Kiteknolojia China iko sawa na nchi za Marekani na Ulaya

Kiteknolojia China iko sawa na nchi za Marekani na Ulaya

Xi Jinping

JF-Expert Member
Joined
Jun 14, 2023
Posts
3,651
Reaction score
11,548
"Kusema ukweli, ni kwamba watu ambao hawaendi China mara nyingi hufikiria kuwa wako nyuma, lakini unapoenda huko unavutiwa na wanachofanya katika teknolojia."
–Brad Smith (Raisi wa Microsoft)

Nchi za Magharibi hazipaswi kudhani kuwa China iko nyuma ya Marekani na Ulaya kwenye maendeleo ya teknolojia, raisi na makamu mwenyekiti wa Microsoft alionya.

Mvutano wa Marekani na China katika miaka michache iliyopita ulijikita katika vita kati ya mataifa hayo mawili ya ukuu wa teknolojia, na kupelekea Marekani kudhibiti mauzo ya chips za hali ya juu nchini China ikitaka kudhoofisha taifa hilo la pili duniani kwa uchumi mkubwa.

Mwishoni mwa mwaka jana, Huawei ya China ilishangaza soko la dunia kwa kutolewa kwa simu mahiri yenye kasi ya upakuaji yenye 5G, na hivyo kuonyesha mafanikio dhahiri katika chip licha ya vikwazo vya teknolojia kutoka Marekani.

Akizungumza katika mkutano wa teknolojia ya Wavuti (Web summit tech conference) huko Lisbon, Ureno, Jumanne 12 Nov. Brad Smith wa Microsoft aliiambia CNBC kwamba;

"Kwa njia nyingi, China iko karibu na au hata inapatana na teknolojia ya nchi za Magharibi."

Alitabiri kuwa makampuni ya China na Marekani yatakuwa yakishindana katika teknolojia katika siku za mbeleni na kuzitaka kampuni za Marekani na Ulaya kushirikiana kukuza uchumi na kuleta maendeleo mapya kama vile akili bandia (AI) kwa dunia nzima.

Maneno kama haya sio mara ya kwanza kuyasikia yakisemwa na viongozi wa makampuni makubwa ya Marekani na Ulaya
, CEOs wa Ford na Apple waliwahi kunukuliwa wakisema:

"Watengenezaji wa magari wa China wanaenda kwa mwendo wa kasi wa mwanga, kwa kutumia akili ya bandia na teknolojia nyingine za hali ya juu katika magari yao tofauti na teknolojia yoyote iliyopo Marekani. Wanatengeneza magari kwa gharama nafuu ili kupunguza gharama na yaliyo na teknolojia za kisasa na wamepanuka kikamilifu katika masoko ya nje ya China, hili ni tishio lililopo kwetu."
–Jim Farley (Ford CEO)
No supply chain in the world is more critical to us than China. We're not in China for low labor costs. In the United States if we have a meeting of tooling engineers and we might not fill a room. In China, we would fill multiple football fields."
–Tim Cook (Apple CEO)

Kauli za viongozi wa juu wa makampuni makubwa ya Marekani na Ulaya ni tofauti sana na wanasiasa wao kama Trump na Biden na sera zao dhidi ya China.

Wanasiasa wa nchi za Magharibi wanaongea kisiasa wakati wakuu wa makampuni makubwa duniani wanazungumzia uhalisia. Kwa sasa hauwezi kuikimbia China katika dunia ya kibiashara na kiteknolojia.
 
China ina supply kubwa ya cheap labors that's it. Engineer wa China analipwa $400 kwa mwezi wakati kiwanja janitor tu anatengeneza hiyo kwa wk na benefits zote from health insurance, paid time off, life insurance, pension nk.
 
China ina supply kubwa ya cheap labors that's it. Engineer wa China analipwa $400 kwa mwezi wakati kiwanja janitor tu anatengeneza hiyo kwa wk na benefits zote from health insurance, paid time off, life insurance, pension nk.
Umemuelewa Tim Cook alichosema hapa?

No supply chain in the world is more critical to us than China.
We're not in China for low labor costs....In the United States if we have a meeting of tooling engineers and we might not fill a room. In China, we would fill multiple
football fields."
 
Ni kweli China Ni mkono ambao huwezi kuukwepa, lakini Bado US kwa mtazamo wangu yupi 20× mbele kuliko tunavyodhani.
Labda hapo mbele hizi Petro Dollar diplomacies zianguke.
Unazipinga kauli za viongozi wa juu wa makampuni makubwa duniani kama Microsoft kuhusu China?

Kwenye critical technologies China is ahead of US. Dunia inaenda kwa kasi sana usikariri

 
Unazipinga kauli za viongozi wa juu wa makampuni makubwa duniani kama Microsoft kuhusu China?

Kwenye critical technologies China is ahead of US. Dunia inaenda kwa kasi sana usikariri

Tukianza Kutuma hizi comparisons Bado US ataendelea kuwa juu, ila kama utasoma In between the lines sio kuwa China hawezi kumpiku US, ila Bado US Yuko Mbali sana na hizi mambo zilianza zamani sana. Post 2008 Market Crash watu walianza kuzungumzia jambo hili, hasa katika nyanja ya Teknolojia
 
Sema Huawei nyie ichukulieni poa
Huawei wako vizuri sana, Marekani waliogopa kasi waliyokuwa wanakuja nayo wakawafanyia figisu

Hebu angalia kituo chao cha R&D ndio ujue Huawei wako serious sana. Wamekizindua mwezi huu jijini Shanghai

The world's largest R&D center

 
Umemuelewa Tim Cook alichosema hapa?

No supply chain in the world is more critical to us than China.
We're not in China for low labor costs....In the United States if we have a meeting of tooling engineers and we might not fill a room. In China, we would fill multiple
football fields."

Two arguments can be true at the same time. T vs T = T.

Yes, wana produce skilled labor wengi ila maslahi yao madogo.

Kiwanja sio kwamba inashindwa kuproduce hiyo workforce, it actually does ila maslahi na haki za wafanyakazi zinazingatiwa sana.

Haki anazopata janitor kiwanja hata CEO huko China hapati. Wachina wenyewe wanajazana nchi za magharibi kila siku kufuata maslahi.

Hii ni nzuri kwa wafanyakazi ila ni changamoto kwa makampuni kuendesha biashara kwa faida ndo maana wanapeleka kazi huko. iPhone ingekua assembled USA ingeuzwa $10000.
 
Tukianza Kutuma hizi comparisons Bado US ataendelea kuwa juu, ila kama utasoma In between the linessio kuwa China hawezi kumpiku US, ila Bado US Yuko Mbali sana.
Screenshot_20240512-143741_Chrome.jpg


Screenshot_20240512-143804_Chrome.jpg


Screenshot_20240512-143936_Chrome.jpg


Screenshot_20240512-143956_Chrome (1).jpg


Screenshot_20240512-144113_Chrome.jpg


Screenshot_20240512-144223_Chrome.jpg


Screenshot_20240512-144327_Chrome.jpg


Screenshot_20240512-144425_Chrome.jpg
 
Yes, wana produce skilled labor wengi ila maslahi yao madogo.
Umemuelewa vizuri hapa Tim Cook alichomaanisha?

We're not in China for low labor costs....In the United States if we have a meeting of tooling engineers and we might not fill a room. In China, we would fill multiple football fields
 
Kiwanja sio kwamba inashindwa kuproduce hiyo workforce, it actually does ila maslahi na haki za wafanyakazi zinazingatiwa sana
Kiwanja hawana uwezo wa kuzalisha kama China.

Upande wa graduates wa STEM (Science, Technology, Engineering, Maths) China ndiyo inaongoza duniani

Mwezi June China imezalisha engineers 1,700,000 wakati Marekani ni 120,000 tu

Mind the gap
 
China ina supply kubwa ya cheap labors that's it. Engineer wa China analipwa $400 kwa mwezi wakati kiwanja janitor tu anatengeneza hiyo kwa wk na benefits zote from health insurance, paid time off, life insurance, pension nk.

hiyo sio sababu kuu.

china wana advantage ya supply chain systems nzima. kila kitu wanatengeneza wao na kina move haraka from point A to point B to point C, to even point Z, mfano china ukitengeneza simu, spika inaweza tengenezwa mwanza, kioo dodoma, chaji kigoma na vyote vikamfikia mtu wa mwisho wa assemble ndani ya masaa machache na yeye akakupa simu yako ikiwa kamili. hiyo ndio supply chain system nzima ambayo inawabeba China.


kama umewai kuagiza mzigo china lazima unajua tabia zao. china hakuna muuzaji mwenye mzigo dukani, pale pale unapoagizwa ndipo wanaanza kuutengeneza kwenye miji yao tofauti tofauti na bado unakamilika fasta na mteja unapewa
 
Kiwanja hawana uwezo wa kuzalisha kama China.

Upande wa graduates wa STEM (Science, Technology, Engineering, Maths) China ndiyo inaongoza duniani

Mwezi June China imezalisha engineers 1,700,000 wakati Marekani ni 120,000 tu

Mind the gap

Population size matters. Vyuo Bora duniani vipo wapi? Wachina wote ndoto yao ni kuja kusoma na kuishi kiwanja waache kazi za kitumwa huko.
 
Haki anazopata janitor kiwanja hata CEO huko China hapati. Wachina wenyewe wanajazana nchi za magharibi kila siku kufuata maslahi.
Umepiga hesabu za cost of living kati ya China na Marekani?

Miaka ya nyuma Marekani ilikuwa ikiwavutia scientists na engineers wa China kwenda huko

These days there is huge exodus of Chinese scientists and engineers leave U.S for China
 
Hiyo mbona sio siri China kwa sasa ndio inaongoza kwenye technological innovation.

Huko kuna hadi maduka yana technology ya kulipia kwa ku-scan kiganja cha mkono tu. Wanawazidi west kwenye kila nyanja technology ya ujenzi wa infrastructure, ubunifu nadhani ni ndio nchi pekee inayotumia vioo ku-reflect mwanga wa jua na kuzalishia umeme, BYD imeipiku Tesla kama brand inayouza magari mengi ya umeme duniani.

Technologically china wako mbali kwa sasa west wanafanya catching up.
 
hiyo sio sababu kuu.

china wana advanyage ya supply chain systems nzima. kila kitu wanatengeneza wao na kina move haraka from point A to point B to point C, to even point Z, mfano china ukitengeneza simu, spika inaweza tengenezwa mwanza, kioo dodoma, chaji kigoma na vyote vikamfikia mtu wa mwisho wa assemble ndani ya masaa machache na yeye akakupa simu yako ikiwa kamili. hiyo ndio supply chain system nzima ambayo inawabeba China.


kama umewai kuagiza mzigo china lazima unajua tabia zao. china hakuna muuzaji mwenye mzigo dukani, pale pale unapoagizwa ndipo wanaanza kuutengeneza na bado unakamilika fasta

Supply chain hata nchi za magharibi zipo up to par na kwa asilimia kubwa China ameiga kila kitu toka West. Hao wafanyakazi na wasafirishaji wanalipwa peanuts huko. Kiwanja a postal service worker analipwa zaidi ya mbunge wa TZ au engineer wa China na haki zote anapata.

Narudia, hii ni nzuri kwa wafanyakazi but Kampuni haziwezi jiendesha kwa faida ndo maana they outsource to China, India, Mexico etc.
 
Back
Top Bottom