenda ndani ya realm of disciples hicho ni lazima kiwe kimetengenezwa na A conscious disciplined being and not the otherwise, kwa upande wa yule aliyetuumba/aliyetutengeneza sisi binadamu (the most complicated disciplined machine) nk, ndiye huyo aitwaye Mungu, hivyo Mungu yupo, na lazima awe Supreme.
 
Napenda mabishano ya hoja mimi hatari, najifunza kuzungumza.

Mada hii mpaka sasa, pamoja na kupingana na imani yangu, nimependa mpambano wa hoja uliokomaa

Mleta mada 1, Mokaze 1

Sisi wenye vihoja vyepesi vyepesi tupo pembeni hapa Tunaendelea kushuhudia hoja.........
 
Katika tumbo la mama kulikuwa na watoto wawili. Mmoja akamuuliza mwenzake: “Je, unaamini maisha baada ya kujifungua?” Yule mwingine akajibu, “Kwa nini, bila shaka. Lazima kuwe na kitu baada ya kujifungua. Labda tuko hapa kujitayarisha kwa kile tutakachokuwa baadaye.” "Upuuzi," wa kwanza alisema. "Hakuna maisha baada ya kujifungua. Je, hayo yangekuwa maisha ya aina gani?” Wa pili akasema, "Sijui, lakini kutakuwa na mwanga zaidi kuliko hapa. Labda tutatembea kwa miguu yetu na kula kutoka kwa midomo yetu. Labda tutakuwa na hisia zingine ambazo hatuwezi kuelewa sasa. Wa kwanza akajibu, “Huo ni upuuzi. Kutembea haiwezekani. Na kula kwa midomo yetu? Kichekesho! Kamba ya umbilical hutoa lishe na kila kitu tunachohitaji. Lakini kamba ya umbilical (kondo la nyuma) ni fupi sana.

Maisha baada ya kujifungua yanapaswa kutengwa kimantiki.” Wa pili alisisitiza, "Nadhani kuna kitu na labda ni tofauti na ilivyo hapa. Labda hatutahitaji kamba hii ya mwili tena." Wa kwanza akajibu, “Upuuzi. Na zaidi ya hayo, ikiwa kuna uhai, basi kwa nini hakuna mtu aliyewahi kurudi kutoka huko? Kujifungua ni mwisho wa maisha, na katika baada ya kuzaa hakuna ila giza na ukimya na usahaulifu. Haitupeleki popote.” “Sawa, sijui,” akasema wa pili, “lakini hakika tutakutana na Mama naye atatutunza.”

Wa kwanza akajibu “Mama? Unamwamini Mama kweli? Hiyo inachekesha. Kama mama yupo, yuko wapi sasa hivi?" Wa pili akasema, “Anatuzunguka pande zote. Tumezungukwa naye. Sisi ni wake. Ni ndani Yake tunaishi. Bila Yeye, ulimwengu huu haungekuwepo na tusingekuwepo." Alisema wa kwanza: "Kweli, simuoni, kwa hivyo ni sawa kwamba Yeye hayupo." Ambayo wa pili alijibu, "Wakati mwingine, unapokuwa kimya na ukizingatia na kusikiliza, unaweza kuona uwepo Wake, na unaweza kusikia sauti Yake ya upendo, ikiita kutoka juu." Labda hii ilikuwa moja ya maelezo bora ya dhana ya MUNGU.


 
Wanao okota makopo sio vichaa
 


🙏🏻🙏🏻🙏🏻🙏🏻 kudos
 
Chief kitabu chako kitakuwa na kurasa ngapi tuanzie hapo Kwanza.
Je! Kinaweza kuzidi kurasa ya vile vitabu ambavyo watu wengi wanaviamini?
Kama jibu ni hapana basi moja kwa moja jua umeishafeli.
Maana hivyo vitabu watu wanavyo viamini vinakurasa nyingi sana na maelezo mengi sana lakini hadi Leo watu wameshindwa kuvielewa.
Sasa sina uhakika kwa hoja za kurasa 50 kama zinaweza kuwatosheleza wasomaji ambao tayari wameisha Soma vitabu vyenye zaidi ya kurasa 600 ambavyo hawajulikani waandishi wake na bado wameshindwa kuvielewa.
Wewe watu wanakujua na wanakufahamu madhaifu yako ni wazi tutakupinga dhahiri.
Katika haya wewe sio wa Kwanza alikuwepo firauni/farao
 
Hakika wewe ni mtunzi mzuri lakini umechukua hadithi ya mazingira ya kwetu ukataka kuiuisha iwe ya kimungu.

Huko si kuthibitisha uwepo wa mungu bali kutengeneza mungu wako na mbingu yako kwa kutumia fikra zako.

uwepo au kutokuwepo kwa mungu kuna mambo yaliyojificha mabayo yanatakiwa kuwekwa wazi na hayo ndiyo yatafungua fikra za wanadamu juu ya uwepo au kutokuwepo kwa huo ulimwengu udhaniwao.
 
Nadhani wewe umesoma na kuelimika hivyo unatambua vema tofauti iliyopo kati ya herufi kubwa na herufi ndogo. Hapo kwenye neno mungu mimi nilimaanisha Mungu lakini wewe kutokana na uandishi wako umemaanisha mungu, hivi ni vitu viwili tofauti kabisa
 
kasema hakuna uchawi sasa wachawi wenzake kivipi
 
na wewe ukaamini
 
mbona umepaniki mkuu,ho wazazi ndio inaweza kua huja yake kuwa hakuna Mungu maana angekuwepo ungetoke bila wazazi,hija ya mikono ni dhaifu,wapo wanaozaliwa hawana mikono wala miguu.tuliza munkari weka hoja
 
kinatoka lini
 
kuna langua
Nadhani wewe umesoma na kuelimika hivyo unatambua vema tofauti iliyopo kati ya herufi kubwa na herufi ndogo. Hapo kwenye neno mungu mimi nilimaanisha Mungu lakini wewe kutokana na uandishi wako umemaanisha mungu, hivi ni vitu viwili tofauti kabisa
je kama kiarabu hawana herufi ndogo wala kubwa manake hayo masharti hayawahusu??kwenye matamshi M na m kuna tufauti?? nani aliyesema M ni herufi kubwa kuliko m au ni kikundi ch watu tu pengine walikua wamelewa? leo wakiamua M iwe ndogo na m indio iwe kubwa masharti yatabadilika na huyo Mungu atachukia??
 
katika watu wanaosoma kwa kukariri ni waislamu.haiitaji utafiti fungua katikati ya msahafu nenda madrasa mpe kijana atakusomea kama anakunywa maji mwambie sasa akwambie maana yake nini hajui
 
hakuna kifo cha Mungu.kifo ni nature perfection
 
Nadhani wewe umesoma na kuelimika hivyo unatambua vema tofauti iliyopo kati ya herufi kubwa na herufi ndogo. Hapo kwenye neno mungu mimi nilimaanisha Mungu lakini wewe kutokana na uandishi wako umemaanisha mungu, hivi ni vitu viwili tofauti kabisa
bahati mbaya sana mimi sijasoma lugha kama somo mama hivyo tafsiri yangu ya "kuelimika" haiko katika utaalamu wa lugha bali uwezo wa kuchakata mambo mbalimbali yaliyoko katika jamii na kuyapa mantiki.

Utaalamu wa lugha nauchukilia kama "background knowledge" ambayo haina nguvu sana katika hoja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…