Kitabu kipya: Tanzania na propaganda za udini na prof. Ibrahim Noor

Kitabu kipya: Tanzania na propaganda za udini na prof. Ibrahim Noor

Mkuu, unajuwa ili uweze kuingiza idea mpya kichwani mwako ni MUHIMU kufanya ubongo wako uko BLANK ili kuruhusu mawazo mapya kuingia na kuchakata kile ambacho kilikuwepo kabla kisha baadae ndio uamue kipi ni kipi. Sasa wewe unaposema mwandishi amesema urongo kuanzia sura ya kwanza ni kwamba unashikilia msimamo wa kile ambacho ulikijua kabla ya kusoma alichoandika mwandishi.
Nikushauri tu, uwe na tabia ya kisomi tena usomi wa kutafuta ukweli: soma kwanza alichokiandika mwandishi ukiwa na blank mind, usiwe tayari na mtizamo hasi, HUTAELEWA. Hata mimi ni mwanahistoria na nimesoma THE PEOPLING OF EAST AFRICA na pengine tulichofundishwa wengi ndicho hicho unachokijua wewe ,lakini LET THE FACT SPEAK FOR ITSELF , tusome mtazamo wa mwandishi kisha tulinganishe kile tunachokijua, halafu ndio tufikie hitimisho. SI KILA WAKATI TULICHOFUNDISHWA VYUONI NI SAHIHI. Tusikaririshwe, tuwe wasomi wa kuchambua mambo.
Ntakupa mfano: kwa miaka mingi sana, tumekuwa tukifundishwa vyuoni kuwa FANI NA MAUDHUI HAVIWEZI KUTENGANISHWA, huu ni mtizamo ambao ulikubalika na wasomi nguli kama kina prof. SENKORO (Kasome kitabu cha FASIHI alichoandika), lakini ni huyu huyu Prof baada ya miaka na mikaka kupita SASA HIVI ANAYAKANA MAANDISHI NA MTIZAMO WAKE WA ZAMANI na ANAKUBALI kuwa fani na maudhui ni vitu vinavyoweza kutenganishwa akitolea mfano wa nyimbo za kubembelezea watoto hasa katika jamii zinazofuata mfumo wa kibaba
Mkuu xiexie, asante, nitaufuata ushauri wako.
Pasco
 
Africans have so much illusions about these organized religions, nothing came from any European or Arab mind that meant to do anything to help us Africans but to facilitate their domination over us, I said nothing….every idea, every religion which was brought here was meant to control and subjugate the African people. Africans were taken as slaves by cruel Arabs long before Europeans set foot in Africa, and when they (Europeans) started doing, it became a commercial and organized. Million of million Africans died from this holocaust but no one seems to care about. We think that our best ways to survive or to go to heaven (as we still think) is to become most those things that unlikely ourselves, and when you start believing in those things unlikely ourselves we become nothing but slaves, and to those whom we are imitating they become our prisoners whether they build a jail or not, and in most cases they don't have to build a jail because "the psychological jail of depending on someone else for religion, culture and image (God) is a more binding jail than any steel can be erected for u" –Dr John Henrik Clarke
 
:nono:
Acha kujidanganya. Uarabu ni lugha,rangi na zaidi ni historia ya familia yako. kama unabisha nenda Sauidi na pua yako ya kibantu alafu uwaambie wewe ni muarabu kwasababu unajua lugha ya kiarabu. Wabantu wa wanaoishi somalia wenye asili ya kizigua wanabaguliwa mpaka leo na wasomali kuwa wao sio waarabu wakati hata waarabu wenyewe wanasema wasomali sio waarabu. Tatizo wabantu wengi wa bwani ya afrika wanakasumba ya kujitambulisha kama waarabu na anaejiona ndio muarabu zaidi basi anaona ndio wa maana zaidi na anahaki zaidi ya wabantu wenzake. hii tabia ndio inao wamaliza somalia kwakuuana maana wote waislam ila koo tofauti lakini wanauana kwa kuona koo zao ni bora na niwazawa wa mtume muhammad. kama unabisha mfatilie Dr. Omar Eno na kaka yake kwenye mijadala ya Bantu Somali. na mfano moja ni huu hapa chini wa Somali Identity
.
https://www.youtube.com/watch?v=UNQbQseoRIU

https://www.youtube.com/watch?v=kRfIUpJGUn8

Sio wabantu tu wa Africa Mashariki bali hata makabila yote yalifikiwa na Uislam huwa wanaamini kuwa Wao ni waarabu, Ukifika Nigeria hasa kabila la Hausa, wao ndio wanajiita waarabu kabisa, nimewahi fanya kazi pia Mali na Mauritania wao pia wanajiita Waarabu japo ni weusi kama sisi tu,
 
Wewe unaongelea ubaguzi> ubaguzi hata Afrika ndio kwenyewe, au huna habari zinazoendelea Afrika ya Kusini? Huko nako ni Waislam wanabaguana na kuuana?

Hata maana ya Saudi Arabia hauijuwi halafu unataka kuongelea Saudi Arabia? Unajuwa ni lini hiyo nchi iliitwa hivyo?

Wacha kuhororoja na kubwabwaja bila mpango, nisome tena, saidiana na Pasco kisha mjibu hili:

Waarabu wengi leo hii wako Afrika, lugha ya kwanza kuongewa na wengi Afrika ni Kiarabu na haijawahi kuwa vinginevyo, jana , juzi , majuzi, rudi nyuma miaka mia, elfi, maelfu upendavyo utakuta ni hayo hayo. Utapofikia katika usomi wako ukakuta "wamekuja" nioneshe nami nipaelewe.

watu wanaama dadangu, Africa kuwa na Waarabu wengi haimaanishi kuwa hao Waarabu wanaasili ya Africa, hao ni waamiaji tu, Wabantu wako wengi sana Africa kusini lakini nao ni waamiaji tu wenyeji ni bushmen (Khoi na San) na kwa sasa wako wachache mno

Kwa kiarabu kuongelewa kwa uwingi wake hapa Africa, haimaanishi kuwa ni Hiyo lugha inachimbuko lake hapa Africa, hiyo ni lugha ya kuja tu,
Spanish ndio lugha kubwa inayoongelewa South America ukitoa Brazil na nchi ndogo chache, lakini haimaanishi hicho Kispanyola kina Asili ya South America, bali ni ya kuja tu
 
yani kitabu kina tuaminisha kuwa Wabantu walifika Visiwani Karne ya 16 na Waarabu walifika maelfu ya miaka iliyopita?....
Ni ajabu la dunia.

Kitabu kina tuaminisha waarabu hawakufanya sana biasha ya utumwa?.....vichekesho.

Warabu walivyo kuja Visiwani walikuja kwa lengo la kufanya biashara, na waliwakuta wenyeji ambao ni wabantu..


Naomba niulize Watumwa walio kuwa wanapelekwa nch za kiarabu kutoka africa, mbona hata watu weusi hawapo uko uwarabuni? waliwauwa? mbona Latin america wapo na hata america wapo?....
 
Kitabu hiki kipigwe marufuku na serikali tukufu ya Tanzania.......ova!!!
 
watu wanaama dadangu, Africa kuwa na Waarabu wengi haimaanishi kuwa hao Waarabu wanaasili ya Africa, hao ni waamiaji tu, Wabantu wako wengi sana Africa kusini lakini nao ni waamiaji tu wenyeji ni bushmen (Khoi na San) na kwa sasa wako wachache mno

Kwa kiarabu kuongelewa kwa uwingi wake hapa Africa, haimaanishi kuwa ni Hiyo lugha inachimbuko lake hapa Africa, hiyo ni lugha ya kuja tu,
Spanish ndio lugha kubwa inayoongelewa South America ukitoa Brazil na nchi ndogo chache, lakini haimaanishi hicho Kispanyola kina Asili ya South America, bali ni ya kuja tu

Huko "South America" unaweza kupata tarehe yao walivyoanza safari ya kwenda huko.

Sasa nisome tena, unielewe:


Waarabu wengi leo hii wako Afrika, lugha ya kwanza kuongewa na wengi Afrika ni Kiarabu na haijawahi kuwa vinginevyo, jana , juzi , majuzi, rudi nyuma miaka mia, elfu, maelfu upendavyo utakuta ni hayo hayo. Utapofikia katika usomi wako ukakuta "wamekuja" nioneshe nami nipaelewe.
 
yani kitabu kina tuaminisha kuwa Wabantu walifika Visiwani Karne ya 16 na Waarabu walifika maelfu ya miaka iliyopita?....
Ni ajabu la dunia.

Kitabu kina tuaminisha waarabu hawakufanya sana biasha ya utumwa?.....vichekesho.

Warabu walivyo kuja Visiwani walikuja kwa lengo la kufanya biashara, na waliwakuta wenyeji ambao ni wabantu..


Naomba niulize Watumwa walio kuwa wanapelekwa nch za kiarabu kutoka africa, mbona hata watu weusi hawapo uko uwarabuni? waliwauwa? mbona Latin america wapo na hata america wapo?....

Tunaomba nukuu za kutoka kwenye kitabu, si kichwani mwako.
 
Sio wabantu tu wa Africa Mashariki bali hata makabila yote yalifikiwa na Uislam huwa wanaamini kuwa Wao ni waarabu, Ukifika Nigeria hasa kabila la Hausa, wao ndio wanajiita waarabu kabisa, nimewahi fanya kazi pia Mali na Mauritania wao pia wanajiita Waarabu japo ni weusi kama sisi tu,

Hapo ndipo nnapoamini kuwa shule ulisomea ujinga.
 
"... Mlango wa Kwanza unahusu “ Taarikh ya
Kuwasili Kwa Wabantu, Washirazi na
Waarabu Pwani ya Afrikaya Mashariki. ” Hapa
anaeleza kwa ushahidi wa taarikh usiokatalika
kwamba Waarabu wamefika Pwani ya Afrika
Mashariki maelfu ya miaka iliopita na
Wabantu wamefika pwani hiyo katika karne ya
16 B.K. Makusudio ya mlango huu ni
kuonesha kwamba Waarabu si wageni bali ni
wenyeji wenye haki hapa sawasasa na
wenyeji wengineo..."

kwa kipande hiki tayari amenivunja moyo kukitafta kitabu chake. warabu hawakuja Africa mashariki kufanya utalii, bali walikuja kwa kusudi la kuchuma. kupitia vito vya thamani na kupitia rasilimali watu.

huyu anasema hayo kwa kuwa yeye si mbantu wala non bantu African societies bali ni mwarabu. hivyo upuuzi wake ni kuonesha warabu ni wenyeji kuliko wabantu. huuu ni ujinga
 
yani kitabu kina tuaminisha kuwa Wabantu walifika Visiwani Karne ya 16 na Waarabu walifika maelfu ya miaka iliyopita?....
Ni ajabu la dunia.

Kitabu kina tuaminisha waarabu hawakufanya sana biasha ya utumwa?.....vichekesho.

Warabu walivyo kuja Visiwani walikuja kwa lengo la kufanya biashara, na waliwakuta wenyeji ambao ni wabantu..


Naomba niulize Watumwa walio kuwa wanapelekwa nch za kiarabu kutoka africa, mbona hata watu weusi hawapo uko uwarabuni? waliwauwa? mbona Latin america wapo na hata america wapo?....

kama ilivyokuwa kwa mzungu kufanya de industrialization kwa kuua na kuwafanya vilema wa kudumu, ndivyo warabu walivyofanya kwa mtu mweusi. kwanza walihasiwa ili wasiweze kusababisha mimba, halafu mwanamke wa kiarabu alifundishwa kumwona nwafrica ni nyani tu na ikitokea amepata mimba aidha mimba iharibiwe au mwarabu auawe.

ndio maana pamoja na kupeleka waafrica wengi kuzidi hata amerika lkn arabuni no black race
 
kama ilivyokuwa kwa mzungu kufanya de industrialization kwa kuua na kuwafanya vilema wa kudumu, ndivyo warabu walivyofanya kwa mtu mweusi. kwanza walihasiwa ili wasiweze kusababisha mimba, halafu mwanamke wa kiarabu alifundishwa kumwona nwafrica ni nyani tu na ikitokea amepata mimba aidha mimba iharibiwe au mwarabu auawe.

ndio maana pamoja na kupeleka waafrica wengi kuzidi hata amerika lkn arabuni no black race

Unaandika tu kwa kuwa unajua kuandika lakini unacho kianda hukijui na huna ithbati nacho.
 
Sasa wewe ni mbaya zaidi kufikiria mambo hata hujakisoma kitabu na kuanza chokochoko, sioni kama kinauzwa misikitini ni duka lililo nje ya msikiti, na misikitini sio sehemu ya kufanya biashara ni sehemu ya ibada.

Masomo bookshop ni mbali kabisa na msikiti. kwanini una chuki zilizowaziwazi na uislam?
binaadamu hatakiwi kuwa hivyo lol
PTER
mimi sina chuki na uislam lakini maudhui ya mchambuzi yana akisi kuwa kitabu kinajenga dhana kuwa kunapropaganda katika elimu ambazo zinaminya uislam,

samahani sana kama nimegusa imani yako halikuwa lengo langu, pengine mchambuzi kaweka ya kwake ngoja nikakitafute nijisomee mwenyewe nimejaribu online hakipo
 
unamfanyia favor kusema ana chembechembe za udini..ni mdini through and through..na hicho kitabu wasome, may be it will make them feel better..besides what else have they zaidi ya hizo feelings zao?
hahaha wanazidi kuongezeana misimamo mikali ili waendelee kujilipua.
 

[/B][/B]Mkuu Maalim , kwanza asante kutupatia taarifa hizi, sisi wapenzi wa kusoma vitabu, tutakinunua na kukisoma hiki kitabu cha Tanzania na Propaganda za Udini, ila hata kabla sijakinunua na kukisoma, kiukweli kabisa toka ndani ya nafsi yangu, the sixth sense inanieleza the 'motive behind' mwandishi wa kitabu hiki, Prof. Ibrahim Noor Shariff, ni 'ill motive!'. Tangu Mlango wake wa Kwanza unaohusu “Taarikh ya Kuwasili Kwa Wabantu, Washirazi na Waarabu Pwani ya Afrikaya Mashariki.” ameanza na maurongo yaliyokubuhu!, hapa anadanyanya wazi mchana kweupe kwa maushahidi yake ya uongo kwamba eti Waarabu wamefika Pwani ya Afrika Mashariki maelfu ya miaka iliopita kabla ya Wabantu, tangu karne ya 16 B.K!. The ill motive ya mlango huu ni kuonesha kwamba Waarabu si wageni bali ni wenyeji wenye haki hapa sawasasa kwenye Pwani ya Afrika Mashariki sawa na wenyeji wengineo.

Yaani hapa huyu Mwarabu, anataka kuwafanyia Afrikanization hawa wavanizi wa Kiarabu ili kuwahalaliasha eti na wao, ni wenyenyeji halali wa Afrika Mashariki, na wakati huo huo, kuwaondolea Wabantu, uenyeji wao wa asili, kwa kuonyesha kuwa hata hao Wabantu, Afrika ya Mashariki sio kwao asili bali nao pia ni wahamiaji tuu kama Waarabu!. Huu ni uongo uliokubuhu wa mchana kweupe!.

Lengo ni kuzuia kinachoweza kuja kuwapata Waarabu wa Afrika Mashariki na sana sana Waarabu wa Zanzibar ambao wametoka kwao Omani juzi juzi tuu mwaka 1832 wakiongozwa na Sultan Seyyed Said aliye yahamisha makao yake makuu toka Oman hadi Zanzibar!. Huyu sio tuu ni mvamizi bali pia ndiye mporaji mkuu, aliyejitwalia visiwa hivyo kama ameviokota as if hakumkuta mtu yoyote ili hali wenyeji walikuwepo!. Siku ile ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar, siungi mkono mauaji yoyote ya Waarabu, bali wangeambiwa tuu kistaarabu, wafungeshe kilicho chao, wao na wazalio wao, wajirudie kwao Omani walikotoka na kutuachia visiwa vyetu!.

Hili swali la Waarabu wamekujaje Pwani ya Afrika Mashariki, litakuja kurudi tuu mbele ya safari hivyo ushauri wangu, ni kujituliza tuu na kuishi kwa unyenyekevu wa hali ya juu sana kwa kujihesabu wanaishi hapo kwa hisani tuu, vinginevyo watatimuliwa warudi kwao Oman walikotoka, wao na vizalia vyao!.

Hizi historia za kutunga tunga kutaka kuwahalalisha madhalimu hawa waliowauza mababu zetu kama bidhaa!, hazitasaidia kitu!, no wonder kila siku wanashinda uchaguzi lakini kamwe hawatakabidhiwa nchi, na 2015 watashinda tena na moto ni ule ule!. Mwarabu atoke kwao, aje akutawale, babu zako awauze, kisha mumpindue halafu leo mumrudishe eti kisa amechaguliwa!, hii haitakaa itokee!.

Kesho ni sikukukuu ya Muungano, tutakukumbusheni hiyo Zanzibar ilikuwa ni sehemu ya Tanganyika, hivyo huu muungano ni wa milele.

As long as hii ni lilterally work, ngoja nikitafute na kukisoma halafu turudi humu kumwaga mbichi na mbivu!, ila kiukweli lazima hata mtoto wa darasa la 4 akiisikia hii acheke, ati Waarabu nao kwao ni Afrika Mashariki, na Wabantu nao pia ni wageni!. OMG!.

Pasco
mkuu Pasco mimi binafsi nimesema wazi kwamba kitabu hiki kinalenga kujenga shari zaidi kati ya waislam na wakristo tofauti na mtoa mada alivyosema, title yake yenyewe inasadifu kilichomo ndani, mbaya zaidi kimekuja katika kipindi ambacho kunachembechembe za udini zinazidi kumea katika nchi yetu. kwangu kwa hadhira ya kawaida it is a worthless book to read.
 
Tunaomba nukuu za kutoka kwenye kitabu, si kichwani mwako.

tunajuwa fika kuwa Wazungu wameshiriki vema kufanya biashara ya utumwa,

wazungu waliwachukuwa watu wengi sana toka africa kwendwa utumwani America, Europe, south america. lakini mpaka sasa tunaona watu weusi bado wapo isikokuwa nch kama Argentina ambapo walibaki na kuwinda na kuuwawa kama swala. lakini marekani, brazili, chile, cuba, england, canada, jamaika na kwingineko watu weusi walio chululiwa kutoka biashara ya utumwa vizazi vyao mpaka leo vipo,

Ushahidi asilimia 12 ya watu million 320 wa marekani ni masalia ya Watumwa.


Dada vipi kwa ndugu zetu walio kuwa wanachukuliwa kwenda Uarabuni! enzi za biashara ya utumwa!?....mbona hatuoni hata masalia?..nch kama Saudia hatuwaoni kabisa vip.........

walienda wapi?.....

walifanywa nini?...

walipotelea wapi?...

Vizazi vyao viko wapi huko?...

vipi kitabu kina tuaminisha kuwa Mapinduzi ya Zanziber hayakuwa halali....

kitabu kina tuaminisha Sultan ni Mzawa na alikuwepo kabla ya Wabantu...hii imekaaje?
 
Hapa nimepata definition mpya ya Uarabu, kumbe ni lugha tu, sio kabila wala rangi, kwa hiyo hata wewe kama unazungumza kiarabu basi ni muarabu?, hata mzungu wa ulaya akiwa mzungumzaji wa kiarabu hatumuiti mzungu tena bali anakua ni muarabu?
Pasco Waarabu hawakuja Afrika, Waarabu asili yao ni Afrika.

Inasikitisha sana kuona kuwa historia iliyowajaza ujinga ikisema Waarabu wamekuja Afrika.

Kwanza kabisa ningependa ufahamu kuwa Uarabu si kabila wala rangi, Uarabu simply ni lugha.

Waarabu wengi leo hii wako Afrika, lugha ya kwanza kuongewa na wengi Afrika ni Kiarabu na haijawahi kuwa vinginevyo, jana , juzi , majuzi, rudi nyuma miaka mia, elfu, maelfu upendavyo utakuta ni hayo hayo. Utapofikia katika usomi wako ukakuta "wamekuja" nioneshe nami nipaelewe.

Tatizo kubwa sana linakuja pale mnapoamini, kwa ujinga tu, kuwa Uarabu ni tabaka la kabila au rangi ya watu fulani. La hasha, huko ni kule mimi nnapokuita kusomea ujinga.

Historia yoyote ile uipendayo, haioneshi na haitoweza kuonesha Mwarabu Afrika alikuja lini kwanza, isipokuwa kuna dhanna tu ya "tarikh" historia inayoonesha Mwaarabu alikutwa lini Afrika, jee na nani? na kwanini akutwe? Fikiri.

Unaanza kuponda "itroduction" iliyowekwa hapa kabla hujakisoma kitabu, jee, ni kwa jina tu la aliyetunga kitabu?

Unataka kutuaminisha kuwa "sixth sense" yako yakufikirika ina maana zaidi ya kitabu ambacho hujakisoma?
 
Back
Top Bottom